Nyenyere
JF-Expert Member
- Sep 9, 2010
- 14,770
- 10,660
Wakuu amani kwenu. Leo nimekuwa natafakari jinsi mambo ya mahusiano ya mapenzi yalivyo kwenye dunia yetu ya leo. Kuna swali najiuliza nabaki kutabasamu tu, hivi kweli leo hii sheria hizi zingetumika, nani angebaki salama?
Kumbukumbu la Torati 22 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹³ Mtu akitwaa mke, akamwingilia na kumchukia,
¹⁴ kisha akamshitaki mambo ya aibu kumzushia jina baya, akasema, Nimemtwaa mwanamke huyu, nami nilipomkaribia sikuona kwake alama za ubikira;
¹⁵ ndipo babaye yule kijana na mamaye watakapotwaa alama za yule kijana za ubikira, wawatolee wazee wa mji langoni;
¹⁶ na baba yake yule kijana awaambie wazee, Mwanamume huyu nilimpa binti yangu awe mkewe, naye amchukia;
¹⁷ angalieni, amemwekea mambo ya aibu, asema, Sikuona kwa binti yako alama za ubikira, nazo hizi ndizo alama za binti yangu za ubikira. Na wayakunjue yale mavazi mbele ya wazee wa mji.
¹⁸ Basi wazee wa mji ule na wamtwae yule mtu mume na kumrudi,
¹⁹ wamtoze shekeli mia za fedha, wampe babaye yule kijana, kwa kuwa amemzulia jina baya mwanamwali wa Israeli; naye awe mkewe; hana ruhusa ya kumwacha siku zake zote.
²⁰ Lakini likiwa nikweli neno hili, la kutoonekana kwake yule kijana alama za ubikira;
²¹ na wamtoe nje yule kijana mlangoni pa nyumba ya baba yake, na waume wa mji wake wampige kwa mawe hata afe; kwa vile alivyofanya upumbavu katika Israeli, kwa kufanya ukahaba katika nyumba ya baba yake; ndivyo utakavyoondoa uovu katikati yako.
Yaani jamaa baada ya kumwoa mke, alipomuingilia kwa mara ya kwanza ilikuwa lazima akute kiwambo, na ushahidi ni kitambaa cheupe ambacho alikihifadhi baba wa binti kama ushahidi wa kumlea vema binti yake baada ya kiwambo kuondolewa.
Afu mambo ya aibu yaliyompata jina baya binti ni KUTOKUWA BIKRA WAKATI WA KUOLEWA. Hii ilikuwa aibu kuu na imeendelea kuwa hivyo kwa Mungu, kwa wanaoelewa maana!!
Hivi kwenye dunia ya leo ardhi yetu ingejaa makaburi ya kina dada!! Hii haijalishi, hata familia nyingi tu za kikristo mawe yangehusika. Tumejikwaa wapi?
Kumbukumbu la Torati 22 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹³ Mtu akitwaa mke, akamwingilia na kumchukia,
¹⁴ kisha akamshitaki mambo ya aibu kumzushia jina baya, akasema, Nimemtwaa mwanamke huyu, nami nilipomkaribia sikuona kwake alama za ubikira;
¹⁵ ndipo babaye yule kijana na mamaye watakapotwaa alama za yule kijana za ubikira, wawatolee wazee wa mji langoni;
¹⁶ na baba yake yule kijana awaambie wazee, Mwanamume huyu nilimpa binti yangu awe mkewe, naye amchukia;
¹⁷ angalieni, amemwekea mambo ya aibu, asema, Sikuona kwa binti yako alama za ubikira, nazo hizi ndizo alama za binti yangu za ubikira. Na wayakunjue yale mavazi mbele ya wazee wa mji.
¹⁸ Basi wazee wa mji ule na wamtwae yule mtu mume na kumrudi,
¹⁹ wamtoze shekeli mia za fedha, wampe babaye yule kijana, kwa kuwa amemzulia jina baya mwanamwali wa Israeli; naye awe mkewe; hana ruhusa ya kumwacha siku zake zote.
²⁰ Lakini likiwa nikweli neno hili, la kutoonekana kwake yule kijana alama za ubikira;
²¹ na wamtoe nje yule kijana mlangoni pa nyumba ya baba yake, na waume wa mji wake wampige kwa mawe hata afe; kwa vile alivyofanya upumbavu katika Israeli, kwa kufanya ukahaba katika nyumba ya baba yake; ndivyo utakavyoondoa uovu katikati yako.
Yaani jamaa baada ya kumwoa mke, alipomuingilia kwa mara ya kwanza ilikuwa lazima akute kiwambo, na ushahidi ni kitambaa cheupe ambacho alikihifadhi baba wa binti kama ushahidi wa kumlea vema binti yake baada ya kiwambo kuondolewa.
Afu mambo ya aibu yaliyompata jina baya binti ni KUTOKUWA BIKRA WAKATI WA KUOLEWA. Hii ilikuwa aibu kuu na imeendelea kuwa hivyo kwa Mungu, kwa wanaoelewa maana!!
Hivi kwenye dunia ya leo ardhi yetu ingejaa makaburi ya kina dada!! Hii haijalishi, hata familia nyingi tu za kikristo mawe yangehusika. Tumejikwaa wapi?