Precious Diamond
JF-Expert Member
- Jun 9, 2023
- 400
- 1,005
“Sitaki kuamini kwa wasomi kama wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na vijana wengine wa Kitanzania kama sisi tunaojitambua na kujielewa, tutashindwa kuifuatilia historia ya nchi hii (Tanzania), na kwa sasa kwa sababu ya uongozi tulionao na kama kawaida ya nchi yoyote, nchi yetu inaongozwa pia na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katiba ambayo imempa kila mtu uhuru wa kutoa maoni, katiba ambayo inampa kila mwananchi nafasi ya kuzungumza analolitaka na kwa aina ya kiongozi ambaye tuko naye nikiwa nina maana ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan naye amefanya vivo hivyo, sitaki kufungua vitabu lakini uhuru huu mwanzo haukuwepo”- Mohammed Kawaida
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Mohammed Kawaida, wakati anazungumza Jumamosi Aprili 13, 2024 katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam ambapo Wasomi wa Chuo kikuu cha Dar es salaam Tawi la UVCCM Mabibo Hostel wamefanya kongamano lenye dhima ya Wasomi na Dkt. Samia Suluhu Hassan.