Mdude_Nyagali
Member
- Dec 11, 2022
- 62
- 1,246
๐๐๐ฎ ๐๐ต๐ฒ๐ฟ๐ถ๐ฎ ๐ต๐ถ๐ถ ๐๐ฎ ๐จ๐ฐ๐ต๐ฎ๐ด๐๐๐ถ ๐ป๐ฎ ๐๐๐บ๐ฒ ๐ต๐ถ๐ถ ๐๐ฎ ๐จ๐ฐ๐ต๐ฎ๐ด๐๐๐ถ ๐ป๐ถ ๐๐ฎ๐๐ถ ๐ธ๐๐ฎ๐บ๐ฏ๐ฎ ๐๐ฐ๐ต๐ฎ๐ด๐๐๐ถ ๐บ๐ธ๐๐ ๐ฎ๐ฌ๐ฎ๐ฑ ๐๐๐ฎ๐ธ๐๐บ๐ฏ๐๐ฎ ๐ป๐ฎ ๐บ๐ฎ๐ฐ๐ต๐ฎ๐ณ๐๐ธ๐ผ.
Nimemaliza kusoma sheria namba 02 ya mwaka 2024 inayoanzisha muundo wa Tume ya Uchaguzi; na nimemaliza kusoma sheria ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani namba 01 ya mwaka 2024. Nilichokiona ni majanga matupu na hofu ya watawala.
1. Kwanza kabisa ukisoma sheria no.01/2024 inayounda Tume ya Uchaguzi inayodaiwa ni huru imeweka wazi kwamba Mwenyekiti wa tume, makamu wake, mkurugenzi wa tume watateuliwa na Rais ambaye ni mmoja wa wagombea katika uchaguzi utakaosimamiwa na hawa wateuliwa.
2. Wajumbe watano wanaounda tume hiyo nao watateuliwa na Rais ambaye ni mgombea kwenye uchaguzi ambao utasimamiwa na wajumbe hawa atakaowateuwa. Sijui kwanini waliingiza neno Tume Huru katika sheria hii wakati mmoja wa wagombea ndiye amepewa mamlaka ya kuteuwa wasimamizi wa uchaguzi.
Ukiachana na sheria ya muundo wa tume ya uchaguzi bado kuna majanga mengine kwenye sheria ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani.
1. Kifungu cha 36 cha sheria hiyo kinampa mamlaka msajili wa vyama vya siasa kuweka pingamizi na kumuondoa mgombea yoyote anayeshiriki uchaguzi. Kumbuka kwamba kwa mujibu wa sheria ya vyama vya siasa kifungu cha 4 na cha 5 kinachoainisha majukumu ya msajili wa vyama vya siasa hakuna sehemu hata moja inayompa mamlaka msajili wa vyama vya siasa kuondoa wagombea kwenye chaguzi isipokuwa kusajili vyama, kuvilea, kusimamia chaguzi za ndani, kugawa ruzuku n.k.
2. Kifungu cha 37 - (3) Kinampa mamlaka pia mwanasheria mkuu wa serikali kuweka pingamizi kwa mgombea yoyote na mgombea huyo akaondolewa. Sasa kama mnavyojua ni kwamba mwanasheria mkuu wa serikali ana maslahi ya moja kwa moja na mmoja wa wagombea Urais hasa Rais anayegombea kwa muhura wake wa pili, hivyo kuweka pingamizi kunaweza kutafsiriwa kama ametumwa na Rais kwa mlango wa nyuma.
3. Kifungu cha 54-(1),(2) na kifungu cha 38-(1),(2) kinaruhusu tume kuengua wagombea ambao wamewekewa mapingamizi na mwanasheria mkuu au msajili na tume ikabakiza mgombea mmoja na mgombea huyo mmoja akapigiwa kura za ndiyo au hapana kama wakati wa Nyerere na chama kimoja.
4. Kifungu cha 85-(2)-(m), kifungu cha 94 - (1)-(e), kifungu cha 103 -(1)-(h) na kifungu cha 104 - (1)-(h) kwa pamoja vifungu hivi vinaruhusu askari polisi kuwepo ndani ya vituo vya kupigia kura wakati wa zoezi la kupiga kura, kuhesabu na kutangaza matokeo. Kumbukeni hapo awali sheria ilikuwa hairuhusu askari kuwepo ndani ya chumba cha kupigia kura isipokuwa nje kwa ajili ya kuimalisha usalama. Lakini bado askari polisi wengi waliingia ndani ya vituo vya kupigia kura na kuingiza kura feki wakati mwingine kutoa mawakala wa upinzani. Sasa sheria hii imehalalisha wao kuwepo ndani ya vituo na sio nje tena kama mwanzo.
5.Kifungu cha 92 - (2) kinaipa mamlaka Tume ya Uchaguzi, Mkurugenzi wa Uchaguzi na msimamizi wa Uchaguzi kwenda kuhesabia kura mahali pengine endapo wataona kituo kilichotumika kupigia kura ni finyu au si salama. Mfano msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Mbeya anaweza kusema Mbeya si salama kuhesabia na kujumlishia kura na akaaamua kuhamishia kazi hiyo Dodoma.
Sasa kwa mazingira haya kuna uchaguzi huru na haki kuanzia muundo wa tume yenyewe mpaka sheria inayosimamia uchaguzi? Wananchi watakubali kuwa Mbuzi wa kafala kama walivyofanyiwa 2019 na 2020? Kwa mateso waliyopitia wananchi kwa hii miaka mitano watakubali tena kuchezewa sharubu na hawa vibaka walioko serikalini ambao wengi wao ndio viongozi?
Binafsi nayaona machafuko makubwa ambayo pengine serikali inaweza kuanguka. Naona sasa itakuwa zamu ya viongozi wa serikali kukimbia nchi badala ya wapinzani.
Mdude Mpaluka Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu
Nimemaliza kusoma sheria namba 02 ya mwaka 2024 inayoanzisha muundo wa Tume ya Uchaguzi; na nimemaliza kusoma sheria ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani namba 01 ya mwaka 2024. Nilichokiona ni majanga matupu na hofu ya watawala.
1. Kwanza kabisa ukisoma sheria no.01/2024 inayounda Tume ya Uchaguzi inayodaiwa ni huru imeweka wazi kwamba Mwenyekiti wa tume, makamu wake, mkurugenzi wa tume watateuliwa na Rais ambaye ni mmoja wa wagombea katika uchaguzi utakaosimamiwa na hawa wateuliwa.
2. Wajumbe watano wanaounda tume hiyo nao watateuliwa na Rais ambaye ni mgombea kwenye uchaguzi ambao utasimamiwa na wajumbe hawa atakaowateuwa. Sijui kwanini waliingiza neno Tume Huru katika sheria hii wakati mmoja wa wagombea ndiye amepewa mamlaka ya kuteuwa wasimamizi wa uchaguzi.
Ukiachana na sheria ya muundo wa tume ya uchaguzi bado kuna majanga mengine kwenye sheria ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani.
1. Kifungu cha 36 cha sheria hiyo kinampa mamlaka msajili wa vyama vya siasa kuweka pingamizi na kumuondoa mgombea yoyote anayeshiriki uchaguzi. Kumbuka kwamba kwa mujibu wa sheria ya vyama vya siasa kifungu cha 4 na cha 5 kinachoainisha majukumu ya msajili wa vyama vya siasa hakuna sehemu hata moja inayompa mamlaka msajili wa vyama vya siasa kuondoa wagombea kwenye chaguzi isipokuwa kusajili vyama, kuvilea, kusimamia chaguzi za ndani, kugawa ruzuku n.k.
2. Kifungu cha 37 - (3) Kinampa mamlaka pia mwanasheria mkuu wa serikali kuweka pingamizi kwa mgombea yoyote na mgombea huyo akaondolewa. Sasa kama mnavyojua ni kwamba mwanasheria mkuu wa serikali ana maslahi ya moja kwa moja na mmoja wa wagombea Urais hasa Rais anayegombea kwa muhura wake wa pili, hivyo kuweka pingamizi kunaweza kutafsiriwa kama ametumwa na Rais kwa mlango wa nyuma.
3. Kifungu cha 54-(1),(2) na kifungu cha 38-(1),(2) kinaruhusu tume kuengua wagombea ambao wamewekewa mapingamizi na mwanasheria mkuu au msajili na tume ikabakiza mgombea mmoja na mgombea huyo mmoja akapigiwa kura za ndiyo au hapana kama wakati wa Nyerere na chama kimoja.
4. Kifungu cha 85-(2)-(m), kifungu cha 94 - (1)-(e), kifungu cha 103 -(1)-(h) na kifungu cha 104 - (1)-(h) kwa pamoja vifungu hivi vinaruhusu askari polisi kuwepo ndani ya vituo vya kupigia kura wakati wa zoezi la kupiga kura, kuhesabu na kutangaza matokeo. Kumbukeni hapo awali sheria ilikuwa hairuhusu askari kuwepo ndani ya chumba cha kupigia kura isipokuwa nje kwa ajili ya kuimalisha usalama. Lakini bado askari polisi wengi waliingia ndani ya vituo vya kupigia kura na kuingiza kura feki wakati mwingine kutoa mawakala wa upinzani. Sasa sheria hii imehalalisha wao kuwepo ndani ya vituo na sio nje tena kama mwanzo.
5.Kifungu cha 92 - (2) kinaipa mamlaka Tume ya Uchaguzi, Mkurugenzi wa Uchaguzi na msimamizi wa Uchaguzi kwenda kuhesabia kura mahali pengine endapo wataona kituo kilichotumika kupigia kura ni finyu au si salama. Mfano msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Mbeya anaweza kusema Mbeya si salama kuhesabia na kujumlishia kura na akaaamua kuhamishia kazi hiyo Dodoma.
Sasa kwa mazingira haya kuna uchaguzi huru na haki kuanzia muundo wa tume yenyewe mpaka sheria inayosimamia uchaguzi? Wananchi watakubali kuwa Mbuzi wa kafala kama walivyofanyiwa 2019 na 2020? Kwa mateso waliyopitia wananchi kwa hii miaka mitano watakubali tena kuchezewa sharubu na hawa vibaka walioko serikalini ambao wengi wao ndio viongozi?
Binafsi nayaona machafuko makubwa ambayo pengine serikali inaweza kuanguka. Naona sasa itakuwa zamu ya viongozi wa serikali kukimbia nchi badala ya wapinzani.
Mdude Mpaluka Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu