Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Mzeeshughuli Bwana,

Nasaha zako safi ndugu yangu. Tatizo ni kuwa unaangalia upande mmoja na mifano yako iko kwenye mshazari huo huo. Ukiongelea Wapalestina inaonekana haikuyumkiini kabisa kuwa Northen Ireland zimepigwa na kulipuliwa mabomu ya kujiuwa kati ya Roman Catholic na Protetants. Pia unawasahau mabudha na mahindu wa kule Korea wanavyokabana makoo wao kwa wao n.k.

Na hapa kwetu ni muislamu yupi aliinuwa slaha kumpiga mkristo wakati waislamu walipouawa kinyama pale Mwembe Chai na kule Pemba. na hao ndio waislamu watanzania ambao saa nyingine unasema wajilipuwe. Ndugu yangu usisingizie dini za wenyewe mambo isiyokuwa nayo; si vizuri.

Wewe uwezo wa kuingia vichwani mwa waislamu na kujuwa huyu ana akili timamu na huyu hana uliupata wapi kama si uchovu tu wa kutafakari mambo na kutokuelewa waislamu hawajafumba macho ufikiriavyo wewe bali tu hawapendi ugomvi na wale wachache wanaochambuwa mambo kwa undani huwa ni tatizo kwa uelewa wako.

Amini usiamini, tumesoma na watoto wetu wamesoma elimu za dunia na akhera kwa kina kirefu na wala tunayoandika si hadithi. Wewe unaona mauaji ya mwembe chai yalikuwa hadithi. Mtu wa ajabu sana wewe!

Mzeeshughuli Bwana said:
Chuki chuki chuki na chuki na hdithi na majazba ni ujinga na upuuzi sana . Ndiyo maana Wapalestina wanaumia kwa kuwa ya imai yao na madai ambayo hayasikilizwi mana yanakuja na chuki na wanaacha kujua kwamba Dunia imeendelea na watumie njia zingine za kuwakabili waisraeli. Jizalendo na nduguzo Tanzania ni ya wote na Mwalimu did well na hakuna wa kukataa hilo .Hubirini watoto wenu wasome na si chuki maana mkichelewa na wao watasoma hadithi kama hizi na wakashindwa kufanya mambo ya maana . Mwalimu alikuwa mwisho wa matatizo kila Muislam mwenye akili timamu knows .
 
Mswahili,

Ukienda mbali kughorodhesha Nyerere alivyofadhiliwa na Waislamu itaonekana kama unawasimanga hawa ndugu zetu. Mimi nisingependa uende huko, si vizuri. Pia siafikiani nawe kuyaleta majina ya akina Magufuli hapa kwani zaidi ya wao kuwa wakristo si dhani ni mahali pa kuwajadili kwenye mada hii. Ukifanya hivyo utaonekana unamkaba shingo kila ambaye ni mkristo. Waachie wao wafanye hilo wewe usiwajoin.

mswahili said:
Mzee Shughuli
chukulia mfano mwepesi Nyerere alikuja na kaptula na waislam hawakuona kinyaa kukaa nae na wakamfundisha hadi kuvaa suruali.

Mzee Shughuli nimelazimika kukuweka sawa ingawa sasa mnatuona sisi waswahili(hatujaendelea)
imagine Mzee una nyumba yako jee unaweza kumpangisha muislam? lakini tizama nyumba za waislam zinapangisha watu wa dini zote fanya utafiti uone waislam walivyo rahimu na hawana chuki unazodai.

au mzee shughuli unaweza kumwita mwanao Magufuri?
 
Jizaledo,
Unazungumza vitu gani hapa hata sikuelewi kabisa.

Nini maana ya kufuru?...

Nakuomba jaribu kutafuna kwanza kabla hujameza tonge, haya sii maji ya kunywa inabidi ufuate taratibu zinazotakiwa laa sivyo yatakushinda.

Imani za dini ndio Uislaam wenyewe yaani usipokuwa na imani hizo imekuondoa ktk UISLAAM. Huu ni mwongozo kwa yule anayetaka kuwa muislaam na sii SUNNI peke yake, ni kwa waislaam wote wala hii sio SIASA. Labda rudia kutafuta maana ya neno SIASA upate kutofautisha misemo hii mkisha uje kutenganisha madhehebu.

Hapa swala la Kufuru halipo kabisa kwani waweza kuwa na imani ya dini na bado ukakufuru kwa kumshirikisha Mungu..Mifano umeitoa wewe mwenyewe - Kwenda kwa mganga kupigiwa bao..Kufuru yake ni kuwa umeshirikisha Mungu ambaye una IMANI naye kwa MUNGU MTU ambaye unaweka IMANI ya utabiri wake.

Kuhusu Mwongozo nimezungumzia nje ya dini kama vile SIASA. dhehebu la sunni halina mwongozo wa viongozi wetu ktk swala hili. Hii ndio maana ya JK ktk hotuba yake na hoja yangu ilikuwa ktk kuelezea hotuba ya JK.

Kama umefuatilia maswala ya Iraq utaona ya kuwa Shia wanao akina Ayatollah ambao kulingana na mwongozo wa dhehebu lao ndio VIONGOZI wanaotakiwa kuwaongoza hata ktk maswala yao ya Siasa. Na wanacho chombo maalum kinachowatayarisha watu hawa kulingana na mwongozo wao. Lakini Sunni wamekuwa wakibebwa ovyo hata watu kama Ossama wameweza kushika jukumu la kudai kuwa wao VIONGOZI. Hakuna mtu anayeweza kusimama na kudai Uongozi kulingana na mwongozo wa dhehebu la Sunni unaompa yeye wadhifa wa kuongoza.... HATUNA kipengele hicho!

Halafu basi napozingumzia neno mwongozo inaonyesha wazi wewe umeelewa kuwa Sunni hawana kabisa mwongozo wa dini....kumbe tunachozungumzia ktk mada hii ni mwongozo ktk kipengele kimoja - VIONGOZI wa jamii sunni...

Ndio sababu nikasema hapo nyuma kuwa kuna mapungufu ya kutokuwa na mwongozo ktk ulimwengu huu wa mafisi kuviziana. Wewe kila mara unazungumzia waislaam wote badala ya kujaribu kuielewa hotuba ya JK.

Pili, Mohammad sio KIONGOZI kwanza ila ni MTUME wa Mungu (Rasul Llah) labda hufahamu maana ya Mtume ama tofauti zilizopo ktk maneno haya. Kiongozi ni yule anayewaongoza watu kufikia malengo yaliyokusudiwa hata kama malengo hayo yawe ni KUFUR na Mtume ni mjumbe aliyekuja wa wahii wa Mwenyezi Mungu kwenu na sii lazima awe kiongozi.

Sasa ikiwa Muhammad ni kiongozi wako na sio Quran kama alivyosema yeye.. Je, ameweza vipi kutuongoza ikiwa utaondoa Quran aliyotuachia kama mwongozo?... Labda hufahamu ya kwamba madhehebu haya yamekuwepo baada ya yeye kuondoka. Sunni tumeamua kufuata kitabu na hakuna kiongozi mbele yetu yaani hata wewe kesho unaweza kusalisha ama kuchukua nafasi mbele ya kutuongoza lakini huwezi kuyakuta haya ktk Shia ama Ismailia. Wao wana chombo kinachowaandaa watu kuongoza na ndiko tunaona hao akina Ayatollah na Agha Khan..Na wanaamini kwa vitendo (ingawa sii kwa Ulimi) kuwa hawa ni - Miungu Watu.

Muhammad sii binadamu kati yako na Mungu, haya ndiyo mafundisho nisiyoyakubali mimi kwa sababu Muhammad kama binadamu hana uwezo wa kumzuia mtu aliyechaguliwa na Mungu. Tunamsalia Mtume wetu kila baada ya sala kwa nini?..Hilo daraja zaidi yangu sikusema hana na ndio maana akaitwa mtume, sijadai utume hapa wala hakuna kati yetu anayedai kuwa na daraja sawa na mtume yeyote yule. Ila kama Sunni siwezi kusimama hapa nikaomba mtu ama Muhammad anifutie madhambi yangu.

Mwisho nadhani hii mada imepoteza mwelekeo na sina haja ya kuendelea zaidi ikiwa tumetoka kwa Nyerere..

Mswahili,
Wapemba hawampendi Jumbe kwa sababu gani?... Je, nikisema Watanganyika hawampendi Nyerere ina maana Nyerere hakufanya kitu kizuri kwa Watanganyika. Wee unawajua Wapemba kweli ama unakisia tu. Jumbe mtu mweusi (kibaraka) kajipendekeza kwao wakamtumia kisha wamemtupa kwani sii mwenzao kama ilivyo kawaida yao. hata mimi nikikusikiliza wewe nitaamini kabisa kuwa Nyerere hapendwi na watanganyika.
 
Mkandara,
Naomba majibu juu ya waraka wa jumbe kwa nyerere? naomba usikimbie kwani una kila nukta ya uovu wa Nyerere au inawezekana nawe ni Simba wa vita wa pili?
 
Mkandara nadhani umetoa Elimu ya kutosha kwa nduguzo waislam lakini wamesha umizwa na akili na kujawa na roho ya chuki. Hivi baada ya kusema ana kujibu juu ya waraka huo tutapata faida gani ? Maana jumbe na Mwalimu sasa ni historia na Tanzania we need to move on .
 
Mugishagwe
hatuwezi ku move on bila kujua wapi tulijikwaa? au ni wewe uliyemshauri Mungai kulifuta somo la historia hadi JK akaja juu.?
Nyerere ni mdini +mkabila
 
Waraka wa Jumbe kwa Nyerere!...

Wee uliuona ama unasimuliwa ktk magazeti yenu!.. Na kwa nini Nyerere alimwite Jumbe Dodoma hali ofisi yake ipo Dar na private zaidi...kama Jumbe alikutana na Nyerere Dodoma ina maana kulikuwa na vikao vya chama.

wajumbe wengine walikuwepo na habari hii isingekuwa siri ya waislaam na Nyerere peke yake. Haya yote yatoke baada ya Jumbe kuandika kitabu? mara ohhh alikuwa Seif aliyemtonya Nyerere kuwa Jumbe alikuwa na Agenda za kuvunja muungano.. sasa tena Huyo huyo Sief anataka kuvunja Muungano mbaya wake ni Karume!... Wajinga kweli waarabu hawa mbona wanamkumbatia Seif!...Na Nyerere angekuwa na waraka ya nini Seif amtonye hali kisha pata waraka!

Ati unauliza Nyerere kujenga msikiti Butiama!...kwani wazanaki hawafai kuwa waislaam isipokuwa waarabu tu na nyie ma colored! mbona moja kati ya sifa za Mwinyi ni ujenzi wa misikiti mingi Tanzania bara.
Tatizo lenu hamuoni mikundu yenu, afadhali wakristu wanaweza kabisa kumshambulia Nyerere , JM Sumaye na hata Papa kwa makosa yake lakini sii muislaam. Kwanza tunazama jina la mtu, akiwa Al Haj basi haiwezekani kuwa muovu hata kama tunalala njaa!

Tazama mwenyewe ktk Mijadala yoteee nchini sijawahi kuona wadini kama nyie mkimlaumu kiongozi yeyote muislaam.. hawa ni ma saint wanaonewa tuu. isipokuwa nimeona wakristu wakiwashutumu viongozi wa dini zao na nyie wepesi sana kudandia bus. Na kibaya zaidi basi mara mnadai kuwa wakristu wote mara Wakatoliki basi ili mradi haijulikani malalamishi yenu wameelemea wapi. Ukiangalia hesabu ya wakristu katoliki serikalini sii kubwa kama mnavyodai, hapo mtabadilisha kuwa wakristu...
 
Mkandara
Umesema wewe ni muislam hutakiwi kutukana watu,sitakujibu matusi hapa.
waraka nimeuona na kopi ninayo unataka nikupatie na waraka na kitabu ni vitu viwili tofauti ulianza waraka 1984 na kitabu kilitoka 1995 nadhani umeona tofauti. sikusema Sharif Hamad alimfitini Jumbe kwa Nyerere naomba ushahidi wa kauli yangu hiyo. unaposema magazeti yenu unakusudia magazeti gani fafanua?

sikuwakweza waislam wa Butiama naomba usinifitinishe na waislam wenzangu.
unasema muislam akikosea hatusemi, mimi niliwashtumu sana Bakwata ktk mada ya Mengi au Bakwata nalo ni baraza la kanisa? ni kamshutumu hadi Mufti ambaye ni kuongozi wangu wa juu sana sawa na Pengo kwa ndugu zetu wakristu.hivyo hapa hapendwi mtu ni sera na ukweli tu.

kama umeshindwa mjadala endelea kutukana hata hao waliokubatiza kuwa ni muislam safi huku unamwaga matusi namna hiyo sijui wametumia vigezo gani?
 
Mkandara
naijua nje ndani issue ya Jumbe.
sitegemei habari za magazetini mie kisima cha habari.
Jumbe yuko London sasa sussex Gardens karibu na Bays water nitakutumia PM kukupa full adress. hapa hatubahatishi mtakaoamua kutuchukia tuchukieni tu, najua ukweli unauma kuna watu bila Mwl wasingekuja Dar sasa tunaposema upande wa pili wa mwl sio rahisi watu hao kukuelewa. ndio maana wapo wanaodiri kusema kuwa kazi za jeshi zilikuwa hazina mzengwe kuzipata. mie nina mjomba wangu alinyimwa kisa hajatoka mara.
 
Nina ngoja majibu yangu juu ya St.Mathews na madai yako ya waseminary kupewa mitihani . Mbiku na University kwa kuwa wewe ni mchunguzi uje na ulilo ipata na mwisho naomba weka waraka wa Jumbe hapa .Yeye kuwepo London unaweza kusema hapa kwa uwazi maana si wewe tu unayejua aliko hata mimi naweza kuandika ukitaka .Hizo si news . Mkandara endelea kuwapa shule hawa ndugu zako ambao leo hawana la kufanya ila kuzua uongo na fitina. Ama mko kazini nini ?
 
Mugishagwe
Masuala ya waraka nimeahidi kumpatia Mkandara kama atataka. humu sitauweka naogopa maisha yangu kukatwishwa. wewe umesema Usalama wa Taifa kuna watu wa seminary za kanisa na huko jeshini unafahamu wazi wako watu wa sehemu gani?
Mkandara nadhani si ndugu yetu kama unavyolazimisha wewe na yeye.
maana sehemu ya kutukana kajitoa ' Amesema nyie waislamu mik.... yenu' angesema yetu.
Father Mbiku yupo pale na nina majina ya WAkristu walioingizwa pale wakiwa na division 3.
pia nina orodha ya wanafunzi zaidi ya miaka 300 ambao mwaka juzi waliomba kuingia kama Private sponsorship lakini ukiwa mkristu basi unapewa goverment sponsorship.
ninao majina ya watu waliopewa Goverment sponsorship na mzee Mkono kwa ukristu wao.
ninao hata waraka wa muungano ambapo umefichwa na Nyerere ila hapa si mahala pake kama nilivyosema hapo juu.
nakupa home work.
ilikuwaje nyerere awa support Biafra? ambao walijitenga na serikali halali? jibu Ukristu wa Nyerere ndio uliomsukuma kufanya hayo.
jiulize Iddi Amin na nguvu iliyotumika kumshambulia ilikuwa nini? kisa nyerere alitaka ukristu utawale Africa ndio maana hata Gaddaf akawa ana msaidia Idd Amin kwani vilikuwa vita vya kidini.
pia hutakiwi kumshambilia mtu hadi ndani mwake Nyerere alipeleka jeshi hadi katikati ya Uganda.tumeingizwa kwenye vita kumsaidia mkatoliki obote.
huyu ndio mwalimu aliyetuwekea usiku hadi bongo haijulikani kwenye ramani ya dunia. kisa udini+ukabila
 
Kitila Mkumbo,

kwanini wewe unahangaika na chadema? unadai kuna mabadiliko ya kweli na uhuru.
kwa faida yako mabadiliko ya kweli hayawezi kuja kama kuna groups za watu tofauti ndani ya nchi moja? hujiulizi kwanini Bagamoyo uliokuwa mji mkuu wa East -Africa wakati wa mjerumani leo uko katika hali mbovu vile? huwezi kufanya mabadiliko bila kujua wapi tumetoka na wapi tunakwenda? ndio maana hata wewe na elimu yako umekuwa na maamuzi ya kubahatisha sana , mfano wewe na usomi wako kwenda kuwa mfuasi wa Mrema ndani ya TLP? AT LEAST ungemfuata Mrema wakati yuko NCCR ningekuelewa.
hata hapo Chadema tizama vizuri usije kupoteza muda wako.

Mfano mzuri. Mwenyekiti wa mwanzo ni Mtei(mchagga) alikuwa Benki kuu. na Mwenyekiti wa sasa mheshimiwa Mbowe(mchagga) na mkwewe mzee Mtei walikuwa wote Benki kuu.

Najua nimekukera kumgusa Mnyika samahani sheria ni msumeno.

ila katika hoja zangu zitakusaidia sana ktk harakati zenu za siasa.
 
Mswahili,

Wewe sasa unaingia mitaa mingine kabisa!.. Bila Nyerere tusingekuja Dar?....Yeye Nyerere mwenyewe katokea wapi?.. nambie nani mzawa wa Dar na hakutokea bara kama sio Waha na wabembe wa Zaire waliokuja pwani utumwani na kujiita wazalamo hali ni Wamanyema. tazama accent zao utajua nazungumza kitu gani. Je, sio sisi wa bara tuliwaletea maendeleo nyie toka enzi za Sansui?
Yes, nimesema waislaam nyie kwani uislaam sii jamii moja wapo wenye mawazo ya kushikiwa na waarabu ambao bila vibandiko vya Ki - Oman hamjakamilika. utaniita unavyotaka lakini najua mimi ni muislaam ngazi tofauti kabisa na wewe. Naamini kutafuta elimu -Iqraa bismi rabbika - mjomba sio kutafuta usongo na watu. haitakusaidia kitu.
Toka Nyerere mmefanya mabadiliko gani? hakuna kazi kulalamika hali leo hii mna kila uwezo wa kujijenga. Maneno mengi sana lakini mmoja wenu aki-punch tu sii muislaam tena hata waislaam wenziwe sio marafiki tena.
Mimi sio ndugu yenu!... wewe na nani? maanake hata Idd mnagombea na vielimu vyenu vya kushikiwa. Tumeisha ambiwa Idd ni siku mwezi utakapo onekana (andama)... leo hii mko tayari kuipinga sayansi kwa sababu hamkuona mwezi kwa macho yenu! yaani sayansi ya 14 century, sasa kama huu sii Ujinga na kujirudisha nyuma, kuanza kusingizia waliopita tutasema nini?.
Hamuwezi ku-advance elimu zenu kufahamu kwamba sii lazima mwezi uonekane kwa macho isipokuwa kuna vipimo vinavyoweza kutuambia kuwa mwezi umeandama!.. bado mnatumia sayansi ya toka enzi za mtume na kukataa kabisa kwenda mbele. Sishangai mnapomlalamikia Nyerere.. mara Idd Amin na usivyokuwa na aibu kuupaka Uislaam mavi. Idd amin nduguyo sio mimi hilo wazi kabisa!... na kama hufahamu makomandoo wote waliokuwa mstari wa mbele kumg'oa Idd Amin walikuwa waislaam vilevile.
Huyo Mwanasiasa na Chadema mbora kuliko wewe uliyekalia kutafuta rangi za watu. Haya sasa hivi imekuwa hata kufanya kazi benki kuu ni tabaka fulani. basi watu wasiowe ama kupewa nafasi kwa sababu tu walifanya kazi sehemu moja na baba mkwe ni kabila fulani? Bado unataka yale ya kusakiziwa mke hata humfahamu kwa sababu tu ya hizo mila za kiarabu...
 
Mkandara,

Huwezi kunielewa kwasababu hutaki kuelewa kwani sioni unapata ugumu upi kujuwa kukufuru nini wakati nimekueleza kuwa kuna njia tatu kuu ambazo zinamtia mtu kwenye kufuru. Inavyoonekana wewe unabishabisha tu bila ya kuangalia maneno yako au bila ya kuelewa unachoandika. Kwa mfano unasema "Imani za dini ndio Uislaam wenyewe yaani usipokuwa na imani hizo imekuondoa ktk UISLAAM" bila ya kujuwa unaandika nini. Mimi nimekueleza kuna usipokuwa na imani hiyo tena kwa ukamilifu wa nguzo zake sita UMEKUFURU, sasa wewe inaandika eti "usipokuwa na imani hizo imekuondoa kwenye uislam" huwezi kuona unajikanganya hapa. Au ujuwavyo wewe ni kuwa mtu anakufuru tu akiwa tayari ni muislam?

Nimekueleza kuwa hili la kutozingatia nguzo za imani zinakutia katika KUFURU moja kwa moja kwa hiyo USIPOAMIN UMEKUFURUUUUUUUUU na kwasababu hiyo wewe unaitwa KAFIRIIIIIII bila kigugumizi. Haya yakwenda kwa waganga ni aina nyingine ya kukufuru hata kama mtu huyo anaonekana (na ninasisitiza anaonekana) kufuata nguzo za imani kwani huwezi ukenda kwa waganga kama hizo nguzo za imani unazielewa na kuzizingatia. Pia nimesema iko aina ya tatu ya kukufuru ambayo sioni haja ya kukueleza kama hata hizi mbili zilizo waziwazi unashindwa kuzielewa.

Ile nikuhitimishie kwa kukwambia kuwa yeyote aliyeingia kwenye kufuru yeye ni KAFIRI na si lazima mtu awe muislamu kwanza halafu ndio tuseme amekufuru. Hakuna mjadala wa kukufuru au la kwa mtu ambaye hana imani ya dini hii ya kiislam, kwani huyu amekufuru moja kwa moja na kwa hiyo ni kafiri asiyetiliwa wasiwasi. Wewe bwana vipi kujifungafunga kwa maneno bila kutaka kuelewa. NIMEKWAMBIA KUWA HILI LA KUTOKUWA NA IMANI YA DINI HII YA KIISLAM NDIYO KUFURU BABU KUBWA. Na ninarudia kuwa HIYO NI KUFURU ndio maana watu kama hawa tunawaita MAKAFIRI bila ya kigugumizi.

Tafadhali jifunze kuelewa yanayosemwa.

Tafadhali tofautisha kati ya maneno kiongozi na mwongozo. Haya ni maneno katika lugha ya kiswahili yanayotaka yaeleweke kama yanavyotumika na sioni tatizo lako hapa. Nabii Muhammad (SAW) yeye ni maulana kwetu sisi waislam utake usitake. Na yeye kuwa maulana halimpi haki ya kuabudiwa na hakuna muislam wa kweli anayemuabudu Nabii Muhammad (SAW). Ila tuna haki ya kuiga matendo yake.

Mwongozo wa Waislam ni mmoja nao ni Qur'an ambayo ndio inayotakiwa kuizingatia katika matendo yetu pamoja mfumo wa serikali zetu na sheria tunazotumia kuamuliana haki. Sasa hivyo vijiongozo unavyotaka wavijenge Waislamu wa Sunni ambavyo haviambatani na mwongozo huu ni mawazo yako ambayo hayana hoja katika dini. Kama wewe ni muislam nilipotaja mwongozo ungeelewa ninasema nini na ungejuwa uzito wa mwongozo huo katika mambo ya uundwaji na utekelezaji mambo ya jamii na serikali pamoja na kusimamia sheria zilizomo humu.

Hiyo sentenso yako ya mwisho hapo chini inakufanya usieleweke kabisa kuhusu kile unachopinga hapa. Wewe unauliza, "Sasa ikiwa Muhammad ni kiongozi wako na sio Quran kama alivyosema yeye.. Je, ameweza vipi kutuongoza ikiwa utaondoa Quran aliyotuachia kama mwongozo?" Kwanza mimi sijampambanisha Nabii Muhammad (SAW) na Qur'an tukufu popote hivyo usinizulie. Hebu nikuulize i) anayetaka mwongozo mwingine badala ya Qur'an ni wewe au ni mimi? ii) Wewe mwenyewe unahoji Nabii Muhammad (SAW) ameweza vipi kutuongoza kwa maana hiyo unasema Nabii Muhammad ni kiongozi halafu papo hapo unabisha kwa kusema si kiongozi. Pili unasema Qur'an aliyotuachia kama mwongozo halafu unabishana kuwa Qur'an ni kiongozi na si mwongozo. Bwana wewe hoja zako zinanishangaza sana!!

Darasa hili limekwisha ninalifunga kwani sina muda wa kupoteza kwako.

=Mkandara]Jizaledo,
Nini maana ya kufuru?...

Imani za dini ndio Uislaam wenyewe yaani usipokuwa na imani hizo imekuondoa ktk UISLAAM. Huu ni mwongozo kwa yule anayetaka kuwa muislaam na sii SUNNI peke yake, ni kwa waislaam wote wala hii sio SIASA.
Hapa swala la Kufuru halipo kabisa kwani waweza kuwa na imani ya dini na bado ukakufuru kwa kumshirikisha Mungu..Mifano umeitoa wewe mwenyewe - Kwenda kwa mganga kupigiwa bao..Kufuru yake ni kuwa umeshirikisha Mungu ambaye una IMANI naye kwa MUNGU MTU ambaye unaweka IMANI ya utabiri wake.

Sasa ikiwa Muhammad ni kiongozi wako na sio Quran kama alivyosema yeye.. Je, ameweza vipi kutuongoza ikiwa utaondoa Quran aliyotuachia kama mwongozo?...
 
Mkandara
Huna elimu ya mwezi kwani uislam wenyewe huujui.
Mwezi Hautizamwi kisayansi una njia zake. wala uislam sio logic unavyofikiria wewe ndio hivyo. na wala uislam haujapitwa na wakati unataka kuleta uongo kuwa karne ya 14 na sasa 21.
Mfano huwezi kuleta ushahidi wa picha kuwa fulani na fulani wamezini, kwani kwenye uislam hakuna ushahidi huo.ila kwa logic zako utasema mbona picha hii na watu wako pamoja.
jee hujawawi kuona mtu kapiga picha na simba kamshika. huku ikiwa picha imeunganishwa?
mkandara rudi tena madrasa kama unadai muislam, au kama ndio akina fulani wanaojitia waislam pale kigogo.
Nimekuuliza kuhusu waraka wa Jumbe lete jibu mheshimiwa.
 
Jizaledo,
Kufuru inakuja baada ya KUAMINI.. ikiwa wewe huamini ama huna IMANI huwezi kutumia neno kufuru isipokuwa kwa dini yake. mathlan, siwezi kusema Manasara ama Wayahudi walimkufuru Mungu kwa sababu hawakuwa na imani hizo sita. yaani hawa walikuwa MAKAFIRI. Na neno kufuru halikuanza baada ya kuwepo hizo Imani. Hata Waarabu Makureish enzi za kuamini jua walisema mtume anafanya Kufuru.. na ilieleweka kuwa madai yao sio imani sita za kiislaam. Isipokuwa mtume alikuwa na imani ya dini yao kisha akasema maneno ya kumdhalilisha Mungu jua, - Mtume hakuwa Kafiri alipoutangaza Uislaam. Hii ni sawa na kuvunja sheria ambayo unaifahamu kwa ULIMI wako.
Mengine jaza wewe mwenyewe! Kifupi rudia hoja yangu ya kwanza kuhusu Hotuba ya JK kisha angalia wapi nimesema Quran sio mwongozo.
Unajua unanikumbusha mjinga mwingine aliyeniuliza kama katiba yetu inasema nini kuhusu ndoa za wasenge.. nikamjibu.. hatuna katiba inayosema kuhusu wasenge... akaruka na kusema haaa! sasa nchi yenu inaongozwa vipi kama haina katiba!.. Yale yalee ndio unayaleta wewe hapa.
Mswahili,
Sijasema Uislaam uko nyuma isipokuwa waislaam wa kushikiwa NYIE!...mbona nchi nyinginezo wanafunga siku moja na kusali Idd siku moja?
Hee hizi za picha za Simba vipi tena ndio elimu yenyewe?....hata sikuelewi. nani kazungumzia picha na simba hapa.
 
Mkandara
Usikwepe waraka wa Jumbe.
Idd haikuwa siku moja, mfano ramadhani ilianza jumamosi, pakistani wameanza jumatatu na ni masaa mawili toka Saudia hadi pakistan, Marekani wameanza jumapili, senegal jumapili, Nigeria kuna Jumapili na jumamosi hata kama umesikiliza BBC leo Amka na BBC kuna mada hiyo kuwa Lebanon kwanini hawakuanza jumamosi na hata London kuna Idd mbili zilikuwepo.pia soma gazeti la Crescent la Mwezi uliopita kuna mada hiyo au wasiliana na jamaa wa moonsighting.com ndio maana kikakwambia uislam sio logic kama wewe ukiona mtu kapiga picha kamshika simba ukaamini kweli yule alikuwa kamshika simba, huenda ni picha ya kuunganisha. ndio nikakwambia uislam kuna vitu haifuati kama huo ushahidi wa picha. kuunita mie muislam wa kushikiwa hakuna taabu mheshimiwa.
Ombi langu waraka wa Jumbe naona unapeleka pembeni mada, ukitaka lete hata habari ya futari na daku.
 
Mkandara,
Heads up man. Mimi najisalimisha katika mjadala huu. Ukianza kumtetea Iddi Amin kwa ukatili aliofanya Uganda eti kwa sababu tu ni Mwislamu, basi mimi na wewe hatuna la kuzungumza. Nilidhani tungeweza kuelimishana katika mada hii lakini namwona Mswahili na Jizalendo ( could it be one and the same?) wana agenda yao.Nitabaki pembeni lakini nikiona uoza unazidi, basi mtanisikia.
 
Mswahili,
Waraka wa Jumbe kuna kitu gani niukwepe?...

Jamani hivi wewe unasoma nayoandika ama?.. nimeuliza kwa nini sisi Tanzania tumekuwa na siku mbili tofauti za Idd! sijasema London wamefungua lini ama Lebanon...Ukiangalia kwa makini ni uvutano wa kijinga tu hakuna sababu maalum!
Nitarudia kusema kwamba ikiwa hamna hoja inayoendeleza mambo ya Nyerere kama mada inavyozungumzia nitawaacha kizani...
Kwa sababu huu umekuwa ujinga mtupu. nazungumzia dhehebu la Sunni na viongozi wake mnarukia habari za mtume. Papa Paul ni kiongozi wa kanisa katoliki mbona hamsemi hapana kiongozi ni YESU!...Nani asiyejua nafasi ya Yesu kuweza kuitenganisha na nafasi ya Papa?...kazi kuyumbisha mada hali mnafahamu ukweli unaozungumziwa.
 
Back
Top Bottom