BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,034
Date::9/6/2008
Wahisani wagoma kueleza lini watatoa fedha kwa Tanzania
Na Boniface Meena
Mwananchi
NCHI wahisani zinazochangia bajeti ya serikali katika miradi ya maendeleo zimesema kuwa, hazijui lini mazungumzo kati yake na serikali yanayoendelea yatakwisha ili wakabidhi mchango huo.
Hivi karibuni, wahisani hao walieleza kuwa wangependa kuendelea kuwa na mazungumzo ya uso kwa uso na serikali mpaka watakapofikia maamuzi ya kutoa fedha hizo baada ya hotuba ya Rais Kikwete bungeni Dodoma Agosti 21 mwaka huu
Akizungumza na Mwananchi Jumapili kwa njia ya simu, mmoja wa maofisa wa ubalozi wa Denmark nchini ambao ndiye mwenyekiti wa wahisani hao alisema pamoja na kuamua kukutana na serikali mara kwa mara ili kuzungumzia suala hilo hawajui ni lini mazungumzo hayo yatafikia ukomo.
"Kwa kweli sijui ni lini mazungumzo yataisha na kufikia uamuzi ila tutaendelea kukutana na serikali hadi hapo tutakapofikia uamuzi wa kutoa fedha hizo," alisema ofisa huyo.
"Kutokana na taarifa ya Rais Kikwete bungeni Dodoma, nchi wahisani zinaona ni vema kuendelea na mazungumzo ya uso kwa uso na serikali na yatakapofikia ukomo, tutatoa taarifa," alisema ofisa huyo.
Kutokana na msimamo wa wahisani hao, ufadhili wa miradi ya maendeleo katika bajeti ya serikali utazidi kuchelewa baada ya nchi wahisani zinazochangia bajeti hiyo kupata kigugumizi cha kusema lini zitaanza kutoa fedha walizoahidi kuchangia katika mwaka wa fedha 2008/09.
Wahisani hao wamekuwa wakikutana na viongozi wa serikali kutoka Wizara ya Fedha na Uchumi kujadili mambo ya kutekelezwa ili waweze kuto fedha hizo, lakini ufisadi wa EPA umekuwa kikwazo kufikia mwafaka.
Walipokutana kwa mara ya mwisho, Julai 19 mwaka huu, hawakutamka ni lini hasa watatoa fedha.
Taarifa ya maandishi kwa gazeti hili Julai 19, kutoka kwa Mwenyekiti wa kundi la wafadhili hao 11, ambaye pia ni Balozi wa Denmark nchini, Bjarne Sorensen, ilisema: "Nathibitisha kwamba, kundi la nchi wafadhili lilifanya mkutano na Mheshimiwa Mkulo, Waziri wa Fedha na Uchumi.
"Mkutano huo ni sehemu ya mikutano ya kawaida na mijadala tunayofanya na mheshimiwa waziri wa fedha, ambako hujadili na kuangalia maendeleo muhimu yatakayotupa fursa ya kuamua ni lini tutaanza kutoa fedha kwa Bajeti ya mwaka 2008/09."
Kutokana na kauli ya wahisani hao, ilionekana bado wanaendelea kuiminya serikali hadi itakapochukua hatua zilizopendekezwa dhidi ya watuhumiwa wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA); ufisadi ndani ya Benki Kuu ya Tanzania na taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG).
Msimamo huu unakwenda sambamba na kauli waliyotoa wakati wakiridhia kusaidia katika bajeti ya mwaka huu, wakisema: "Kabla ya kutoa fedha kusaidia bajeti hiyo tunatazamia kupokea taarifa zaidi za utekelezaji wa namna serikali inavyopambana na tuhuma za rushwa, kuboresha utawala, na utekelezaji wa mapendekezo ya CAG yaliyohusu ukaguzi wa hesabu za Benki Kuu ya Tanzania kwa mwaka wa fedha wa 2005/06."
Wafadhili hao wameahidi kuchangia asilimia 34 kwenye bajeti ya mwaka huu ya Sh 7.2 trilioni, hali ambayo inaiweka serikali kwenye wakati mgumu kama hazitatolewa kwa wakati kwani ndizo zinategemewa kuendesha miradi ya maendeleo.
Mara ya mwisho wafadhili kuibana serikali katika bajeti yake ni wakati wa utawala wa Rais wa awamu ya pili ya Ali Hassan Mwinyi, walipokataa kufadhili Tanzania kutokana na serikali kushindwa kukusanya kodi kiasi cha Sh bilioni 70 wakati huo.
Makusanyo ya kodi serikalini wakati huo, yaani mwaka 1995, ilikuwa ni Sh 28 bilioni kwa mwezi. Kiasi kikubwa cha kodi ambazo hazikukusanywa ilikuwa ni misamaha ya kodi pamoja na wafanyabiashara wakubwa kukwepa kodi. Hali hiyo ilidhibitiwa baada ya Rais Benjamin Mkapa kuingia madarakani.
Wahisani wagoma kueleza lini watatoa fedha kwa Tanzania
Na Boniface Meena
Mwananchi
NCHI wahisani zinazochangia bajeti ya serikali katika miradi ya maendeleo zimesema kuwa, hazijui lini mazungumzo kati yake na serikali yanayoendelea yatakwisha ili wakabidhi mchango huo.
Hivi karibuni, wahisani hao walieleza kuwa wangependa kuendelea kuwa na mazungumzo ya uso kwa uso na serikali mpaka watakapofikia maamuzi ya kutoa fedha hizo baada ya hotuba ya Rais Kikwete bungeni Dodoma Agosti 21 mwaka huu
Akizungumza na Mwananchi Jumapili kwa njia ya simu, mmoja wa maofisa wa ubalozi wa Denmark nchini ambao ndiye mwenyekiti wa wahisani hao alisema pamoja na kuamua kukutana na serikali mara kwa mara ili kuzungumzia suala hilo hawajui ni lini mazungumzo hayo yatafikia ukomo.
"Kwa kweli sijui ni lini mazungumzo yataisha na kufikia uamuzi ila tutaendelea kukutana na serikali hadi hapo tutakapofikia uamuzi wa kutoa fedha hizo," alisema ofisa huyo.
"Kutokana na taarifa ya Rais Kikwete bungeni Dodoma, nchi wahisani zinaona ni vema kuendelea na mazungumzo ya uso kwa uso na serikali na yatakapofikia ukomo, tutatoa taarifa," alisema ofisa huyo.
Kutokana na msimamo wa wahisani hao, ufadhili wa miradi ya maendeleo katika bajeti ya serikali utazidi kuchelewa baada ya nchi wahisani zinazochangia bajeti hiyo kupata kigugumizi cha kusema lini zitaanza kutoa fedha walizoahidi kuchangia katika mwaka wa fedha 2008/09.
Wahisani hao wamekuwa wakikutana na viongozi wa serikali kutoka Wizara ya Fedha na Uchumi kujadili mambo ya kutekelezwa ili waweze kuto fedha hizo, lakini ufisadi wa EPA umekuwa kikwazo kufikia mwafaka.
Walipokutana kwa mara ya mwisho, Julai 19 mwaka huu, hawakutamka ni lini hasa watatoa fedha.
Taarifa ya maandishi kwa gazeti hili Julai 19, kutoka kwa Mwenyekiti wa kundi la wafadhili hao 11, ambaye pia ni Balozi wa Denmark nchini, Bjarne Sorensen, ilisema: "Nathibitisha kwamba, kundi la nchi wafadhili lilifanya mkutano na Mheshimiwa Mkulo, Waziri wa Fedha na Uchumi.
"Mkutano huo ni sehemu ya mikutano ya kawaida na mijadala tunayofanya na mheshimiwa waziri wa fedha, ambako hujadili na kuangalia maendeleo muhimu yatakayotupa fursa ya kuamua ni lini tutaanza kutoa fedha kwa Bajeti ya mwaka 2008/09."
Kutokana na kauli ya wahisani hao, ilionekana bado wanaendelea kuiminya serikali hadi itakapochukua hatua zilizopendekezwa dhidi ya watuhumiwa wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA); ufisadi ndani ya Benki Kuu ya Tanzania na taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG).
Msimamo huu unakwenda sambamba na kauli waliyotoa wakati wakiridhia kusaidia katika bajeti ya mwaka huu, wakisema: "Kabla ya kutoa fedha kusaidia bajeti hiyo tunatazamia kupokea taarifa zaidi za utekelezaji wa namna serikali inavyopambana na tuhuma za rushwa, kuboresha utawala, na utekelezaji wa mapendekezo ya CAG yaliyohusu ukaguzi wa hesabu za Benki Kuu ya Tanzania kwa mwaka wa fedha wa 2005/06."
Wafadhili hao wameahidi kuchangia asilimia 34 kwenye bajeti ya mwaka huu ya Sh 7.2 trilioni, hali ambayo inaiweka serikali kwenye wakati mgumu kama hazitatolewa kwa wakati kwani ndizo zinategemewa kuendesha miradi ya maendeleo.
Mara ya mwisho wafadhili kuibana serikali katika bajeti yake ni wakati wa utawala wa Rais wa awamu ya pili ya Ali Hassan Mwinyi, walipokataa kufadhili Tanzania kutokana na serikali kushindwa kukusanya kodi kiasi cha Sh bilioni 70 wakati huo.
Makusanyo ya kodi serikalini wakati huo, yaani mwaka 1995, ilikuwa ni Sh 28 bilioni kwa mwezi. Kiasi kikubwa cha kodi ambazo hazikukusanywa ilikuwa ni misamaha ya kodi pamoja na wafanyabiashara wakubwa kukwepa kodi. Hali hiyo ilidhibitiwa baada ya Rais Benjamin Mkapa kuingia madarakani.