Uchawi na ushirikina sehemu za kazi unavyoteketeza wengi

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,675
698,690
Kuna kundi katika jamii wanaopinga uwepo wa uchawi na ushirikina hii si dhambi wala si kosa ni haki yao kutokana na makuzi uelewa imani na mazingira yao.

Lakini hili jambo lipo Sana kwenye kila nyanja ya maisha yetu, kwenye dini zetu biashara zetu,maisha yetu mitaani nk
Sehemu ambako uchawi na ushirikina vimetamalaki hasa ni sehemu zetu za kazi na bajeti kubwa huenda kwa waganga wa kienyeji ili tu;

-Kumuondoa fulani kwenye nafasi aliyonayo
-Apate cheo fulani
-Apate upendeleo fulani kazini
-Apate ajira
-Alinde ajira aliyo nayo
-Apate mamlaka na nguvu fulani za kiutawala na mamlaka

Ni katika michakato ya namna hii waganga hudanganya kuwa anayezuia hili au lile ni mfanyakazi Fulani au fulani ndio kaziba nyota yako.... mambo mengi ya jinsi hiyo...!!! Nafasi zenye hayo mambo sana ni ukurugenzi, secretary, transport officer, procurement public relations nk nk.

Ni wachache sana katika hao ambao mikono yao ni misafi na hawajawahi kushiriki hizi mambo. Vifo vingi vinavyotokea makazini sio kwa Mapenzi yao Mungu bali ni kurogana na kufanyiana, ushirikina, naamini kabisa wengi wetu hapa jamvini wana habari ya kusimulia kuwahusu haya vyovyote viwavyo.

Mungu ndie anayegawa riziki, na kila mtu ana kipimo chake, kufanya ushirikina na uchawi kwa ajili ya maslahi ya kazi ni kujitafutia laana isiyofutika.
 
Hali hii ipo sana kwenye taasisi za uma, na mashirika yake mathalani mwaka mmoja aliingia mkurugenzi mmoja ambaye kulikuwa na kila dalili za kupewa madaraka hayo kaka alikufa kifo cha ajabu mnoo
 
Hali hii ipo sana kwenye taasisi za uma, na mashirika yake mathalani mwaka mmoja aliingia mkurugenzi mmoja ambaye kulikuwa na kila dalili za kupewa madaraka hayo kaka alikufa kifo cha ajabu mnoo

Unakumbuka ishu ya bungeni wakati wa bunge la mzee wa spidi na viwango?
 
Kuna jamaa alienda kuripoti katika ofisi na kiti chake..hakutaka kuripoti na kukalia kile kiti...uchawi upo..
 
Hii nukuu nimeitoa katika Book of Ceremonial Magic by Arthur Waite which would seem to suggest ushirikina upo Vatican.

They belong to the late end of the eighteenth century. Dr. Encausse, the head of the French Martinists, suggests that they were all fabricated at Rome and infers--as seen previously--that we owe them to the industry of priests, which seems to follow somewhat loosely from the evidence, is characteristic of himself and his school, and is indeed of much the same value as the statement in Isis Unveiled,that the habitual practice of Black Magic at the Vatican could be ''easily proved''
 
Umesema kwel mkuu, makazini huko watu wanauana sana sie tulioajiriwa juzi na vielimu vyetu ndo shida zaid. Lkn yote ni kumuomba Mungu tu!
 
mmi shuuda nilipoajiliwa tasisi moja yakimataifa.l was around 29years assistant wangu was in the early 40s she tossed me left right kuingia offisin kichwa kilikua kinauma but ukitoka inje fresh. then one day madrivers walikuja kunipa pole ninavoteswa.one of them alijitolea kunisaidia alikua mpemba. since that day l started enjoying my office.
 
Unakuta mtu anabisha uwepo wa uchawi ila akikuta mayai yamevunjwa njia panda huku kukiwa hakuna harufu ya uwepo wa mkaanga chips karibu hayakanyagi.
 
Kweli kabisa, hali ni mbaya, huwezi hata kuonesha uwezo wako kazini kisa uoga wa kulogwa
 
Binafsi nimekuwa mhanga wa uchawi tangu nikiwa mtoto mdogo mpaka nilipopata deliverance hivi majuzi kwenye spiritual church.

I know what pains and suffering mtu anapitia akiwa amepigwa fusho...hexes, curse, warlock, evil eye, sorcerer, jin e.t.c

Asante Mungu wa Zumaridi kwa kunifungua,kuniponya na kuniweka huru sitakusahau siku zote za maisha yangu hapq duniani mungu uliyezitanda mbingu na nchi.

Hallelujah!
 
Back
Top Bottom