Kuna makundi mawili yenye nguvu ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo yanayodaiwa kupishana mitazamo ya namna ya kuendesha siasa kuelekea chaguzi za SM na ule mkuu wa 2025.
Kundi la kwanza inaelezwa linaongozwa na Mwenyekiti FAM huku lingine likiongozwa na Makamu M/kiti TAL.
Uchunguzi uliofanywa na 'wafukunyuku'(wapekuzi wa habari za ndani kabisa), unaonyesha, kundi la TAL lina nguvu sana kwa sababu linaungwa mkono na wanaharakati wa ndani na nje ya nchi huku lile la FAM likiwa na uungwaji mkono kutoka kwa wanachama wa kawaida ambao uelewa wao ktk mambo ya siasa ukiwa mdogo.
Makundi haya kwa hali ilivyo sasa ni kama mafuta na maji.....imefikia wakati kundi moja kutumia pesa nyingi kwenye chaguzi za ndani ili wagombea waliowafuasi wao washinde. Ref: kauli ya TAL kule Iringa.
Tofauti za makundi haya yanaegemea kwenye namna ya kufanya siasa ;
Kundi la TAL(wakiwemo wanaharakati) linadaiwa kuendesha siasa zenye matamshi makali yenye kukosa staha kwa viongozi wa serikali. Inaelezwa pia kuwa wanaeleza mambo magumu ambayo hayaeleweki kwa wananchi wa kawaida. Linatuhumu vilevile kundi lingine kutumia pesa chafu, zisizoelewweka zitokako.
Kundi la FAM linadaiwa kuendesha siasa laini ambazo haziamshi hisia za wananchi, hivyo kukipa mwanya chama tawala CCM kupita kwa urahisi katika chaguzi zijazo.
Taarifa zaidi zinapasha, mgogoro wa 'Wabunge' 19 wakiongozwa na HJM nao ni chanzo cha MTIFUANO kwa makundi hayo.
Kundi la FAM linadaiwa kulegeza kamba dhidi ya 'wabunge' hao huku lile la TAL likikaza kudu kwa hoja kwamba ni fedheha kwa chama 'kugeuka jiwe'.
Za ndani kabisa ni kwamba, kuna vikao kundi la FAM lilikaa na baadhi ya akina HJM na kukubaliana watoe sehemu ya mapato yao ya bungeni ili yasaidie kuimarisha chama , kisha watangazwe kusamehewa.
Vyanzo fiche kutoka CDM vinaeleza, jambo hilo lilipingwa na kundi la wanaharakati walioapa kutoliweka hata kwenye mijadala ya kawaida ya chama. Ama vinginevyo wagawane mbao.
Kwenye MTIFUANO huu, CDM wakitoboa na kuwa wamoja, nawaona IKULU 2025
Kundi la kwanza inaelezwa linaongozwa na Mwenyekiti FAM huku lingine likiongozwa na Makamu M/kiti TAL.
Uchunguzi uliofanywa na 'wafukunyuku'(wapekuzi wa habari za ndani kabisa), unaonyesha, kundi la TAL lina nguvu sana kwa sababu linaungwa mkono na wanaharakati wa ndani na nje ya nchi huku lile la FAM likiwa na uungwaji mkono kutoka kwa wanachama wa kawaida ambao uelewa wao ktk mambo ya siasa ukiwa mdogo.
Makundi haya kwa hali ilivyo sasa ni kama mafuta na maji.....imefikia wakati kundi moja kutumia pesa nyingi kwenye chaguzi za ndani ili wagombea waliowafuasi wao washinde. Ref: kauli ya TAL kule Iringa.
Tofauti za makundi haya yanaegemea kwenye namna ya kufanya siasa ;
Kundi la TAL(wakiwemo wanaharakati) linadaiwa kuendesha siasa zenye matamshi makali yenye kukosa staha kwa viongozi wa serikali. Inaelezwa pia kuwa wanaeleza mambo magumu ambayo hayaeleweki kwa wananchi wa kawaida. Linatuhumu vilevile kundi lingine kutumia pesa chafu, zisizoelewweka zitokako.
Kundi la FAM linadaiwa kuendesha siasa laini ambazo haziamshi hisia za wananchi, hivyo kukipa mwanya chama tawala CCM kupita kwa urahisi katika chaguzi zijazo.
Taarifa zaidi zinapasha, mgogoro wa 'Wabunge' 19 wakiongozwa na HJM nao ni chanzo cha MTIFUANO kwa makundi hayo.
Kundi la FAM linadaiwa kulegeza kamba dhidi ya 'wabunge' hao huku lile la TAL likikaza kudu kwa hoja kwamba ni fedheha kwa chama 'kugeuka jiwe'.
Za ndani kabisa ni kwamba, kuna vikao kundi la FAM lilikaa na baadhi ya akina HJM na kukubaliana watoe sehemu ya mapato yao ya bungeni ili yasaidie kuimarisha chama , kisha watangazwe kusamehewa.
Vyanzo fiche kutoka CDM vinaeleza, jambo hilo lilipingwa na kundi la wanaharakati walioapa kutoliweka hata kwenye mijadala ya kawaida ya chama. Ama vinginevyo wagawane mbao.
Kwenye MTIFUANO huu, CDM wakitoboa na kuwa wamoja, nawaona IKULU 2025