Yajue magonjwa kumi hatari zaidi duniani

Bitoz

JF-Expert Member
Aug 27, 2015
30,823
126,539
Kuna usemi kwamba afya ni uhai pia mtaji wa maskini ni nguv zake ikimaainisha afya njema huchangia mtu kuwa na maendeleo maana ukiwa na afya mgogoro basi utapoteza muda na pesa nyingi kujiuguza
Basi leo nawaletea magonjwa 10 hatari zaidi duniani kwa kupeleka watu wengi makaburini
IMG_20180808_120526.jpeg

NB:
Mimi siyo daktari wala mtu wa kada ya afya maana niliishia darasa la 5 hivyo nimejitahidi tu kutumia lugha ya kitabibu ingawa naweza kuwa nimekosea hivyo ni jambo la kawaida tu
...................... .................................................


10/Malaria
89def69c7699fa2385d1b874d9b55c57.jpg
c2ad3636cbde27518bcbdfe455b08fd5.jpg
210b4c44e68021eb5ddeda43623af06f.jpg

Huu ugonjwa huenezwa na mbu jike aitwaye Anopheles
Unashambulia zaidi bara la Afrika kutokana na hali ya kijiografia ambayo ni ya kitropiki
Mnakumbuka serikali ilianzisha kampeni ya kugawa vyandarua vya dawa....watu wailiishia kuvulia kambale tu maana hakikueienea kitandani
Kama unaishi Dar na hujawahi kuugua malaria basi labda una seli mundu

Husababisha vifo takribani Milioni 1 kila mwaka
 
9/Kifua Kikuu
f425f37e59ab36d35f202df87d1beb01.jpg
0a355dd8ef402d74feb31c9c03cfefa2.jpg
667c9d03c3bfac5f880bd49bc3575e19.jpg

Aliyefananisha penzi na kikohonzi hayuo serious
Huu ugonjwa huenezwa na bacteria kwa njia ya hewa...huathiri zaidi mapafu lakini pia huweza kuenea hadi katika viungo zingine
Mgonjwa hupoteza uzito kwa kiwango kikubwa
Kuna uhusiano mkubwa kati ya Kifua Kikuu na mtu kuwa na VirusiVya Ukimwi

Husababisha vifo 1.4 Milioni kwa mwaka
 
8/Saratani
7b6cbe30a0192bb0edc5620ccc4e3f79.jpg
dfaef5b80eaaae737ce987fc2b740c54.jpg
d47179e73307edbbb68c4313de9d627a.jpg
Saratani kutokea pale seli zinaposhindwa kufanya kazi(kufa}..ikumbukwe viungo vyote kwenye mwili wa binadamu vimeumbwa kwa seli hivyo basi kila kiungo kina saratani yake, wanawake hushambuliwa na saratani ya matiti na kizazi wakati wanaume ni tezi dume(hii inamtesa mzee Majuto)
°saratani ya ubongo
*saratani ya ngozi
*saratani ya kibofu
*saratani ya shingo ya kizazi
*saratani ya damu
*saratani ya utumbo
*saratani ya kinywa
n.k
Saratani husababishwa na sababu za kibaolojia. uvutaji sigara n.k
Ugonjwa huu ndo ugonjwa uliowaua Kambarage Nyerere,Daudi Balali,Samwel Sitta huku Jakaya Kikwete akiponea chupuchupu kwa saratani ya tezi dume baada ya kuwahi matibabu

Husababisha vifo 1.5 milioni kwa mwaka
 
7Ukimwi
d939c21fee5fb1b024f904eaa249eb34.jpg
5e3db1bedf4f13e66ce5a920d9c16420.jpg
91980670fcf88e416829633c389aa23f.jpg

Ferouz alikiri wazi kwamba starehe zimemponza ila MwanaFA kwa umbea akasema marehemu alikufa kwa ngoma
Siku hizi kila mtu ni bonge sasa sijui utamtambuaje
Ugonjwa huu huenezwa zaidi kwa kujamiiana(hatuachi ng'o)
Hadi sasa ugonjwa huu hauna tiba/dawa bali una kinga(kondomu)....
Zamani mtu akiugua hili gonjwa ilikuwa ni rahisi kumjua ila siku hizi ARV zimewafanya watu wanenepe na kupunguza vifo vya mapema

Huua watu 1.8 Milioni kwa mwaka.
 
6/Kuhara
948d6b498e217bc79704d5452d0a0c8e.jpg
b1d532a16544652a9b44ea8dadf1b55f.jpg
5a5b039b379e927131654be7e0b94bb2.jpg
Kuhara kwa kawaida humshambulia mtu kwa siku 1 hadi 2...
Gonjwa kuu la kuhara ni kipindupindu
Sisi tunaoishi uswahilini kuharisha siyo kesi ni kama fasheni tu...tunaharisha siku mbili tatu kisha tunaendelea tu kudunda
Kuhara husababishwa na kunywa maji yasiyochemshwa,kula vyakula vichafu n.k
Ukiumwa kipindupindu ujue umelishwa kinyesi na nzi au mikono yako mwenyewe


Huua watu 2.5 Milioni kwa mwaka
 
5/Vifo vitokanavyo na uzazi
73fb3c33c2651a8a898b01c24d3a05f9.jpg
14484ef0effe186a0a0d50aa9a036c88.jpg
097e453f610767cc52520dd6331d6edc.jpg

Kuna usemi kwamba ujauzito ni nusu ugonjwa
Kilichomtokea mke mdogo wa Mzee Yusuf juzijuzi hapa kila mtu anakijua...inasikitisha sana
Vifo vinavyoongelewa ni vya mama wajawazito pamoja na vya watoto wachanga wakati wa kujifungua
Huathiri zaidi nchi maskini kutokana na huduma mbovu za afya na elimu duni ya masuala ya uzazi

Kina mama nusu Milioni na watoto zaidi ya 2.5 milioni hufariki kila mwaka jumla ni vifo 3+ milioni
 
4/Ugonjwa wa Mapafu
74ce9efaa39d7d0e1879377b86d12a1d.jpg
adba2c7eb54666db53a80c5da9bf9f62.jpg
89307dee215699aca60ec5899e865316.jpg

Mwana vuta tu sigara maana mapafu ni mali yako pia sigara unanunua kwa pesa yako ila elewa tu huo sio ujanja na mapafu yako yamejaa masizi kama sufuria la maharage kwenye jiko la kuni
Unafahamika zaidi kitaalamu kama CORD..Unaweza kuwa wa muda mfupi au muda mrefu
Uvutaji sigara huchangia kwa kiasi kikubwa mtu kuugua huu ugonjwa

Unaua takribani watu 3.3 milioni kwa mwaka
 
3/Maambukizi katika njia ya upumuaji
6ace91a8665d6b74db3dd1155575b5ae.jpg
679340a8dcef66d18bf425854fb5bbf6.jpg
462f9c5f9338b7c37dbcfe4b5fb71377.jpg
Hakuna mswahili asiyeujua ugonjwa wa pumu
Pia juzijuzi kuna mwanaJf mwenzetu kapoteza maisha kutokana na maradhi ya upumuaji{RIP Ibra)
Huu ushambulia mfumo wa upumuaji...Unaweza kuwa pneumonia au bronchitis
Tunasisitizwa kufanya mazoezi,kula vyakula salama kwa afya,kuishi kwenye nyumba zenye hewa swaafi yaani madirisha yanayoruhusu hewa kupita,pia tupandikize miti nyumbani,kuepuka kazi za vumbi n.k
Ndiyo ugonjwa uliowaondoa mapacha maarufu na vipenzi vya watu Afrika Mashariki akina Maria na Consolata Mwakikuti

Husababisha vifo 3.5 milioni kwa mwaka
 
2/Kiharusi
798c612b1a0645caf0fe710ccf511384.jpg
63cb8f18b31553253559cb7023613882.jpg
f814f321bcc4bd3f3cd4789d00f24fdd.jpg

Huu ugonjwa ni janga bora tu uitwe kimsiba badala ya kiharusi
Kitaalamu unaitwa Stroke kwa Lugha rahisi ni kupoozaIkumbukwe ili ubongo iweze kufanya kazi unahitaji hewa ambayo husafirishwa kupitia kwenye damu hivyo chakula cha ubongo ni damu sasa kiharusi hutokea pale damu inapofeli kufika ubongoni au kufika chini ya kiwango kwa sababu mbalimbali mfano mishipa kupasuka, shinikizo la juu la damu n.k
Mgonjwa wa kiharusi sio tu hupooza mwili bali pia akili{kupoteza kumbukumbu)

Ugonjwa huua watu takribani 6.1 milioni kwa mwaka
 
1/Ugonjwa wa Moyo
b378472f83def2fdc74aa99004b9185c.jpg
e9ba76c22b502f6f5d48ce5cf401aa56.jpg
f4219b9d1eaf7b45d9379072b7dfd0a5.jpg
Moyo ndo injini ya mwili na waswahili husema kazi ya moyo ni kusukuma damu ..kupenda ni kiherehere
Huu ndo ugonjwa mbaya zaidi duniani..huweza husababishwa na sababu mbalimbali km vile,.. kisukari, shinikizo la jyu la damu na uzito uliopitiliza
Kwa kugundua uzito wa tatizo hili serikali imeanzisha Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete pale Muhimbili
Ndio ugonjwa unaomsumbua yule tajiri wa Yanga ila bwana yule na jamaa yake hawamwonei huruma wamekomaa tu na Mhindi wa watu na kufikia hatua kumpa kesi ya kubwia unga

Huua watu takribani milioni 7.2 kwa mwaka
.
.
................ ....................... ........... .. ...............
Baada ya kufuatilia nimegundua list ina upungufu kwa kutoutaja ugonjwa mmoja uitwao Kisukari ambao unatajwa kusababisha vifo vya watu takribabi 1.5 milioni kwa mwaka
Pia ugonjwa wa kisukari husababisha watu wengi kuisji na vilema kutoana na kukatwa miono au miiguu na viungo vingine kaa vile vidole
.........................................................................
.
.
.
.
.
Mwisho
The Bitoz
................
 
Back
Top Bottom