Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,717
Wakati nilipokuwa na umri mdogo kule kijijini nilikuwa nimezoea mara nyingi sana wakati tukiwa kwenye harakati za shambani au kutafuta kuni huku nikiwa na baba na vijana wengine wakubwa,walipokuwa wanajisaidia haja ndogo halafu akatokea mwanamke au binti hurudi kwa kasi sana kule alikotoka ili asione utupu wa anaejisaidia haja ndogo
Leo nimejikuta nikijiuliza maswali mengi sana kuhusiana na hili
Ni kwamba,nilikuwa natoka eneo moja na kwenda lingine,huku nikiwa na safari yangu kwa miguu nilikuwa nimeongozana na wadada wawili,wao walikuwa mbele mimi nilikuwa nyuma na walikuwa wanaongea mambo tofauti tofauti,kama mjuavyo uswazi kuna vinjia vingi na vingine ni vya vichochoro sana,nasi tulipitia kwenye kichochoro kimoja na ghafla binti mmoja alistuka na kusimama na yule mwingine nae alisimama na kisha kumuuliza mwenzake "kuna nini"?
Yule binti mwingine alimuambia "humuoni huyo jamaa hapo anakojoa"?,yule mwingine akamwambia "sasa ndio ustuke hivyo? Mbona umesimama?,mwenzake akamjibu "Huoni anajisaidia"? mwingine akamuambia "sasa cha ajabu nini? Si twende"?,waliendelea na safari yao na wakati huo nilikuwa nimewapita baada ya kubishana pale njiani
Ilibidi sasa fikra zangu zihamia kwa hawa madada na mara kwa mara nilikuwa nageuka kuwaangalia,Wakati wanamkaribia yule jamaa aliyekuwa anajisaidia walimgeukia na kumuangalia kisha wakaendelea na mmoja wao alisema nadhani ni yule ambae alimshangaa mwenzake kusita kuendelea kutembea alipomuona huyu jamaa anajisaidia haja ndogo kwakuwa nilikuwa naangalia mbele na wao walikuwa nyuma yangu,huyu dada alimuambia mwenzake "mi nakushangaa sana kwa kushindwa kuendelea saa ile,mbona tumeshaona nyingi tu"?
Mwenzake alicheka na kuitikia "ni kweli lakini",nilijikuta natafakari mengi sana,hawa mabinti walikuwa ni wadogo sana kiumri na kama ni kweli wakisemacho basi huko beleni inaweza kuja kuwa ni hatari sana ,kama binti mdogo kama yule "ameshaona nyingi" vipi akikua?
Nimestaajabu sana jioni ya leo ....!!
Leo nimejikuta nikijiuliza maswali mengi sana kuhusiana na hili
Ni kwamba,nilikuwa natoka eneo moja na kwenda lingine,huku nikiwa na safari yangu kwa miguu nilikuwa nimeongozana na wadada wawili,wao walikuwa mbele mimi nilikuwa nyuma na walikuwa wanaongea mambo tofauti tofauti,kama mjuavyo uswazi kuna vinjia vingi na vingine ni vya vichochoro sana,nasi tulipitia kwenye kichochoro kimoja na ghafla binti mmoja alistuka na kusimama na yule mwingine nae alisimama na kisha kumuuliza mwenzake "kuna nini"?
Yule binti mwingine alimuambia "humuoni huyo jamaa hapo anakojoa"?,yule mwingine akamwambia "sasa ndio ustuke hivyo? Mbona umesimama?,mwenzake akamjibu "Huoni anajisaidia"? mwingine akamuambia "sasa cha ajabu nini? Si twende"?,waliendelea na safari yao na wakati huo nilikuwa nimewapita baada ya kubishana pale njiani
Ilibidi sasa fikra zangu zihamia kwa hawa madada na mara kwa mara nilikuwa nageuka kuwaangalia,Wakati wanamkaribia yule jamaa aliyekuwa anajisaidia walimgeukia na kumuangalia kisha wakaendelea na mmoja wao alisema nadhani ni yule ambae alimshangaa mwenzake kusita kuendelea kutembea alipomuona huyu jamaa anajisaidia haja ndogo kwakuwa nilikuwa naangalia mbele na wao walikuwa nyuma yangu,huyu dada alimuambia mwenzake "mi nakushangaa sana kwa kushindwa kuendelea saa ile,mbona tumeshaona nyingi tu"?
Mwenzake alicheka na kuitikia "ni kweli lakini",nilijikuta natafakari mengi sana,hawa mabinti walikuwa ni wadogo sana kiumri na kama ni kweli wakisemacho basi huko beleni inaweza kuja kuwa ni hatari sana ,kama binti mdogo kama yule "ameshaona nyingi" vipi akikua?
Nimestaajabu sana jioni ya leo ....!!