Wasichana na umri wa mahusiano

Manyanza

JF-Expert Member
Nov 4, 2010
9,832
15,170
Wengi wao wakiwa na umri wa miaka 18-25 huwavutia wanaume wengi kwa ajili ya Ndoa ,lakini wao huwa hawapo tayari kuolewa kwa sababu mbalimbali

1. Umri wangu Bado mdogo kuolewa
2. Kwa sasa Bado nahitaji kuendelea kusoma
3. Nataka nitafute kwanza pesa zangu
4. Ndoa zenyewe zimejaa matatizo,sihitaji kuolewa
5.Nahitaji uhuru wangu Sio kwenda kuchungwa chungwa na mwanaume

6: huwa na kundi la wapenzi kwa ajili ya kula bata ,haoni shida ,kuwa nao 4 Kila mtu na jukumu lake. Wa Kodi,kula,bata,kuvaa nk

Umri wa miaka 25_30
Huenda tayari kahitimu chuo,kapata kazi au ana biashara zake ,ama mambo yameenda hivyo sana yupo na wazazi wake nyumbani ndipo maswali huwa mengi toka kwa wazazi na ndugu

1. Ina maana Bado huna mwanaume wa Kukuoa?

2. Umri hausimami tafuta mtu akuoe.

3. Basi tafuta hata mwanaume uzae nae tu.

4. Badilisha mfumo wa maisha yako,acha hizo nguo fupi,kwenda kumbi za starehe ,unatakiwa upate bwana uolewe

5. Sawa una pesa unaweza jihudumia lakini tafuta ndoa ikuheshimishe

6. Mwamposa atakuwa na mkutano wa siku 5 hebu uwe una hudhuria unaweza funguliwa ukapata bwana wa kukuoa

Baada ya kufika miaka 30_na kuendelea
Hapa huanza kuwaza na kuwazua nini kifanyike Baada ya ndugu na rafiki wa umri wake wengi wameolewa. Kwa sasa nae anaitamani ndoa

1. Mkrisito huanza kuhudhuria mikutano,kwenda Kila ibada,.muislamu huanza kufunga na kwenda msikitini tofauti na siku za nyuma

2. Huanza mahusiano hata na mume wa mtu ,yupo tayari kuwa hata mke wa pili

3. Aliye kuwa mkali na mwenye dharau akiombwa namba,sasa hivi yeye ndio hutoa namba

4. Huamua kuingia kwenye makundi ya mitandaoni kutafuta marafiki au wapenzi watakao kuwa wapenzi Kisha ndoa

5. Hupunguza vigezo vya mwanaume anae muhitaji,ndo husema Ili mradi anapumua. Wakati mwanzo alisema anataka awe mrefu,mweusi mwenye pesa au kaz nzuri

KUMBUKA

Mungu hupanga hatima ya Kila mtu kwa wakati wake,hivyo unaweza umia sana kumbe wakati wako Bado.

Umri Sio kigezo kuoa au kuolewa muhimu uwe na mtu sahihi. Bora uchelewe umpate mtu sahihi kuliko kuwahi ukamie

Kuna wanawake wapo safi tangu wajitambue ila hawakubahatika kupata wenza sahihi,hivyo bado wanasubiri

Kuna wanawake walipata wenza sahihi lakini wao walikuwa na mambo mengi, saiz wanatamani siku zirudi nyuma wafuatwe tena Ili waolewe

Ukimpata mwanaume au Mwanamke sahihi basi fanya kutimiza ndoto yako ,
.
Kila kitu Kina mwisho
Upweke wako una mwisho pia
Maumivu yako yataisha pia
Kuwa tayari wakati wowote
 
Wengi wao wakiwa na umri wa miaka 18-25 huwavutia wanaume wengi kwa ajili ya Ndoa ,lakini wao huwa hawapo tayari kuolewa kwa sababu mbalimbali

1. Umri wangu Bado mdogo kuolewa
2. Kwa sasa Bado nahitaji kuendelea kusoma
3. Nataka nitafute kwanza pesa zangu
4. Ndoa zenyewe zimejaa matatizo,sihitaji kuolewa
5.Nahitaji uhuru wangu Sio kwenda kuchungwa chungwa na mwanaume

6: huwa na kundi la wapenzi kwa ajili ya kula bata ,haoni shida ,kuwa nao 4 Kila mtu na jukumu lake. Wa Kodi,kula,bata,kuvaa nk

Umri wa miaka 25_30
Huenda tayari kahitimu chuo,kapata kazi au ana biashara zake ,ama mambo yameenda hivyo sana yupo na wazazi wake nyumbani ndipo maswali huwa mengi toka kwa wazazi na ndugu

1. Ina maana Bado huna mwanaume wa Kukuoa?

2. Umri hausimami tafuta mtu akuoe.

3. Basi tafuta hata mwanaume uzae nae tu.

4. Badilisha mfumo wa maisha yako,acha hizo nguo fupi,kwenda kumbi za starehe ,unatakiwa upate bwana uolewe

5. Sawa una pesa unaweza jihudumia lakini tafuta ndoa ikuheshimishe

6. Mwamposa atakuwa na mkutano wa siku 5 hebu uwe una hudhuria unaweza funguliwa ukapata bwana wa kukuoa

Baada ya kufika miaka 30_na kuendelea
Hapa huanza kuwaza na kuwazua nini kifanyike Baada ya ndugu na rafiki wa umri wake wengi wameolewa. Kwa sasa nae anaitamani ndoa

1. Mkrisito huanza kuhudhuria mikutano,kwenda Kila ibada,.muislamu huanza kufunga na kwenda msikitini tofauti na siku za nyuma

2. Huanza mahusiano hata na mume wa mtu ,yupo tayari kuwa hata mke wa pili

3. Aliye kuwa mkali na mwenye dharau akiombwa namba,sasa hivi yeye ndio hutoa namba

4. Huamua kuingia kwenye makundi ya mitandaoni kutafuta marafiki au wapenzi watakao kuwa wapenzi Kisha ndoa

5. Hupunguza vigezo vya mwanaume anae muhitaji,ndo husema Ili mradi anapumua. Wakati mwanzo alisema anataka awe mrefu,mweusi mwenye pesa au kaz nzuri

KUMBUKA

Mungu hupanga hatima ya Kila mtu kwa wakati wake,hivyo unaweza umia sana kumbe wakati wako Bado.

Umri Sio kigezo kuoa au kuolewa muhimu uwe na mtu sahihi. Bora uchelewe umpate mtu sahihi kuliko kuwahi ukamie

Kuna wanawake wapo safi tangu wajitambue ila hawakubahatika kupata wenza sahihi,hivyo bado wanasubiri

Kuna wanawake walipata wenza sahihi lakini wao walikuwa na mambo mengi, saiz wanatamani siku zirudi nyuma wafuatwe tena Ili waolewe

Ukimpata mwanaume au Mwanamke sahihi basi fanya kutimiza ndoto yako ,
.
Kila kitu Kina mwisho
Upweke wako una mwisho pia
Maumivu yako yataisha pia
Kuwa tayari wakati wowote
Mwisho wa upweke sio mpaka uwe na mtu, upweke inapaswa mtu auondoe mwenyewe. Hili jambo la upweke linaleta toxic relationships na trauma-like bond relationships.

Ujumbe mzuri ila tuache asili ifanye kazi yake.
 
Tulishafunga mjadala...

KATAA NDOA,
Ndoa inahitaji mwanaume aliyekamilika na mwanamke aliye tayari.

Tatizo watu wengi wanakurupuka. Ndoa ni jambo jema sana maana familia zilizo stable na watoto wenye maadili wanajengwa humo.

Ndoa inahitaji mwanamke na mwanaume afanye jukumu lake, mwanaume ampende mwanamke na ajipende pia na mwanamke ampe heshima mume wake. Mabadiliko ya mwanamke kitabia ndani ya ndoa asilimia kubwa inatokana na menstrual cycle yake na pia kama mume wake atashindwa kusimama kama mwanaume kamili.

Mwanaume inabidi ndo uwe na dira kichwani kuhusu mahusiano ya ndoa, mwanamke ni supporter tu, mwanaume ni lazima uwe mtoaji kila sekta ikiwemo kutoa best sex kwa mwenza wako, kuchunguza zile spot za mwili wake, kiufupi yale mliyokuwq mnayafanya kipindi cha uchumba yaendelee kufanyika baada ya ndoa. Ndoa ni zaidi ya kuwa na watoto.
 
Msichana yupo primary au O level kama sio advance secondary school.

Mwanamke anakuwa umri wa kuolewa huko na kuishi na mwanaume no discussion.
Asante Mkuu.
Uzi unasomeka wasichana na umri wa mahusiano, nikahisi unawahusu wasichana pekee kuja kuangalia na wamama wa 33+ tumehusishwa nikahisi labda ni mimi nashindwa kutofautisha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom