Waziri Dkt. Stergomena Tax Asimulia Kuanzishwa kwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ)

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
2,033
974

DKT. STERGOMENA ASIMULIA KUANZISHWA KWA JESHI LA WANANCHI WA TANZANIA (JWTZ)

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax amesema Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) limepitia hatua mbalimbali za mabadiliko mara baada ya uhuru wa Tanganyika Disemba 9,1961 ambapo miongoni mwa mabadiliko hayo ni maasi ambayo waliyafanya kwenye Jeshi la wakoloni

Dkt. Stergomena ameyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika kuelekea maadhimisho ya miaka 60 ya Mungano wa Tanganyika na Zanzibar

Dkt. Stergomena amesema wakati huo Jeshi la JWTZ lilikuwa likiitwa Jeshi la Tanganyika hivyo Januari 20, 1961 katika kambi ya Colito ambayo sasa ni Lugalo wanajeshi wa Tanganyika walifanya maasi kwenye Jeshi ya kikoloni na maasi hayo ndio yaliyopelekea kuanzishwa kwa Jeshi la wananchi wa Tanzania(JWTZ)

Dkt. Stergomena amesema maasi hayo yalitokana na Jeshi la Mkoloni kuendelea kushikilia uongozi wa Juu wa Kijeshi kwa kutetea dola ya kikoloni japo kulikuwa na mabadiliko ya uongozi wa bendera ambayo waliwakabidhi Jeshi la Tanganyika
 

Attachments

  • FN5L-LdXIAUTlsUNBVCFTRE.jpg
    FN5L-LdXIAUTlsUNBVCFTRE.jpg
    71.9 KB · Views: 6
uongo na porojo tupu, jeshi la kikoloni maana yake ni royal british armed forces ambapo commander in chief ni english monarchy sasa hawa kolokoloni wakafanye uasi mbele ya british armes forces?
 
uongo na porojo tupu, jeshi la kikoloni maana yake ni royal british armed forces ambapo commander in chief ni english monarchy sasa hawa kolokoloni wakafanye uasi mbele ya british armes forces?
Una wakati mgumu sana na taarifa hizo.

Ugumu huo ni wakujitakia, wa makusudi na hauna nafasi Tanzania.

Hamia Burundi.
 
Una wakati mgumu sana na taarifa hizo.

Ugumu huo ni wakujitakia, wa makusudi na hauna nafasi Tanzania.

Hamia Burundi.

hata logic ya kawaida tu inakushinda, jeshi la tanzania lilianzishwa kwa 100% na wakoloni kilichofanyika ni kubadilisha jina tu ktk kdf kwenda jwtz lkn kila kitu kilibakia na kimebakia jinsi kilivyo sasa mtoto aende kupindua british armed forces iliyo command english empire yote ? mnadanganywa sana, kwanza jeshi lenyewe kila kitu msaada ktk kwa hao hao halafu eti wakawapindue?
 
hata logic ya kawaida tu inakushinda, jeshi la tanzania lilianzishwa kwa 100% na wakoloni kilichofanyika ni kubadilisha jina tu ktk kdf kwenda jwtz lkn kila kitu kilibakia na kimebakia jinsi kilivyo sasa mtoto aende kupindua british armed forces iliyo command english empire yote ? mnadanganywa sana, kwanza jeshi lenyewe kila kitu msaada ktk kwa hao hao halafu eti wakawapindue?
hata logic ya kawaida tu inakushinda, jeshi la tanzania lilianzishwa kwa 100% na wakoloni kilichofanyika ni kubadilisha jina tu ktk kdf kwenda jwtz lkn kila kitu kilibakia na kimebakia jinsi kilivyo sasa mtoto aende kupindua british armed forces iliyo command english empire yote ? mnadanganywa sana, kwanza jeshi lenyewe kila kitu msaada ktk kwa hao hao halafu eti wakawapindue?

Kwani haya mashindano ya Insha? Kha.

Ndio nimesema, una wakati mgumu kweli. Hata Ukisema nini, Jeshi ni la Watanzania.

Hamia huko Uingereza, wanakupenda sana.
 
Kwani haya mashindano ya Insha? Kha.

Ndio nimesema, una wakati mgumu kweli. Hata Ukisema nini, Jeshi ni la Watanzania.

Hamia huko Uingereza, wanakupenda sana.

hahaha mara hii tu umeshamsahau toni blair? sasa nani ahamie huko uingereza labda?
 
Back
Top Bottom