TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Bukoba Mjini

WEBSITE YA BUKOBA MUNICIPAL COUNCIL


52dc82350217fd69439474008f23c29f.jpg
0b96c333e40966a194926bab76b1bcfe.jpg
e59914886dab64df70298887425d51b6.jpg
04a5dce35abe52602f5b04d3e80db373.jpg
a541282633fad2d28ddfa6daeee92279.jpg
30c8dc20eeca3b8c1d7884c1c9004ea7.jpg


Website updated 2012, taarifa zote zilizopo na matangazo yaliyoandikwa 'NEW' ni ya 2012. Taarifa ya idadi ya watu ni ya sensa ya 2002 . Website haijui hata kama uwanja wa ndege ulishapanuliwa na kwasasa una lami, manispaa haijui hata kama kuna ndege zinatokea dar na kuja moja kwa moja Bukoba.

Yeyote anayetamani kuwekeza Bukoba akifungua website yetu haangalii hata mara mbili anakua keshaghairi. Sijui tunatangaza vipi fursa zilizopo, sijui tunatoa taarifa kwa wananchi wetu kwa njia gani
Idara ya IT







TUONE WENZETU WA IRINGA, MOROGORO NA KINONDONI WANAFANYAJE

46f116d0f33ec65574cb4c8fa7754a66.jpg
0e493ac0023787a01b10d2773fdcce86.jpg
21d655d03feb649e21d5e785b5a87f9b.jpg





NA TUONE BASI ENTEBBE WAMEFANYAJE

972c59a7d6931df69afadd0526dfb269.jpg
df1f656e1dfa05e6984d34de8888158f.jpg
90ffc27114bd5cfe63d5e29006ce9009.jpg
3a34a930dc34fb9f03cd0a0f180f6268.jpg
b4494f175c211d2f5b473a2c8ae69e05.jpg
01185982fe96f0f8b1616b563ada5290.jpg
dc80da7bedd16db119b726687b143266.jpg
73114f40cd1c06af427e66fa1f67aa78.jpg
98475c5696e89f318762e8746e8c862a.jpg
3f5b001c5f3208f3e39e530e9a235a7e.jpg
4f1103818450994472364559e43d49a7.jpg


Kuna vitu huonekana kuwa vidogo sana lakini vina maana kubwa kiuchumi, tusivipuuze. Tutengeneze website yetu ya Bukoba Manispaa kibiashara ili kuvutia uwekezaji na kutoa taarifa kirahisi kwa wananchi. Wananchi wanaotumia mtandao ni wengi sana

Bukoba Kazi, Amani na Maendeleo
4 years no update, viongozi waone aibu,
 
4231e422a93c363ed5519c5c6701b3af.jpg
9645c35a20a501738b9e601ba93c6658.jpg
f77d2578695004e95b4fe83660612108.jpg
fa216a10eca8dee1d6237053ffcb1ead.jpg


Huu pia ni mradi unaoendelea pia manispaa. Ni ujenzi wa jengo la kitega uchumi litakalojengwa ilipo stand ya sasa. Jengo litakua na ghorofa tisa (9) kwenda juu, pia litakua na basement na ground floor. Mradi huu hauko katika vipaumbele vya Tushirikishane.

Hatua zilizofikiwa katika mradi huu ni zifuatazo;

- Michoro, usanifu na upembuzi ya kinifu umekamilika

- Andiko la mradi limekamilika

- Ukokotoaji gharama za mradi umekamilika

- Shirika la NSSF liko tayar kwa mazungumzo ya ubia muda wa ujenzi utakapofika


Tunasubiria Inshaallah
Huu ujenzi unaanza lini na hizo hatua zimefikiwa lini dada make isije kuwa ni mambo yaliyokwishafikiwa toka miaka hiyo mpaka leo hatua ni zile zile za miaka 3 iliyopita
 
MAAGIZO KWA MH. LWAKATARE


Anaandika Ramadhan Kingi

Likumbushe Bunge kuhusu mchango wa Kagera katika kutafuta Uhuru wa Tanganyika. Wakumbushe kabisa jinsi wanavyoupuuza mkoa wa Kagera! Wakumbushe hata JPM alikozaliwa na kusomea. Lwakatare don't flinch an inch from the whole truth. Let us know kwamba Kagera must have its rightful place katika Political life! Nyerere asingelikwenda UNO kama si Kagera! Wamtafute mtoto wa Al Marhum Kandoro awape kitabu cha baba yake na humo wamtafute Mar. ALI Migeyo na mchango ws Kagera katika Mkutano wa TANU 1958. Waonyeshe kwamba tumekasirika sana. Watu wa kwanza kuwekwa jela kwa sababu ya kudai UHURU ws nchi hii waambie! Wala si Nyerere bali mar.
Ally Migeyo alifungwa! Mar. Mzee Jaafary Rwabyo alifungwa
Mar. Ayoub Rubai alifungwa. Hawakufungwa kwa wizi ama Lugumi bali katika kuutafuta Uhuru wa Nchi hii. Waulize wakutajie na wengine waliofungwa kwa kujinasibisha na TANU!
Naiweka humo na CHATU. Kwanza na hiyo Chatu inapaswa kuilipa fidia KAG3RA kwa kulelewa kwa miaka yote. Leo Chatu ni mtoto wa kambo!!! Kamsahau babu yake!!!
TELL THEM LWAKATARE tell them usiogope! You will have nothing to be ashamed of!! OTAKUPOKYA!
WAAMBIE KAGERA HAISTAHILI KUPUUZWA HASA WAKATI HUU WA TETEMEKO. Mwisho wakumbushwe kwamba hata JWTZ isingelishinda vita baina yetu na Uganda kama si umoja na uzalendo wa watu wa KAGERA. Kagera hatupendi siasa za kimzahamzaha!!!!

Mzee wa kwanza Mtanzania kumtandika kofi Mwingereza (district officer) tena ofisini mwake hapa Bukoba baada ya ukereketwa wa uhuru wa Tanganyika ni mar. Abdallah Kaluandira kwake hapo Busimbe Bukoba! Wapo wengine nitawataja ambao hawakukubaliana kabisa na matakwa ya Wakoloni. Mnaweza mkajiuliza hata wengine kwa nini ni Kamachumu tu kilijengwa kituo cha Polisi!!! Msubiri tufe halafu mje mjifarague vizuri! Lwakatare waambie!

Anaongezea LUCAS MNUBI

Ramadhani Kingi, niulize, hivi hadi leo mwezi wa pili hiyo misaada ya maafa ya tetemeko imepelekwa wap? Sio Kagera! Aah huh....Lakini, pia, ninaona una manung'uniko ya kihistoria kwa kutaja majina ya mashujaa wa kudai, Uhuru kutoka "Akagera" ambao unalalamika kusahauliwa, kulikoni, muungwana? Je, hicho kituo cha polisi cha mkoloni bado kinatumika kwa watuhumiwa wa kosa yapi? Mzee Ally Migeyo, John Rupiya na kikundi cha wahindi kutoka Singida na Dar majina yao yametwa miongoni watu waliochanga hela za tiketi ya kumpeleka mtu mmoja UNO, Tanu, wakamteua Nyerere kwa kauli "moja" kuzungumzia Uhuru. Ambapo kikundi cha wakulima Meru(Tanganyika) na Meru(Kenya) wakachangishana vihela vya tiketi ya ndege ili Japhet Krilo, Mmeru kutoka T'nyika kwenda UNO kudai ardhi ya Wameru iliyokuwa imekaliwa na masetla! Historia ipo, ila nadhani kwa sababu za makusudi, hila, roho mbaya, chuki binafsi, na elimu kama miundombuni, kuwa mikononi wa chache, bila shaka mengi zaidi au hata machache mazuri hayajawekwa wazi....juu ya nani alitamka kauli ya kwanza kudai Uhuru!
Mengine kama nini mchango wa Mkoa wa Kagera dhidi ya mikoa mingine katika kufanikisha ushindi katika kampeni ya kijeshi wakati wa vita ya 1978/79, ambayo inafahamika rasmi kama Vita ya Kagera (Kagera War) sijui ila kinachojulikana duniani, ni kwamba Kagera iliathirika zaidi (collateral damage) kwa sababu vita ilipiganiwa kwenye ardhi yake! Rudisha moyo nyuma rafiki yangu.

APOLLO LWEIKIZA anaunga mkono hoja


Mzee Joel Rweikiza Alita nyumba yake akamkabizi Mwl. Baba wa Taifa. Hapo Hamgembe akawapa TANU bure. Akumbukwi!!!!! Lol


TUNAOKOTEZA HISTORIA YA KAGERA KUTOKA KWAA WAZEE WETU
Dada hebu tusaidie utujulishe pia na ile miradi yetu ya tushiriishane kipi kimeendelea toka mwezi jana ni hatua gani imefikiwa
 
Asanteè...mbunge wa bukoba mjini kiukweli anafaa japokuwa sio mbunge wa jimbo langu ila siku moja nilibahatika kukaa naye karibu ...ana mikakatii mizitooo...tumuombee
 
Huyu mbunge ni jipu na janga jingine.
Mitandaoni haonekani, akijibu anajibu kama kakalia msumari, alitaka tumsaidie kwa pamoja lakini sahivi kila akiulizwa haonekani kokote na wala hafungui kinywa chake, yale yale na ameanza kurudia mle mle. The means justifies the end!
Sio Mbunge pekee bali pia Meya na naibu meya nao wote wamekaa kimya sana hawasemi chochote wala kujibu hoja zetu.
Hii ni dharau ya hali ya juu na ni aibu kubwa kumuona naibu meya akiwa concerned na mambo yanayoendelea kwa wenzao lakini wakashindwa kujibu hoja zilizotoka kwa wananch wao.
mi nasubiri uitishwe mkutano wowote wa wananchi na Mbunge siku hiyo watakimbia jukwaa maana sasa wameudhihirishia umma wa wanasiasa wote baba yao mmoja.
Mh. Lwakatare anatakiwa kufahamu kuwa alichaguliwa kuwa mbunge kwakuwa hakukuwa na jinsi na ili ndo tatizo kubwa ambalo linai face bukoba nadhani ni muda sasa vijana wenye machungu ya maendeleo kuanza kujiandalia njia maana huyu mbunge hiki ndo kipindi chake cha mwisho.
hatambui kuwa kuna nguvu kubwa ilifanya kazi ya ziada bila hata kumtaarifu yeye nguvu hii ilitokana na vijana wazalendo wenye tamaa ya kuiona bukoba ikipiga hatua sasa tumwambie tu kuwa nguvu ile ile itatumika 2020 kumuweka pembeni akapumzike. Tumechoka na ahadi hewa.
 
Asanteè...mbunge wa bukoba mjini kiukweli anafaa japokuwa sio mbunge wa jimbo langu ila siku moja nilibahatika kukaa naye karibu ...ana mikakatii mizitooo...tumuombee
Mikakati mingi mda wake unafikia ex.date hata kuanza haijaanza ...siku ikianza ndo muda muafaka wa kupongeza
 
Asanteè...mbunge wa bukoba mjini kiukweli anafaa japokuwa sio mbunge wa jimbo langu ila siku moja nilibahatika kukaa naye karibu ...ana mikakatii mizitooo...tumuombee

Livinus Mikakati isiyo na utekelezaji au isiyoonyesha mwelekeo ni mikakati mfu. kwenye miradi ya Tushirikishane hawakutakiwa kuji commit kuleta mikakati mizito wasiyoweza kuibeba walitakiwa waweke malengo yaliyo ndani ya uwezo wao. sioni kama hiyo miradi tajwa ina uelekeo wa kutekelezwa zaidi ni adithi za alinacha tu.
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Livinus Mikakati isiyo na utekelezaji au isiyoonyesha mwelekeo ni mikakati mfu. kwenye miradi ya Tushirikishane hawakutakiwa kuji commit kuleta mikakati mizito wasiyoweza kuibeba walitakiwa waweke malengo yaliyo ndani ya uwezo wao. sioni kama hiyo miradi tajwa ina uelekeo wa kutekelezwa zaidi ni adithi za alinacha tu.
Ni kweli unachokisema mkuu..na vizuri ata huyu mwenye mawazo ata kama hayatotekelezwaa yote ila atlest anakuja na changamoto
 
Sio Mbunge pekee bali pia Meya na naibu meya nao wote wamekaa kimya sana hawasemi chochote wala kujibu hoja zetu.
Hii ni dharau ya hali ya juu na ni aibu kubwa kumuona naibu meya akiwa concerned na mambo yanayoendelea kwa wenzao lakini wakashindwa kujibu hoja zilizotoka kwa wananch wao.
mi nasubiri uitishwe mkutano wowote wa wananchi na Mbunge siku hiyo watakimbia jukwaa maana sasa wameudhihirishia umma wa wanasiasa wote baba yao mmoja.
Mh. Lwakatare anatakiwa kufahamu kuwa alichaguliwa kuwa mbunge kwakuwa hakukuwa na jinsi na ili ndo tatizo kubwa ambalo linai face bukoba nadhani ni muda sasa vijana wenye machungu ya maendeleo kuanza kujiandalia njia maana huyu mbunge hiki ndo kipindi chake cha mwisho.
hatambui kuwa kuna nguvu kubwa ilifanya kazi ya ziada bila hata kumtaarifu yeye nguvu hii ilitokana na vijana wazalendo wenye tamaa ya kuiona bukoba ikipiga hatua sasa tumwambie tu kuwa nguvu ile ile itatumika 2020 kumuweka pembeni akapumzike. Tumechoka na ahadi hewa.
Mkuu nakuunga mkono 200%. Hawa jamaa wana matatizo sana aisee, mie sikuwepo kwenye mkutano wa bumudeco 2015 lakini muhtasari wa kilichosemwa na majukumu yalivyowekwa niliyapata walau kwa kiasi.

Hebu tuanze na BUMUDECO, na ikumbukwe Mbunge ndo alikuwa mwandaaji wa tukio hilo. Alizunguka kila kona kutangaza na kwa sifa kedekede kwamba sasa tumuamini kabadirika, sahivi yuko na wapiga kura, anataka kuwa wa mfano n.k, na baada ya hapo yakapitishwa maazimio na kwa kiasi kikubwa ofisi yake kupitia kwa mayor wake ilipewa maagizo ya kuchukua na kufanya. Cha hajabu hadi leo mwaka unaelekea kuisha hatujawahi kumsikia hata popote pale na wala kufanya mkutano jimboni kuwaambia wananchi ni nini kilipangwa ama kutoa taharifa ya utekelezaji kwa yale yaliyotokana na BUMUDECO, yeye na meya wako wamekuwa wasiri kweli kweli, wamekuwa manunda na mabubu. Ila wanasema tuwasaidie, unamsaidiaje asiyetayari kusaidika na ni wapi wananchi wakakataa kupokea habari nzuri za miradi yao wenyewe?

Likaja la pili, Leo tunaona picha za miradi ile ile iliyoletwa mtandaoni tokea 2012. Tunajua wakati ule ilikwama kwasababu ya kugawanyika kwa baraza la madiwani, lakini leo chini ya mayor b.la madiwani liko chini ya chama chake na hakuna mgawanyiko, bado mpaka leo tunaoneshwa picha, kazi imekwama nini katika baraza hili hawataki kusema. Wamemaliza mwaka sasa hakuna hata jiwe moja la msingi lililopelekwa pale site. Hawa hawa ukiwasikiliza ndo wanaochambua mwaka 1 wa JPM kafanya nini na kashindwa nini ila ukiwauliza wao wapi wameweza hapo unawatafuta ubaya, kana kwamba wao hawakupewa majukumu kwenye maeneo/kata na manispaa zao.

Sasa huyu mbunge anaweza akawa hajui kiini haswa cha yeye kupewa kura 2015. Yawezekana kasahau unyenyekevu wake alipochaguliwa na jinsi wanabukoba walivyosimama kumpigania hadi wabibi wakikesha siku 3 vituoni kusubiri kupiga kura kwenye BVR. Leo haonekani akiitisha mikutano, haonekani Jf wala kwenye mitandao akingea na waliompeleka Dodoma, ameshindwa kusahihisha makosa yake tena kwa mara ya pili. Tunakaa hapa tunamuuliza Happy maswali ambayo alitakiwa kuulizwa mbunge na timu yake chini ya meya, ila hawapo na hawako tayari.

Hakika, mwaka 2020 hautapita hawa watu hawajaojiwa. Ni Bukoba na Tabora kisiasa panajulikana, msimu mmoja waweza kutosha kuwapa wananchi kukufanyia tathimini na ukaondoka, ila kwa Lwakatare kusuka na kunyoa atachagua mwenyewe na anayo hiyo nafasi bado ya kuchagua palipo sahihi.
 
Livinus Mikakati isiyo na utekelezaji au isiyoonyesha mwelekeo ni mikakati mfu. kwenye miradi ya Tushirikishane hawakutakiwa kuji commit kuleta mikakati mizito wasiyoweza kuibeba walitakiwa waweke malengo yaliyo ndani ya uwezo wao. sioni kama hiyo miradi tajwa ina uelekeo wa kutekelezwa zaidi ni adithi za alinacha tu.
Mkuu nakuunga mkono 200%. Hawa jamaa wana matatizo sana aisee, mie sikuwepo kwenye mkutano wa bumudeco 2015 lakini muhtasari wa kilichosemwa na majukumu yalivyowekwa niliyapata walau kwa kiasi.

Hebu tuanze na BUMUDECO, na ikumbukwe Mbunge ndo alikuwa mwandaaji wa tukio hilo. Alizunguka kila kona kutangaza na kwa sifa kedekede kwamba sasa tumuamini kabadirika, sahivi yuko na wapiga kura, anataka kuwa wa mfano n.k, na baada ya hapo yakapitishwa maazimio na kwa kiasi kikubwa ofisi yake kupitia kwa mayor wake ilipewa maagizo ya kuchukua na kufanya. Cha hajabu hadi leo mwaka unaelekea kuisha hatujawahi kumsikia hata popote pale na wala kufanya mkutano jimboni kuwaambia wananchi ni nini kilipangwa ama kutoa taharifa ya utekelezaji kwa yale yaliyotokana na BUMUDECO, yeye na meya wako wamekuwa wasiri kweli kweli, wamekuwa manunda na mabubu. Ila wanasema tuwasaidie, unamsaidiaje asiyetayari kusaidika na ni wapi wananchi wakakataa kupokea habari nzuri za miradi yao wenyewe?

Likaja la pili, Leo tunaona picha za miradi ile ile iliyoletwa mtandaoni tokea 2012. Tunajua wakati ule ilikwama kwasababu ya kugawanyika kwa baraza la madiwani, lakini leo chini ya mayor b.la madiwani liko chini ya chama chake na hakuna mgawanyiko, bado mpaka leo tunaoneshwa picha, kazi imekwama nini katika baraza hili hawataki kusema. Wamemaliza mwaka sasa hakuna hata jiwe moja la msingi lililopelekwa pale site. Hawa hawa ukiwasikiliza ndo wanaochambua mwaka 1 wa JPM kafanya nini na kashindwa nini ila ukiwauliza wao wapi wameweza hapo unawatafuta ubaya, kana kwamba wao hawakupewa majukumu kwenye maeneo/kata na manispaa zao.

Sasa huyu mbunge anaweza akawa hajui kiini haswa cha yeye kupewa kura 2015. Yawezekana kasahau unyenyekevu wake alipochaguliwa na jinsi wanabukoba walivyosimama kumpigania hadi wabibi wakikesha siku 3 vituoni kusubiri kupiga kura kwenye BVR. Leo haonekani akiitisha mikutano, haonekani Jf wala kwenye mitandao akingea na waliompeleka Dodoma, ameshindwa kusahihisha makosa yake tena kwa mara ya pili. Tunakaa hapa tunamuuliza Happy maswali ambayo alitakiwa kuulizwa mbunge na timu yake chini ya meya, ila hawapo na hawako tayari.

Hakika, mwaka 2020 hautapita hawa watu hawajaojiwa. Ni Bukoba na Tabora kisiasa panajulikana, msimu mmoja waweza kutosha kuwapa wananchi kukufanyia tathimini na ukaondoka, ila kwa Lwakatare kusuka na kunyoa atachagua mwenyewe na anayo hiyo nafasi bado ya kuchagua palipo sahihi.

Ndugu Umeongea kweli tupu.
Binafsi niliudhuria kongamano la BUMUDECO mwaka jana lilikuwa ni kongamano lilikuwa na mtazamo mpana na wenye kujenga shauku kwa wengi walioudhuria wakiwa na nia ya kuona mkwamo wa kimaendeleo kwa Bukoba ukifika kikomo.
wanakagera na wapenda wmaendeleo wengi walisupport na kumuona mbunge kuwa sasa kaja kivingine lakini ukiwauliz walio wengi kama kuna uelekeo kwa kile walichokitegemea nadhani wengine watakupiga makofi. Lilikuwa ni kongamano lililorudisha matumaini mapya. nakumbuka Mzee Rugemalira alitoa taarifa kuwa alitaka kufanya uwekezaji mkubwa kwa kujenga Hospital kubwa ya moyo. sasa kinachoshangaza manispaa kwa sasa iko mikononi mwa watu wanaozungumza lugha moja hapa namaanisha kuwa Mbunge, Meya na Naibu Meya na idadi kubwa ya madiwani wanatokea chama kimoja je kama hiyo miradi yao bado haijawa na mwelekeo wanashindwa nini kusaidia na kusukuma mradi huu wa ujenzi wa hospital kubwa ambayo tayari mwekezaji tena ambaye ni mzawa yuko tayari?

Nimwambie tu mbunge wetu kuwa asione wananchi wako kimya akadhani ukimya wao unamuweka in a safe side bali atambue tu kuwa anajikaanga kwa mafuta yake na kama anatuona sisi tunaozungumza hapa akatuchukulia kama wapinzani wake basi asubiri siku akiitisha mkutano wa wananchi ndo haya haya atakutana nayo maana wengi hawana pa kuyasemea na tunaposikia tunajitahidi kuyaleta sehemu amabako tunaamini yanamfikia moja kwa moja.
 
Mkuu nakuunga mkono 200%. Hawa jamaa wana matatizo sana aisee, mie sikuwepo kwenye mkutano wa bumudeco 2015 lakini muhtasari wa kilichosemwa na majukumu yalivyowekwa niliyapata walau kwa kiasi.

Hebu tuanze na BUMUDECO, na ikumbukwe Mbunge ndo alikuwa mwandaaji wa tukio hilo. Alizunguka kila kona kutangaza na kwa sifa kedekede kwamba sasa tumuamini kabadirika, sahivi yuko na wapiga kura, anataka kuwa wa mfano n.k, na baada ya hapo yakapitishwa maazimio na kwa kiasi kikubwa ofisi yake kupitia kwa mayor wake ilipewa maagizo ya kuchukua na kufanya. Cha hajabu hadi leo mwaka unaelekea kuisha hatujawahi kumsikia hata popote pale na wala kufanya mkutano jimboni kuwaambia wananchi ni nini kilipangwa ama kutoa taharifa ya utekelezaji kwa yale yaliyotokana na BUMUDECO, yeye na meya wako wamekuwa wasiri kweli kweli, wamekuwa manunda na mabubu. Ila wanasema tuwasaidie, unamsaidiaje asiyetayari kusaidika na ni wapi wananchi wakakataa kupokea habari nzuri za miradi yao wenyewe?

Likaja la pili, Leo tunaona picha za miradi ile ile iliyoletwa mtandaoni tokea 2012. Tunajua wakati ule ilikwama kwasababu ya kugawanyika kwa baraza la madiwani, lakini leo chini ya mayor b.la madiwani liko chini ya chama chake na hakuna mgawanyiko, bado mpaka leo tunaoneshwa picha, kazi imekwama nini katika baraza hili hawataki kusema. Wamemaliza mwaka sasa hakuna hata jiwe moja la msingi lililopelekwa pale site. Hawa hawa ukiwasikiliza ndo wanaochambua mwaka 1 wa JPM kafanya nini na kashindwa nini ila ukiwauliza wao wapi wameweza hapo unawatafuta ubaya, kana kwamba wao hawakupewa majukumu kwenye maeneo/kata na manispaa zao.

Sasa huyu mbunge anaweza akawa hajui kiini haswa cha yeye kupewa kura 2015. Yawezekana kasahau unyenyekevu wake alipochaguliwa na jinsi wanabukoba walivyosimama kumpigania hadi wabibi wakikesha siku 3 vituoni kusubiri kupiga kura kwenye BVR. Leo haonekani akiitisha mikutano, haonekani Jf wala kwenye mitandao akingea na waliompeleka Dodoma, ameshindwa kusahihisha makosa yake tena kwa mara ya pili. Tunakaa hapa tunamuuliza Happy maswali ambayo alitakiwa kuulizwa mbunge na timu yake chini ya meya, ila hawapo na hawako tayari.

Hakika, mwaka 2020 hautapita hawa watu hawajaojiwa. Ni Bukoba na Tabora kisiasa panajulikana, msimu mmoja waweza kutosha kuwapa wananchi kukufanyia tathimini na ukaondoka, ila kwa Lwakatare kusuka na kunyoa atachagua mwenyewe na anayo hiyo nafasi bado ya kuchagua palipo sahihi.
Mkuu nakuunga mkono 200%. Hawa jamaa wana matatizo sana aisee, mie sikuwepo kwenye mkutano wa bumudeco 2015 lakini muhtasari wa kilichosemwa na majukumu yalivyowekwa niliyapata walau kwa kiasi.

Hebu tuanze na BUMUDECO, na ikumbukwe Mbunge ndo alikuwa mwandaaji wa tukio hilo. Alizunguka kila kona kutangaza na kwa sifa kedekede kwamba sasa tumuamini kabadirika, sahivi yuko na wapiga kura, anataka kuwa wa mfano n.k, na baada ya hapo yakapitishwa maazimio na kwa kiasi kikubwa ofisi yake kupitia kwa mayor wake ilipewa maagizo ya kuchukua na kufanya. Cha hajabu hadi leo mwaka unaelekea kuisha hatujawahi kumsikia hata popote pale na wala kufanya mkutano jimboni kuwaambia wananchi ni nini kilipangwa ama kutoa taharifa ya utekelezaji kwa yale yaliyotokana na BUMUDECO, yeye na meya wako wamekuwa wasiri kweli kweli, wamekuwa manunda na mabubu. Ila wanasema tuwasaidie, unamsaidiaje asiyetayari kusaidika na ni wapi wananchi wakakataa kupokea habari nzuri za miradi yao wenyewe?

Likaja la pili, Leo tunaona picha za miradi ile ile iliyoletwa mtandaoni tokea 2012. Tunajua wakati ule ilikwama kwasababu ya kugawanyika kwa baraza la madiwani, lakini leo chini ya mayor b.la madiwani liko chini ya chama chake na hakuna mgawanyiko, bado mpaka leo tunaoneshwa picha, kazi imekwama nini katika baraza hili hawataki kusema. Wamemaliza mwaka sasa hakuna hata jiwe moja la msingi lililopelekwa pale site. Hawa hawa ukiwasikiliza ndo wanaochambua mwaka 1 wa JPM kafanya nini na kashindwa nini ila ukiwauliza wao wapi wameweza hapo unawatafuta ubaya, kana kwamba wao hawakupewa majukumu kwenye maeneo/kata na manispaa zao.

Sasa huyu mbunge anaweza akawa hajui kiini haswa cha yeye kupewa kura 2015. Yawezekana kasahau unyenyekevu wake alipochaguliwa na jinsi wanabukoba walivyosimama kumpigania hadi wabibi wakikesha siku 3 vituoni kusubiri kupiga kura kwenye BVR. Leo haonekani akiitisha mikutano, haonekani Jf wala kwenye mitandao akingea na waliompeleka Dodoma, ameshindwa kusahihisha makosa yake tena kwa mara ya pili. Tunakaa hapa tunamuuliza Happy maswali ambayo alitakiwa kuulizwa mbunge na timu yake chini ya meya, ila hawapo na hawako tayari.

Hakika, mwaka 2020 hautapita hawa watu hawajaojiwa. Ni Bukoba na Tabora kisiasa panajulikana, msimu mmoja waweza kutosha kuwapa wananchi kukufanyia tathimini na ukaondoka, ila kwa Lwakatare kusuka na kunyoa atachagua mwenyewe na anayo hiyo nafasi bado ya kuchagua palipo sahihi.

Unafiki na siasa zisizo na mlengo ndo zinazotupeleka kusiko. Meya na baraza lake la madiwani ndo dira ya halmashauri kukiwa na meya ambaye ana vision na akawa creative basi mambo yataflow. hivi manispaa yetu imeingia mkenge kwa siasa hizi hizi unafiki pamoja na kwamba jimbo liko mikononi mwa wapinzani lakini kwenye nafasi ya meya walikosea kabisa maana, tayari Mh. Amani ni part ya ukawa na kwakuwa lengo lilikuwa ni kusonga mbele huyu ndiye alikuwa right candidate angeweza kuisukuma hii miradi kwakuwa yeye ndiye master planner wa miradi hii. Kwakuwa unafiki ndo unaowasukuma viongozi wetu sidhani kama hata kumtumia kupata consultation yake katika utekelezaji wa hii miradi kupo. kwa hali hii tusitarajie jipya unless ashuke malaika aje afutilie mbali hiki kizazi, zaidi zaidi tutegemee yaleyale ya "ABANA BASHOME"
 
MBUNGE AIOMBA SERIKALI KUONDOA KODI YA VIFAA VYA UJENZI KWA MKOA WA KAGERA KUTOKANA NA TETEMEKO

Mbunge wa Bukoba Mjini, Wilfred Lwakatare ameiomba Serikali kuangalia uwezakano wa kuwaondolea kodi wananchi wa mkoa wa Kagera kwenye vifaa vya ujenzi kutokana na maafa waliyoyapata lilipotokea tetemeko la ardhi.

Lwakatare aliyasema hayo alipokuwa akichangia mjadala bungeni kuhusu mapendekezo ya mpango wa maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na mwongozo wa kuandaa mpango wa bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2017 / 2018, mjini Dodoma.

Picha na Edwin Mjwahuzi

ab221b14e5e3b8c6024f1fb5485e6cee.jpg
 
ATHARI YA TETEMEKO LA ARDHI

Anaandika Mutalemwa Alex

Tunataka kujua kwanini serikali ya ccm inatuchukia hivi sisi wana Bukoba? Kwanini hela ya waanga na vifaa mpaka leo hatujui iko wapi? Iweje tunafungua akaunti ya maafa ya Bukoba na baada ya watu kuanza kupiga kelele kuhusu kutopewe hiyo misaada akaunti inabadirishwa jina kutoka Waanga wa Tetemeko kwenda Kamati ya mahafa Bukoba.. Je imechangwa kiasi gani na kiasi gani kimetumika kwa waanga wa tetemeko... Miundombinu serikali itumie kodi zetu nasio misaada ya waathirika wa tetemeko.. Period

Kwasasa tunaomba mvua isinyeshe kabisa maana hatuna pa kulala na nyumba zitaanguka

Geofray Kamugisha

Serikal hii hakika imeoza mtu kapigwa hasara kibao eti wao wanatoa mifuko mi5 ya cement ivi inaingia akilin kwel?. pongezi kwa mh Willbroad lwakatare kwa juhud zake za kuendelea kuwatetea wananch wa bk town

Flora Ngaiza

Kweli kabisa adi inasikitisha kwakweli mana dunia nzima imetoa mchango ajili ya wahanga wa tetemeko bk lakini kilichonishangaza nimekuta vijijini wanapewa sukari nusu kilo na mchele kilo 1 kweli kwa kila kaya na unakuta mtu anafamilia ya watu kuanzia 4 na kuendelea mh kweli serikali iliangalie ilo inasikitisha xna xna.
 
MBUNGE AIOMBA SERIKALI KUONDOA KODI YA VIFAA VYA UJENZI KWA MKOA WA KAGERA KUTOKANA NA TETEMEKO

Mbunge wa Bukoba Mjini, Wilfred Lwakatare ameiomba Serikali kuangalia uwezakano wa kuwaondolea kodi wananchi wa mkoa wa Kagera kwenye vifaa vya ujenzi kutokana na maafa waliyoyapata lilipotokea tetemeko la ardhi.

Lwakatare aliyasema hayo alipokuwa akichangia mjadala bungeni kuhusu mapendekezo ya mpango wa maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na mwongozo wa kuandaa mpango wa bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2017 / 2018, mjini Dodoma.

Picha na Edwin Mjwahuzi

ab221b14e5e3b8c6024f1fb5485e6cee.jpg
[/QUOTE

Tunamshukuru kwa kwa kuliongelea ilo lakinitunaomba tetemeko lisiwe kichaka cha kutokuendelea na malengo mengine.
kuna maisha baada ya tetemeko. kwa sasa ukiongea na Lwakatare atakwambia kwa sasa anashughulikia masuala ya tetemeko ila mi nataka nimwambie kupitia tetemeko sasa ndo ulikuwa wakati muafaka wa kuzisongesha harakati.
 
Unafiki na siasa zisizo na mlengo ndo zinazotupeleka kusiko. Meya na baraza lake la madiwani ndo dira ya halmashauri kukiwa na meya ambaye ana vision na akawa creative basi mambo yataflow. hivi manispaa yetu imeingia mkenge kwa siasa hizi hizi unafiki pamoja na kwamba jimbo liko mikononi mwa wapinzani lakini kwenye nafasi ya meya walikosea kabisa maana, tayari Mh. Amani ni part ya ukawa na kwakuwa lengo lilikuwa ni kusonga mbele huyu ndiye alikuwa right candidate angeweza kuisukuma hii miradi kwakuwa yeye ndiye master planner wa miradi hii. Kwakuwa unafiki ndo unaowasukuma viongozi wetu sidhani kama hata kumtumia kupata consultation yake katika utekelezaji wa hii miradi kupo. kwa hali hii tusitarajie jipya unless ashuke malaika aje afutilie mbali hiki kizazi, zaidi zaidi tutegemee yaleyale ya "ABANA BASHOME"
Hakuna lolote hapa,miaka mitano sio mingi mtakuja humu humu kumuuliza alichokifanya,lakini hili litakuwa fundisho na limeshakuwa fundisho kwa wapiga kura kukurupuka na kufanya maamuzi bila kuwaza mbele kutatokea nini,hii ni sawa tungemrudisha Mujuni Joseph Kataraia tungetegemea jipya gani katika yeye?ni mwak sasa hakuna mrejesho wowote?hakuna mkutano wowote?hakuna lililofanywa lolote na alikuwepo jimboni anazunguka na gari limejaa vijana tuache ushabiki wanabukoba mjini hatuitaji mtu wa kusemasema tu bungeni tunahitaji kiongozi/mbunge mwenye uthubutu ndani yakw sio kila kitu wewe uililie serikali bana
 
ANAANDIKA FAHAMI MATSAWILI


Bukoba haipaswi kuwa na njaa kuna sehemu kuna Tatizo.....

Wilaya ya Bukoba ni kati wilaya 8 zinazounda Mkoa wa kagera . kisiasa wilaya ya Bukoba imegawanyika katika majimbo mawili ya Ubunge, Bukoba Vijijini na Bukoba Mjini. Kiutawala Bukoba inaundwa na Halmashauri ya Bukoba Vijijini na Bukoba Mjini.

Katika Halmashauri ya Bukoba mjini shughuli ya kiuchumi ni Biashara, Uvuvi ziwa Victoria na Ujasiriamali.

Wapo wafanyabiashara wakubwa wana changamoto zao za kisera na kikodi ambazo ni muhimu kuzitazama kwa jicho la kuwandolea vikwazo.

Wapo wafanyabiashara ndogo ndogo na wajasiriamali kama boda boda, mama ntilie, machinga hawa nao wanazo changamoto kadhaa zikiwemo za mitaji, maeneo ya kufanyia biashara kutokuwa rafiki, kutotambuliwa rasmi..

kuna vijana wengi mfano. Fundi uashi, seremala, Fundi gereji, lakini tangu waanze kazi katika maeneo yao hawajawahi kufikiwa na viongozi wa kisiasa hivyo kwenye mipango na budget zinazopangwa bira shaka hawafikiliwi namna ya kuwanyanyua...

Wapo wananchi wanaojishughulisha na sekta ya uvuvi Wilaya Bukoba imepakana na ziwa Victoria wananchi wetu wanatumia fursa hiyo kuendesha shughuli za uvuvi.

Lakini bado wanakabiliana na changamoto kadhaa zikiwemo za kikodi, za mitaji, zana za uvuvi za kizamani, samaki kupungua ziwani, n.k

Lazima wananchi wetu wasaidiwe..

Eneo la ziwa Victoria, Ziwa ikimba na MTO Ngono, ni sehemu ambazo zina uwezekano mkubwa wa kufuga samaki wa kibiashara. Watu wanaweza kujiunga katika vikundi au wenye uwezo wanaweza kujenga mabwawa ya kufugia samaki. Kama viongozi wa kisasa watalihamasisha kwa weledi mzuri..

Halmashauri ya Bukoba Vijijini asilimia 85 ya wananchi hutegemea kilimo kuendesha maisha yao..

Wananchi wengi ni Wakulima wadogo wenye mashamba ya Wastani ya ukubwa wa hekta 1.5. Hivyo mabadiliko yoyote ya kuleta mapinduzi ya kilimo yanapaswa kuwa ni kubadilisha mashamba madogo kuwa ya kisasa...

Mazao yanayozalishwa ni pamoja na Maharage, Ndizi, kahawa, muhogo, viazi mviringo na chai.
Lazima tuweke mikakati madhubuti kuwasaidia wananchi hawa.

1. Kuwapatia Wakulima kanuni za kilimo bora kupitia kwa maafisa kilimo, mashirika binafsi kupitia semina ili wakulima wetu waweze kuzalisha kwa tija.

2. Kuanzishwe mashamba makubwa ya mfano ili kutoa Ushauri kwa wakulima kwa njia ya mashamba darasa, katika vikundi, mitandao ya wakulima na mkulima mmoja mmoja.

Matumizi Bora ya zana za kilimo. Halmashauri lazima inunue angalau trekta 20 kwa uchache kwa sababu halmashauri ina kata 29. Ili kuchochea kilimo cha kisasa na kuachana na kilimo cha mkono.

3. Uhimizaji wa matumizi ya mbolea kwa maana mbolea ya asili na viwandani kazi hii inaweza kufanyika kupitia mashamba darasa na vikundi vya ushauri...

Tunahitaji viwanda ili kuwa na uhakika wa mazao yetu lakini na viwanda vinahitaji uhakika wa malighafi za kutosha sio wa msimu mmoja hapa ipo kazi ya kufanya.
 
MCHORO WA STAND MPYA YA MABASI NA MALORI

ce47dc8eb109d99aa128db464283a466.jpg
39aab9b9c8e99f4670ec6d140080f2cb.jpg
344963ab3160294b255c4d6853dfa26e.jpg
4c7472b4fb8fc1cbf92b31a158fa296f.jpg
245e6d90a1b744316feb047b42a6b0d4.jpg
d3595bc2e40ea3f4cafa4419de6cffcd.jpg
5a00534af117a0c96fb6770afcbcc393.jpg
9317bf24acb522bb7f140de3f1f6d264.jpg
b2749ea02c321c0176987912a3bbe72b.jpg


Ujenzi wa stand pia ni kipaumbele namba moja. Kujua hatua zilizofikiwa rejea katika report ya mwezi post za nyuma kidogo
 
Back
Top Bottom