Viboko Mashuleni Kukomeshwa, Je Imechangia Kwa Maadili Kuporomoka Au Maadili Mema Kuongezeka?

Msukusu

JF-Expert Member
Jun 28, 2022
216
409
Wakubwa habari zenu mimi ni kijana wa 30+ na hivi karibuni natarajia kupata mtoto wa pili, majaliwa ya mwenyezi mungu.

Haya tujikite kwenye mada hapo juu, kwa jamii ninayo ishi nimeshuhudia vitendo viovu na maadili mabaya hasa kwa wadogo zetu, wengine watoto ambao unao uwezo wa kumzaa.

Nilishuhudia mtoto wa miaka saba anamjibu mama mmoja vibaya, pale alipoambiwa aende nyumbani kuoga, mtoto alimjibu achana na mimi kwani wwe ni mama yangu.

Kisa cha pili kuna kibinti cha kidato cha pili mara nyingi sana naona, hasa wadada na kina mama wanavaa kanga moko na nguo ya ndani halafu wanaenda gengeni, mara nyingi hutokea nyakati za jioni au asubuhi sababu sijui.

Basi huyo binti alikuwa anakatiza kwa watu wazima wamekaa na hiyo kanga moko yake, kuna mubaba mmoja alikuwa anamuangalia sana, yule binti akamwambia mbona unaniangalia sana unataka k.

Kama unataka sema sio kunitolea mimacho. Twende mashuleni kipindi tunasoma wale waliozaliwa miaka ya 80 na 90 tulichapwa sana viboko mashuleni.

Sio shuleni tu hadi wazazi walitutandika sana viboko pale tulipokosea. Kipindi tunasoma ukikutana na mwalimu hujachomekea ni viboko sana, kwa sasa unaweza pishana na wanafunzi wa kiume hajachomekea na mwalimu ukimuadhibu kwa viboko utatengenezewa kamati.

Wasichana ukikutwa umefuga kucha au kupanga rangi ni viboko, kwa kizazi hiki hakuna mwalimu anayeshughulika na wewe ufuge kucha, upake rangi utajijua kimpango wako. Kumiliki simu shuleni ni sawa umekutwa na nyara za serikali au biashara haramu.

Na pia ilikuwa ni kosa la kumfukuza mwanafunzi shule pale utakapokutwa simu, kwa sasa mwanafunzi wa kidato cha kwanza anamiliki simu, walimu hawana muda wa kukemea na wala wazazi hawana muda huo.

Walimu naona watoto wamewashindwa wao kwa sasa wanafundisha tu ili mradi mishahara inaingia, habari ya kukipizana au kuchapa mtoto wa mtu hawana habari hizo.

Na tunajua kabisa swala la maadili ni kijamii nzima. Wazazi ndio wa kwanza kabisa wanaofuata ni walimu sababu kule mashuleni watoto wetu wanakutana na watoto wenzao walio lelewa na familia tofauti.

Jamii inapopinga viboko mashuleni je wazazi mtaweza kuwalea watoto wenu kwenye maadili mema?
 
1. Mkuu viboko vya nini? Mbona ambao hatukuchapwa tunadunda na hata "ban" moja tu JF, leo almost 10 years + haijapata kutuhusu?

2. Vipi Ulaya na Marekani linganisha na Palestina huko!

3. Nani asiyevisikia viboko vya madrassa?

4. Linganisha na kwa beberu kunakoundwa hadi madege na kimbilio la wajasilia uchumi.

Ritz, Malaria 2, FaizaFoxy, MK254, Mzee Kigogo, Moisemusajiografii na wale wengine: miongozo yenu tafadhali.
 
Kwanini usimtandike mwanao unataka mwalimu amtandike kwa niaba? Kazi ya kumkuza mtoto mwenye maadili ni ya mama na baba, mwalimu anasisitizia tu.
 
Mi kwa kweli ni mhafidhina, huwa nawachapa vizuri sana wanafunzi bila hata ruhusa ya mkuu wa shule. Mi mwenyewe nilichapwa sana tu na walimu wangu, tena vipoko vya mgogoni na kwenye supu za miguu mpaka damu zinavia mwilini. Mara nichapwe kwa uchelewaji, mara maji, mara ufagio, mara kelele darasani, mara nimekosa hesabu, mara madaftari sikukusanya yakasahihishwe, mara nimeweka wino kwenye michoro ya penseli mwendo ni kuchapwa tu mpaka sekondari. Kuna wakati nilichapwa viboko vya mgongoni na mkuu wa shule mbele ya mzazi wangu kisa tu sikuomba ruhusa siku mbili mzazi akanipeleka shuleni nikaazibiwe. Vitoto ni vidogo lakini navipa viboko saizi yao vitulie darasani sitaki kelele. Huo ndio mtindo wangu wa class control
 
Mi kwa kweli ni mhafidhina, huwa nawachapa vizuri sana wanafunzi bila hata ruhusa ya mkuu wa shule. Mi mwenyewe nilichapwa sana tu na walimu wangu, tena vipoko vya mgogoni na kwenye supu za miguu mpaka damu zinavia mwilini. Mara nichapwe kwa uchelewaji, mara maji, mara ufagio, mara kelele darasani, mara nimekosa hesabu, mara madaftari sikukusanya yakasahihishwe, mara nimeweka wino kwenye michoro ya penseli mwendo ni kuchapwa tu mpaka sekondari. Kuna wakati nilichapwa viboko vya mgongoni na mkuu wa shule mbele ya mzazi wangu kisa tu sikuomba ruhusa siku mbili mzazi akanipeleka shuleni nikaazibiwe. Vitoto ni vidogo lakini navipa viboko saizi yao vitulie darasani sitaki kelele. Huo ndio mtindo wangu wa class control
Umechapwa viboko hadi umewehuka.

Yaani umchape mtoto kisa sijui ufagio? 😹😹😹

Tena unamchapa hadi damu inaivilia mwilini! Heeeeeh!

Kwa kweli ni lazima sasa viboko vifutwe kama hawa PSYCHOPATHS ndio walimu!
 
Vikomeshwe tu atakayelea vibaya haina shida magereza yapo !
Mzigo wako beba mwenyewe

Ukikushinda walimwengu tutafundisha wenyewe , sisi tukimfundisha ataelewa tu hata kama ni slow leaner!

Tukimshindwa hakuna kurudia ,tunamuwahisha kwa aliyemuumba.
 
Wakubwa habari zenu mimi ni kijana wa 30+ na hivi karibuni natarajia kupata mtoto wa pili, majaliwa ya mwenyezi mungu.

Haya tujikite kwenye mada hapo juu, kwa jamii ninayo ishi nimeshuhudia vitendo viovu na maadili mabaya hasa kwa wadogo zetu, wengine watoto ambao unao uwezo wa kumzaa.

Nilishuhudia mtoto wa miaka saba anamjibu mama mmoja vibaya, pale alipoambiwa aende nyumbani kuoga, mtoto alimjibu achana na mimi kwani wwe ni mama yangu.

Kisa cha pili kuna kibinti cha kidato cha pili mara nyingi sana naona, hasa wadada na kina mama wanavaa kanga moko na nguo ya ndani halafu wanaenda gengeni, mara nyingi hutokea nyakati za jioni au asubuhi sababu sijui.

Basi huyo binti alikuwa anakatiza kwa watu wazima wamekaa na hiyo kanga moko yake, kuna mubaba mmoja alikuwa anamuangalia sana, yule binti akamwambia mbona unaniangalia sana unataka k.

Kama unataka sema sio kunitolea mimacho. Twende mashuleni kipindi tunasoma wale waliozaliwa miaka ya 80 na 90 tulichapwa sana viboko mashuleni.

Sio shuleni tu hadi wazazi walitutandika sana viboko pale tulipokosea. Kipindi tunasoma ukikutana na mwalimu hujachomekea ni viboko sana, kwa sasa unaweza pishana na wanafunzi wa kiume hajachomekea na mwalimu ukimuadhibu kwa viboko utatengenezewa kamati.

Wasichana ukikutwa umefuga kucha au kupanga rangi ni viboko, kwa kizazi hiki hakuna mwalimu anayeshughulika na wewe ufuge kucha, upake rangi utajijua kimpango wako. Kumiliki simu shuleni ni sawa umekutwa na nyara za serikali au biashara haramu.

Na pia ilikuwa ni kosa la kumfukuza mwanafunzi shule pale utakapokutwa simu, kwa sasa mwanafunzi wa kidato cha kwanza anamiliki simu, walimu hawana muda wa kukemea na wala wazazi hawana muda huo.

Walimu naona watoto wamewashindwa wao kwa sasa wanafundisha tu ili mradi mishahara inaingia, habari ya kukipizana au kuchapa mtoto wa mtu hawana habari hizo.

Na tunajua kabisa swala la maadili ni kijamii nzima. Wazazi ndio wa kwanza kabisa wanaofuata ni walimu sababu kule mashuleni watoto wetu wanakutana na watoto wenzao walio lelewa na familia tofauti.

Jamii inapopinga viboko mashuleni je wazazi mtaweza kuwalea watoto wenu kwenye maadili mema
 
Watoto siku hizi tunawalea kimayai sana ndio maana wanatupanda kichwani Hadi wazazi wakati ule tulikuwa tunaadhibiwa nyumbani,na jamii na shuleni ndio maana tulikuwa na nidhamu na hata heshima pia Kwa wakubwa na jamii Kwa ujumla ila kwasasa tunawapoteza watoto kwenye malezi Kwa kivuli cha haki za binadamu ndio maana vijana wanakengeuka angalia wadogo...
 
Wote tumepita shuleni tumeona namna walimu wanavyopata shida kwenye kudhibiti nidhamu hizo adhabu mbadala bado zinaonekana kama za kawaida tuu Kwa wanafunzi wa siku hizi viboko viendelee kuwepo
 
Back
Top Bottom