Kitila Mkumbo
JF-Expert Member
- Feb 25, 2006
- 3,355
- 1,955
Mkandara hicho kipande chako chatosha. Kama mtu hataki basi asaga chupe kisha---
Jasusi said:Jizalendo,
What is your point?
Mkandara,
Sema mdogo wangu, sema!
Baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bwana Jakaya Kikwete kuipa changamoto BAKWATA juu ya mali kadhaa za Waislamu kupotea mikononi mwao, Sheikh maarufu nchini, Yahya Hussein, ameibuka na kulipua bomu zito.
Sheikh Yahya ametaja majumba kibao yaliyoko Jijini baadhi yakiwa yanatumiwa na viongozi wa juu wa Serikali ambayo amedai yote yalikuwa mali ya Waislam.
Madai hayo ya Sheikh Yahya yamekuja baada ya changamoto ya Rais Kikwete aliyoitoa wakati akizungumza kwenye Baraza la Iddi el Fitr juzi Jijini Arusha.
Katika taarifa yake, Sheikh Yahya ameambatanisha vielelezo kadhaa vya kuthibitisha maelezo yake juu ya upotevu wa mali hizo za Waislamu.
Amesema kwa kuwa aliwahikuwa msimamizi wa mali za Waislamu kupitia BAKWATA miaka '96 hadi '98, anafahamu na anavyo vielelezo vya kutosha kuonyesha kile anachokisema.
Akasema Sheikh Yahya katika taarifa yake kuwa hapo kabla, Waislamu kupitia Jumuiya zao za Tanzania Muslim Welfare Society na East African Muslim Welfare Society walikuwa na mali zao kadhaa ambazo baadaye, wakati wa Serikali ya awamu ya kwanza, mali hizo ziliamuriwa kwenda mikononi mwa BAKWATA ambao nao walitakiwa wazifuatilie na kuzichukua.
Baada ya hapo, anasema Sheikh Yahya kuwa BAKWATA ilijikuta ikipoteza mali hizo nyingi, huku majumba mengine yakitwaliwa na Shirika la Nyumba NHC na mengine yakichukuliwa na watu binafsi.
Akasema Sheikh Yahya kuwa kwa sababu hiyo, anaungana na nasaha za Rais juu ya BAKWATA kusimamia vyema mali za Waislamu na kuhakikisha kuwa inajijenga upya ili kurejesha imani kwa Waislamu.
Mkandara said:Jizaledo,
Binafsi namheshimu sana Sheikh Yahya Hussein kwa sababu ambazo ni nje ya dini. Anaweza kuwa na point isipokuwa hakuziweka kiutaalam kwani Utaifishaji halikuwa swala la kidini.
Mali za watu wengi na hasa biashara zilitaifishwa na ndio maana ya kutaifisha...
Mimi nimeukubali Uislaam na hasa Sunni kwa sababu moja tu kubwa sana. Nayo ni - Hakuna binadamu yeyote kati yangu na Mungu! yaani hakuna mbora kwa Mungu kati yetu isipokuwa yule mwenye kufanya ibada.
Lakini imani hii pia imekuja na madhara yake. Moja kubwa ni la hapa duniani! Sunni hatuna kiongozi wa kidini ktk maisha ya kila siku zaidi ya kuwasikiliza walimu, graduates ama wenye elimu ya juu ya dunia kwa ushauri wao. Nje ya kitabu (quran na hadith) We can choose to listen or not! - Kila mtu na mzigo wake duniani na akhera!... Hii kkt maisha ya kuviziana kama mafisi ni hatari kubwa sana.
Till today bob sunni hatuna mwongozo zaidi ya sheikh fulani wa msikiti fulani, nje ya msikiti Sheikh hana sauti. Hii ndio sababu tumepewa chombo cha Bakwata kuweza kutusimamia kama tulivyokuwa tukisimamiwa na TMWS.
Pia hii ndiyo ilikuwa hotuba ya JK kutufahamisha majukumu yetu na chombo kama Bakwata tukitumie kwa manufaa yetu... lakini wapi! tunarudi nyumaa na kuanza kudai nyumba za Tanzania Muslim Welfare Society na East African Muslim Welfare Society, hali jumuiya za Kibaniani, Masingasinga, wazungu (wakristu) wa madhehebu tofauti wote walitaifishwa majumba.
Upanga, downtown na O'bay kote hapakuwepo na mali ya mswahili yeyote...
Mkandara said:Jizaledo,
Tunapoambiwa waislaam tujitahidi tupate kufanikisha kitu haina maana kwamba JK karudi nyumbani na atawafunga kamba wengine ili sisi tupate urahisi wa safari yenu....
Mimi nimeukubali Uislaam na hasa Sunni kwa sababu moja tu kubwa sana. Nayo ni - Hakuna binadamu yeyote kati yangu na Mungu! yaani hakuna mbora kwa Mungu kati yetu isipokuwa yule mwenye kufanya ibada. Huyo Sheikh I can challenge him/her. Lakini imani hii pia imekuja na madhara yake. Hii kkt maisha ya kuviziana kama mafisi ni hatari kubwa sana.
Till today bob sunni hatuna mwongozo Hii ndio sababu tumepewa chombo cha Bakwata kuweza kutusimamia kama tulivyokuwa tukisimamiwa na TMWS.
Mkandara said:Jizaledo,
Hakuna kufuru yoyote ktk maelezo yangu kwa sababu KUFURU ni kumshirikisha MUngu kwa njia yeyote ile. Labda wewe ndio hufahamu maana ya kufuru na tofauti ya Sunni na madhehebu mengine. Mfano niliposema:- Hakuna binadamu yeyote kati yangu na Mungu. sikuwa na maana zaidi ya kuwa Sunni hatuna MUNGU MTU. Mtu ambaye anaaminika kuwa karibu na Mungu na anaweza kukufutia madhambi ama kukuombea msamaha kwa Mungu. Ama kuuthamini kidini ukoo wa mtume na kuwafanya wawe saints ama mamlaka ktk dini...Mungu pekee ndiye anayemfahamu saint ni nani.
Najua wewe umevuka mpaka na kujiuliza kuhusu Mitume, je sio watu kati yako na Mungu?... nasema kuwa Mitume ni mwongozo wao ktk Quran na hadithi nje ya hapo hawa ni binadamu kama mimi na tunawaombea pepo vilevile.
Nimemaliza!...
Hatuna Mwongozo, haina maana nje ya kuwepo na mwongozi ktk maisha yetu ya kila siku nje ya dini..i.e POLITICS...
Kiongozi wetu ni Quran na hadithi sio binadamu.
Kabish!
quarz said:kama wewe ndugu jizaledo au mswahili manaona nyerere aliwaonea, mnaweza kwenda kufungua kesi mahakani na mpeleke na ushahidi huko,hapa kwa sasa tunaomba mtuanche tujadili SIASA.