Bitoz
JF-Expert Member
- Aug 27, 2015
- 30,823
- 126,539
Hapa Tanzania Hasheem Thabeet ni maarufu kutokana na urefu wake aliojaaliwa na Mwenyezi Mungu
Pia kuna jamaa fulani mwaka juzi alikuwa gumzo baada ya urefu wake kumzidi kabisa Hashim kiasi cha kushindwa kupatiwa matibabu ya mifupa pale Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI}. Na ndiye anaaminika pengine kuwa ndiye Mtanzania mrefu zaidi mpaka sasa.
Pia kuna jamaa fulani mwaka juzi alikuwa gumzo baada ya urefu wake kumzidi kabisa Hashim kiasi cha kushindwa kupatiwa matibabu ya mifupa pale Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI}. Na ndiye anaaminika pengine kuwa ndiye Mtanzania mrefu zaidi mpaka sasa.
Unamfahamu Manute Bol ?
Anatajwa kuwa ndiye mcheza mpira wa kikapu mrefu kwenye historia ya NBA
Jamaa alikuwa akitaka kufunga anajifungia tu kama kuweka hela kwenye mkono wa shati ila urefu wake ulikuja kumsababishia matatizo makubwa ya mifupa na huo ukawa mwisho wake wa kucheza kikapu.
Sasa leo nakuletea watu kumi warefu kuwahi kuishi duniani
"""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""
Futi 1 = Inchi 12
Inchi 1= Sm 2.54
Futi 1 = Sm 30.48
==================
10/Brahim Takioullah
Ni raia wa Morocco aliyezaliwa mnamo mwaka 1982
Huyu jamaa anashikilia rekodi ya dunia kwenye Guinness Book of World Records ya mtu mwenye miguu mirefu zaidi duniani anayeishi
Pa ndiye mtu wa pili wa muda wote mwenye miguu mikubwa zaidi kuwahi kutokea duniani(nazungumzia makanyagio) miguu yake ina urefu wa inchi 15 yaani kiatu kinatakiwa kiwe hivyo kwahiyo jamaa ili apate kiatu lazima aweke order
Huyu jamaa sababu ya urefu wake ni uvimbe(tumor) ambao umeathiri tezi(gland) na kumfanya awe ngongoti
Ana urefu wa Futi 8 na inchi 1