Serikali na CCM Iviaibishe Vyama Vya Upinzani Kwa Kufanya Mabadiliko Ya Msingi Kwenye Sheria Za Uchaguzi, Kama Huwa Inashinda Kwa Haki.

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
19,531
49,369
CHADEMA katika kampeni yake ya NO REFORM NO ELECTION, haitafuti upendeleo bali inatafuta haki na ulinzi wa thamani ya kura. Hivi CCM kama huwa inashinda kwa haki, si ndiyo ungekuwa muda sahihi kukubali mapendekezo yote yatakayoufanya mchakato wa uchaguzi kuwa huru, wa haki na wa uwazi ili wawadhihirishie Watanzania na Dunia nzima kuwa wamekuwa wanashinda kwa haki? Kwa nini waligomea maoni ya wananchi na taasisi za dini, chama cha wanasheria Tanganyika na chama cha wanasheria wanawake, na hata maoni yaliyotolewa na watu maarufu katika Taifa letu?

Taasisi za dini, vyama vya upinzani, Chama cha wanasheria Tanganyika, Chama cha wanasheria wanawake, watu maarufu kama Jaji Warioba, Prof. Shivji, Butiku; wote waliwiana katika mapendekezo yafuatayo:

1. Mwenyekiti na makamishna wote wa TUME YA UCHAGUZI wasiteuliwe na Rais - CCM na Serikali yao wamegoma.

2. Uchaguzi usisimamiwe na wakurugenzi wala watumishi wa umma -- CCM na serikali yao wamegoma.

3. Matokeo ya uchaguzi, kwa ngazi zote, kuanzia udiwani mpaka Urais, kunapokuwa na haja, yahojiwe mahakamani - CCM na serikali yao wamegoma.

4. Watendaji wa Tume ya Uchaguzi, wakifanya uovu wanapotekeleza wajibu wao, washtakiwe mahakamani - CCM na serikali yao wamegoma.

5. Uhesabuji kura na majumuisho, vifanyike kwa uwazi kama inavyofanyika kwenye mataifa mengine - CCM na serikali yake wamegoma.

6. Polisi waondolewe kwenye michakato ya uchaguzi, wabakie na wajibu wao wa kulinda usalamawa raia - CCM na serikali yake, wamegoma.

Jiulize hayo mambo yote yaliyopendekezwa na wadau mbalimbali yalikuwa na kasoro gani? Kwa kugomea mapendekezo haya yaliyokuwa na dhamira njema, kuna mtu yeyote bado anaamini CCM ya sasa ina dhamira njema na Taifa hili?

Watanzania wenye dhamira njema, hata kama wamo ndani ya CCM, tuungane dhidi ya ushetani wa kupora mamlaka ya wananchi.

NO REFORM NO ELECTION.
 
Hawawezi kufanya hivi bila kulazimishwa kwa maana huwa hawashindi.
Hakika kwa kugomea mapendekezo hayo mema ya wadau, CCM inadhihirisha pasipo shaka kuwa huwa inapora uchaguzi.

Tusikubali kuendelea kuibiwa. Chama kinachoingia madarakani kwa wizi na uporaji wa haki, kama CCM, lazima kitatengeneza Serikali ya wizi na serikali ya kupora haki za watu, ndiyo maana tunashuhudia wakifanya ufisadi mkubwa, wakiteka na kuua watu.

NO REFORM NO ELECTION, ni mpango wa kuokoa uhai wetu kutoka kwa hawa wadhulumaji wa haki za kuishi, haki za kutoa maoni na kukosoa. NO REFORM NO ELECTION ni mpango wa kurudisha madaraka na umiliki wa nchi kwa wananchi, kutoka kwa manyang'au waporaji.
 
CHADEMA katika kampeni yake ya NO REFORM NO ELECTION, haitafuti upendeleo bali inatafuta haki na ulinzi wa thamani ya kura. Hivi CCM kama huwa inashinda kwa haki, si ndiyo ungekuwa muda sahihi kukubali mapendekezo yote yatakayoufanya mchakato wa uchaguzi kuwa huru, wa haki na wa uwazi ili wawadhihirishie Watanzania na Dunia nzima kuwa wamekuwa wanashinda kwa haki? Kwa nini waligomea maoni ya wananchi na taasisi za dini, chama cha wanasheria Tanganyika na chama cha wanasheria wanawake, na hata maoni yaliyotolewa na watu maarufu katika Taifa letu?

Taasisi za dini, vyama vya upinzani, Chama cha wanasheria Tanganyika, Chama cha wanasheria wanawake, watu maarufu kama Jaji Warioba, Prof. Shivji, Butiku; wote waliwiana katika mapendekezo yafuatayo:

1. Mwenyekiti na makamishna wote wa TUME YA UCHAGUZI wasiteuliwe na Rais - CCM na Serikali yao wamegoma.

2. Uchaguzi usisimamiwe na wakurugenzi wala watumishi wa umma -- CCM na serikali yao wamegoma.

3. Matokeo ya uchaguzi, kwa ngazi zote, kuanzia udiwani mpaka Urais, kunapokuwa na haja, yahojiwe mahakamani - CCM na serikali yao wamegoma.

4. Watendaji wa Tume ya Uchaguzi, wakifanya uovu wanapotekeleza wajibu wao, washtakiwe mahakamani - CCM na serikali yao wamegoma.

5. Uhesabuji kura na majumuisho, vifanyike kwa uwazi kama inavyofanyika kwenye mataifa mengine - CCM na serikali yake wamegoma.

6. Polisi waondolewe kwenye michakato ya uchaguzi, wabakie na wajibu wao wa kulinda usalamawa raia - CCM na serikali yake, wamegoma.

Jiulize hayo mambo yote yaliyopendekezwa na wadau mbalimbali yalikuwa na kasoro gani? Kwa kugomea mapendekezo haya yaliyokuwa na dhamira njema, kuna mtu yeyote bado anaamini CCM ya sasa ina dhamira njema na Taifa hili?

Watanzania wenye dhamira njema, hata kama wamo ndani ya CCM, tuungane dhidi ya ushetani wa kupora mamlaka ya wananchi.

NO REFORM NO ELECTION.
acha upotoshaji basi gentleman,
eti hiyo namba 2 unapotoshaje kuhusu wakurugenzi kusimamia uchaguzi? inamaana hujui?

athari za kususa michakato ya kidemokrasi na mabadiliko ya sheria za uchaguzi vimeanza kukuumbua wewe gentleman kabla ya wenzako, dah!🤣
 
CHADEMA katika kampeni yake ya NO REFORM NO ELECTION, haitafuti upendeleo bali inatafuta haki na ulinzi wa thamani ya kura. Hivi CCM kama huwa inashinda kwa haki, si ndiyo ungekuwa muda sahihi kukubali mapendekezo yote yatakayoufanya mchakato wa uchaguzi kuwa huru, wa haki na wa uwazi ili wawadhihirishie Watanzania na Dunia nzima kuwa wamekuwa wanashinda kwa haki? Kwa nini waligomea maoni ya wananchi na taasisi za dini, chama cha wanasheria Tanganyika na chama cha wanasheria wanawake, na hata maoni yaliyotolewa na watu maarufu katika Taifa letu?

Taasisi za dini, vyama vya upinzani, Chama cha wanasheria Tanganyika, Chama cha wanasheria wanawake, watu maarufu kama Jaji Warioba, Prof. Shivji, Butiku; wote waliwiana katika mapendekezo yafuatayo:

1. Mwenyekiti na makamishna wote wa TUME YA UCHAGUZI wasiteuliwe na Rais - CCM na Serikali yao wamegoma.

2. Uchaguzi usisimamiwe na wakurugenzi wala watumishi wa umma -- CCM na serikali yao wamegoma.

3. Matokeo ya uchaguzi, kwa ngazi zote, kuanzia udiwani mpaka Urais, kunapokuwa na haja, yahojiwe mahakamani - CCM na serikali yao wamegoma.

4. Watendaji wa Tume ya Uchaguzi, wakifanya uovu wanapotekeleza wajibu wao, washtakiwe mahakamani - CCM na serikali yao wamegoma.

5. Uhesabuji kura na majumuisho, vifanyike kwa uwazi kama inavyofanyika kwenye mataifa mengine - CCM na serikali yake wamegoma.

6. Polisi waondolewe kwenye michakato ya uchaguzi, wabakie na wajibu wao wa kulinda usalamawa raia - CCM na serikali yake, wamegoma.

Jiulize hayo mambo yote yaliyopendekezwa na wadau mbalimbali yalikuwa na kasoro gani? Kwa kugomea mapendekezo haya yaliyokuwa na dhamira njema, kuna mtu yeyote bado anaamini CCM ya sasa ina dhamira njema na Taifa hili?

Watanzania wenye dhamira njema, hata kama wamo ndani ya CCM, tuungane dhidi ya ushetani wa kupora mamlaka ya wananchi.

NO REFORM NO ELECTION.
Ni watawala wachache sana wanaokubali kwa hiari yao kufanya reforms zinazoweza kusababisha wang’oke madarakani. Obviously, CCM isn’t one of them!
 
Back
Top Bottom