TRA mnajisikiaje kukamua kodi kutoka kwa wafanyabiashara wanaopata hasara kwa kukosa umeme na maji?

Ukiamka vizuri Huwa unakuwa na hoja ,usikilizwe
Nadhani TRA wakae na Wizara za Kisekta kuwaelimisha utendaji unaolinda uchumi wa Taifa
Ukiangalia rationale ya mgao na hata sababu za kukosa umeme wa uhakika asilimia kubwa ni ukiritimba kwenye taratibu za manunuzi.

Niwape mfano mmoja hai. TTCL imekuja na mradi maridhawa wa Fiber Mlangoni kwako. Maeneo mengi wameshaanza kutandaza miundombinu lakini mradi umesimama zaidi ya mwaka wamesimamisha ukamilishwaji wa mradi, ukiwauliza wanasema taratibu za manunuzi...

Tukija kwenye sekta ya maji, inakuwaje watu wanakosa maji ilihali serikali imewekeza mtandao wa maji katibu nchi nzima?

Hizi hujuma zitokanazo na uzembe ama makusudi zinakwamisha ukuaji wa mitaji hususan hupelekea uwekezaji kuwa mchungu zaidi
 
TRA Tanzania hii hoja naiweka mezani kwenu.

Mnakusanya kodi kwa niaba yetu ili tuweze kuwekeza kwenye maendeleo ya nchi.

Lakini sasa, serikali inashindwa kuprovide umeme wa uhakika na kupelekea gharama za uzalishaji kuwa juu kwa sababu ya kutumia vyanzo mbadala vya nishati ya umeme.

Anguko la wafanyabiashara hususani viwandani na wasindikaji ni kubwa sana. Najiuliza, TRA mnapata guts gani kufurahia kukusanya kodi kutoka kwa wawekezaji wanaoporomoka kiuchumi?

Tuelimishane hapa
Haya ni maoni yangu na nipo tayari kukosolewa maa na sote tunajifunza. Nachoelewa mimi TRA kazi yao kubwa ni kukusanya kodi na bungeni kwa Spika Tulia baada ya Waziri wa fedha kupeleka mswada hukubaliana wabunge namna ya matumizi.

Sasa kwenye changamoto za umeme sidhani kama TRA ukiwahusisha ni sawa maana wafanyabiashara kuna changamoto nyingi ambazo zinaweza kufanya mapato yao yakashuka. Mfano wale waliokuwa Manyara na kukumbana na lile janga ili waweze rejea tena ni changamoto. Sidhani kama tra wanafurahia sababu kuanguka kwa biashara ni kusababisha kodi kupungua. Ila kinachobainisha mapato ya mfanyabioahsra ni records na wengi hapa ndipo tunapofisha ukweli . Wapo wachache wanaosababisha wengi tuonekane ni waongo kwa kuweka taarifa ambazo si za kweli.

Kama TRA wanatangaza mafanikio katika kukusanya sioni kama jambo baya maana kama ulivyosema inasaidia katika maendeleo ya nchi yetu sote. Ikivuka malengo ni jambo zuri. Mradi ni kwamba makusanyo siyo ya kimabavu.
 
Haya ni maoni yangu na nipo tayari kukosolewa maa na sote tunajifunza. Nachoelewa mimi TRA kazi yao kubwa ni kukusanya kodi na bungeni kwa Spika Tulia baada ya Waziri wa fedha kupeleka mswada hukubaliana wabunge namna ya matumizi.

Sasa kwenye changamoto za umeme sidhani kama TRA ukiwahusisha ni sawa maana wafanyabiashara kuna changamoto nyingi ambazo zinaweza kufanya mapato yao yakashuka. Mfano wale waliokuwa Manyara na kukumbana na lile janga ili waweze rejea tena ni changamoto. Sidhani kama tra wanafurahia sababu kuanguka kwa biashara ni kusababisha kodi kupungua. Ila kinachobainisha mapato ya mfanyabioahsra ni records na wengi hapa ndipo tunapofisha ukweli . Wapo wachache wanaosababisha wengi tuonekane ni waongo kwa kuweka taarifa ambazo si za kweli.

Kama TRA wanatangaza mafanikio katika kukusanya sioni kama jambo baya maana kama ulivyosema inasaidia katika maendeleo ya nchi yetu sote. Ikivuka malengo ni jambo zuri. Mradi ni kwamba makusanyo siyo ya kimabavu.
Hawatoi elemu ya kutuza hizo record wanacho jua wao ni kukusanya tu
 
Haya ni maoni yangu na nipo tayari kukosolewa maa na sote tunajifunza. Nachoelewa mimi TRA kazi yao kubwa ni kukusanya kodi na bungeni kwa Spika Tulia baada ya Waziri wa fedha kupeleka mswada hukubaliana wabunge namna ya matumizi.

Sasa kwenye changamoto za umeme sidhani kama TRA ukiwahusisha ni sawa maana wafanyabiashara kuna changamoto nyingi ambazo zinaweza kufanya mapato yao yakashuka. Mfano wale waliokuwa Manyara na kukumbana na lile janga ili waweze rejea tena ni changamoto. Sidhani kama tra wanafurahia sababu kuanguka kwa biashara ni kusababisha kodi kupungua. Ila kinachobainisha mapato ya mfanyabioahsra ni records na wengi hapa ndipo tunapofisha ukweli . Wapo wachache wanaosababisha wengi tuonekane ni waongo kwa kuweka taarifa ambazo si za kweli.

Kama TRA wanatangaza mafanikio katika kukusanya sioni kama jambo baya maana kama ulivyosema inasaidia katika maendeleo ya nchi yetu sote. Ikivuka malengo ni jambo zuri. Mradi ni kwamba makusanyo siyo ya kimabavu.
Umeeleza vyema kabisa.
Kwa minajili ya ukusanyaji kodi maridhawa je TRA wanatimiza wajibu wao au ni walipakodi ndo wanapaswa kutimiza wajibu wasioujua?
 
Hawatoi elemu ya kutuza hizo record wanacho jua wao ni kukusanya tu
Nadhani ni eneo ambalo kama wanaona ni pazuri pa kuanzia elimu endelevu ili sote tuelewe na tuweze fanya biashara zetu bila tatizo lolote
 
Haya ni maoni yangu na nipo tayari kukosolewa maa na sote tunajifunza. Nachoelewa mimi TRA kazi yao kubwa ni kukusanya kodi na bungeni kwa Spika Tulia baada ya Waziri wa fedha kupeleka mswada hukubaliana wabunge namna ya matumizi.

Sasa kwenye changamoto za umeme sidhani kama TRA ukiwahusisha ni sawa maana wafanyabiashara kuna changamoto nyingi ambazo zinaweza kufanya mapato yao yakashuka. Mfano wale waliokuwa Manyara na kukumbana na lile janga ili waweze rejea tena ni changamoto. Sidhani kama tra wanafurahia sababu kuanguka kwa biashara ni kusababisha kodi kupungua. Ila kinachobainisha mapato ya mfanyabioahsra ni records na wengi hapa ndipo tunapofisha ukweli . Wapo wachache wanaosababisha wengi tuonekane ni waongo kwa kuweka taarifa ambazo si za kweli.

Kama TRA wanatangaza mafanikio katika kukusanya sioni kama jambo baya maana kama ulivyosema inasaidia katika maendeleo ya nchi yetu sote. Ikivuka malengo ni jambo zuri. Mradi ni kwamba makusanyo siyo ya kimabavu.
labda nikusaidie kidogo tripleec. Nachoelewa ni kuwa kimahesabu tra wao wanakata kodi kwa aina mbili kwa wasiotunza kumbukumbu wale wadogo na kuna wale wanautunza kumbukumbu . Maana yake ni kwamba kama kuna garama za kibiashara basi unachukua mauzo yako na kutoa garama zile za bishara kinachobaki kinatozwa kodi. Hawa wasiotunza na wengi ni wale wadogo hata kodi yao imewekwa kwenye madaraja nalikumbuka moja tu la 100,000 kwa wale wenye mauzo ya 4,000,001 mpaka 7,000,000 kwa mwaka.Nadhani cha msingi ni kama alivyosema mdau kupata uelewa wa pamoja umuhimu wa hizi kumbukumbu ( elimu) ili kuondokana na dhana nzima kuwa ukipata garama za kibiashara hazikubaliki
 
TRA Tanzania hii hoja naiweka mezani kwenu.

Mnakusanya kodi kwa niaba yetu ili tuweze kuwekeza kwenye maendeleo ya nchi.

Lakini sasa, serikali inashindwa kuprovide umeme wa uhakika na kupelekea gharama za uzalishaji kuwa juu kwa sababu ya kutumia vyanzo mbadala vya nishati ya umeme.

Anguko la wafanyabiashara hususani viwandani na wasindikaji ni kubwa sana. Najiuliza, TRA mnapata guts gani kufurahia kukusanya kodi kutoka kwa wawekezaji wanaoporomoka kiuchumi?

Tuelimishane hapa
Mlipakodi anatakiwa kulipa kodi ya mapato kulingana na kile anachokipata. Na kwenye kutafuta kile alichopata tunachukua mauzo tunatoa na gharama za kuendeshea shughuli yake ya uchumi. Muhimu ni kwa kila anachonunua kuwe na risiti ya EFD inayothibitisha manunuzi yake. Pia atatoa gharama zingine kama kuwalipa wafanyakazi n.k..

MAKADIRIO YA KODI:
Tunaomba pia wale wote ambao hawajakadiria kodi ya mapato ya mwaka 2024 waweze kufanya hivyo ili wasipate adhabu pale wanapochelewa kufanya makadirio baada ya tarehe 31 Machi 2024. Pamoja Tunajenga Taifa Letu.
 
Mlipakodi anatakiwa kulipa kodi ya mapato kulingana na kile anachokipata. Na kwenye kutafuta kile alichopata tunachukua mauzo tunatoa na gharama za kuendeshea shughuli yake ya uchumi. Muhimu ni kwa kila anachonunua kuwe na risiti ya EFD inayothibitisha manunuzi yake. Pia atatoa gharama zingine kama kuwalipa wafanyakazi n.k..

MAKADIRIO YA KODI:
Tunaomba pia wale wote ambao hawajakadiria kodi ya mapato ya mwaka 2024 waweze kufanya hivyo ili wasipate adhabu pale wanapochelewa kufanya makadirio baada ya tarehe 31 Machi 2024. Pamoja Tunajenga Taifa Letu.
Nashukuru kwa jibu fupi linaloeleweka.

Natumaini mtatimiza wajibu wenu kwa kutoa elimu kwa mlipakodi huausani wakati huu ambao mazingira yameongeza gharama za uendeshaji
 
Mlipakodi anatakiwa kulipa kodi ya mapato kulingana na kile anachokipata. Na kwenye kutafuta kile alichopata tunachukua mauzo tunatoa na gharama za kuendeshea shughuli yake ya uchumi. Muhimu ni kwa kila anachonunua kuwe na risiti ya EFD inayothibitisha manunuzi yake. Pia atatoa gharama zingine kama kuwalipa wafanyakazi n.k..

MAKADIRIO YA KODI:
Tunaomba pia wale wote ambao hawajakadiria kodi ya mapato ya mwaka 2024 waweze kufanya hivyo ili wasipate adhabu pale wanapochelewa kufanya makadirio baada ya tarehe 31 Machi 2024. Pamoja Tunajenga Taifa Letu.
Maelezo mafupi ila yamebeba maana kubwa sana.
 
Mamlaka ya mapato Tanzania ni chombo muhimu sana ktk kuijenga nchi kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni. TRA wana majukumu makubwa ya kukusanya mapato ili kufanikisha ulipaji wa gharama mbalimbali Za kuendesha Serikali (Matumizi,Miradi,Ulipaji madeni yanayokopwa nje na ndani).

Kimsingi sheria Za kodi za Tanzania ni photocopy ya sheria Za kodi toka ktk mataifa yaliondelea kiuchumi kama Uingereza hivyo ni sheria ngumu kwa kuzingatia utofauti wa mifumo ya kiuchumi,Elimu na uwezeshaji.

Miaka michache iliopita Wafanyabiashara,wajasiliamali na Wawekezaji walipitia kwenye ubatizo wa moto kutokana na approach Za ubabe, maguvu. Vilivyoenda sambamba na Uporaji mali,Rushwa na ukosefu wa uadirifu,Makadirio kandamizi.

Maafisa wengi wa TRA na wengine kupitia TASK FORCE walitajirika sana kupitia ukandamizaji,Unyongaji biashara,Uharamia wa kimamlaka..Ufungaji biashara,Ukwapuaji fedha kwenye akaunti za wafanyabiashara. Michakato hii ilipekekea wafanyabiashara wengi kufirisika,kufunga biashara,kujiua,Kukimbia nchi,Kuhamisha biashara na uwekezaji wao.

Mambo yamerudi yamerudi upya sasa..Maafisa kodi,Mameneja na waandamizi wamevaa koti na mavazi mapya ya Tax force. Wafanyabiashara wameanza kuishi kama digidigi, hofu, wasiwasi, huzuni na kukosa tumaini. Maafisa wamegeuka miungu watu. Mfanyabiashara anaamka anakuta EFD zimefungwa,akaunti zimezuiwa.

Kimsingi ktk makusanyo yanayofanyika,Wafanyakazi wasio waadirifu wana chukua robo na zaidi ya mapato kupitia Rushwa na mirungura. Ndio maana wengi wa watumishi ktk TRA wanaishi na kufanya uwekezaji mkubwa (Majumba, Magari, Apartments, Mitambo, Shares, Bonds, Extravagants life) kinyume na uhakisia wa vipato halali. Wengi wanafanya uwekezaji haramu na kutakatisha fedha kupitia ndugu,jamaa,marafiki kukwepa mikono ya dola na kujulikana.

Simu zinapigwa asubuhi,Mchana na jioni..akifika anapewa mkeka wa makadirio Vitisho, usumbufu, ubabe. Mwisho wa siku Rushwa, Mirungura, Vilio.

NINI KIFANYIKE
1: TRA lazima wapanue na kuongeza wigo wa walipa kodi (TRA must widen Tax base).Hili litasaidia sana kuepusha ku suffocate biashara chache zilizopo kwa kuzingatia idadi ya watu na mahitaji ya nchi sasa na baadae.

2: Wafanyakazi waongezwe, TRA is advised to recruit more staff to facilitate down top approach compliance sensitization. TRA inahitaji taaluma mtambuka kusaidia ktk kujenga mahusiano, kuelimisha, ni wakati wa kuwa na Relationship Officers, Relationship Managers, Transformations Officers, Business Advisors, Commercial Consultants. Wenye wigo wa kusaidia weredi ktk compliances badala ya kuwa wakusanya madeni kama Yono au Majembe, Adili..Court brokers..

Wafanyabiashara ni business partners/Affilliates wa nchi,TRA. Sio wezi, Majambazi, Maharamia. They deserve respect, honour, proffessional treatments. Consultative approached zitumike kudai kodi.

3: Review employee rotational strategy. Wafanyakazi wanakua aggressive kuomba na kupokea rushwa pindi wakihamishiwa kwenye vitengo vyenye fulsa dhidi ya vitengo/kanda/Mikoa mikavu.

4:SHERIA ZA KODI ZIFANYIWE MAREKEBISHO ILI KUENDANA NA UHALISIA WA BIASHARA NA MAZINGIRA YA NCHI. Mfano, VAT, PAYEE, SDL, Corporate Tax, Income Tax.

5: Corporate Tax ishushwe kufikia 20% ili kuwezesha ukuaji wa biashara,makampuni,uwekezaji.

6: Kuwe na Category rasmi za kibiashara ktk mifumo ya kodi na kodi zitofautiane. SME, Large Enterprises, Congromerates. Multinational Enterprises, Foreign State Owned Enterprises.

7: Kutokana na unyeti wa kazi ya ukusanyaji mapato na kulindima kwa vitendovya matumizi mabaya ya madaraka,Rushwa na Ufisadi kuundwe idara maaalumu ya ufuatiliaji wa maadili wa watumishi wa TRA nje ya mfumo wa TRA. Ama kuwe na vitengo ktk taasisi kama JWTZ, TAKUKURU ,DPP, etc.

8: Taratibu za kisheria (Mahakama) zifuatwe ktk utekelezaji wa maamuzi ya kufunga biashara,Kufunga Akaunti,Uchotaji fedha toka kwenye akaunti za wafanyabiashara kwa maguvu na ubabe.

9: Consultative Approach zitumike kuwajenga,Kuwasaidia na kuwainua wafanyabiashara ili kuwafanya kuwa more compliants (Voluntary)..Wakue ktk viwango vya ulipaji,waneemeke na kazi wafanyazo..Biashara sio mateso,jehanamu..

10:Misamaha ya kodi zisizolipika itolewe kusaidia kufufua biashara zinazokufa sababu ya malimbikizo makubwa ya kodi,penati na faini..Tuinue uchumi,Tukuze uchumi..

11:Tax incentives na Tax Holidays kwa SME..

12:Mikopo isio ya Lazima isikopwe na wanasiasa kuepuka mzigo mkubwa kwa walipa kodi wachache..Tukope kwenye miradi yenye tija endelevu..Sio miradi ya kisiasa..Makamishna wa kodi wawepo kwenye team za ukopaji kusaidia kutetea na kupigania uhalisia wa viwango na mizigo ya ulipaji..

13:Nguvu kubwa mnoo itumike kwenye kudhibiti upotevu wa mapato kupitia taasisi mbalimbali (CAG report).Hatua kali zichukuliwe kuwatia moyo wafanyakazi na wafanyabiashara wanao kosa usingizi kufanya biashara kwa jasho na damu ili kulipa kodi..
 
Back
Top Bottom