Watoto wa kike wanaokosa malezi ya baba wapo hatarini kuanza matendo ya ndoa katika umri mdogo na kupelekea mimba za utotoni

Nov 6, 2016
89
221
WATOTO WA KIKE WANAOKOSA MALEZI YA BABA WAPO HATARINI KUANZA MATENDO YA NDOA KATIKA UMRI MDOGO NA KUPELEKEA MIMBA ZA UTOTONI

Na Comrade Ally Maftah
KING OF ALL SOCIAL MEDIA

Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali inaonyesha kwamba mtoto anayekosa malezi ya baba anakuwa hatarini kupata mimba za utotoni kutokana na kujiingiza katika shughuli za kimapenzi na matendo ya ndoa mapema.

INATOKEAJE
Baba anaweza kumchelewesha mtoto kuanza ukaribu na wanaume au kifupi mpenzi wa kwanza wa mtoto wa kike huwa ni baba yake mzazi, hapa elewa vizuri, madeko ya mtoto wa kike ya kwanza huanza kwa baba yake ndio maana unaweza kukuta mtoto anapokuwa mdogo anamsogelea zaidi baba yake na kumkumbatia pamoja na kumbusu hapo mtoto anakuwa ameanzisha hisia za kimapenzi ambazo si mbaya kwa sababu bado hazijaanza kuathiri mwili,

Mtoto anapokosa malezi ya baba basi anatafuta nafasi ya kudeka na kupeleka hisia zake za kwanza za kubembelezwa, ndipo anapojikuta mikononi mwa haramia moja mtaani au shuleni, haramia hilo likitumia hiyo nafasi kiubinafsi bila huruma linamtia mimba mtoto huyo. katika mazingira hayo mtoto huyo anakuwa hajui kama anolifanya ni kosa la kihisia, na kujikuta tayari kanasa mimba.

WITO WANGU
Wanawake ambao nimekuwa nikiwasikia mkihamasisha huu uhuni wa SINGLE MOTHER mkisema kwamba mnaweza kulea watoto wenyewe nawaomba muwe wastaarabu, sio kwa sababu wewe umeshindwa kudumu kwenye ndoa kwa sababu ya mapungufu yako, kutokuwa na hekima na heshima kwa mumeo, au kutokana na changamoto mbalimbali pengine ulijikuta upo kwenye ndoa na mwanaume wa hovyo, au ulianzisha mahusiano na mume wa mtu, usiwahamasishe wenzako kuwa single mother.

Mimi nilipata kusikia sauti ya kwamba et mimi nitakuwa single mother nikitaka mwanaume nitatoka na kuuridhisha mwili wangu ila kwa sasa sitaki mwanaume yoyote, hii aliitoa aliyekuwa mke wangu alipokomalia kudai talaka bila kuchoka, bahati nzuri watoto wangu ni wa kiume hawatoangukia kwenye hili, makala ijayo nitaelezea kuhusu madhara wanayopata watoto wa kiume kwa kukosa malezi ya baba, mimi nikiwa ni muhanga wa hili kwani nimeshindwa kabisa kuwa karibu na watoto wangu kutokana na changamoto anazonipa mama yao.

Ndimi Comrade Ally Maftah
KING OF ALL SOCIAL MEDIA
 

Attachments

  • COMRADE.mp4
    1.5 MB
Wa kiume ndio hatari zaidi....kukosa malezi ya baba

Out of topic: leo uko vizuri, ile blichi hadi kwenye ndevu sio....
 
Back
Top Bottom