Unyanyasaji kwenye ubalozi wa Marekani

Karungikana

JF-Expert Member
Jan 8, 2017
852
795
Kuna unyanyasaji nilioushuhudia ubalozi wa Marekani nilipoenda kushughulikia visa.

Kwanza pale getini, unaambiwa unaacha kila kitu huingii na chochote! Ila cha kushangaza, hawajaweka hata sehemu ya kuhifadhi mkoba au simu. Sasa sijui wanategemea ukienda huko usiende na pochi? Na je simu unamwachia nani?

Zamani wakati visa zinashughulikiwa ubalozi wa Uingereza, kulikuwa na lockers nje unaweka simu yako na kupewa kikaratasi. Sasa hawa binafsi sijawaelewa.

La pili; Ukishaingia ndani ya compund, nje ya ofisi zao, mnapanga foleni hapo nje mmesimama, hakuna hata benchi la kukaa! Iwe mvua liwe jua! Nikajiuliza je, na wenye ulemavu inakuwaje? Wanashindwa nini kuweka shed fulani na benchi angalau watu wakae?

Kutafuta visa ya Marekani ni kama kutafuta ruhusa ya kwenda mbinguni, wakati wao, wanaweza hata kupata visa airport! WHY?

Naamini wakiambiwa wanaweza kujirekebisha. Hakuna sababu ya kutunyanya kiasi hicho!
 
Kuna unyanyasaji nilioushuhudia ubalozi wa marekani nilipoenda kushughulikia visa.

Kwanza pale getini, unaambiwa unaacha kila kitu huingii na chochote! Ila cha kushangaza, hawajaweka hata sehemu ya kuhifadhi mkoba au simu. Sasa sijui wanategemea ukienda huko usiende na pochi? Na je simu unamwachia nani?

Zamani wakati visa zinashughulikiwa ubalozi wa uingereza, kulikuwa na lockers nje unaweka simu yako na kupewa kikaratasi. Sasa hawa binafsi sijawaelewa.

La pili; Ukishaingia ndani ya compund, nje ya ofisi zao, mnapanga foleni hapo nje mmesimama, hakuna hata benchi la kukaa! Iwe mvua liwe jua! Nikajiuliza je, na wenye ulemavu inakuwaje? Wanashindwa nini kuweka shed fulani na benchi angalau watu wakae?

Kutafuta visa ya marekani ni kama kutafuta ruhusa ya kwenda mbinguni, wakati wao, wanaweza hata kupata visa airport! WHY?

Naamini wakiambiwa wanaweza kujirekebisha. Hakuna sababu ya kutunyanya kiasi hicho!
Kuna ngozi nyeupe nayo ilikuwepo kwenye kupanga mstari au ni black
 
Kuna wakati nilihudhuria semina fulani ya taaluma yangu hapo ubalozini kwao. Huo ulinzi ni balaa, unakaguliwa mara tatu ndio uingie ndani kabisa uliko ukumbi wa mikutano. Ilifika zamu yangu kukaguliwa na ile mitambo yao nikapigiwa king'ora na mtambo wao, ikabidi niwekwe pembeni kwa ukaguzi zaidi. Kumbe ni bakoli ya mkanda tu ndiyo iliyopigiwa king'ora na mtambo wao, sikuwa na silaha au kitu cha hatari. Kwa ukaguzi niliofanyiwa peke yangu nilifedheheka sana japo sikuvua nguo ila nilimbezewa scanner mwili mzima
 
Kuna wakati nilihudhuria semina fulani ya taaluma yangu hapo ubalozini kwao. Huo ulinzi ni balaa, unakaguliwa mara tatu ndio uingie ndani kabisa uliko ukumbi wa mikutano. Ilifika zamu yangu kukaguliwa na ile mitambo yao nikapigiwa king'ora na mtambo wao, ikabidi niwekwe pembeni kwa ukaguzi zaidi. Kumbe ni bakoli ya mkanda tu ndiyo iliyopigiwa king'ora na mtambo wao, sikuwa na silaha au kitu cha hatari. Kwa ukaguzi niliofanyiwa peke yangu nilifedheheka sana japo sikuvua nguo ila nilimbezewa scanner mwili mzima
Wenzio suruali zao hazikuwa na bakoli?
 
Kuna unyanyasaji nilioushuhudia ubalozi wa Marekani nilipoenda kushughulikia visa.

Kwanza pale getini, unaambiwa unaacha kila kitu huingii na chochote! Ila cha kushangaza, hawajaweka hata sehemu ya kuhifadhi mkoba au simu. Sasa sijui wanategemea ukienda huko usiende na pochi? Na je simu unamwachia nani?

Zamani wakati visa zinashughulikiwa ubalozi wa Uingereza, kulikuwa na lockers nje unaweka simu yako na kupewa kikaratasi. Sasa hawa binafsi sijawaelewa.

La pili; Ukishaingia ndani ya compund, nje ya ofisi zao, mnapanga foleni hapo nje mmesimama, hakuna hata benchi la kukaa! Iwe mvua liwe jua! Nikajiuliza je, na wenye ulemavu inakuwaje? Wanashindwa nini kuweka shed fulani na benchi angalau watu wakae?

Kutafuta visa ya Marekani ni kama kutafuta ruhusa ya kwenda mbinguni, wakati wao, wanaweza hata kupata visa airport! WHY?

Naamini wakiambiwa wanaweza kujirekebisha. Hakuna sababu ya kutunyanya kiasi hicho!
Taarifa zilishatolewa ktk Ofisi za Balozi zao zote hapa duniani mara tu baada ya shambulizi la kigaidi ktk Balozi zao hapa Tanzania, Kenya na Uganda mwaka 1998
 
Kama hakuna ulazima kwako unaenda kufanya nini?. Hiyo ni viza ya kwenda mbinguni ndio maana inang'ang'ania nayo.

Hujasema ulivyaambiwa uache simu na pochi uliviachaje hapo? Kama uliacha kwa mlinzi ndio utaratibu huo

Ukikaa kwa utulivu ni rahisi kuachia mabomu uliyobeba. Ndio maana inatakiwa usimame ni rahisi mitambo yetu kutruck. Ukitisika tu hapo uliposimama tunajua unataka kuachia tiktak zako tunakuchomoa na risasi moja tu ya kichwa
 
Kama hakuna ulazima kwako unaenda kufanya nini?. Hiyo ni viza ya kwenda mbinguni ndio maana inang'ang'ania nayo.

Hujasema ulivyaambiwa uache simu na pochi uliviachaje hapo? Kama uliacha kwa mlinzi ndio utaratibu huo

Ukikaa kwa utulivu ni rahisi kuachia mabomu uliyobeba. Ndio maana inatakiwa usimame ni rahisi mitambo yetu kutruck. Ukitisika tu hapo uliposimama tunajua unataka kuachia tiktak zako tunakuchomoa na risasi moja tu ya kichwa
Sidhani kama uko sahihi
 
Kuna unyanyasaji nilioushuhudia ubalozi wa Marekani nilipoenda kushughulikia visa.

Kwanza pale getini, unaambiwa unaacha kila kitu huingii na chochote! Ila cha kushangaza, hawajaweka hata sehemu ya kuhifadhi mkoba au simu. Sasa sijui wanategemea ukienda huko usiende na pochi? Na je simu unamwachia nani?

Zamani wakati visa zinashughulikiwa ubalozi wa Uingereza, kulikuwa na lockers nje unaweka simu yako na kupewa kikaratasi. Sasa hawa binafsi sijawaelewa.

La pili; Ukishaingia ndani ya compund, nje ya ofisi zao, mnapanga foleni hapo nje mmesimama, hakuna hata benchi la kukaa! Iwe mvua liwe jua! Nikajiuliza je, na wenye ulemavu inakuwaje? Wanashindwa nini kuweka shed fulani na benchi angalau watu wakae?

Kutafuta visa ya Marekani ni kama kutafuta ruhusa ya kwenda mbinguni, wakati wao, wanaweza hata kupata visa airport! WHY?

Naamini wakiambiwa wanaweza kujirekebisha. Hakuna sababu ya kutunyanya kiasi hicho!
Urusi unakwenda bila visa.....china wapo mchakatoni....wamarekani ni wehu,,,,,,jirani na ubalozi kuna vigrosari fedenge uwe unaombea vitu vyako hapo,,,,hata hivyo si lazima kwenda marekani.
 
Huyu si alipigwa bani enzi za magu, na bado haijaondolewa? Hawezi hta kusogelea getini!
Sio getini tu Nchi yeyote iliyopo kwenye Jumuiya ya Madola hawezi kwenda nakumbuka alivyosema kwani lazima nije USA hata China naweza kwenda Balozi wa China hapo Daslm akamwambia malizana na USA kwanza ndio tutakupa visa huyo ni kama Msomali akigusa popote wanamkamata kama anabisha atoke...
 
Back
Top Bottom