Zijue mbinu za wanawake wanazotumia kuchepuka bila kukamatwa

Simplicity.

JF-Expert Member
Dec 19, 2013
2,636
1,656
Wanaume wameleta sana mbinu za kuchepuka, kama vile hawajui wanawake ndio vinara na kuwashika inahitaji mbinu za ziada (kwa mbinu za kiteknolojia kumshika mkeo, nipm, NB: nasisitiza, ni kumshika mkeo sio girlfriend wala mchepuko).

Naweka baadhi ya mbinu ambazo wanawake wanatumia kuchepuka, na baadhi ya mazingira ambayo ni "potential" kwa wanawake kuchepuka au kuchepuliwa:

1. Kusafiri, yaani anakuambia anaenda kusalimia kumbe ameenda kwa hawara.

2. Kuwasiliana na mchepuko kama vile ni ndugu yake; stuka messages hizi: "Ahsante kaka, msalimie wifi, nitakuja nikipata muda, njoo tutembelee", wakati huyo anayeitwa kaka au ndugu humjui.

3. "Huyu ni binamu/mfanyakazi mwenzangu" - stuka, halafu mawasiliano ya mara kwa mara, ukiangalia mawasiliano ni kwa ajili gani hasa, unakuta hayana umuhimu wowote, maisha yalivyo busy hasa Dar, wewe huyo mtu anapata wapi muda wa kumwandikia mkeo messages bila interests?

4. Safari za kikazi hasa ambazo hazina maelezo ya kutosha, za ghafla au ambazo unaona kabisa kwa uzoefu wako safari kama hiyo mkeo kuipata ni ngumu - Mkeo anaenda sijui kuwakilisha kampuni/serikali/ofisi kwenye mkutano wa CEOs/au wowote ule Johannesburg, London, Paris, hata kama ndani ya nchi, wewe angalia aina ya dili, na nafasi yake ofisini, na ni wakongwe wangapi na wenye uzoefu au wanaofaa kwenye hiyo nafasi zaidi hawajaenda ila mkeo kachaguliwa - offer ya bosi, au ametangulia bosi au mkeo mwingine anafuata nyuma - stuka

4. Messages za mara kwa mara kati ya watu/mtu na mkeo, Text, Emails, WhatsApp, Facebook, Insta, Viber, Skype, JF, (Ukimkuta Badoo na JF, toa talaka hapohapo) - stuka (kumbuka mara nyingi hizo messages huonekana ni za heshima - hapa ni texts tu, za JF na kwingine ukiziona utazimia), au sijui za kuchekesha, au zile za kuforwardiana, au zenye picha hasa za kuforward (hii huwa pia ni gia itumiwayo na wanaume kumwingia mkeo, anaanza kumtumia picha, au kumwomba picha yake, au kumsifia, ukimwuuliza mkeo huyu nani, anakuambia ni classmate (tena hawa ukikuta nyumbani kwako, au mkeo akikuambia kuna classmate anataka kuja kusalimia, mwambie sawa, kisha akishakuja, kung'uta, kama una bunduki piga risasi za vidoleni) tumesoma naye muda mwingi, au mtoto wa mjomba hanifahamu, sijui wa shangazi ukiuliza undugu haueleweki - stuka.

5. Naenda vikoba au mwanamke kujiingiza kwenye makundi kama ya kukopeshana, sijui wanaita michezo, kila leo naenda kwenye mkutano wa vikoba, mchezo, n.k., - stuka. Hicho ni kichaka cha kufa mtu, mkeo anaweza kutumiwa hata hela ya kuhongwa, halafu anakuambia leo ilikuwa zamu yangu kuchangiwa.

6. Mwanaume anakuja nyumbani kwako kusalimia - mkeo anakuambia ni ndugu, cha ajabu undugu wenyewe ukiufuatilia ni wa kuunga mpaka basi au haupo, akija kazi kunyanyuanyanyua vitoto muda wote na kuviita uncle, mara kaleta pipi, sijui biskuti, mara amsifie mkeo kwa chakula, mara shemeji umependeza, mara tu anapoingia kwako - sijui shemeji waooo, wanakumbatiana, wa hivyo kama una bunduki toka nayo ndani piga risasi mguuni (Tena kama jua halijachoea mchukue mkeo na watoto mkapime na DNA kabisa).

7. Mke kila mtandao wa kijamii yupo, show-offs za kufa mtu, anapewa likes na comments na mijamaa fulani, kila post yake wapo, hasa facebook - stuka

8. Mke yupo karibu makundi yote ya WhatsApp Tanzania nzima, sijui kundi la waliosoma kimwerimweri, sijui wamama wa ukweli (Tena makundi ya wanawake ndio channel 5 ya wanawake kujifunza uozo na kuunganishwa na wanaume, sometimes kwenye kundi unalodhani ni la wanawake, wanaume ndio wengi zaidi na wanafuatilia kwa ukaribu mno, mfano namba ya mkeo mara nyingi itachukuliwa na bazazi kupitia simu ya mke wake, halafu anaanza kuwasiliana naye taratibu, kwa sababu anajua emotions na feelings za mkeo kupitia posts zake, lazima ampate). Huko wanawake wanaeleza hisia zao, halafu wanawake wengine wanawashirikisha wanaume zao, na mabazazi wanajua kwenye kundi mke yupi ana tatizo gani na natakiwa kumwingiaje ili kumpata. Ukitaka kupata mchepuko asubuhi, uwe unachungulia WhatsApp group la wanawake ambamo mkeo amejiunga, utapata asubuhi kabla ya ule muda ambao sisi UKAWA tulitaka kushika nchi. Kule wanatumiana hadi madushelele, halafu unakuta wote wanacomment, nitampata wapi wa hivi! Au unakuta mdada anapost yuko so desperate anataka wenzake wamwombee apate mume - kula kichwa, lakini stuka pia mkeo kuwemo humo. Mwambie mkeo ajitoe kwenye makundi yasiyo na msingi (kama kuna makundi ya maana wahtsapp Tz nzima, sidhani kama yanazidi kumi, ukiondoa lile ambalo mimi ni admin), akigoma, tumia njia niliyokueleza hapo juu, kuwakamata na kuwakung'uta wanawake wengine kwenye kundi - mpaka akome, tena akiwa anachat nao wanamchora.

9. Mkeo kuweka profiles pictures za utata, hii ni facebook na Whatsapp zaidi, kama vile za kusikitisha, sijui majonzi, mara za kuonyesha sehemu za mwili wake kama nyonyo, matako. Hapo ataanza kupewa mara pole, sifa, etc, kutegemea na aina ya picha, atapatikana na wanaume mabazazi kwa kujifanya wanamfariji au kumsifia, kulingana na situation - stuka.

10. Mkeo kushinda kanisani; kila leo Baba mchungaji alisema hivi, mara anaambatana na mchungaji kwenye mikutano, sijui yeye ndiye mtunza ofisi ya Baba mchungaji - ataliwa.

11. Angalia kuna watu wamezoea kuja nyumbani kwako kwa mgongo wa imani - hasa ukristo, kila leo bila sababu ya msingi, pia wamejenga mawasiliano ya karibu sana na mkeo, huwa wanaita wake za watu wapendwa - stuka

12. Mkeo kukuambia kuna kazi natakiwa kwenda kuifanya ofisini weekend - stuka.

13. Mkeo kupewa lift - hasa Dar, wewe utakuwa fala, labda apewe lift akiwa amezimia ameokotwa anapelekwa hospitalini (mbaya zaidi wewe hata gari huna) - stuka wewe fala.

14. Mkeo hataki kushirikiana na wewe kwenye mambo mengi ya maendeleo nyumbani kwako, hela zake anavyozitumia hujui, msiri, anapartner na watu huwajui au hata kama unawajua - stuka

15. Mkeo anamsifia mwanaume mwingine yoyote yule hata kama anastahili sifa kwa jambo alilofanya haiwezekani, mfano "nampendaje Steven, dah anajitambua halafu yuko smart mpaka raha", piga makofi hapohapo, labda kama ni kwenye movie, na anayesifiwa kwenye movie yuko mbali kama vile US ambako mkeo hata ka afike.

16. Mkeo anakuonyesha jeuri, hakusikilizi, hakuheshimu, anakutukana - hata kama uwe na kosa gani, mme ni kichwa - stuka.

17. Mkeo amewahi kukudanganya kwa jambo lolote lile - anacheat/anaweza kucheat au ni potential cheater - stuka.

18. Mkeo anadai uhuru wa kujiachia, kwenda atakapo, kutembelea sijui marafiki, ndugu, mara anadai unambana - mbaya zaidi anaenda sehemu bila ruhusa, halafu ukigundua anakuambia samahani nilipitiwa, ana kampani ya marafiki hawana msaada kabisa, na wala hawatakiwi kuhusiana naye, kwa sababu za kijinga (kampani ya mkeo yoyote ile isiyokuwa na mchango kwenye ustawi wa maendeleo ya familia ni uchuro) - stuka.

19. Mkeo anaimba kwaya, kila leo anachelewa anakuambia tulikuwa na mazoezi makali leo, kwaya yenyewe imejaa vijana - hasa hizi kwaya za kilutheri - ooohhooo - stuka.

20. Umeoa, rafiki yako, mfanyakazi mwenzio au mtu mwingine yeyote yule, kila akikupigia simu, anaishia kukuambia, naomba mpe shemeji simu niongee naye, nimsalimie, wanaanza kuongea halafu mkeo anacheka, yaani unamwona kabisa anafurahi kuliko hata anavyoongea na wewe, halafu ipo siku anakupigia mnaongea, sasa awamu hii anakuuliza, vipi upo ofisini au nyumbani, unamjibu ofisini, then anakuambia naomba namba ya shemeji nimsalimie, sijamwona wala kuongea naye siku nyingi - yaani wewe ndio unamuuza mkeo - kama una akili mwambie huna sababu njema wala ya msingi kutaka namba ya mke wangu - over.

21. Ni hatari kuliko unavyodhani mkeo kuwa na namba za simu za marafiki zako, wafanyakazi wenzio (wanaofanya kazi pamoja na wewe) wa ofisini, wakati hakuna kabisa jambo la msingi la kuwasiliana kati ya wao na mkeo, hasa kama namna alivyopata hizo namba inatia shaka. Au mkeo anakuambia, Batez alipiga simu anakusalimia - what? Yaani simu yako wewe haijui, na yeye ni mwanaume mwenzio? Mkeo anakujenga kisaikolojia uone mawasiliano hayo ni ya kawaida. Mawasiliano halali na yenye nia njema kwenye familia yako, yanatakiwa kupitia kwako wewe mwanaume, hasa yanapofanywa na mwanaume mwenzio. - stuka

22. Kuna mdau ameongezea mbinu ya kufuta sms (hii mbinu naijua sana), tatizo la hii mbinu kwa wanawake huwa inafeli kwa kujisahau, au mapenzi yakinoga analewa anakuwa hajali sana, pia message inaweza kutumwa ikakaa hewani, unashangaa saa mbili kamili usiku mnapata dinner mezani, message inaingia kwenye simu ya mkeo ndi ndi! Hii mbinu huwafanya wakamatwe, lakini mara nyingi watakataa hiyo message kwamba hawamjui huyo mtu, au amekosea, n.k, wachache sana watakubali hasa iwapo hiyo namba ni ya mtu ambaye hata wewe mwanaume unamjua na unaijua hiyo namba iliyotuma message kwenye simu ya mkeo, vinginevyo ataruka mita mia. Kama mkeo anatumia mbinu ya sms, dalili namba moja ni message ikiingia kwenye simu yake anaiwahi haraka vibaya mno, akiona ni ya mchepuko anadelete (ukimwuuliza hiyo message vipi, anakuambia ni message za promosheni za Tigo, huku akionekana kukerwa na usumbufu unaoletwa na messages za namna hiyo), akiona ni message njema, hadi wewe atakushirikisha ikiwezekana kwa kukuonyesha ili kuendelea kukujengea imani. Pia wanawake hawa simu zao zina password, hasa wanaotumia android, wanatumia kitu kinaitwa "patterns". Ukimwuuliza kwa nini hiyo pattern, anakuambia inaweza kuibiwa, kwa hiyo mtu hataweza kuchukua taarifa zangu! - stuka

23. Mbinu ambayo ni advanced na ina mafanikio sana kwa wanawake ni "physical meeting", hii ni kwamba mwanamke anaupa mchepuko onyo kali, hakuna hata siku moja kutuma message wala kupiga simu, mambo yote tutapanga kwa kukutana tu. Hii inafanywa na wafanyakazi katika ofisi moja - yaani mke na mchepuko wake ambao wana uhakika wa kuonana siku za kazi. Na kwa sababu haiwezekani kabisa kuepuka mawasiliano, mwanamke mchepukaji makini hutoa onyo kwa jamaa kwa kumwambia, never ever, usinipigie isipokuwa mimi ndio nitakutafuta. Ikitokea jamaa amepiga, kwa sababu mapenzi huwa yanaleta ulevi, mke hupokea simu kwa wasiwasi, halafu unaona jamaa ataongea maneno kama vile "vipi familia haijambo, jamaa kaenda kazini au yupo, jana uliniambia mtoto wako anaumwa, anaendeleaje, n.k", hapo jamaa anasearch kama mke yupo mwenyewe au na mmewe, majibu ya mwanamke yatamwoonyesha, ndipo mission halisi huanza. - stuka.

Sasa naomba wanawake waje, watupe mbinu mbalimbali wanazotumia kuchepuka na mazingira ambayo wao kwa uzoefu wao huwasababishia kuishia kuchepuka. Kuwa "honest" ili tusaidie kunusuru ndoa zinazovunjika kila siku. Nitaendelea kuongeza kwenye list kadri michango itakavyotolewa na kadri nitakavyoendelea kubaini kwa mjibu wa uchunguzi wangu - kumbuka pia kuna interview naendelea kuifanya huku kitaa, kuhusiana na mbinu za wanawake za kuchepuka.


Yafuatayo ni maoni yangu:

NB: Biblia ina huu msitari:

"Enyi Wanaume Ishini na Wake Zenu Kwa Akili".

Naamimi kabisa Mungu anatambua mwanaume yoyote mwenye hekima na busara, anaposoma au kukumbuka huu msitari anatakiwa amalizie mwenyewe kipande alichokiacha Mungu kwa kuusoma kama hivi:

"Enyi Wanaume Ishini na Wake Zenu Kwa Akili, kwa maana Hawana Akili".

Unajua kabisa Mungu asingeweza kufanya hivyo, maana jinsi hawa watu wanavyodai haki sawa, duniani pasingekalika!


Biography

Simplicity. Is a social capitalist, author of conflicting ideas, a science researcher and advocate, a primer sexologist, and a comic who likes reading and writing from disguise. He is actively involved in one of the world's top researches believed to outpouring the course of human destiny. He is married with three children, who he believes they are responsible for elicitation of the future generation of thinkers. He has since his marriage been living intimately and happily wife his wife, Shasha, who occasionally blows dazzling emotional signals of love which Simplicity. remarkably acknowledges with a spectrum of smile. He understands that a wife is like a dormant insurgence of a legal marriage regime who can one day fiercely burst with fires that can consume an iced island. He doesn't believe that North Korea will one day neither blast America nor be the cause of World War III, but strongly supports the assertion that the World War IV will erupt from the intense fire ejected from a divorced woman's heart. He is currently authoring two innovative books, namely; “Devil is Too Good to be Blamed” and “ A brief History of Mysterious Time”. Simplicity. has however, authored a famous book, entitled “The Paradox of Woman Heart”, which no one else read it except himself.
 
Kumbuka: Ni uzi wangu wa mwisho, nitaandika uzi mwingine mwakani, msilalamike ni mrefu. Isipokuwa nitaendela kuupdate huu uzi.
Muheshimiwa Mkuu Simplicity nakupa salute na heshima tele,mtu yeyote mwenye uelewa hata kidogo tu anatakiwa akupe shukrani na kukupa BRAVO,mimi nadiriki kusema wewe umekwenda shule na pia PSYCHOLOGY ni somo lako uliolimudu,hakika wewe unajua akili ya binadamu inafanya kazi vipi,nashindwa sijui nikushukuru vipi kwa somo uliotupa,sababu litaokoa majanga ya KUTALIKIANA ,sababu wanawake ni wepesi KURUBUNIWA,yaani wakisifiwa plus viji trick fulani fulani na pia wakionyeshwa SIMPATHY kwa kiwango fulani,basi wako tayari kulipa hisani kwa KUPANULIWA mapaja.
 
Ndefu kama notes za History ll.
Mkuu Head Prefect,nakusalimu kwanza,naomba niweke wazi jambo fulani hapa jukwaani hasa kwa sisi hasa mimi mkurupukaji wakati mwingine, ni hivi huwa tunawakosea watu bila sisi kujitambua,sababu hatutulii na kusoma katikati ya mistari, hii husababisha sisi kujibu upupu wakati mwingine ingawa sio wakati wote,nisiandike maneno meengi na kuwachosha wana jukwaa letu, ni hivi nimegundua baadhi ya wachangiaji humu wamekwenda shule vizuri na wanastahili kuungwa MKONO na wala sio KUBEZWA, mfano ni huyu ndugu yetu Simplicity, hanijui simjui lakini nimemkubali, sababu ametumia muda wake wa thamani kutuelimisha wanaume na wanawake wa jukwaa hili elimu ambayo ni nadra kuipata out of a nutshell, nina majina ya wachangiaji humu jukwaani ambao sintawataja sasa hivi ila hapo baadae.halafu tutawapongeza na kuwapa sifa zao ambazo ni haki yao bila kudanganya au kuwaonea wivu.
 
ccd3fb2453272624086a2132dc5a55b6.jpg
Pata kitabu changu hiki na hakika uchepukapo utakuwa salama!
 
Andika Na Mbinu za wanaume kuchepukaa bila kukamatwa
.USITUZINGUE TUKAKUZINGUA...Balance Story....wanawake wamekukosea nini Kaka Simplicity??
Hey we binti mtake radhi SIMPICITY sababu anaokoa wanawake na wanaume,yeye kaongelea jinsi nyie wanawake mnavyodanganywa na wanume mpaka mnahatarisha ndoa zenu,na pia anawaelimisha wanaume kuacha LAANA ya KUVUNJA NDOA ZA WATU.
 
Damnt...hiyo #6 kuna siku niliitendea haki..Bajaj driver niliekuwa namtumia tumia kwa safari za hapa na pale kuna siku alijifanya yeye mwema sana eti anampa mwanangu wa miezi9 hela ya soda,tatizo haikuwa kumpa ila kiasi alichompa ndio kina ukakasi,unampa mtoto wa miezi9 Tsh 10,000/= kwa ajili ya soda ye soda hizo atazinywea wapi kama sio kutafuta kuzoeana na mke wangu chukua kikaratsi chako potea huku nimenyanyua kipande cha tofali..na alimpa huku anamsifia sifia wife kwa uzao wake huo huku anacheka cheka,nilimpa maneno magumu hakukaa kukatiza tena mtaa nnaoishi.hawa watu huwa wanajifanya kuwapa watoto vijisent vya soda sijui pipi ili kutafuta chance ya kuzoeana na mama zao ili iwe rahisi kumwaga verses zao ovu.
 
Back
Top Bottom