Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 51,636
- 23,072
Wajameni tunaulizia kwa wataalamu wa JF dawa gani za kuongeza mbegu za kiume yaani idadi zake na kuongeza nguvu za kiume ukiacha viagra.
Tuwe serious kutoa msaada.
Ufafanuzi wa jumla wa tatizo la nguvu za kiume na tiba yake
Kuishiwa nguvu za kiume ni jambo la kawaida kwa wanaume wengi. Ni kushindwa kwa uume kudumu kusimama barabara kwa ajili ya tendo la ndoa, au kuwahi kufika kileleni.Tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume huongezeka siku had I siku. Tafiti mbalimbali zinasema wanaume wengi wenye umri kuanzia miaka 35 na kuendelea ndio wanaosumbuliwa na tatizo hili kwa kiasi kikubwa. Wanaume wenye elimu ndogo juu ya utendaji kazi wa mwili na afya ndio wanaokabiliwa sana na tatizo hili.
Hii ni kutokana na kwamba wengi wao wanakuwa hawaelewi aina ya vyakula vinavyoongeza nguvu za kiume na za mwili kwa ujumla, namna wanavyotakiwa kuishi ili kupunguza janga hilo, wanakunywa pombe na hawajishughulishi na mazoezi ya viungo. Mazoezi ya viungo hupunguza tatizo la kuishiwa nguvu za kiume kwa asilimia kubwa sana.
Kupungukiwa nguvu za kiume kunaweza pia kuwa kumetokana na mambo ya kihisia, kwa kiingereza ‘emotional causes’. Vitu vingine vinavyoweza kusababisha kupungua kwa nguvu za kiume ni pamoja na magonjwa kama vile ugonjwa wa Kisukari na Shinikizo la juu la damu.
Asilimia 51 mpaka 61 ya wanaume wanaosumbuliwa na kisukari wanapatwa na tatizo la uume kushindwa kusimama vizuri. Kadharika wagonjwa wa kiharusi na wale waliotekwa na ulevi nao ni miongoni mwa watu wanaoweza kupatwa kirahisi na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume. Walevi wengi wa pombe kwa mfano wanakabiliwa na tatizo la uzalishaji mchache wa mbegu za kiume (manii).
Wengine wenye hatari ya kupatwa na tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume ni pamoja na wanaume wenye shinikizo la juu la damu, wenye matatizo ya tezi, waliowahi kufanya upasuaji katika viungo vya uzazi wakabaki na majeraha, watu wanaotumia dawa zenye kemikali kiholela bila kushauriwa na wataalamu na wale wanaougua maradhi yanayodhoofisha msukumo wa damu kwenda katika mishipa ya uume.
Pamoja na hayo, tatizo la upungufu wa nguvu za kiume linaweza kutibika kwa watu wa rika zote.
Nini Sababu ya uume kushindwa kusimama?
Kushindwa kwa uume kusimama pia hutambulika kama kuishiwa nguvu za kiume. Ni kitendo cha mtu kushindwa kusimamisha uume au kudumisha usimamaji wa uume kwa muda wa kutosha kufanya tendo la tendo na mwenza wake.
Pamoja na ukweli kuwa mara zote Mwanaume lazima atafika kileleni, hali huweza kuwa tofauti kwa upande wa pili kwani mwanamke anahitaji mwanaume akawie zaidi ili na yeye (mwanamke) aweze kutosheka.
Mkeo hupendelea ukawie na ikiwezekana ukawie zaidi. Kama utakuwa unawahi kumaliza, basi mkeo anakuwa hapati raha kamili.
Ingawa, kama una tatizo la kuwahi kufika kileleni hauko peke yako. Asilimia 30 hadi 40 ya wanaume wa rika zote wanakabiliwa na tatizo la kuwahi kufika kileleni au kupungukiwa kwa nguvu za kiume. Hata hivyo kutambuwa tu kwamba wanaume wengine pia wana tatizo kama lako siyo sababu ya wewe kukaa tu bila kutafuta suluhisho la tatizo lako.
Habari njema ni kuwa zipo njia zinazoweza kuleta matokeo mazuri na hatimaye kulimaliza tatizo hili bila madhara mabaya hapo baadaye.
Wakati mwingine uume kushindwa kusimama inaweza kuwa si tatizo, lakini jambo hilo linapojitokeza kila mara na kwa kipindi kirefu inaweza kuleta msongo wa mawazo kwa mume na hata kwa mke.
Sababu nyingine ambazo zinaweza kupelekea uume usisimame vizuri ni pamoja na matatizo ya mhemko kama:
- Wasiwasi
- Hasira
- Msongo wa mawazo (Stress)
- Huzuni
- Hofu na mashaka
- Kukosa hamu ya tendo la ndoa n.k
Mfumo wako wa neva uwe na afya nzuri inayopelekea mpwito neva (nerve impulses) katika ubongo, uti wa mgongo na uume.
Mishipa ya ateri iliyo na afya ya ndani na iliyo karibu na corpora cavernosa Misuli laini yenye afya na tishu za ufumwele (fibrous tissues) ndani ya corpora cavernosa
Kiwango sahihi cha oksidi nitriki (nitric oxide) ndani ya uume.
Uume kshindwa kusimama vizuri kunaweza kusababishwa pia kama kipengele kimojawapo hapo juu hakifanyi kazi vizuri. Mambo mengine yanayopelekea kupunguwa kwa nguvu za kiume, uume kushindwa kusimama vizuri na kuwahi kufika kileleni ni:
- Uzee
- Kisukari
- Kujichua/Punyeto
- Uzinzi
- Kukosa Elimu ya vyakula
- Kutokujishughulisha na mazoezi
- Shinikizo la juu la damu
- Ugonjwa wa moyo
- Uvutaji sigara/tumbaku
- Utumiaji uliozidi wa kafeina.
- Kudhurika kwa neva au uti wa mgongo
- Madawa ya kulevya
- Kupungua kwa homoni ya testerone
- Athari kutoka kwa baadhi ya dawa
- Pombe
Unaweza kujibu ni msisimko. Ni kweli, Jibu lako linaweza kuwa sahihi. Hata hivyo msisimko ni matokeo. Kipo kinachosababisha kutokea huo msisimko. Bila hicho, hakuna msisimko unaoweza kutokea.
Kila mwanaume anatakiwa kujuwa jibu sahihi la swali hili ili atakapopatwa na tatizo atambuwe wapi pa kuanzia na pa kuishia. Siyo lazima uwe daktari, Elimu ya kutambua mfumo wako wa mwili unavyofanya kazi ni mhimu sana kwa kila mtu na si kwa madaktari pekee kama watu wengi mnavyodhani.
Kutokusoma soma lolote kuhusu miili yetu inavyofanya kazi ndiyo sababu kubwa inayotufanya kuparamia dawa kiholela na hivyo kujikuta tunapata madhara zaidi badala ya kujitibu.
Mzunguko wa damu ndicho kitu kinachofanya uume USIMAME. Na kabla hujaendelea kusoma tambua jambo moja muhimu; ‘’Asilimia 94 ya damu ni maji’’. Hii ni kusema katika kila lita 10 za damu, lita 9 kati ya hizo 10 ni maji. Kwa kifupi maji ndiyo kila kitu mwilini, nakushauri upendelee Kunywa maji bila KUSUBIRI KIU.
Mzunguko wa damu unaofanya kazi vizuri kama inavyotakiwa na usio na hitilafu yeyote ni kipengele muhimu sana katika afya ya mwili, mishipa na kusimama kwa uume wako.
Tiba yake.
Chakula bora ni tiba ya kwanza ya nguvu za kiume na mazoezi ya viungo pia kama tatizo litazidi unashauriwa kwenda hospitali kumuona dakari ili upatiwe matibabu ya kitaalamu.
Baadhi ya vyakula unavyoshauriwa kutumia ili kuondoa tatizo la nguvu za kiume.
1. Blueberry
Blueberry ni matunda yanayosaidia sana kuongeza nguvu za kiume, wengi hupendelea kuyaita ‘viagra’ asilia kutokana na kazi inayoifanya mwilini. Blueberries ina virutubisho vinavyoimarisha mishipa ya damu na kusaidia mzunguko mzuri wa damu mwilini. Damu ndio kila kitu katika nguvu za kiume. Vilevile, blueberries zina nyuzinyuzi (fiber) ambazo husaidia kuondoa kolesteroli (Cholestrol) mwilini kabla hazijanganda kwenye mishipa ya damu. Kuwa na mzunguko mzuri wa damu husaidia mwanaume aweze kuhimiri mapenzi wa muda mrefu zaidi.
2. Mtini (Figs)
Mtini (figs) ni matunda yenye kiwango kikubwa cha amino asidi, ambayo ni kiungo kikubwa katika kuzalisha homoni mwilini. Homoni ndio kishawishi cha nguvu za kiume mwilini. Kukosa amino asidi huweza kusababisha kukosa hamu ya mapenzi au kupungukiwa na nguvu za kiume.
3. Chaza/Kombe wabichi (Raw Oysters)
Chaza wana kiwango kikubwa cha madini ya zinc. Madini za zinc hutumika katika utengenezaji wa homoni ya testosterone, shahawa na mbegu za kiume. Uwingi wa uzalishwaji wa testosterone mwilini huathiri pia hamu ya mapenzi na nguvu za kiume – ikiwa kidogo huondoa hamu, ikiwa nyingi hupelekea hamu na nguvu zaidi.
Kupungukiwa kwa madini ya zinc husababisha kupungua kwa nguvu za kiume, udhaifu (uhanithi), na kushuka kwa kiwango cha uwezo wa kufanya mapenzi.
4. Karanga
Karanga ni chanzo kikubwa cha kujenga protini mwilini. Karanga huwa na kiwango kikubwa cha amino asidi ambayo husaidia kuweka vizuri mfumo wa damu, hivyo kusababisha kuongezeka kwa kiwango cha ufanyaji mapenzi.
5. Vitunguu saumu
Kitunguu saumu kina allicin, kiambato kinachosaidia mzunguko mzuri wa damu kwenye viungo vya uzazi. Kuwa na mzunguko mzuri wa damu kwenye uume ni sababu kubwa ya kuongeza stamina ya kufanya mapenzi.
6. Ndizi
Kuwa na stamina ni muhimu katika ufanyaji mapenzi. Ndizi ni chanzo kikubwa cha vitamin B ambayo husaidia sana katika kuongeza stamina na nguvu mwilini hasa wakati wa kufanya kazi nzito. Ndizi ina kimeng’enyo cha Bromelain ambacho huongeza nguvu za kiume, ashki ya mapenzi (libido).
Vyakula ni bora kuliko madawa makali
Mie binafsi nashauri kutumia njia asilia katika kutatua matatizo yako yote ya kiafya. Mwili una njia zake za kurekebisha kila kitu. Ukiona kuna tatizo inaashiria kuna upungufu ambao unatakiwa kurekebishwa. Kutumia madawa makali hudhoofisha mwili na hivyo kuupunguzia uwezo wa kufanya kazi kama inavyotakiwa. Ni vizuri kama utamuona daktari kama ukiona hakuna kinachowezekana kabla hujaanza kutumia madawa.
Mara nyingi njia asilia hutumia muda mrefu sana kuleta mabadiliko, lakini matokeo yake hudumu zaidi kuliko kutumia madawa makali ambayo hutibua mfumo wa kawaida wa ufanyaji kazi wa mwili wako. Mie nashauri uangalie jinsi unavyokula, nenda kapime vizuri. Kama jogoo ameshindwa kupanda mtungi, ruksa kuangalia njia mbadala.
Ni vizuri kula kwa kiasi kabla ya kufanya mapenzi, hasa wakati wa usiku kabla ya kwenda kulala. Kuvimbiwa husababisha mwili kufanya kazi ya ziada ya kumeng’enya chakula hivyo kuingiwa na uchovu, uvivu na kunyong’onyea. Hii husabisha kukosa usingizi na kupungua kwa umahiri wako katika kufanya shughuli nyingi zinazohitaji nguvu, ikiwemo mapenzi, kwa ufasaha. Usije kumtafuta mchawi wakati wewe ndio unajiroga, kuwa makini.
Kama ilivyo ada kwenye mambo mengi ya kiafya, hakuna muarobaini. Ni vizuri ukajaribu kubadilisha chakula unachokula, fanya mazoezi mara kwa mara ili kupata mwili wenye nguvu. Kama utakuwa na swali, weka maoni hapo chini nasi tutakujibu bila kusika hukusu njia zaidi za kutatua tatizo la nguvu za kiume.
BAADHI YA MAONI NA UFAFANUZI ULIOTOLEWA NA WADAU WA JF KUHUSU TATIZO HILI
---Mambo yanayochangia Upungufu wa nguvu za kiume
LEO ninataka tuangalie kwa kina mambo yanayochangia tatizo hilo upungufu wa nguvu za kiume.
Ningependa tulio katika ndoa, ukishaisoma makala hii tuwahusisishe wenza wetu nyumbani au mpigie rafiki yako na kumueleza kuwa ana nafasi ya kujilinda kupoteza nguvu za kiume na hivyo kuwa na uhakika wa amani nyumbani.
Nasema amani kwa sababu tatizo hili huingilia amani nyumbani kwani kuna kuhisiwa kuwa mwanaume anajihusisha na nyumba ndogo maarufu. Uzoefu katika vituo vyetu vya Marie Stopes kina mama ndio huja kutafuta ushauri kwa nini mzee kabadilika na wafanye nini ili kumrudisha nyumbani. Zifuatazo ni sababu amabazo kitaalamu zinatajwa kuchangia kupungua kwa nguvu za kiume na nyingi kama si zote zinaepukika.
Msongo wa mawazo: Ni dhahiri kuwa akili na tendo la ngono vinategemeana sana. Inajitokeza mara nyingi sana kwa watu wenye matatizo katika biashara, kazini na sehemu nyingine hujikuta hawako katika hali ya kuwa na hamu ya tendo la ndoa mpaka pale watakapotulia. Hii inaweza kuwapata watu wa rika zote na tatizo hili linaweza kuisha haraka kutegemeana na shughuli zao zinavyorudi katika hali ya kawaida.
Magonjwa ya moyo na mishipa ya damu. Mzunguko wa damu mwilini una maana sana kwani kama damu haizunguki vizuri itachangia uume kutosimama vizuri kwa sababu usimamaji hutegemea kiasi na kasi ya damu inayoingia kwenye mishipa ya sehemu hiyo. Dawa zinazotumika kutibu shinikizo la damu huchangia pia kupungua kwa nguvu za kiume.
1. Unywaji pombe kupita kiasi: Pombe inaweza kuathiri mishipa ya damu na mishipa ya fahamu kwa wakati mmoja. Wakati mwingine mtu akilewa sana huathiri ubongo na kukata mawasiliano kisaikologia na hivyo kushindwa kuwa katika hali ya kuwa na hamu ya ngono na hivyo kutosimamisha.
2. Unene. Unene huwa unaambatana na mafuta mengi mwilini. Mafuta hayo wakati mwengine huzidi kwenye kuta za ndani za mishipa ya damu na hivyo kupunguza ukubwa wa mrija kiasi kwamba damu inipita kidogo na kwa shida. Hii huchangia kupungua kwa nguvu za kiume kwa sababu kiasi cha damu kinachotakiwa kisimamisha uume kitakuwa kidogo sana. Wakati mwingi uume unaweza kusimama kidogo na kulala kabla shughuli haijakamilika.
3. Kutokufanya mazoezi: Tusipofanya mazoiezi pia mzonguko wa damu kutokuwa mzuri na hivyo kutoparuhusu damu ya kutosha kusimamisha uume. Kwa watu wanaotembelea magari na shughuli za kukuaa maofisini mda mrefu na hasa kama hawafanyi mazoezi asubuhi au jioni wako kwenye hatari zaidi kuliko watu wanotembea kwa miguu mwendo mrefu na kufanya kazi ngumu za kuuchosha mwili.
5. Matatizo ya kisukari: Kisukari ni ugonjwa unaoathiri mishipa ya fahamu na kufanya mishipa ya damu kutofanya kazi yake viuri ili kuruhusu damu kujaa kwenye uume. Hii himfanya mgonjwa wa kisukari kushindwa kusimamisha hata kama ana hamu ya kufaya tendo hilo.
5. Umri: Inaelezwa kuwa kadri umri unavyopanda ndio uwezo wa nguvu za kiume utaendelea kupungua. Baadhi ya watu huanza kuona tatizo hili wanapofikia umri wa miaka 40 na kuendelea na hasa kama maisha yao hayakuwa na mazoezi ya mwili.
Sababu nyingine ni kama utumiaji madawa ya kulevya, kuumia katika uti wa mgogongo, uvutaji sigara nk. Sababu nyingi zinachangia kupungua kwa nguvu za kiume zinaepukika kwa hiyo tunashauriwa kuwasiliana na wataalamu ili kujifunza jinsi ya kujikinga au kutibu matatizo hayo.
Kwa ushauri piga simu 0655744433 kuanzia jumatatu mpaka ijumaa saa kumi mpaka saa kumi na mbili jioni au tuma email kwenda info@mst.or.tz
Chanzo: Mambo yanayochangia upungufu wa nguvu za kiume.
---Causes for low sperm count:
Infected semen
Tight underpants, bathing in very hot water, sitting for long hours, over weight in which fat layers sag on testicles reduce sperm count
Very frequent semen ejaculation also lead to lowered sperm count and man may become effectively infertile. Hence maintaining a gap of 3 days between two consecutive ejaculations keeps a man more fertile.
Smoking, Excessive alcohol intake.
Over exertion physically and mentally
Zinc deficiency
Infections present in prostate gland.
Malformed genital organs.
Anabolic steroid use
10 Ways you can Increase Your Sperm Count
1. Have sex & masturbate less often - the more times you ejaculate, the less dense your semen will be. Maintain a gap of 3 days between two consecutive ejaculations.
2. Refrain from habits like smoking, alcohol consumption etc. - Alcohol affects your liver function, which, in turn, causes a dramatic rise in estrogen levels. Even two drinks a day will have long-term effects on sperm production
3. Exercise regularly.Exercising your PC muscle can help you shoot further than ever before.
4. Eat Nutritious Food - Diet that's low in fat, and high in protein, vegetables, and whole grains is good for your health and for your sperm. Avoid bitter, astringent and spicy foods.Reduce caffeine intake
5. Avoid heating of testicles - Wear loose, cotton boxer shorts, Avoid hot baths and saunas
6. Lose any excess weight, which tends to cause testosterone/oestrogen imbalances.
7. Reduce stress levels by learning relaxation techniques - Keep your mind and body healthy by regular practice of YOGA and MEDITATION.
8. Massage body with herbal oil, which improves blood circulation.
9. Try supplements - Certain natural supplements promise to increase sperm production. Checkout some Natural and Herbal, no side effects supplements at
10. Make love in the early morning or afternoon. Sperm levels are often highest in the mornings.
---LOW SPERM COUNTCauses for low sperm count:
Infected semen
Tight underpants, bathing in very hot water, sitting for long hours, over weight in which fat layers sag on testicles reduce sperm count
Very frequent semen ejaculation also lead to lowered sperm count and man may become effectively infertile. Hence maintaining a gap of 3 days between two consecutive ejaculations keeps a man more fertile.
Smoking, Excessive alcohol intake.
Over exertion physically and mentally
Zinc deficiency
Infections present in prostate gland.
Malformed genital organs.
Anabolic steroid use
10 Ways you can Increase Your Sperm Count
1. Have sex & masturbate less often - the more times you ejaculate, the less dense your semen will be. Maintain a gap of 3 days between two consecutive ejaculations.
2. Refrain from habits like smoking, alcohol consumption etc. - Alcohol affects your liver function, which, in turn, causes a dramatic rise in estrogen levels. Even two drinks a day will have long-term effects on sperm production
3. Exercise regularly.Exercising your PC muscle can help you shoot further than ever before.
4. Eat Nutritious Food - Diet that's low in fat, and high in protein, vegetables, and whole grains is good for your health and for your sperm. Avoid bitter, astringent and spicy foods.Reduce caffeine intake
5. Avoid heating of testicles - Wear loose, cotton boxer shorts, Avoid hot baths and saunas
6. Lose any excess weight, which tends to cause testosterone/oestrogen imbalances.
7. Reduce stress levels by learning relaxation techniques - Keep your mind and body healthy by regular practice of YOGA and MEDITATION.
8. Massage body with herbal oil, which improves blood circulation.
9. Try supplements - Certain natural supplements promise to increase sperm production. Checkout some Natural and Herbal, no side effects supplements at
10. Make love in the early morning or afternoon. Sperm levels are often highest in the mornings.
---NAMNA YA KUTUMIA TIKITI MAJI KUTIBU TATIZOSaturday, October 3, 2009
... Yanawachanganya sana wanaume!
Wengine wanayaita "Watermelon"Ingawa matiti ni kwa ajili ya chakula cha mtoto mchanga, baba ndiye hujikuta mara zote anaishia kuchezea kama mali zake na pia wapo wanawake wengi sasa ambao hawataki kunyonyesha kabisa watoto ili kulinda matiti yao yabaki umbo lilelile ambalo wanaume wanatawafurahia virtually.
Titi ni jug la asili la maziwa ya motto ingawa huja katika size na shape tofauti na huvalishwa bra kwa design tofauti kwa gharama toauti kutokana na hadhi ya mwanamke wakati sehemu zingine duniani mwanamke hutembea kufua wazi bila tatizo.
Matiti yamekuwa yakipewa heshima (kuabudiwa na kushabikiwa) tangu enzi za zamani hata hivyo attention ambayo matiti yanapewa leo hii (information society) inashangaza na imefika mahali wanawake (hasa mabinti) wanatumia pesa nyingi ili kufanyia upasuaji kuwa na umbo ambalo wanaume wengi husherehekea wakiyaona.
Matiti yamepewa majina mbalimbali na jamii tofauti kama vile Nido, Mtindi, Jugs, Apples, Balloons, Bean bags, Boobies, Boobs, Bullets, Glands, grapefruits, quaver, hand-warmer, Hills, Headers, Lulus, Mams, Mangoes, Meatballs, Meat loaves, Melons, Milk cans, Milk shop, Mountains, Natures fonts, Ninnies, Nuts, Oranges, pair. Papaya, pears, Pillows, Pumpkins, Rib cushions, Sandbags, Sphere, shakers, Upper deck, Warheads, Watermelons, Yams na mengine mengi unayojua wewe.
Swali bado ni kwa nini wanaume huchanganywa sana na matiti?
Kwanza matiti huwafanya wanaume kujisikia utulivu, kuburudika, kuliwazwa, kulegezwa, kustarehe, kupoa, kupozwa, kupumzishwa na kujisikia shwari (calmness) kutokana na ulimwengu chepe, korofi, unaokwaruza na rafu, hivyo kwa matiti kuwa soft; yanayokarirbisha na hayatishi, mwanaume hujisikia yupo salama (Naongelea mke na mume hahahaha!)
Kwani tangu mwanaume akiwa mtoto, ikitokea kuna hatari au kitu chochote ambacho kinamtisha na hata kuanza kulia, alikimbia kifuani kwa mama yake kunyonya titi na kunyamaza hivyo kulindwa na kile kinachomuumiza au kukutana na ubaya wowote.
Pili matiti ni alama (symbol) ya uzazi kwa mwanamke hivyo matiti hutoa dalili kwamba huyu mwanamke anauwezo wa kuzaa na kuendeleza kizazi, kwani huwezi kukutana na msichana ambaye hajabalehe na ana NIDO za uhakika bali akishabalehe huwa na matiti ya uhakikika kuonesha yupo tayari kuzaa au kuwa na uzazi (not all the time).
Kutokana na maelezo ya Charles Darwin (Natural Selection) mwanaume hujikuta anatumia kigezo cha matiti kuchagua partner ambaye ana matiti umbo fulani bila yeye kujua, kumbe ni kuchagua partner mwenye afya na mwenye uwezo wa kuzaa.
Kutokana na maelezo ya bwana Darwn, wanaume hutiwa na kuchanganyikiwa kabisa na matiti sharp kwani ni dalili kwamba huyo mwanamke anauwezo wa kuendeleza species yao.
Tatu matiti ni ufunguo (key) kwa mwanamke kusisimka kimapenzi.
Muulize mwanaume yeyote ambaye ni mzuri kimapenzi (good lover) atakwambia kwamba matiti yana direct connection na msingi wa mwanamke kusisimka kimapenzi (libidinal zones), hivyo mwanaume anapenda matiti na anachanganyikiwa nayo kwa sababu yanaweza kumsisimua mke wake vizuri na kuwa tayari kuwa mwili mmoja.
Kwa hiyo moja ya Home Entertainment Center ya mwanaume ni matiti ya mkewe so mwanamke anayejua siri huhakikisha mume anaitumia hiyo hardware.
Nne matiti husisimua wanaume visually kwani wanaume husisimka kwa kile wanaona, matiti yaliyosimama (shape, A class) husisimua zaidi na kutoa attention kubwa kwa mwanaume, ukiacha genitals, pia matiti ni moja ya physical feature ambayo inamtambulisha mwanamke na kumvutia mwanaume (attraction).
Tano, mwanaume huchanganyikiwa na matiti kwa sababu ya msukumo wa jamii.
Kwani ni binadamu peke yao (katika wanyama wote) ambaye hutumia matiti (fondling) ili kusisimuana kimapenzi.
Magazeti, Televisions, mamodel, Catalogs, matangazo ya biashara, fashions, movies, films yote ni source ya kutangaza uzuri wa mwanamke na matiti 24/7 katika siku 365 za mwaka, mwanaume anayekutana macho kwa macho ya vyote hivi kwa nini asichanganyiwe akiona kifua cha mwanamke ndiyo maana mara nyingi wanaume wanapoongea na mwanamke huangalia kifuani badala ya usoni kwa mwanamke!
Swali la kujiuliza hivi ingekuwaje kama matiti yangekuwa hayafunikwi?
Kama masikio au pua au shingo au lips yangepata attention kama yanavyofichwa?
Binadamu ana sifa moja kubwa ya kutaka kupata kile kimefichwa;
je hii inaweza kuwa proved?
Na je, ni kweli wanaume wanastahili kulaumiwa kwa kuwa attracted na matiti ya mwanamke yeyote?
Je, matiti ni sifa muhimu kwa mwanaume kuzingatia wakati wa kuoa hasa kutokana na msukumo wa jamii, saikolojia na mvuto kimwili ili aoe mke ambaye matiti yake yatamfanya mwanaume ayasherehekee na kuyafurahia?
srce
mbilinyi.blogspot.com
---NAMNA WANAWAKE WANAVYOWEZA KUSAIDIA KUTIBU TATIZOPia, kama mwanaume ameishi na mwanawake kwa muda mrefu na amekuwa na desturi ya kufanya mepenzi mara kwa mara katika mazingira yale yale anaweza kukumbwa na kasoro hiyo. Hivyo anashauriwa kubadili mazingira ya kufanyia mapenzi, kupeana mahaba mapya, kuamsha mapenzi kwa kujaliana, pia kuondoa fikra zote zenye kukinaisha ikiwa sambamba na kuzingatia usafi wa mwili. Yakifanyika hayo mwili utaitikia taarifa ya akili na nguvu zitapatikana.
Kwa wanaoshindwa kurudia tendo wanatakiwa kufuata kanuni hizo hapo juu. Jambo kubwa ni suala la kuuzoeza mwili. Usiulazimishe kuanza mara moja kwenda mara nyingi wakati mapenzi yako yamekuwa ya kuiba mpaka baba alale na wakati mwingine muda wako wa kutoka kazini umebana na hivyo kukufanya ufanye mapenzi ya chap chap kila siku. Ukiwa mtu wa namna hii haiwezi ikatokea siku moja ghafla tu ukafanya mapenzi mara tatu bila kuchoka.
Pia inawezekana mwanaume akashindwa kurudia tendo si kwa sababu hana nguvu bali hapewi ushirikiano wa kutosha toka kwa mpenzi wake. Hivyo wakati wa kutafuta uwezo wa kwenda raundi nyingi ni vema usaidizi wa mwanamke ukatolewa, isitokee kupokea lawama tu za "huwezi, sijatosheka" kwani hizo ndizo zinazowafanya wanaume washindwe kabisa kwa hofu kuwa wanaaibika. Mawazo ya kuaibika yanapopewa kipaumbele huufanya uume kuzidi kusinyaa, kwa maana hiyo ni vema kuyatupilia mbali na kuacha kujihukumu.
Pia kuna hitilafu ya wakati wa kuridhishana, inaweza kutokea mwanamke akawa kamaliza raundi yake ya kwanza, wakati anaingia msisimko wa pili mwanaume anafika kileleni, kinachotokea ni mwanamke kumlazimisha mwanaume arudie tendo kwa muda mfupi tangu amalize, jambo ambalo ni vigumu. Sasa ikitokea mwanaume kachezewa na hana msisimko anapata hofu kuwa hawezi, ikijengeka hivyo hata iweje jambo hilo halitawezekana tena. Hivyo ni bora kupeana muda wa kupumzika kabla ya hatua ya pili ya mchezo.
Pale inapotokea hamasa ya kurudia haipo fikra za mwanaume zisipewe nafasi ya kushindwa kwani nyakati, mchoko, makujukumu, hofu za maisha na mambo kama hayo yanapokuja katika siku ya kustarehe ni wazi kuwa kiwango cha ufanyaji mapenzi kitakuwa chini na hali hii huwatokea wanaume wote, hata walio hodari wa kwenda raundi kumi kwa siku.
Sambamba na hilo wanawake wanashauriwa kutoonesha kujali pindi inapotokea hali hiyo, badala yake wawaambie wenzao kuwa siku hiyo inatosha hata kama hawajatosheka, lengo ni kuondoa hofu ambayo ndiyo msingi wa wanaume kuishiwa uwezo wa kufanya mapenzi. Hata hivyo maudhi, kufanya mapenzi na usiyempenda, msongo wa mawazo na kutokuaminiana huchangia kupoteza msisimko wa kuwa ‘kidume'.
Ushauri wangu ni kwamba chochote ambacho unataka mwili wako ukifanye lazima uuzoeze. Ukizoea kuamka saa 12 asubuhi mwili utatii kanuni hiyo. Na ukizoea kufanya mapenzi kila siku mara mbili au tatu hali itakuwa hivyo. Mwisho katika sura hii ni vema wanaume na wanawake wakajifahamu kuwa uwezo wa kufanya mapezni unapungua kufuatana na umri, isitokee mtu akakosa raha kisa hawezi kwenda mara nyingi kama zamani wakati anajua kabisa umri wake umekuwa mkubwa.
Jamani kutafuta nguvu za ujana zirudie uzeeni ni kujipa taabu ya bure. Wakimbiaji hodari wa zamani leo hawezi kutimua mbio kama ilivyokuwa enzi za ujana wao! Ikiwa tumeingia kwenye umri wa utu uzima lazima tufahamu kwamba mwili unaishiwa uwezo, hivyo ni vema tukakubaliana na hali. Lakini jambo la kushangaza siku hizi hata vikongwe wanapanga foleni kwa waganga kutafuta tiba ya kufanya mapenzi mara tatu kwa siku! Mapenzi yanataka uwezo wa akili na mwili tusishindane na uwezo asili tutapoteza muda na pesa bure.
Tatizo la mwisho ambalo nalo linatajwa kuwasumbua zaidi wanaume ni maumbile madogo ya uume. Wanaume wengi wamekuwa wakilalamika kuwa maumbile yao yanawazuia kuwapa dozi wapenzi wao. Lakini kama nilivyosema huko nyuma kwamba mapenzi hayana kanuni kwamba lazima mtu awe hivi ili amtosheleze mwenzake. Kinacholeta raha katika mapenzi ni hisia, hii ikiwa na maana kwamba mwanaume au mwanamke anaweza kufurahia mapenzi kwa kutomasana na kuhamasishana kwa viungo vingine vya mwili na kujikuta wameridhika hata bila ya kuingiliana.
Kwa maana hiyo wale ambao wanamaumbile madogo wanaweza kutafuta wanawake ambao nao wanamaumbile ya aina yao. Baadhi ya wataalamu wanasema kwamba kwa kawaida umbile la nyeti za mtu linakwenda sambamba na urefu wa mwili wake.
Kwa maana hiyo wanawake wafupi (si wote) wanatajwa kuwa na nyeti zinazolingana na maumbo yao. Hivyo wanaume wenye kasoro hii wanatakiwa kutafuta wanawake wenye maumbile madogo na zaidi wajifunze michezo ya kimapenzi. Kwa sababu za kimaadili ni vema wenye tatizo hili wakawasiliana nami.
Hitimisho la makala haya kwa ujumla. MOJA ni kuepuka hofu. Ikitokea siku moja umeshindwa katika tendo la ndoa haina maana una kasoro, bali ni hali ya kawaida, hivyo usifadhaike, utakuza tatizo. Kwa wale wenye tatizo hili wapunguze wasiwasi na wajiamini. PILI, nguvu za kiume zinahitaji mwili wenye nguvu, hivyo ni busara kula lishe bora na kufanya mazoezi yasiyokuwa makali sana. TATU, kumfundisha mwanamke namna ya kukusisimua. NNE, kuepuka mawazo ya kuhuzunisha wakati wa tendo. TANO, kupata muda wa kupumzisha mwili. SITA, kuepukana na pupa, tumia muda usiopungua dakika 20 kufanya romance. SABA, kujiamini.
---MATIKITI MAJI NA TIBA YA NGUVU ZA KIUMEMatikiti Maji Yanaongeza Nguvu za Kiume
Watafiti wa nchini Marekani wamegundua kwamba matikiti maji yanaongeza nguvu za kiume na yanasaidia kutoa tiba kwa wanaume wenye upungufu wa nguvu za kiume.
Watafiti katika chuo kikuu cha Texas A&M wamegundua kwamba matikiti maji yanaweza yakatumika kama "Viagra ya Asili" kwa wanaume wenye matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume.
Watafiti hao walisema kuwa tikiti maji lina amino acid nyingi za citrulline ambazo huifanya mishipa ya damu itanuke na iwe katika hali kama ile ambayo mtu anayetumia viagra au madawa ya kuongeza nguvu za kiume huwa nayo.
Citrulline ikiwa mwilini hugeuka kuwa "arginine" mojawapo ya aina za amino acid. Hali hii husababisha kuongezeka kwa kiwango cha nitric oxide kwenye damu. Nitric oxide husaidia kuifanya mishipa ya damu itanuke.
Hata hivyo watafiti hao hawakuweka wazi idadi ya matikiti maji ambayo mwanaume anatakiwa kula ili aweze kuwa na nguvu za kiume kama za viagra.
Bhimu Patil, mkurugenzi wa maabara iliyofanya utafiti huo alisisitiza kuwa ulaji wa tikiti maji wa mara kwa mara unasaidia kuzuia tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.
Mojawapo ya faida nyingine ya tikiti maji iliyotajwa ni kusaidia kushusha shinikizo la damu.
---VYANZO NA TIBA ZA NGUVU ZA KIUME Tunapozungumzia upungufu wa nguvu za kiume tunakuwa katika uwanja mpana zaidi wa tafakari za kibaiolojia na kisaikolojia walizonazo wanaume. Lakini kwa kufupisha mlolongo wa mambo sehemu kuu tatu zinaweza kabisa kukidhi mchanganuo mzima wa jinsi tatizo hili linavyowasumbua wanaume wengi duniani.
Sehemu kubwa ya malalamiko ya wanaume katika sakata hili yanagusa zaidi maeneo matatu ambayo ni KUKOSA MSISIMKO, KUSHINDWA KURUDIA TENDO NA KUKOSA KABISA NGUVU, huku kufika kileleni mapema kukihusishwa pia kama pacha wa janga hili ambalo linawasumbua zaidi wanaume, ingawa na wanawake wanakabiliwa na sehemu ndogo ya tatizo hili.
Hata hivyo uchunguzi wa hivi karibuni uliowahusisha wanaume wanaofika kliniki au kupata tiba za tatizo la upungufu wa nguvu za kiume umeonesha kuwa, sio wanaume wengi wenye sababu za kibaiolojia zinazowafanya wakose nguvu za kiume, isipokuwa wengi wao huwa na matatizo ya kisaikolojia zaidi ambayo wahusika wanaweza kujiponya nayo bila hata kutumia vidonge wala dawa za miti shamba.
Ingawa Matabibu wanataja magonjwa ya moyo, kisukari, shinikizo la damu, magonjwa ya zinaa, unene wa kupita kiasi, umri mkubwa kuwa ndiyo chanzo cha wanaume kupungukiwa na nguvu za kiume, lakini imebainika kuwa idadi kubwa ya wanaume wanaofika hospitalini kutafuta nguvu za kiume hawana magonjwa hayo
Huu ni ushahidi kuwa wanaokabiliwa na janga hili wamebeba tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kimawazo zaidi kuliko hali halisi. Ukweli wa mambo ulioibuliwa na wanasaikolojia umebaini kuwa, wale wote
wanaolalamikia/lalamikiwa kuwa hawana nguvu iwe ya kufika kileleni mapema, kutokuwa na msisimko na kushindwa kurudia tendo wamekosa maarifa tu ya kufahamu na hawaijui miili yao na kwamba wanaishi kwa kusikia zaidi ya kujitambua.
Katika hali ya kawaida kila mwanadamu ameumbwa kwa njinsi yake na inapotokea kushabihiana basi ni bahati, lakini mara nyingi usawa hupatikana kwa mmoja kujifunza au kusaidiwa kufikia kiwango cha mtu anayemuhitaji kuwa nae katika maisha hasa ya kimapenzi. Jambo hili wataalamu wanasema kuwa miili iko tayari kutii mafunzo na kubadilisha tabia zake kulingana na utashi wa mhusika.
Tatizo kubwa lililopo kwa wapenzi wengi wanaolalamikia upungufu wa nguvu ni kwamba maisha yao wanayachezea kwenye viwanja vya wenzao wanaokutana nao katika vijiwe na sehemu za kazi. Usikivu wa mazungumzo toka kwa wanaume wengine wenye uwezo wa kwenda mara nne hadi saba katika tendo au wanatumia dakika arobaini kufika kileleni umewafanya wanaume wengi kujihisi tu kuwa wao wanakasoro eti kwa kuwa huishia mara mbili au moja katika kufanya tendo.
Dhana ya kujiona ni mwenye kasoro inapojengeka akilini mwa mwanaume, huchipua hofu na hatimaye kumfanya ashindwe kabisa kusisimka anapofikiria au kukutana na mwanamke. Matokeo ya hangaiko la akili hushusha uwezo wa mwili na kumuongoza mtu kwenye kuwaza ugonjwa kisha kukimbilia hospitali au kwa waganga kutafuta tiba ya ugongwa ambao kimsingi hanao.
Lakini ukweli uko wazi kwamba kukimbilia kutafuta uwezo wa kufanya mapenzi mara sita au saba hakumfanyi mwanaume awe mlinganifu mwenye kusifiwa na wanawake wengi, kwani si wanawake wote wana uwezo wa kufanya mapezi kwa raundi hizo na si wote wanapenda kutumia takika 30 kucheza mpira wa kikubwa, wengine hukinai mapema na huona kero kuwa na wanaume vinganganizi wenye sifa za kuganda wanapopewa.
Kwa kufahamu haya utagundua kuwa kukimbilia kutafuta tiba ya kumudu kwenda mara saba ni jitihada mfu kabisa zisizohitajika katika maisha ya mwanaume hasa ukizingatia kwamba wenye uwezo wa kufanya mapenzi mara nyingi hawakuzaliwa hivyo, bali walijizoeza kupitia mazingira ya malezi na makuzi yao. Maana hawezi kuwa mzoefu wa raundi mvulana aliyelelewa katika mafundisho ya kukatazwa ngono na kulindwa hadi akakakua.
Kadhalika hawi hodari wa kimapenzi msichana aliyefundishwa kujitunza, yote yatakayofuata kwa mvulana au msichana humea baada ya kupandwa na tabia chipukizi za ukubwani. Kwa msingi huo mwanaume anajukumu la kuutengeneza mwili wake uwe katika staili aitakayo. Ndiyo maana kuna wengine hawamudu kulala bila kufanya ngono, hii ikiwa na maana kuwa wamejizoeza tu, si kwamba wameumbwa na nguvu hizo.
Labda ili kufikia kilele cha somo hili ni vema tukalejea matatizo matatu niliyosema hapo juu ili tujue ni jinsi gani tunaweza kuepukana nayo bila hata kumeza vidonge na tukawa wanaume wa mbegu kama wengi wenu mjuavyo. Kwa kuanza tuzungumzie Kukosa msisimko. Hapa tunatakiwa kuajitambua sisi wenyewe kwanza, tukijua historia na mazingira yetu ya kimapenzi.
Kwa wanaume ambao wamebanwa sana kikazi na hufanya mapenzi mara moja moja, hukabiliwa na tatizo la kukosa msisimko kwa sababu miili yao imezoea. Sasa ili kuifanya ichangamke lazima waanze kuirejesha kwa kufanya mapenzi mara kwa mara na kwa raundi chache. Kisha wanatakiwa kufanya mazoezi na kula vyakula, vinywaji vyenye nguvu ili kujipa nguvu.
Pia kama mwanaume ameishi na mwanawake kwa muda mrefu na amekuwa na desturi ya kufanya mepenzi mara kwa mara katika mazingira yale yale anaweza kukumbwa na kasoro hiyo. Hivyo anashauriwa kubadili mazingira ya kufanyia mapenzi, kupeana mahaba mapya, kuamsha mapenzi kwa kujaliana, pia kuondoa fikra zote zenye kukinaisha ikiwa sambamba na kuzingatia usafi wa mwili. Yakifanyika hayo mwili utaitikia taarifa ya akili na nguvu zitapatikana.
Kwa wanaoshindwa kurudia tendo wanatakiwa kufuata kanuni hizo hapo juu. Jambo kubwa ni suala la kuuzoeza mwili. Usiulazimishe kuanza mara moja kwenda mara nyingi wakati mapenzi yako yamekuwa ya kuiba mpaka baba alale na wakati mwingine muda wako wa kutoka kazini umebana na hivyo kukufanya ufanye mapenzi ya chap chap kila siku. Ukiwa mtu wa namna hii haiwezi ikatoke siku moja ghafla tu ukafanya mpenzi mara tatu bila kuchoka.
Pia inawezekana mwanaume akashindwa kurudia tendo si kwa sababu hana nguvu bali hapewi ushirikiano wa kutosha toka kwa mpenzi wake. Hivyo wakati wa kutafuta uwezo wa kwenda raundi nyingi ni vema usaidizi wa mwanamke ukatolewa, isitokee kupokea lawama tu za huwezi, sijatosheka kwani hizo ndizo zinazowafanya wanaume washindwe kabisa kwa hofu kuwa wanaaibika. Mawazo ya kuaibika yanapopewa kipaumbele huufanya uume kuzidi kusinyaa, kwa maana hiyo ni vema kuyatupilia mbali na kuacha kujihukumu.
Pia kuna hitilafu ya wakati wa kuridhishana, inaweza kutokea mwanamke akawa kamaliza raundi yake ya kwanza, wakati anaingia msisimko wa pili mwanaume anafika kileleni, kinachotokea ni mwanamke kumlazimisha mwanaume arudie tendo kwa muda mfupi tangu amalize, jambo ambalo ni vigumu. Sasa ikitokea mwanaume kachezewa na hana msisimko anapata hofu kuwa haweze, ikijengeka hivyo hata iweje jambo halitawezekana tena. Hivyo ni bora kupeana muda wa kupumzika kabla ya hatua ya pili ya mchezo.
Pale inapotokea hamasa ya kurudia haipo fikra za mwanaume zisipewe nafasi ya kushindwa kwani nyakati, mchoko, makujukumu, hofu za maisha na mambo kama hayo yanapokuja katika siku ya kustarehe ni wazi kuwa kiwango cha ufanyaji mapenzi kitakuwa chini na hali hii huwatokea wanaume wote, hata walio hodari wa kwenda raundi kumi kwa siku.
Sambamba na hilo wanawake wanashauriwa kutoonesha kujali pindi inapotokea hali hiyo, badala yake wawaambie wenzao kuwa siku hiyo inatosha hata kama hawajatosheka, lengo ni kuondoa hofu ambayo ndiyo msingi wa wanaume kuishiwa uwezo wa kufanya mapenzi. Hata hivyo maudhi, kufanya mapenzi na usiyempenda, msongo wa mawazo na kutokuaminiana huchangia kupoteza msisimko wa kuwa kidume.
Ushauri wangu ni kwamba chochote ambacho unataka mwili wako ukifanye lazima uuzoeze. Ukizoea kuamka saa 12 asubuhi mwili utatii kanuni hiyo. Na ukizoea kufanya mapenzi kila siku mara mbili au tatu hali itakuwa hivyo. Mwisho katika sura hii ni vema wanaume na wanawake wakajifahamu kuwa uwezo wa kufanya mapezni unapungua kufuatana na umri isitokee mtu akakosa raha kisa hawezi kwenda mara nyingi kama zamani wakati anajua kabisa umri wake umekuwa mkubwa.
Jamani kutafuta nguvu za ujana zirudie uzeeni ni kujipa taabu ya bure. Firbath Bayi hawezi kutimua mbio kama alivyokuwa zamani! Ukiona umeingia kwenye utu uzima na mwili wako unaishiwa uwezo, kubaliana na hali. Lakini jambo la kushangaza siku hizi hata vikongwe wanapanga foleni kwa waganga kutafuta tiba ya kufanya mapenzi mara tatu kwa siku! Mapenzi yanataka uwezo wa akili na mwili tusishindane na uwezo asili tutapoteza muda na pesa bure.
Tatizo la mwisho ambalo nalo linatajwa kuwasumbua zaidi wanaume ni maumbile madogo ya uume. Wanaume wengi wamekuwa wakilalamika kuwa maumbile yao yanawazuia kuwapa dozi wapenzi wao. Lakini kama nilivyosema huko nyuma kwamba mapenzi hayana kanuni kwamba lazima mtu awe hivi ili amtosheleze mwenzake. Kinacholeta raha katika mapenzi ni hisia, hii ikiwa na maana kwamba mwanaume au mwanamke anaweza kufurahia mapenzi kwa kutomasana na kuhamasishana kwa viungo vingine vya mwili na kujikuta wameridhika hata bila ya kuingiliana.
Kwa maana hiyo wale ambao wanamaumbile madogo wanaweza kutafuta wanawake ambao nao wanamaumbile ya aina yao. Baadhi ya watalaam wanasema kwamba kwa kawaida umbile la nyeti za mtu linakwenda sambamba na urefu wa mwili wake. Kwa maana hiyo wanawake wafupi, ingawa si wote wanatajwa kuwa na nyeti zenye ukomo mfupi zaidi ya warefu na wembamba wa umbo.
Mbali na chaguo la mtu mwenye kuendena naye umbo, wanaume wenye kasoro hii wanatakiwa kujifunza sana michezo ya kimapenzi ambayo itawasaidia kuwafikisha kileleni wapenzi wao. Ni muhimu kwao kutumia sanaa na mitindo inayopunguza umbali na ukomo wa nyeti za kike.
Mwisho ni misingi ya tiba hii:
MOJA ni kuepuka hofu. Ikitokea siku moja umeshindwa katika tendo haina maana una kasoro, bali ni hali ya kawaida, hivyo usiingize huzuni na hofu utakuza tatizo. Hivyo kwa wale wenye tatizo hili wapunguze wasiwasi na wajiamini kuwa hawana tatizo. PILI, nguvu za kiume zinahitaji mwili wenye nguvu, hivyo ni busara kula lishe bora na kufanya mazoezi yasiyokuwa makali sana.
TATU, kumfundisha mwanamke namna ya kukusisimua. NNE, kuepuka mawazo ya kuhuzunisha wakati wa tendo. TANO, kupata muda wa kupumzisha mwili. SITA, kuepukana na pupa, tumia muda usiopungua takika 20 kufanya romance. SABA, kujiamini.
Labels: SAIKOLOJIA
---FORMULA NA MAZOEZIHabar tena ndugu zangu wakubwa shkamooni
Nimeud tena baada ya lawama nyingi ya formula
Hii ni formula ilonisaidia kupona kwa kuzingatia nishart ya matunda mboga mboga na mazoezi
Kabla ya kuanza kwa hii tiba lazima uache
Pombe jambo kwa kipindi cha hii tiba japo kawaida pombe ni adui wa uume wako
Acha puunyeto usiwe unajitibu ila ttzo kuu hujaliacha
Uweze kuvuilia sex kwa week 3 had 4
Ili vyakula viweze Fanya kazi
Usile wala kunywa vyakula vyenye kemikali utaua Dawa mfano masoda hayo tumia juice fresh
Ukiweza hayo sasa twende kwenye formula
Kwa muda wa week hizo 3 hadi 4 uwe na uwezo wa kuyapata haya mahitaji maana kwa mda huu ni kila siku upate ila ukishapona unaweza kua ndo mfumo wako ama Siku nyengine ukapotezea kulinganga na maisha yetu
1 ukiamka anza kuuchangamsha mwili kwa mazoezi ya viungo ikiwa ndani ikiwa beach ama gym
2kitu cha mwanzo kutia tumbon mwako iwe chai iliochemshwa na tangawizi na mdalasini ukishachuja usieke sukar no mbaya kwenye mwili eka asali kijiko kimoja chai hii itasaidia kushtua mishipa ama misuli iliolala ilioregea ama ilioziba
3 ukimaliza hapo kama ndo kawaida unakula vitafunwa ni sawa ila hakikisha usipende vyenye mafuta mengi kama vitumbua sasa hapo ni muda wa kula matunda ndizi 2 na vipande 2 vya tikiti hakikisha unatafuna na kumeza kokwa za tikiti ndizi
4 utaendelea na ratiba zako za kawaida usisahau maji unatakiwa kunywa maji ya kutosha kwa sababu maji ni muhimu katika mwili wa binadam tunajua dam ndio hufanya mwanadam kua katika hali ya viungo vyote kufanya kazi kikawaida na asilimia kubwa ya damu ni maji kwaio maji ni muhimu sanaaaaaaa pia maji hukusababisha kukojoa Mara kwa Mara na hii husaidia mwisho nitakuambia umuhimu wa kukojoa kila muda
Wakat unaendelea na ratiba zako za msosi wa mchana usio na madhara kwa mwili wako ikiwa na uwezo pata tena matunda hayo mchana kama huna inatosha ulokula asubuh
5 vegetable soup wengi tumezoea kula supu nyama kuku haya si masupu bora kabisa tuige wazungu chukua kitunguu maji chemsha pamoja na kerot zuchini ama zukini lipo kama tango hill sokon yamejaa tele kitunguu somu kidogo na tangawizi kwa mbali eka chumvi ya mawe haina madhara hakikisha umevikata vipande vipande ili viwah kuiva vikichemka saga kwa blenda hakikisha maji yasiwe mengi ili soup iwe nzito nzito kila siku usiku unatakiwa kula bakuli moja
5vitunguu somu chopchop vitunguu som punje 6 kama ni vile vidogo kama vikubwa punje 2 tu vikate Kate vidogodogo alaf Meza na maji kama Dawa alaf ndo ulale kwa hivi vitunguu som unaweza Fanya Sikh moja Siku nyengine ukaacha maana vinaweza kukuumiza kichwa
7kengel mazoezi haya ni muhimu sana asilimia 50 ya hii formula ni mazoezi haya
Sasa hapa utakumbuka kule nilipokwambia unywe maji mingi na mkojo ni muhimu
Kikawaida hua hatujichunguzi sisi katika mfumo wetu tuna kimshipa flani ivi kipo chini ya korodani karibu na anus pa haja kubwa hua kipo mfano ukiisi mkojo ukibana usitoke had I choooni ule mshipa unaoukaza ili mkojo usitoke ndo huo sasa huo ndo kila kitu hata ukisex ukiubana huo bao halitok sasa kila unapoenda kukojoa hakikisha unakijoa alaf unabana mkojo kwa sekunde kadhaa alaf unaachia mkojo unabana tena ivoivo hadi unaisha na si lazima uwe na mkojo hata ikiwa nyumban kazin njian unaweza kuashum kama unamko alaf choo kipo mbali unabana alaf unaachia
Mazoezi hayo hukuza misuli kukaza misuli ilioharibiwa na punyeto kuipa nguvu na kuirejesha kwenye hali yake ya kawaida
Nakuahid ukifanya haya kwa usawa unaenda kua mume mpya mwanamme jasiri huezi lia tena mm ni shuhuda wa hili
Naamini na ww utarejeshea feedback nzur
Nawatakia mafanikio mema asanteni
Nakaribisha maswali kwa asofaham kipengele chochote
View attachment 850605View attachment 850609
Sent using Jamii Forums mobile app
---Nimechelewa kukujibu sababu ya majukumu mengine.
Upungufu wa nguvu za kiume "erectile dysfonction" husababishwa na vitu vingi.
Utanisamehe kwa Kiswanglish.
1. Magonjwa kama Kisukari na Shindikizo la damu.
2. Unene kupita kiasi na ugonjwa wa usingizi "Sleep Apnea".
3. Matumizi ya tumbaku.
4. Baadhi ya tiba kama Mionzi kwa ajili ya Saratani, opareshi ya Tezi dume nk.
5. Tiba kama za msongo wa mawazo "antidepressants", Tiba za shindikizo la damu nk
6. Magonjwa kama magonjwa ya saikolojia "Depressions, Antiety and Stress".
7. Kunywa pombe kupita kiasi.
8. Kuumizwa kwenye sehemu za nyonga kwenye michezo nk "Physical injuries on pelvic region".
9. Upungufu wa homoni za kiume "Low testosterone".
10. Baadhi ya magonjwa ya mishipa ya fahamu "Some neurological diseases".
11. Matatizo ya kimahusihano kati ya mgonjwa na mwenza wake. (Relationship problems due to stress, poor communication or other concerns).
Hizo ni baadhi ya sababu "Risk Factors" zinazopelekea mtu kukumbwa na tatizo la nguvu za kiume.
Tiba yake inategemea na sababu yake, kwahiyo tiba inatofautiana mtu.
1. Tiba bora ya Shindikizo la damu na Kisukari
2. Kupunguza unene kwa kufanya mazoezi na lishe bora.
3. Kuacha matumizi ya tumbaku.
4. Kupunguza kunywa pombe kupita kiasi au kuacha kabisa.
5. Pata tiba bora ya saikolojia.
6 Uwe maelewano mazuri na mwenza wako.
7. Viagra hutumika kutibu kwa sababu imethibitishwa kwa matumizi ya "erectile dysfonction"
Hizi ni baadhi vitu unawezakufanya ili kukisaidia kuondokana na tatizo hilo.
Hiyo Kidaktari, tofauti na kiswahili swahili mtaani zile tiba za asili ALKASUSU, MCHUZI WA PWEZA, VUMBI LA KONGO na zingine nyingi, hazina uthibitisho kisayansi lakini zinasaidia kiasi fulani kuongeza kujiamini kitaalamu inaitwa "Placebo effect" . Au inawezekana kuwa zinatibu kweli.
-----Habari wakuu,
Leo nawaletea njia bora ya asili itakayowezesha kuimarisha mahusiano au ndoa za watu wengi kwa kutumia kipande cha tikiti maji.
Andiko hili linatokana na ujuzi zoefu (empirical knowledge), sijanakili kutoka popote ni wazo langu nililo lifanyia utafiti na majaribio yake yalileta matokeo chanya.
View attachment 1857838
(Picha kutoka google)
MAHITAJI MUHIMU
JINSI YA KUTUMIA
- Kipande cha tikiti maji lililo komaa vizuri (vipande viwili, kila kipande huuzwa Tsh mia tano )View attachment 1857842
- Bakuli dogo View attachment 1857851
Njia hii ni nzuri pia itaimarisha afya yako kwa kuupatia mwili madini aina ya Zinc, chuma, Folate, Magnesium na potasium. Inafanya kazi kwa ufanisi mkubwa.
- Toa mbegu zote zilizopo kwenye vipande vyote viwili vya tikiti maji kisha zihifadhi ktk bakuli
- Tafuna mbegu zote masaa sita kabla ya tendo la ndoa
- Kwa wasio weza kustahimili radha ya mbegu hizo wakati wa kuzitafuna, wanaweza kula tikitiki maji hivo hivo bila kuliondolea mbegu lakini iwe masaa sita mpaka 12 kabla ya tendo la ndoa
Nimeandika uzi huu sio kwa lengo la kujipatia pesa, Lengo langu ni kuisaidia jamii kuondokana na tatizo la nguvu za kiume kwa kutumia njia salama zaidi na yenye gharama nafuu, LIKE na kisha UPIGIE KURA uzi huu ili uweze kuonekana kirahisi ktk jukwaa hili na uwafikie watu wengi zaidi.
Nakaribisha maswali kwa ufafanuzi zaidi wa kisayansi
Matikiti Maji Yanaongeza Nguvu za Kiume
Watafiti wa nchini Marekani wamegundua kwamba matikiti maji yanaongeza nguvu za kiume na yanasaidia kutoa tiba kwa wanaume wenye upungufu wa nguvu za kiume.
Watafiti katika chuo kikuu cha Texas A&M wamegundua kwamba matikiti maji yanaweza yakatumika kama "Viagra ya Asili" kwa wanaume wenye matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume.
Watafiti hao walisema kuwa tikiti maji lina amino acid nyingi za citrulline ambazo huifanya mishipa ya damu itanuke na iwe katika hali kama ile ambayo mtu anayetumia viagra au madawa ya kuongeza nguvu za kiume huwa nayo.
Citrulline ikiwa mwilini hugeuka kuwa "arginine" mojawapo ya aina za amino acid. Hali hii husababisha kuongezeka kwa kiwango cha nitric oxide kwenye damu. Nitric oxide husaidia kuifanya mishipa ya damu itanuke.
Hata hivyo watafiti hao hawakuweka wazi idadi ya matikiti maji ambayo mwanaume anatakiwa kula ili aweze kuwa na nguvu za kiume kama za viagra.
Bhimu Patil, mkurugenzi wa maabara iliyofanya utafiti huo alisisitiza kuwa ulaji wa tikiti maji wa mara kwa mara unasaidia kuzuia tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.
Mojawapo ya faida nyingine ya tikiti maji iliyotajwa ni kusaidia kushusha shinikizo la damu.
PIA UNASHAURIWA KUSOMA MADA HIZI:
= > Suluhisho rahisi kwa wanaodhani wamepungukiwa nguvu, wanaosumbuka kurudia tendo au kuwahi kufika
= > Ushuhuda: Upungufu wa nguvu za kiume - Tiba halisi
= > Tatizo la kuwahi kufika kileleni kwa wanaume: Fahamu chanzo chake na namna ya kutibu tatizo hili