DIDAS TUMAINI
JF-Expert Member
- Nov 11, 2014
- 234
- 657
Kulikuwa na timu iliyoitwa Everton kutoka kitongoji cha Merseyside cha jiji la Liverpool nchini England.
Timu hii ilikuwa ikitumia uwanja wa Anfield, uliokuwa ukimilikiwa na mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa klabu hiyo, John Houlding, mfanyabiashara mkubwa wa Freemason kutoka jiji la Liverpool.
Ukatokea mzozo mkubwa baina yake na bodi ya klabu, wajumbe wakipinga masharti yake mapya kwa Everton kuukodi uwanja wa Anfield.
Mzozo huo ukapelekea wajumbe kuamua kuihamisha timu kutoka uwanja wa Anfield na kujenga uwanja wao karibu yake na kuuita Goodson Park.
Freemason Houlding akabaki na uwanja bila timu, hivyo akaamua kuanzisha timu yake ili itumie ule uwanja.
Watu wa kitongoji cha Merseyside na jiji zima la Liverpool hawakulipenda wazo la Houlding la kuanzisha timu katika mji wao lao kwani hawakutaka timu nyingine katika mji wao zaidi ya Everton.
Freemason ni Freemason tu, akakomaa na wazo lake la kuanzisha timu, hadi likafanikiwa…timu hiyo ndiyo Liverpool FC.
Ule mgogoro wa uwanja na upinzani wa kuanzisha timu mpya ukasabisha uhasama mkubwa kati ya timu mpya, Liverpool FC, na ile kongwe, Everton FC.
Uhasama huu ndiyo ukazaa dabi kubwa katika kitongoji chao cha Merseyside inayoitwa Merseyside Derby.
Dabi ni dabi tu, hakuna raha kama kumuona mpinzani wako akiteseka kwa maumivu hasa uliyomsababishia wewe.
Ndiyo raha wanayoipata Everton muda huu. Kuwakatisha Liverpool matumaini ya ubingwa ni jambo kubwa kwao zaidi ya alama tatu walizozipata.
Timu hii ilikuwa ikitumia uwanja wa Anfield, uliokuwa ukimilikiwa na mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa klabu hiyo, John Houlding, mfanyabiashara mkubwa wa Freemason kutoka jiji la Liverpool.
Ukatokea mzozo mkubwa baina yake na bodi ya klabu, wajumbe wakipinga masharti yake mapya kwa Everton kuukodi uwanja wa Anfield.
Mzozo huo ukapelekea wajumbe kuamua kuihamisha timu kutoka uwanja wa Anfield na kujenga uwanja wao karibu yake na kuuita Goodson Park.
Freemason Houlding akabaki na uwanja bila timu, hivyo akaamua kuanzisha timu yake ili itumie ule uwanja.
Watu wa kitongoji cha Merseyside na jiji zima la Liverpool hawakulipenda wazo la Houlding la kuanzisha timu katika mji wao lao kwani hawakutaka timu nyingine katika mji wao zaidi ya Everton.
Freemason ni Freemason tu, akakomaa na wazo lake la kuanzisha timu, hadi likafanikiwa…timu hiyo ndiyo Liverpool FC.
Ule mgogoro wa uwanja na upinzani wa kuanzisha timu mpya ukasabisha uhasama mkubwa kati ya timu mpya, Liverpool FC, na ile kongwe, Everton FC.
Uhasama huu ndiyo ukazaa dabi kubwa katika kitongoji chao cha Merseyside inayoitwa Merseyside Derby.
Dabi ni dabi tu, hakuna raha kama kumuona mpinzani wako akiteseka kwa maumivu hasa uliyomsababishia wewe.
Ndiyo raha wanayoipata Everton muda huu. Kuwakatisha Liverpool matumaini ya ubingwa ni jambo kubwa kwao zaidi ya alama tatu walizozipata.