Nataka kumshitaki Rose Mhando kwa utapeli

Rose kwa kuvuta bangi ni hataree hata vijana wake wa shooo wanaju.Dada siyo tena yule ni msaka mavumba.
 
Ninataka kumshtaki Rose mhando kwa utapeli. Tafadhari naomba wabobezi Wa kisheria hapa Ndani. Mara ya kwanza niliandaa tukio tanga hakutokea sbb alipata ajali, nilimlipa nikasamehe. Mara ya pili niliandaa tamasha Morogoro.. Nikamlipa hakutokea kwa maelezo aliyojieleza.. Mara ya tatu nimeandaa tamasha Tanga hajatokea tena mara hii nikiwa nimeandikishana nae. Kilichoniuma zaidi ni pale aliponidanganya kwa kutaka pesa zaidi na kuniambia yuko njiani anakuja nimtumie pesa ya mafuta ya Gari.. Kumbe hata wazo la kuja Kwenye tamasha. Hana mpaka sasa ameshakula zaidi ya milioni nne kwa style. Tofauti je naweza fungua kesi mahakamani. Naomba msaada. Sasa hivi nilimpigia simu hapokei..

Nanyie mnajitakia wenyewe MTU anakupiga Mara 1bado unamuamini Mara nyingine hao watu ni matapeli wa Kawaida tu......Mbona waimbaji wako wengi kwanini mnang'ang'ania hao hao
 
Pole sana kwa tatizo, naamini umeshapata msaada hadi sasa. Asikudanganye mtu eti uweke mkataba hapa! Achana na hio habari. Kama unasema hata Msama amemchoka basi samehe kwa mara ya mwisho then move forward tena kama utaweza futa kabisa huu uzi.

Nilishasikia kipindi fulani kuwa kawapiga pesa watu wa Manyara nadhani.... au kuna mtu anatumia namba yake? Mmeshaongea hivi uso kwa uso?

Ahsante kwa ushauri makini. Kuhusu hao Wa manyara sina hakika lakini Mimi mpaka naingiza huu Uzi hapa nimeshafanya jitihada nyingibna kusamehe mara nyingi nadhani nikiwa muelewa kuliko waandaji wengi.
 
Acheni kucheza na akili za watu nyie...
Kama wewe unajua umempa pesa na kuandikishiana na kwenye hiyo show hajatokea na ni mara ya tatu sijui kuna haja gani ya kutuuliza sie umshtaki ama laa...wee nawe utakua promota feki tuu hujitambui ndio maana Mshamba anakupiga mapesa hovyo!!!

Ahsante inaelekea una hekima sana ndugu.
 
yaani umemlipa mara ya kwanza hajatokea, ukamlipa tena mara ya pili, ukaona haitoshi ukamlipa ba mara ya tatu, sijawahi ona gharama kubwa ya ujinga kama hii!!
 
  • Thanks
Reactions: nao
Kwa nini huyu mtu bado mnamwamini na kumpa hizo promo angali upo ushahidi wa watu wengi kulizwa nae, sasa ifikie mahali iwe mwisho kabisa wa kumwita kwenye makongamano na kumlipa,...asialikwe tena!!
 
rose-muhando-post.jpg



Lakini nimeshawahi kumsikia mara nyingi akilalamikiwa..tatizo nini???? Kafulia au?
Nanyi wapendwa wenzake kama mnahitaji mziki wake kiasi hicho kwanini msitafute njia ya kumsaidia aenende kwa misingi ya imani yenu??? Naona inakua TOO MUCH..... ROSE ROSE ROSE doooh
 
Waliimbaga wimbo mmoja hivi hawa wasanii wa nyimbo za injili wanaimani na nini yule, wakajitanabaisha wamefanya utafiti bila kueleza sample size, methodology na rule of generalisation lastly iliwaletea mizengwe na wenzake wa cohort hiyo. Jaman usanii ni kitu cha ajabu kuna mmoja wao hataki kuitwa msanii Wa nyimbo za injili
 
Toka nimesikia ni Tapeli, hivi inawezekana watu wakaendelea kumpa kazi? Tena kwa advance payment? This is a shit.
 
hapo ndipo mtakapojua mnawahitaji sana wanasheria, wawasaidie namna ya kuandika mikataba yenu hiyo. mimi ni mwanasheria, lakini kwasababu wewe uliyeandika hapa ninakufahamu, ni mimi nimpendwa mwenzako, hakushauri achana na kupelekana mahakamani,nenda kaongee naye uso kwa uso, asipokuelewa nenda kwa mzee wake wa kanisa, asipokuelewa tafuta rafikir zake/waimbaji wenzake kadhaa waombe mwende mkasuluhishane, ....akigoma maeneo yote haya jua ni tapeli hivyo nenda mahakamani, lakini kabla haujafanya hayo usiende mahakamani kwasababu atakachokipata mahakamani (madhara) na wewe yatakuathiri. najua ninachokisema.

Kafie mbele wewe, unamtia woga mwenzako kwanini? na wewe sio mwanasheria wala nini, NI TAPELI MWINGINE TU.
 
Back
Top Bottom