herzegovina
JF-Expert Member
- Oct 28, 2015
- 3,139
- 4,717
PASKO one thing unachokosea (labda kwa kujifanya haujui) ni kuwa ukishaingia bungeni kwa tiketi ya CCM unakuwa sio wewe tena. Huwezi kulisaidia taifa wala Serikali. Unakuwa ni daraja tu la kupitisha mambo ya Serikali kwa maagizo ya Serikali na kumsifia rais. Hiyo ndiyo kazi yako.Wanabodi,
Kila nipatapo fursa, huja na makala elimishi kuhamasisha uzalendo kwa taifa letu kupitia makala elimishi hizi za " Kwa Maslahi ya Taifa"
Swali katika mada yangu ya leo ni katika kuwapata wagombea wa CCM, Jee Vikao vya uteuzi vya CCM, vitazingatia tuu matokeo ya kura za maoni, ambayo ndio maslahi ya CCM, au navyo vitangulize mbele maslahi ya taifa kwa kutupatia wagombea wazuri, watu safi, waadilifu na wenye uwezo wa uongozi hata kama kwenye kura za maoni, wamepa kura sifuri?.
Vikao vya uteuzi vya CCM, vinakaa wiki hii, kuteua wagombea ubunge na udiwani, hivyo hili ni bandiko la ushauri, info pack kwa chama changu cha Mapinduzi, CCM, kwa kuwajulisha kuwa miongoni mwa watangaza nia kupitia CCM, kuna watu wazuri, watu safi, watu waadilifu na wenye uwezo wa uongozi waliogombea kupitia CCM na kutaka kuingia Bungeni kwa lengo la kwenda kulisaidia Taifa, Bunge, na kumsaidia JPM kwa dhati kabisa ya kusaidia kufuatia kubaini madhaifu mbalimbali ya Bunge na serikali, na kufuatia uadilifu wao, watu safi wazuri, waadilifu hawa, hawakutoa hata senti tano!, na kwa vile watu hawa hawakutoa hata senti 5!, na kufuatia ule msemo wa Waswahili usemao "Mkono mtupu haulabwi", wajumbe walifanya yao!.
Kama sasa na vikao vya uteuzi vya CCM, vitazingatia tuu kura za wajumbe na matokeo ya kura za maoni pekee, then CCM, itapoteza watu wengi safi, wazuri, waadilifu na wenye uwezo wa uongozi, lakini watakosa kuteuliwa kwasababu hawakutoa chochote na matokeo yake hawakupigiwa kura zozote na wajumbe.
Mimi ni miongoni mwa kundi hili ambaye nilitangaza nia kugombea kupitia CCM, sikutoa hata senti tano kwa yoyote, na katika kura za maoni, nikavuna nilichopanda!.
Hizi ni baadhi ya agenda zangu zilizonivutia kwenda Bungeni.
Japo wajumbe walifanya yao, lakini kufuatia trends za siasa za Tanzania kwa sasa zinaonyesha Bunge lijalo linakwenda kuwa ni Bunge la CCM predominantly, bado naamini ili Bunge hili liwe na impact ya kuisaidia serikali, linahitaji baadhi ya mijitu bold na critical thinkers ambao watakuwa critical kule Bungeni, vinginevyo kama tutajaza wapiga meza tuu kuunga mkono kila kitu, then kiukweli kabisa, Bunge lijalo lita...
Naomba nisimalizie.
Mungu waongoze wajumbe wa vikao vya maamuzi, kutuchagulia watu wazuri, waadilifu wenye uwezo ambao sio tuu watawasaidia wananchi, watalisaidia Bunge na kuisaidia serikali ikiwa ni kumsaidia Rais John Pombe Joseph Magufuli.
Mungu Ibariki Tanzania
Mungu Ibariki CCM.
Paskali
Kada wa CCM.
KUMBUKA
1. Suala la korosho Wabunge wote wa kusini waliambiwa wataondoka
2. Katika kupitisha bajeti katibu Mkuu wa CCM huwa anaenda kuangalia watoro wakiamini hawaiungi mkono bajeti
N.k
CCM siyo wajinga kuwafanyia wanachowafanyia....wanajua hata uwe na hoja vipi, hutazitumia kule bungeni. Hata uwe Profesa kule bungeni unakuwa ni darasa la tatu B