Tusiwachukulie poa wauza madafu

johnsonmgaya

JF-Expert Member
Oct 16, 2015
2,818
3,727
Nipo zangu feri kwenye kivuko cha Magogoni narudi nyumbani saa 7 mchana huu.

Kichwa hakiko Sawa maana “mchongo” niliofata town umebuma hivyo nikajiwazia zangu heri nirudi mapema nikacheze na watoto wangu tu atleast.

Mar pah macho yangu yanavutwa kutazama kundi la wauza madafu wengi wakiwa wamepaki baiskeli zao wakipiga story, kiukweli wanafuraha pengine kuliko mimi kwa siku ya leo

Nilichovutiwa zaidi ni kuwaona wakiwa na mabaki ya madafu mzigo wote waliopandisha nao town kwa siku ya leo wameshaumaliza na ndio kwanzaaa saa 7.

Sijawahi wahi vuka hapa muda kama huu pengine ndio maana nimejikuta nawashangaa hawa ndugu zangu leo pengine ndio maisha yao ya kila siku pengine saa 7 tu hivi wanakuwaga watamu wamemaliza Mali.

Swali nililo nalo hapa kichwani pengine nimesukumwa tu na wivu wangu kwao
Je, hawa jamaa wanaingiza bei gani?
Je, wanabeba madafu mengi kiasi gani?

Nafahamu bei moja ya Dafu mjini ni shilling 1000 tukijua kwa siku wanabeba madafu mangapi kwenye vikapu vyao tutajua wanajngiza kiasi gani kwa masaa 7 (sio siku)

Mwisho:
Vijana tuache ubishoo na upumbavu wa heri uwe chawa wa fulani wakati kuna kazi kama hizi fasta tu ukipiga au ukiwekeza ndani ya masaa yako 7 hukosi 50,000/- ya kuchagua na wewe chawa unaowataka.
 
Ukijituma Mungu atabariki hustles zako. Muhimu ni kujituma tu. Though sio siku zote wanamaliza madafu ndani ya saa 7 na 50K kama profit. Nguvu anayotumia kumaliza kuuza hayo madafu ni zaidi ya faida anayopata.
Mku umeandika vitu vichache sana ila vina maana kubwa sana,

Hapo kwenye nguvu anayotumiwa ni kubwa kuliko faida anayopata ndio hapo binadamu tupotofautiana mawazo,

Pengine ndio maana kuna watu wapo tu duniani kazi yao kuuza mawazo,

Ila. (Acha nitoe fursa ya bure hapa)

Mtu unaweza ukatafuta location nzuri Posta
ukajenga kiosk cha kiswahili (kizuri ila Chenye mandhari ya kishwahili) ie makuti au Mbao nk
Ukaweka benches nzuri za kuvutia
Ukawauza madafu labda na bites tu
Unaagiza mzigo mkubwa kidogo ambao unaweza siku siku 3/4 (kuondoa gharama ya usafiri )
Ukawa unauza hadi usiku kama inafaa Nina hakika
Faida ya 100,000 utaipata bila jasho wala nguvu.

Sidhani kama serikali (watu wa jiji) watakuzuia maana wauza miwa wanaruhusiwa.
 
Mku umeandika vitu vichache sana ila vina maana kubwa sana,

Hapo kwenye nguvu anayotumiwa ni kubwa kuliko faida anayopata ndio hapo binadamu tupotofautiana mawazo,

Pengine ndio maana kuna watu wapo tu duniani kazi yao kuuza mawazo,

Ila. (Acha nitoe fursa ya bure hapa)

Mtu unaweza ukatafuta location nzuri Posta
ukajenga kiosk cha kiswahili (kizuri ila Chenye mandhari ya kishwahili) ie makuti au Mbao nk
Ukaweka benches nzuri za kuvutia
Ukawauza madafu labda na bites tu,
Unaagiza mzigo mkubwa kidogo ambao unaweza siku siku 3/4 (kuondoa gharama ya usafiri )
Ukawa unauza hadi usiku kama inafaa Nina hakika
Faida ya 100,000 utaipata bila jasho wala nguvu.

Sidhani kama serikali (watu wa jiji) watakuzuia maana wauza miwa wanaruhusiwa.
Excellent Idea 👏👏👏👏 unapata faida safi na mwili hauchoki ingawa madafu ni bidhaa inayotakiwa kuisha siku hiyo hiyo. Dafu likilala linapungua ubora.
 
Still sio rahisi kama unavyofikria. Pengne Leo wamepiga hela kuliko sku zingine, hata hvyo hujawauliza Gharama za uendeshaji na Adha zingine
 
Mkuu wewe ni kabila gani? Naona neno pengine limetumika sana kwenye andiko lako usijekua poti.
 
Still sio rahs kama unavyofkria. Pengne Leo wamepiga hela kuliko sku zingine , hata hvyo hujawauliza Gharama za uendeshaji na Adha zingine

Kwa kuwa walikuwa wengi na wote wapo comfortable, kusema kuwa ni zali la mentali tu leo sishawishiki kukubali.

Ila Nina hakika hii ndio ratiba yao ya kila siku.

Ofcoz kila kitu kina gharama ya uendeshaji, kwa biashara hii labda gharama ni manpower.

Kufata mzigo shambani, kuendesha baiskeli yenye mzigo toka huko shamba hadi mjini kila siku na hata huko mjini kwenyewe hawakai tu sehemu moja. Hivyo ukiacha na Gharama ya nguvu hakuna nyingine.
 
Kwa kuwa walikuwa wengi na wote wapo comfortable, kusema kuwa ni zali la mentali tu leo sishawishiki kukubali.

Ila Nina hakika hii ndio ratiba yao ya kila siku.

Ofcoz kila kitu kina gharama ya uendeshaji, kwa biashara hii labda gharama ni manpower.

Kufata mzigo shambani, kuendesha baiskeli yenye mzigo toka huko shamba hadi mjini kila siku na hata huko mjini kwenyewe hawakai tu sehemu moja. Hivyo ukiacha na Gharama ya nguvu hakuna nyingine.
Pata mda uwaulize wana mda gan wanafanya hii kazi wakikuambia ni Zaid ya miaka mitano, bas jua hela wanayopata hapo ni hela ya Kula. Miaka mitano inatosha kabisa kumtoa mtu level moja kwenda nyingine kama inalipa.
 
Nipo zangu feri kwenye kivuko cha magogoni narudi nyumbani saa 7 mchana huu,
Kichwa hakiko Sawa maana “mchongo” niliofata town umebuma hivyo nikajiwazia zangu heri nirudi mapema nikacheze na watoto wangu tu atleast,

Mar pah macho yangu yanavutwa kutazama kundi la wauza madafu wengi wakiwa wamepaki baiskeli zAo wakipiga story, kiukweli wanafuraha pengine kuliko mimi kwa siku ya leo

Nilichovutiwa zaidi ni kuwaona wakiwa na mabaki ya madafu mzigo wote waliopandisha nao town kwa siku ya leo wameshaumaliza na ndio kwanzaaa saa 7.

Sijawahi wahi vuka hapa muda kama huu pengine ndio maana nimejikuta nawashangaa hawa ndugu zangu leo pengine ndio maisha yao ya kila siku pengine saa 7 tu hivi wanakuwaga watamu wamemaliza Mali.

Swali nililo nalo hapa kichwani pengine nimesukumwa tu na wivu wangu kwao
Je hawa jamaa wanaingiza bei gani?
Je wanabeba madafu mengi kiasi gani?
Nafahamu bei moja ya Dafu mjini ni shilling 1000 tukijua kwa siku wanabeba madafu mangapi kwenye vikapu vyao tutajua wanajngiza kiasi gani kwa masaa 7 (sio siku)

Mwisho:
Vijana tuache ubishoo na upumbavu wa heri uwe chawa wa fulani wakati kuna kazi kama hizi fasta tu ukipiga au ukiwekeza ndani ya masaa yako 7 hukosi 50,000/- ya kuchagua na wewe chawa unaowataka.
ukiipenda biashara yako na ni ya halali basi mungu nae hakutupi kwenye mafanikio
 
Mkuu wewe ni kabila gani?? naona neno pengine limetumika sana kwenye andiko lako usijekua poti
Kama ni jina halisi Mgaya ni wahehe.

Turudi kwa mleta uzi.

Dafu linaanzia kuuzwa 500. Tukikubali bei uliyotaja ya 1000 na kusema muuzaji kaingiza 50K inamaanisha alitoka na madafu 50.

Swali kwako mleta uzi. Umewahi kukutana na muuza madafu kapakia madafu 50 kwenye baiskeli?
 
Kama ni jina halisi Mgaya ni wahehe.

Turudi kwa mleta uzi.

Dafu linaanzia kuuzwa 500. Tukikubali bei uliyotaja ya 1000 na kusema muuzaji kaingiza 50K inamaanisha alitoka na madafu 50.

Swali kwako mleta uzi. Umewahi kukutana na muuza madafu kapakia madafu 50 kwenye baiskeli?
Madafu 50 unaona ni mengi sana au?
 
Kama ni jina halisi Mgaya ni wahehe.

Turudi kwa mleta uzi.

Dafu linaanzia kuuzwa 500. Tukikubali bei uliyotaja ya 1000 na kusema muuzaji kaingiza 50K inamaanisha alitoka na madafu 50.

Swali kwako mleta uzi. Umewahi kukutana na muuza madafu kapakia madafu 50 kwenye baiskeli?

Dafu mjini ni 1,000/-
image-2021-01-19-11:23:59-209.jpg


Kwa ujazo wa hivi vitenga 3 kila moja wanauwezo wa kubeba 20 20, so ni equivalent idadi ya 60.
 
Pata mda uwaulize wana mda gan wanafanya hii kazi wakikuambia ni Zaid ya miaka mitano, bas jua hela wanayopata hapo ni hela ya Kula... Miaka mitano inatosha kabisa kumtoa mtu level moja kwenda nyingine kama inalipa

Mkuu usinichekeshe aisee,
Kwenye maisha sio kipato pekee ndio kinabadilisha maisha ya mtu,
Akili ndio kila kitu kwenye maisha

Kuna watu wanavipato vikuu lakini hawana hata viwanja, kuna watu wana mishahara mikubwa lakini hawana hata biashara pembeni kama backup,

Kwa mada yetu hii iliyopo mezani kitu cha kujiuliza hapa ni kwamba hawa watu haya madafu wananunua huko mashambani? Kwa bei gani? Je wananunua moja moja au mti mzima?

Tukijua hili tutajua cash on hand baada ya kutoa gharama zote ni kiasi gani, na je wanajtumia kweli hiyo faida wanayobaki nayo?

Kwa maisha haya ukiwa na uhakika wa kulaza 10,000/- tu bank kila siku wewe ni kidume.
 
Mkuu usinichekeshe aisee,
Kwenye maisha sio kipato pekee ndio kinabadilisha maisha ya mtu,
Akili ndio kila kitu kwenye maisha

Kuna watu wanavipato vikuu lakini hawana hata viwanja, kuna watu wana mishahara mikubwa lakini hawana hata biashara pembeni kama backup,

Kwa mada yetu hii iliyopo mezani kitu cha kujiuliza hapa ni kwamba hawa watu haya madafu wananunua huko mashambani? Kwa bei gani? Je wananunua moja moja au mti mzima?

Tukijua hili tutajua cash on hand baada ya kutoa gharama zote ni kiasi gani, na je wanajtumia kweli hiyo faida wanayobaki nayo?

Kwa maisha haya ukiwa na uhakika wa kulaza 10,000/- tu bank kila siku wewe ni kidume.
We jamaa vip, kulaza 10000 Kwa sku hyo ni hela ya Kula , hakuna kitu hapo jombaa, kununua kiwanja huo ni uoga wa maisha , mzungu hanunui kiwanja ye ananunua nyumba .... Kuwa na pesa ya kutosha ndo mpango mzima regadless huna nyumba au kiwanja.... Pesa ndo kila kitu mzee, we kuwa na akili alaf mwenzako awe na hela uone kama hutaonekana kinyesi Tu hapa mjin
 
We jamaa vip, kulaza 10000 Kwa sku hyo ni hela ya Kula , hakuna kitu hapo jombaa, kununua kiwanja huo ni uoga wa maisha , mzungu hanunui kiwanja ye ananunua nyumba .... Kuwa na pesa ya kutosha ndo mpango mzima regadless huna nyumba au kiwanja.... Pesa ndo kila kitu mzee, we kuwa na akili alaf mwenzako awe na hela uone kama hutaonekana kinyesi Tu hapa mjin



Nakosa cha kuandika!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom