Wabunge walipe kodi, wabunge kutolipa kodi ni rushwa inayotolewa na Serikali

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,077
22,790
Wabunge walipe kodi. Katika nchi nyingi ulipaji wa kodi ni majawapo katika sifa kuu kwa wagombeaji wa ubunge kuwa nayo ili wakidhi kuchaguliwa.

Ni wazi kuwa kwa Wabunge wetu hawa kwa kutolipa kutolipa kodi wanakosa uhalali wa kuikosoa serikali pamoja na jukumu la kuhimiza ulipaji wa kodi.

Sasa hivi tunawaona wabunge wanavyoisifia Serikali kwa kuwatoza kodi kibao wananchi wanaowawakilisha kama chanzo kikuu cha mapato.

Swali linalonisumbua kama mwananchi ni sababu zipi zilipelekea hawa wawakilishi wetu wenye kipato na marupurupu maradufu kutolipa kodi.

Kila mbunge anayesimama bungeni cha kwanza kinachotoka kinywani kwake ni shukhrani kwa serikali na sifa pekee kwa kingozi Mkuu wa serikali.

Je bunge letu ni rubber stamp ya serikali na Rais wa nchi? Je kutolipa kodi ni mojawapo katika utekelezaji wa state sponsored corruption?

Hata wakitumia lugha gani katika utetezi ukweli utabaki pale pale; kwa kutolipa kodi wabunge wetu wanakula rushwa inayotolewa na serikali.
 
Wabunge walipe kodi. Katika nchi nyingi ulipaji wa kodi ni majawapo katika sifa kuu kwa wagombeaji wa ubunge kuwa nayo ili wakidhi kuchaguliwa...

Hata wakitumia lugha gani katika utetezi ukweli utabaki pale pale; kwa kutolipa kodi wabunge wetu wanakula rushwa inayotolewa na serikali.
Ni kweli na ndio maana mambo ya makodi kodi kwao hawaoni madhara
 
Wabunge walipe kodi. Katika nchi nyingi ulipaji wa kodi ni majawapo katika sifa kuu kwa wagombeaji wa ubunge kuwa nayo ili wakidhi kuchaguliwa.

Ni wazi kuwa kwa Wabunge wetu hawa kutolipa kutolipa kodi wanakosa uhalali wa kuikosoa serikali pamoja na jukumu la kuhimiza ulipaji wa kodi.
Mkuu Mag3 , naunga mkono hoja, tena sio wabunge tuu, hata rais wetu alipe kodi, na hili nilishauri Kuepuka Double Standards ya Kodi, Nashauri Rais Uongezwe Mshahara, Ili Alipe Kodi, Wote Tulipe Kodi!
P
 
Naona mnaona kodi tu kumbe maeneo mengi kodi inapotea.

Mimi ninachojua kuwa wabunge hawapo hata kwenye mifuko ya hifadhi ya Jamii

Hii ni changamoto kubwa ndio maana hawawezi kukiongelea Kikokotoo

Hawa ilitakiwa wakishaingia kwenye ajira wawe kama waajiriwa hata mishahara yao ipangwe na Bodi ya mishahara

Hizi Pension zao hazina formula wala HAKUNA mtu au mkampuni inayoweza kulipa hizo pension zao wanazolipwa

Haya mambo Mwigulu alitakiwa aiweke kama vyanzo vipya kabisa vya mapato nchini sio mitozo tu kuongezeka kila uchao wakati wengine ni free-laider ety kwasababu ni wanasiasa
 
Ni kweli na ndio maana mambo ya makodi kodi kwao hawaoni madhara
Kwa maana nyingine ni kwamba bungeni wamejaa wawakilishi wa serikali ya CCM na kwa hila serikali hiyo hiyo ndiyo ilihakikisha wanachaguliwa mwaka 2010.

Bungeni kwa sasa hatuna hoja mbadala wala kauli mbadala na kwa kauli zaoo wenyewe bungeni kwa sasa wanaitetea serikali kuliko hata wakati wa chama kimoja.

Bunge la sasa halina tofauti na kikao cha mkutano mkuu wa CCM na hili lilipangwa kwa makusudi liwe hivyo. Vikao vya bunge havina tofauti na timu ya kampeni.

Wabunge bila aibu wanasifia wananchi kulipishwa kodi lukuki huku wakijua kwamba wao kama kupe wanaishi na kuneemeka kwa kodi zetu na jasho letu wananchi.

Kila wanachomiliki hao wabunge kimetokana na kodi zetu na imefikia mpaka wanamsifia waziri wa fedha kwa kuwa mbunifu katika kutukamua hadi tunatoka damu.

Kweli Tanzania itaendelea kujengwa na wenye moyo huku ikitafunwa na wenye meno. Kwa ubinafsi wa Wabunge wetu unaotisha wanadiriki hadi kutunga sheria zisizowabana wao.
 
Hivi ni kweli Hawalipi Kodi au Tunawasingizia tuu!!! Hivi hata Aibu hawaoni kweli,Mama ntilie Alipe kodi wao wasilipe,Mi siamini Aisee...
 
Wabunge walipe kodi. Katika nchi nyingi ulipaji wa kodi ni majawapo katika sifa kuu kwa wagombeaji wa ubunge kuwa nayo ili wakidhi kuchaguliwa.

Ni wazi kuwa kwa Wabunge wetu hawa kutolipa kutolipa kodi wanakosa uhalali wa kuikosoa serikali pamoja na jukumu la kuhimiza ulipaji wa kodi.

Sasa hivi tunawaona wabunge wanavyoisifia Serikali kwa kuwatoza kodi kibao wananchi wanaowawakilisha kama chanzo kikuu cha mapato.

Swali linalonisumbua kama mwananchi ni sababu zipi zilipelekea hawa wawakilishi wetu wenye kipato na marupurupu maradufu kutolipa kodi.

Kila mbunge anayesimama bungeni cha kwanza kinachotoka kinywani kwake ni shukhrani kwa serikali na sifa pekee kwa kingozi Mkuu wa serikali.

Je bunge letu ni rubber stamp ya serikali na Rais wa nchi? Je kutolipa kodi ni mojawapo katika utekelezaji wa state sponsored corruption?

Hata wakitumia lugha gani katika utetezi ukweli utabaki pale pale; kwa kutolipa kodi wabunge wetu wanakula rushwa inayotolewa na serikali.
Crikali inajua kwa nn haitaki kuwatoza kodi ili waendelee kupitisha ujinga wote kwa masilahi ya watawala
 
Mshahara wa wabunge ni hela ya kodi, sasa kwa nini walipe kodi? Ni sawa na kumpa hela mwanao na halafu unamwambia akugawie hela ulizompa. Kama unahitaji hela mpe kidogo, nyingine ubaki nazo.
 
Mkuu Mag3 , naunga mkono hoja, tena sio wabunge tuu, hata rais wetu alipe kodi, na hili nilishauri Kuepuka Double Standards ya Kodi, Nashauri Rais Uongezwe Mshahara, Ili Alipe Kodi, Wote Tulipe Kodi!
P
Tatizo ni Bunge. Bunge ndilo linalotunga sheria na ndilo linaisimamia serikali kwa niaba yetu. Udhaifu wa bunge ndio chanzo cha kujikuta linashindwa kutimiza wajibu wake. Udhaifu huu unatokea kwa sababu wabunge wote ni wala rushwa.

Bunge ni mateka wa rushwa kwani waligombea kwa rushwa na wakachaguliwa kwa rushwa. Mateka wa rushwa hana uhalali, uwezo wala ujasiri wa kuipiga vita rushwa. Matokeo yake wameipa serikali ruhusa ya kuwafinyanga kama inavyotaka.

Na kwa bahati mbaya rushwa ziko za aina nyingi...za wazi na zisizo za wazi, za matajiri na za masikini, za wenye nguvu na hohe hahe, za walinzi na walindwa n.k.
 
Back
Top Bottom