Tafadhali Usininukuu: Kwenye Dini Na Siasa Kuna Mahali Tunakosea...

maggid

JF-Expert Member
Dec 3, 2006
1,084
1,246
Ndugu zangu,

Nahofia tunachanganya na kushindwa kutofautisha kati ya dini, siasa na siasa za vyama.

Mengi ya kila siku maishani yana siasa ndani yake lakini si lazima yawe na siasa za vyama. Kiongozi wa kiimani anapaswa kuwa huru kuzungumzia kwa ujumla wake masuala ya kijamii kwa lengo la kuelimisha na hata kuasa.

Kiongozi wa kiimani kwenye kusanyiko la waumini wenye itikadi tofauti si vema na busara kumtafuta kondoo wa dhambi wa kunyoshewa kidole na waumini kwa mtazamo wa siasa za vyama.

Na viongozi wa kiimani wanaweza mioyoni mwao kuwa na mitazamo binafsi ya kiitikadi na hata mapenzi kwa vyama vya siasa, lakini, hawapaswi kuyaonyesha hayo mbele ya waumini wao na jamii kwa kupitia majukwaa ya kiimani.

Kutokufanya hivyo, tutafika mahali tutawaona waumini nao wenye kuonyesha hisia zao za kiitikadi kwenye nyumba za ibada. Hapo tutakuwa tumepotea njia.

Maana, kwa kiongozi wa kiimani, waumini wote ni wake, bila kujali tofauti zao za kiiitikadi.

Na hakika, ni busara na hekima, kwa mwanadamu kutambua na kuheshimu mamlaka iliyopo na zaidi, inayotokana na watu.

Kutambua na kuheshimu mamlaka inayotokana na sheria, kanuni na taratibu za mahali husika, hivyo basi, mamlaka inayotokana na Katiba ya wakati huo.

Na mwanadamu huyo, midhari amefanya mawili hayo, ana lazima ya kufanya jambo la tatu; kuyaenzi mamlaka hayo.

Tafadhali Usininukuu."

Maggid Mjengwa.

0688 37 36 52 ( Whatsapp)
 
Ukishaona mtu anaanza na maneno haya katika andiko lake "" tafadhali usininukuu"" tayari naye hapendi kukosolewa.
Mdogo wangu mjengwa umeanza kukengeuka haukai tena kwenye hoja kama zamani.
Jifunze kuusimamia ukweli na sio kuyumbishwa kwa minajili ya kutafata UDC au vyeo vingine.
 
Maggid ndugu yangu Biblia inasema dhambi ikemewe na waliopewa kazi ya kukemea dhambi ni viongizi was dini na kwa kutambua kuwa dini inaumuhimu kila maali ndiyo maana katiba ya jamuhuri wa muungano wa Tanzania ikaweka kipengele cha viongovi kuapa kwa kutumia vitambu vya dini zao sababu mojawapo ya kufanya hivyo ni ili wakikosea waonywe na viongozi
 
Maggid ndugu yangu Biblia inasema dhambi ikemewe na waliopewa kazi ya kukemea dhambi ni viongizi was dini na kwa kutambua kuwa dini inaumuhimu kila maali ndiyo maana katiba ya jamuhuri wa muungano wa Tanzania ikaweka kipengele cha viongovi kuapa kwa kutumia vitambu vya dini zao sababu mojawapo ya kufanya hivyo ni ili wakikosea waonywe na viongozi
Kila siku tunauliza hatujibiwi... dhambi anayokemea huyo askofu ni ipi? Tukianzia hapo tutajua uhalali wa kauli yake.
 
Ndugu zangu,

Nahofia tunachanganya na kushindwa kutofautisha kati ya dini, siasa na siasa za vyama.

Mengi ya kila siku maishani yana siasa ndani yake lakini si lazima yawe na siasa za vyama. Kiongozi wa kiimani anapaswa kuwa huru kuzungumzia kwa ujumla wake masuala ya kijamii kwa lengo la kuelimisha na hata kuasa.

Kiongozi wa kiimani kwenye kusanyiko la waumini wenye itikadi tofauti si vema na busara kumtafuta kondoo wa dhambi wa kunyoshewa kidole na waumini kwa mtazamo wa siasa za vyama.

Na viongozi wa kiimani wanaweza mioyoni mwao kuwa na mitazamo binafsi ya kiitikadi na hata mapenzi kwa vyama vya siasa, lakini, hawapaswi kuyaonyesha hayo mbele ya waumini wao na jamii kwa kupitia majukwaa ya kiimani.

Kutokufanya hivyo, tutafika mahali tutawaona waumini nao wenye kuonyesha hisia zao za kiitikadi kwenye nyumba za ibada. Hapo tutakuwa tumepotea njia.

Maana, kwa kiongozi wa kiimani, waumini wote ni wake, bila kujali tofauti zao za kiiitikadi.

Na hakika, ni busara na hekima, kwa mwanadamu kutambua na kuheshimu mamlaka iliyopo na zaidi, inayotokana na watu.

Kutambua na kuheshimu mamlaka inayotokana na sheria, kanuni na taratibu za mahali husika, hivyo basi, mamlaka inayotokana na Katiba ya wakati huo.

Na mwanadamu huyo, midhari amefanya mawili hayo, ana lazima ya kufanya jambo la tatu; kuyaenzi mamlaka hayo.

Tafadhali Usininukuu."

Maggid Mjengwa.

0688 37 36 52 ( Whatsapp)

Shida ni kwamba wahusika wakitembelea nyumba hizo za Ibada wanataka wasifiwe na kupewa pia fursa ya kusalimu/toa nasaha za kisiasa, hata kama sio utaratibu kwa wageni kupewa nafasi za namna hiyo katika hali ya kawaida! Wanapo nyooshewa vidole tuwaache wenyewe wajipime dhamiri zao na kuona kama wana dhambi au la! Ni swala binafsi la kiongozi tajwa na sio swala la serikali, wala chama, wala wapambe! Dhambi haiondoki kwa njia hizo! Kama ipo dawa yake ni kuitubu tuuuu!!
 
Kila siku tunauliza hatujibiwi... dhambi anayokemea huyo askofu ni ipi? Tukianzia hapo tutajua uhalali wa kauli yake.
Yaani ktk clip ya Askofu akikemea watawala na kuwataka watubu hukuiona au kuisikia? Kama hukuiona itafute humu au angalia reaction za makada na viongozi wa serikali. Kama hawakuona hoja wala wasingejaribu kutetea yasiyowezekana.

Vv
 
Shida ni kwamba wahusika wakitembelea nyumba hizo za Ibada wanataka wasifiwe na kupewa pia fursa ya kusalimu/toa nasaha za kisiasa, hata kama sio utaratibu kwa wageni kupewa nafasi za namna hiyo katika hali ya kawaida! Wanapo nyooshewa vidole tuwaache wenyewe wajipime dhamiri zao na kuona kama wana dhambi au la! Ni swala binafsi la kiongozi tajwa na sio swala la serikali, wala chama, wala wapambe! Dhambi haiondoki kwa njia hizo! Kama ipo dawa yake ni kuitubu tuuuu!!
Kama viongozi wa Kisiasa wanaheshimiwa makanisani na kupewa nafasi ya kuzungumza neno,busara hiyo hiyo ingetumika kuwakumbusha kutenda haki.
Baba au Mama hawashambuliani sebuleni
 
Siasa gani inafanyika kanisani? Wanasemaga CCM hoyeeee au peiplessss? Tuache Ujinga Katika hili.. Pengo kila siku anamhubiri mheshimiwa mbona haikuwa nongwa? Huwezi kutofautisha siasa na maisha ya kawaida. Kakobe aliongea ujumla wa maneno tu lakini hakusema tuchague chama flani... tukubali kukemewa na viongozi wa kiroho maana ndiyo wanafunga na kuomba kwa ajili yetu.
 
Yaani kuambiwa tu kutubu kwa rais wenu ndio kusema kakosewa heshima?!

Kwanini wanaposifiwa hao miungu watu wenu hamuhoji kama ndani ya hizo nyumba za ibada wako tusiofurahishwa na mienendo ya serikali kwa ujumla wake, hivyo kuleta mgawanyiko wa kiitikadi ndani ya nyumba za ibada? Kwahiyo kwenye kusifiwa kuna kuwa hakuna mgawanyiko lakini kukosolewa kuna kuwa na mgawanyiko?!

Acheni kujidanganya taifa hili haliko pamoja tena kama awamu zilizopita, waacheni viongozi wa dini waseme yaliyo kweli ili taifa lipone.

Nyie walamba viatu kwa jicho la kusaka vyeo mmeshindwa kushauri yaliyo sahihi ili taifa liende katika uelekeo ulio sahihi, kwahiyo waacheni wanaotumia akili zao sawa sawa kuliponya taifa hili.
 
Mjengwa mnafiki sana,ni ndugu yangu wa Iringa,lakini "tender" za vyuo vya Maendeleo ya Jamii anazopata na zile za NGO yake ya mfukoni ya Karibu Tanzania anayowapiga Wasweden misaada,ndio vinamfanya asifie kila kitu toka serikalini...Maana anajua akiwa kinyume,atafungiwa milango
 
Ndugu zangu,

Nahofia tunachanganya na kushindwa kutofautisha kati ya dini, siasa na siasa za vyama.

Mengi ya kila siku maishani yana siasa ndani yake lakini si lazima yawe na siasa za vyama. Kiongozi wa kiimani anapaswa kuwa huru kuzungumzia kwa ujumla wake masuala ya kijamii kwa lengo la kuelimisha na hata kuasa.

Kiongozi wa kiimani kwenye kusanyiko la waumini wenye itikadi tofauti si vema na busara kumtafuta kondoo wa dhambi wa kunyoshewa kidole na waumini kwa mtazamo wa siasa za vyama.

Na viongozi wa kiimani wanaweza mioyoni mwao kuwa na mitazamo binafsi ya kiitikadi na hata mapenzi kwa vyama vya siasa, lakini, hawapaswi kuyaonyesha hayo mbele ya waumini wao na jamii kwa kupitia majukwaa ya kiimani.

Kutokufanya hivyo, tutafika mahali tutawaona waumini nao wenye kuonyesha hisia zao za kiitikadi kwenye nyumba za ibada. Hapo tutakuwa tumepotea njia.

Maana, kwa kiongozi wa kiimani, waumini wote ni wake, bila kujali tofauti zao za kiiitikadi.

Na hakika, ni busara na hekima, kwa mwanadamu kutambua na kuheshimu mamlaka iliyopo na zaidi, inayotokana na watu.

Kutambua na kuheshimu mamlaka inayotokana na sheria, kanuni na taratibu za mahali husika, hivyo basi, mamlaka inayotokana na Katiba ya wakati huo.

Na mwanadamu huyo, midhari amefanya mawili hayo, ana lazima ya kufanya jambo la tatu; kuyaenzi mamlaka hayo.

Tafadhali Usininukuu."

Maggid Mjengwa.

0688 37 36 52 ( Whatsapp)
Umeongea vema, Tatizo kubwa linasababishwa na viongozi wenyewe kwa kushindwa kufuata kanuni ,sheria na taratibu. Katika mfumo wa vyama vingi ni muhimu kuzingatia hayo. Mathalani kuna watanzania wanaudhika kuona Rais anatumia Rasilimali za serikali kukinufaisha chama chake.
Kuna wakuu wa Mikoa na Wilaya ni makada na ndio wanaharibu chaguzi. ipo siku wanao onewa watachoka kuvumilia na kuamua liwalo na liwe, Amani ikiharibika nani atakuwa amesababisha? Asipo ambiwa ukweli, ataona yuko sahihi. Ni bora alivyo ambiwa ukweli atatafakari na kuona wapi alikose.
Kuwa waoga ndio ujinga uliopitiliza. watu lazima waseme. Yeyote akikosea lazika tumuoneshe wapi amekosea. Ukichezea wembe, ukukate palepale! siyo mwakani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom