Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 16,981
- 11,284
Ndugu zangu Watanzania,
Michago ya kumchangia Lissu Fedha za kununulia Gari imewaumbua sana CHADEMA, imewapa aibu,fedheha ,imewavua nguo hadharani na imeonyesha na kuthibitisha kauli yangu nayosemaga humu jukwaani kuwa CHADEMA imepuuzwa na inaendelea kupuuzwa na mamilioni ya watanzania kila uchwao.
Michago inayoendelea kuchangwa imeonyesha CHADEMA haina wanachama hai hata million moja tu.imeonyesha CHADEMA huwa wanapika takwimu ili kuwapofua macho na akili wafuasi wake kiduchu na wafadhili wao. Sasa kwa sasa tangia michango imeanza kuchangwa kwa ajili ya Lissu, CHADEMA na wana CHADEMA mpaka muda huu wameshindwa kufikisha millioni 30.
Sasa tizama mahesabu haya kutoka kwangu Mwashambwa Lucas kada kindaki Ndaki wa CCM.
Kama CHADEMA ingekuwa na walau wafuasi na wanachama hai hata laki tano Tuuuu yaani 500,000 na kila mwanachama akachanga walau elfu moja tu maana yake mpaka sasa ingekuwa imepatikana Million mia tano keshi. Yaani
500,000×1000= 500,000,000/=
je pesa hizi zisingetosha kununua gari analolitaka Lissu na chenji kubaki??
Kama CHADEMA ingekuwa na wafuasi Million moja na kila mtu akachanga walau shilingi mia tano maana yake ni kuwa bado Lissu angepata millioni mia tano keshi.
Sasa hao mamilioni ya wanachama ambao CHADEMA huwa inasema inao wengi kuliko wana CCM wapo wapi? Wamejificha wapi? Hawajaona na kusikia kuwa Lissu anahitaji na kuomba walau hata miatano tu? Ikumbukwe kuwa CHADEMA huwa wanasema wana wanachama zaidi ya millioni kumi.
Sasa kama kati ya wanachama zaidi ya milioni kumi wanashindikana kupatikana hata wanachama laki tano tu wa kuchangia elfu moja tu ili kupata million mia tano.je hamuoni kuwa chama hiki kinapika takwimu mara nyingi?
Hata zile kura alizopata Hayati Lowassa mwaka 2015,zilitokana na mgawanyiko uliotoka ndani ya CCM katika upatikanaji wa mgombea Urais. Hata katika ngazi ya ubunge mahali popote pale wanapopata ubunge CHADEMA huwa ni kura za wana CCM wenzetu wanaokuwa wamegawanyika nakupiga kura za hasira kwa upinzani kama sehemu ya kutoridhishwa wakati mwingine na jina linalokuwa limerejeshwa na vikao vya juu.
Lakini kama sisi sote Wana CCM Pamoja na mashabiki wetu na wakereketwa na wanachama kindaki ndanki tukiamua kupigia kura wagombea wetu,nawahakikishia CHADEMA na upinzani wote kuwa hakuna kiti kinachoweza kwenda upinzani kuanzia mwenyekiti wa kitongoji hadi ngazi ya Urais. Upinzani hauwezi kuambulia chochote kile.
Na kwa sasa wale Wana CCM wachache waliokuwa wanapiga kura za hasira kwa upinzani hasa CHADEMA wamejifunza na kujutia makosa yao kwa machozi na maumivu makali sana.wametambua kuwa walikuwa wanajikomesha wenyewe na siyo chama.maana wameona upinzani kazi yao ni kupinga kila kitu na kila jambo pasipo kumpigania mwananchi kwa lolote lile. Kwa hiyo huu mserereko na mteremko waliokuwa wakipata CHADEMA kwa sasa wasahau kabisa kuupata.maana kila mwana CCM amejilia kiapo cha kuipa kura ya ndio CCM Katika kila ngazi ya uchaguzi.
Naweka kalamu yangu chini na kuishia hapa. CHADEMA njooni Nataka tubishane kwa hoja na siyo makelele na matusi. Weka hesabu nami niweke hesabu. Weka takwimu nami nishushe nondo za uhakika. Raha ya CCM Ni kubishana kwa hoja na siyo matusi.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa. Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Michago ya kumchangia Lissu Fedha za kununulia Gari imewaumbua sana CHADEMA, imewapa aibu,fedheha ,imewavua nguo hadharani na imeonyesha na kuthibitisha kauli yangu nayosemaga humu jukwaani kuwa CHADEMA imepuuzwa na inaendelea kupuuzwa na mamilioni ya watanzania kila uchwao.
Michago inayoendelea kuchangwa imeonyesha CHADEMA haina wanachama hai hata million moja tu.imeonyesha CHADEMA huwa wanapika takwimu ili kuwapofua macho na akili wafuasi wake kiduchu na wafadhili wao. Sasa kwa sasa tangia michango imeanza kuchangwa kwa ajili ya Lissu, CHADEMA na wana CHADEMA mpaka muda huu wameshindwa kufikisha millioni 30.
Sasa tizama mahesabu haya kutoka kwangu Mwashambwa Lucas kada kindaki Ndaki wa CCM.
Kama CHADEMA ingekuwa na walau wafuasi na wanachama hai hata laki tano Tuuuu yaani 500,000 na kila mwanachama akachanga walau elfu moja tu maana yake mpaka sasa ingekuwa imepatikana Million mia tano keshi. Yaani
500,000×1000= 500,000,000/=
je pesa hizi zisingetosha kununua gari analolitaka Lissu na chenji kubaki??
Kama CHADEMA ingekuwa na wafuasi Million moja na kila mtu akachanga walau shilingi mia tano maana yake ni kuwa bado Lissu angepata millioni mia tano keshi.
Sasa hao mamilioni ya wanachama ambao CHADEMA huwa inasema inao wengi kuliko wana CCM wapo wapi? Wamejificha wapi? Hawajaona na kusikia kuwa Lissu anahitaji na kuomba walau hata miatano tu? Ikumbukwe kuwa CHADEMA huwa wanasema wana wanachama zaidi ya millioni kumi.
Sasa kama kati ya wanachama zaidi ya milioni kumi wanashindikana kupatikana hata wanachama laki tano tu wa kuchangia elfu moja tu ili kupata million mia tano.je hamuoni kuwa chama hiki kinapika takwimu mara nyingi?
Hata zile kura alizopata Hayati Lowassa mwaka 2015,zilitokana na mgawanyiko uliotoka ndani ya CCM katika upatikanaji wa mgombea Urais. Hata katika ngazi ya ubunge mahali popote pale wanapopata ubunge CHADEMA huwa ni kura za wana CCM wenzetu wanaokuwa wamegawanyika nakupiga kura za hasira kwa upinzani kama sehemu ya kutoridhishwa wakati mwingine na jina linalokuwa limerejeshwa na vikao vya juu.
Lakini kama sisi sote Wana CCM Pamoja na mashabiki wetu na wakereketwa na wanachama kindaki ndanki tukiamua kupigia kura wagombea wetu,nawahakikishia CHADEMA na upinzani wote kuwa hakuna kiti kinachoweza kwenda upinzani kuanzia mwenyekiti wa kitongoji hadi ngazi ya Urais. Upinzani hauwezi kuambulia chochote kile.
Na kwa sasa wale Wana CCM wachache waliokuwa wanapiga kura za hasira kwa upinzani hasa CHADEMA wamejifunza na kujutia makosa yao kwa machozi na maumivu makali sana.wametambua kuwa walikuwa wanajikomesha wenyewe na siyo chama.maana wameona upinzani kazi yao ni kupinga kila kitu na kila jambo pasipo kumpigania mwananchi kwa lolote lile. Kwa hiyo huu mserereko na mteremko waliokuwa wakipata CHADEMA kwa sasa wasahau kabisa kuupata.maana kila mwana CCM amejilia kiapo cha kuipa kura ya ndio CCM Katika kila ngazi ya uchaguzi.
Naweka kalamu yangu chini na kuishia hapa. CHADEMA njooni Nataka tubishane kwa hoja na siyo makelele na matusi. Weka hesabu nami niweke hesabu. Weka takwimu nami nishushe nondo za uhakika. Raha ya CCM Ni kubishana kwa hoja na siyo matusi.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa. Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.