Tundu Lissu: Kuna ushirika wa ajabu unashambulia hotuba zangu, yupo Kinana, Nape na Halima Mdee

Heparin

Senior Member
Sep 24, 2021
153
577
Tundu Lissu ameendelea na Mikutano ya Hadhara na leo yupo wilaya ya Mpwapwa ambapo pamoja na mambo mengine amesema tangu atoe hoja zake siku ya Muungano, Aprili 26, 2024, wamekuwepo watu wengi wanaomshambulia akiwemo Abdulrahman Kinana, Nape Nnauye na Halima Mdee ambaye kwa maneno yake kamuita Mbunge wa COVID 19, mbunge asiye na chama.

"Kwanza nifanye ufafanuzi wa jambo moja katika hayo ninayotaka yasikilizwe na Watanzania walioko nje ya hapa. Wiki hii na ile iliyopita kuba kelele nyingi sana zinzonihusu, au hamjazisikia? Tarehe 26 nilizungumza habari ya Muungano kwa sababu ilikuwa ni siku ya sherehe ya muungano." amesema.

Lissu ameendelea kusema "Hiyo mikutano 5 niliyofanya imezua taharuki kubwa kwelikweli, ukisikiliza kwa makini yanayosemwa utafikiri nimeua binadamu, sijaua. Mawe nayorushiwa utafikiri nimefanya kosa gani sijui, sijafanya kosa la jinai na ingekuwa vile ningekuwa nimeshtakiwa na kukamatwa na hawa maaskari ambao mara nyingi huwa wanatumwa kuja kunikatama. Sijakamatwa kwa kuwa hakuna kosa"

"Kuna shida gani? nimezungumza matatizo ya muungano na katiba yetu, nilipokuwa Iringa nilizungumza tuwe macho na pesa za Abdul na mama yake kwa sababu zinatumika kuchafua chaguzi zetu. Hakuna anayesema nimedanganya, wengine wananiambia aaaah ungeyasemea ndani. Hii rushwa inayoangamiza taifa unatakiwa uizungumzie ndani"

"Kuna ushirika wa ajabu unaonishambulia wanasema haya mambo yazungumziwe ndani ukizungumza hadharani unakichafua chama. Hapana ukizungumza hadharani kukemea rushwa unasafisha chama, unaonesha wananchama kwamba chama chetu hakitaki rushwa”.

"Sasa, katika hao waliopiga kelele ni hawa wafuatao, Abdulrahman Kinana, Amos Makalla, Nape Nnauye bungeni, na niliona ajabu kidogo Halima Mdee COVID 19 wale wabunge wanawake waliokuwa Chadema waliohongwa na Ndugai na Magufuli wakaapishwa uchochoroni na yeye amelalamikia hotuba yangu ya Iringa"

Lissu amesema hatakoma kuzungumza kwani Rushwa imenunua watu wengi kutoka Chadema ikiwemo makatibu wakuu waliopita na ni kweli pia Rais Samia anauza maeneo kama alivyobainisha awali.
 
Kuna ushirika wa ajabu unaonishambulia wanasema haya mambo yazungumziwe ndani ukizungumza hadharani unakichafua chama. Hapana ukizungumza hadharani kukemea rushwa unasafisha chama, unaonesha wananchama kwamba chama chetu hakitaki rushwa”.
Hapa yuko sahihi...

Haya mambo ya kujificha ndiyo yanaleta ule uongo wa kina Lema na mambo ya fadhila...
 
Tundu Lissu ameendelea na Mikutano ya Hadhara na leo yupo wilaya ya Mpwapwa ambapo pamoja na mambo mengine amesema tangu atoe hoja zake siku ya Muungano, Aprili 26, 2024, wamekuwepo watu wengi wanaomshambulia akiwemo Abdulrahman Kinana, Nape Nnauye na Halima Mdee ambaye kwa maneno yake kamuita Mbunge wa COVID 19.

"Kwanza nifanye ufafanuzi wa jambo moja katika hayo ninayotaka yasikilizwe na Watanzania walioko nje ya hapa. Wiki hii na ile iliyopita kuba kelele nyingi sana zinzonihusu, au hamjazisikia? Tarehe 26 nilizungumza habari ya Muungano kwa sababu ilikuwa ni siku ya sherehe ya muungano." amesema.

Lissu ameendelea kusema "Hiyo mikutano 5 niliyofanya imezua taharuki kubwa kwelikweli, ukisikiliza kwa makini yanayosemwa utafikiri nimeua binadamu, sijaua. Mawe nayorushiwa utafikiri nimefanya kosa gani sijui, sijafanya kosa la jinai na ingekuwa vile ningekuwa nimeshtakiwa na kukamatwa na hawa maaskari ambao mara nyingi huwa wanatumwa kuja kunikatama. Sijakamatwa kwa kuwa hakuna kosa"

"Kuna shida gani? nimezungumza matatizo ya muungano na katiba yetu, nilipokuwa Iringa nilizungumza tuwe macho na pesa za Abdul na mama yake kwa sababu zinatumika kuchafua chaguzi zetu. Hakuna anayesema nimedanganya, wengine wananiambia aaaah ungeyasemea ndani. Hii rushwa inayoangamiza taifa unatakiwa uizungumzie ndani"

"Kuna ushirika wa ajabu unaonishambulia wanasema haya mambo yazungumziwe ndani ukizungumza hadharani unakichafua chama. Hapana ukizungumza hadharani kukemea rushwa unasafisha chama, unaonesha wananchama kwamba chama chetu hakitaki rushwa”.

"Sasa, katika hao waliopiga kelele ni hawa wafuatao, Abdulrahman Kinana, Amos Makalla, Nape Nnauye bungeni, na niliona ajabu kidogo Halima Mdee COVID 19 wale wabunge wanawake waliokuwa Chadema waliohongwa na Ndugai na Magufuli wakaapishwa uchochoroni na yeye amelalamikia hotuba yangu ya Iringa"

Lissu amesema hatakoma kuzungumza kwani Rushwa imenunua watu wengi kutoka Chadema ikiwemo makatibu wakuu waliopita na ni kweli pia Rais Samia anauza maeneo kama alivyobainisha awali.
Akimaliza kuropokwa arudi kwao ubelgiji
 
Hotuba zake zinashambuliwa na watqnzania wote, ni za kishenzi na kibaguzi
 
Mdee na wenzake wameanza harakati za kutafuta malisho pengine, kituo kinachofuata kinaweza kuwa ni CCM.
 
Tundu Lissu ameendelea na Mikutano ya Hadhara na leo yupo wilaya ya Mpwapwa ambapo pamoja na mambo mengine amesema tangu atoe hoja zake siku ya Muungano, Aprili 26, 2024, wamekuwepo watu wengi wanaomshambulia akiwemo Abdulrahman Kinana, Nape Nnauye na Halima Mdee ambaye kwa maneno yake kamuita Mbunge wa COVID 19, mbunge asiye na chama.

"Kwanza nifanye ufafanuzi wa jambo moja katika hayo ninayotaka yasikilizwe na Watanzania walioko nje ya hapa. Wiki hii na ile iliyopita kuba kelele nyingi sana zinzonihusu, au hamjazisikia? Tarehe 26 nilizungumza habari ya Muungano kwa sababu ilikuwa ni siku ya sherehe ya muungano." amesema.

Lissu ameendelea kusema "Hiyo mikutano 5 niliyofanya imezua taharuki kubwa kwelikweli, ukisikiliza kwa makini yanayosemwa utafikiri nimeua binadamu, sijaua. Mawe nayorushiwa utafikiri nimefanya kosa gani sijui, sijafanya kosa la jinai na ingekuwa vile ningekuwa nimeshtakiwa na kukamatwa na hawa maaskari ambao mara nyingi huwa wanatumwa kuja kunikatama. Sijakamatwa kwa kuwa hakuna kosa"

"Kuna shida gani? nimezungumza matatizo ya muungano na katiba yetu, nilipokuwa Iringa nilizungumza tuwe macho na pesa za Abdul na mama yake kwa sababu zinatumika kuchafua chaguzi zetu. Hakuna anayesema nimedanganya, wengine wananiambia aaaah ungeyasemea ndani. Hii rushwa inayoangamiza taifa unatakiwa uizungumzie ndani"

"Kuna ushirika wa ajabu unaonishambulia wanasema haya mambo yazungumziwe ndani ukizungumza hadharani unakichafua chama. Hapana ukizungumza hadharani kukemea rushwa unasafisha chama, unaonesha wananchama kwamba chama chetu hakitaki rushwa”.

"Sasa, katika hao waliopiga kelele ni hawa wafuatao, Abdulrahman Kinana, Amos Makalla, Nape Nnauye bungeni, na niliona ajabu kidogo Halima Mdee COVID 19 wale wabunge wanawake waliokuwa Chadema waliohongwa na Ndugai na Magufuli wakaapishwa uchochoroni na yeye amelalamikia hotuba yangu ya Iringa"

Lissu amesema hatakoma kuzungumza kwani Rushwa imenunua watu wengi kutoka Chadema ikiwemo makatibu wakuu waliopita na ni kweli pia Rais Samia anauza maeneo kama alivyobainisha awali.
Rushwa na CCM ni sawa na uji na mgonjwa.
 
Aweke akiba ya maneno maana Mdee 2025 anarudi kundini
mdee na wenzake hao ni wadudu wa COVID19 kamwe wasikubaliwe kurudi CHADEMA. Walishaonekana ni wasaliti na si waaminifu, waende CCM na vyama vingine wakafanye siasa huko
 
Back
Top Bottom