ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 44,987
- 51,812
Serikali iliwahi kusema inatumia Bil.550 Kwa mwaka Kuagiza magari, vipuri, mafuta na matengenezo Kila mwaka.
--
Akijibu swali la Mbunge Asia Abdulkarim Halamga aliyehoji sababu za Serikali kutumia Wakala wa Huduma za Ununuzi Serikalini (GPSA) ambaye ananunua Magari kwa gharama kubwa kuliko bei ya Soko la Dunia, Waziri wa Fedha, Dkt, Mwigulu Nchemba amesema Serikali inatazamia kuanza kuwakopesha Watumishi wenye sifa ili kuondoa mzigo wa Mafuta na Matengenezo Serikalini.
Kuhusu utaratibu wa kuagiza Magari moja kwa moja Viwandani badala ya kutumia Mawakala, Dkt. Mwigulu amesema "Kuna baadhi ya mazingira yanaruhusu Serikali kununua kwa mawakala, pia, baadhi ya Viwanda havipendi wanunuzi waende moja kwa moja Viwandani".
Kwa mujibu wa taarifa iliyowasilishwa na Wizara ya Fedha Bungeni mwaka 2022, Serikali ilikuwa na Magari 15,742, Pikipiki 14,047 na Mitambo 373 huku ikitumia zaidi ya Tsh. Bilioni 500 kila mwaka kwaajili ya Ununuzi wa Magari mapya, Mafuta, Vipuri na Matengenezo.
My Take
Naona Kuna kigugumizi Cha kuchukua maamuzi.
Toka mwaka juzi mnaongelea hili jambo na hamfiki Muafaka.
Semeni kama Serikali kwamba deadline itakuwa lini? Na Je Madereva mtaajiri wa Umma au Kila boss na dereva wake?
--
Akijibu swali la Mbunge Asia Abdulkarim Halamga aliyehoji sababu za Serikali kutumia Wakala wa Huduma za Ununuzi Serikalini (GPSA) ambaye ananunua Magari kwa gharama kubwa kuliko bei ya Soko la Dunia, Waziri wa Fedha, Dkt, Mwigulu Nchemba amesema Serikali inatazamia kuanza kuwakopesha Watumishi wenye sifa ili kuondoa mzigo wa Mafuta na Matengenezo Serikalini.
Kuhusu utaratibu wa kuagiza Magari moja kwa moja Viwandani badala ya kutumia Mawakala, Dkt. Mwigulu amesema "Kuna baadhi ya mazingira yanaruhusu Serikali kununua kwa mawakala, pia, baadhi ya Viwanda havipendi wanunuzi waende moja kwa moja Viwandani".
Kwa mujibu wa taarifa iliyowasilishwa na Wizara ya Fedha Bungeni mwaka 2022, Serikali ilikuwa na Magari 15,742, Pikipiki 14,047 na Mitambo 373 huku ikitumia zaidi ya Tsh. Bilioni 500 kila mwaka kwaajili ya Ununuzi wa Magari mapya, Mafuta, Vipuri na Matengenezo.
My Take
Naona Kuna kigugumizi Cha kuchukua maamuzi.
Toka mwaka juzi mnaongelea hili jambo na hamfiki Muafaka.
Semeni kama Serikali kwamba deadline itakuwa lini? Na Je Madereva mtaajiri wa Umma au Kila boss na dereva wake?