Hatimaye ile siku imewadia,leo ndio uzinduzi rasmi wa ndege mbili za TGFA zitakazokodiwa na ATCL kwa ajili ya matumizi ya usafiri wa ndani na nje ya nchi.Zaidi ya ndani ya mipaka ya Tanzania,ndege mpya za ATCL zinatazamiwa kuwa na "route" ya kuelekea Hahaya-Commor ambapo imekuwa na soko la uhakika hata wakati ikiwa na ndege moja tu.
Uzinduzi huo unategemewa kufanywa na Rais wa JMT Mh.John P. Magufuli.Eneo la ufunguzi litakuwa ni eneo la maegesho ya Wakala wa Ndege za Serikali(Tanzania Gvt Flight Agency)maandalizi ya uzinduzi huo yanaendelea na tayari ndege hizo zimetolewa eneo la "Apron" ya JWTZ-Air Wing na kuletwa TGFA.
Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari,wafanyakazi wa taasisi mbalimbali zinazofanya kazi uwanja wa ndege kama TAA,TGFA,TCAA,Swissport,Precision,ATCL,Police,State Security,JWTZ-Airwing na TMA watawakilisha raia wengine.
Kwa sbb za kiusalama na unyeti wa eneo,itakuwa ngumu kwa raia wengi kutoka nje bila kibali na vitambulisho kuingia moja kwa moja.Mpaka sasa utepe na eneo la kufanyia uzinduzi lipo tayari....Tutaendelea!!!
===== ======. =========
Hatimaye agizo limetoka na Raia wameruhusiwa kuingia na tayari kwa kumsubiri Rais anayetarajiwa kufika saa nne na nusu