Shivji: Chimbuko la wasiokuwa na Hoja au uthubutu wa Kuhoji, linalo ligharimu Taifa (Part 2)

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
28,181
36,169
Sanjari na alivyokuwa akisisitza Nyerere (RIP):

"Tunataka kuona katika Taifa hili, vijana jeuri na wenye kujiamini, si vijana waoga, akina "ndiyo bwana mkubwa", vijana wanaohoji na kupiga vita mifumo ya jamii isiyoshabihiana na matakwa na matarajio ya jamii ya kitanzania. Tunataka vijana waasi dhidi ya mifumo kandamizi, ubwana na ufisadi katika Taifa"

8 Apr 2024 kuelekea kumbukizi ya kifo cha hayati Sokoine miaka 40, SUA Morogoro; bila kutarajiwa, Prof Shivji aliuvunja ukimya kuhusu ombwe la vijana hawa jeuri nchini, chanzo cha matatizo:

1. Yalisemwa mengi mema kabisa ya kumtofautisha hayati Sokoine kuelekea kumbukizi hiyo huko Morogoro:

PROF. ISSA[1]_page-0001_1.jpg


2. Katika wazungumzaji wakuu, Joseph Warioba, Anna Makinda, Prof. Shivji, Prof. Mkenda, Dk. Biteko kuwataja wachache; walikuwa na mawasilisho bora kabisa yenye kuakisi uthubutu na ya kujifunza; yenye kumtofautisha waziri mkuu huyu, aliyefariki akiwa na umri wa miaka 44; na wengi wengine.

3. Ikumbukwe Sokoine aliteuliwa kuwa wazIri mkuu kwa mara ya kwanza akiwa na umri wa miaka 39.

4. Akichaguliwa kuwa mbunge akiwa na umri wa miaka 27, akateuliwa kuwa naibu waziri akiwa na miaka 29 na waziri kamili (ulinzi) akiwa na miaka 34!

5. Kwa hakika Sokoine hakuwa aina za vijana wale wa "hovyo" wa zama za kwetu.

6. Ombwe la vijana jeuri liliongelewa na wachokoza mada watatu; likianzishwa na kuchomekewa kwa ufupi, uchungu na uangalifu; na profesa nguli, Issa Shivji:

a) Shivji: ndani ya wasilisho lake alisema alijisikia ilikuwa ni muhimu sana kulisemea. Kwamba, hata hivyo angependa aepuke sana kumnyooshea mtu kidole.

kwamba:
(i) hili lilikuwa ni matokeo mabaya kabisa ya matumizi ya nguvu kubwa iliyopitiliza ya kuuuwa uhuru wa kujieleza na hasa kuuwa hamasa ya midahalo, kwenye taasisi za elimu na zaidi sana kwenye elimu ya juu.
(ii) Kukapotezwa dhana ya nguvu ya hoja na kuwa ni muhimu sana hoja kushindanishwa kupata iliyo bora.
(iii) Ubora wa hoja ukabinafshwa kuwa kwa matabaka. Ikawa wenye hoja bora ni wale au yule tu; bila kujali kasema nini; au wengine nao wanasema je.
(iv)Haya yakitokea, zaidi sana yakipewa msukumo mkubwa na serikali za ndani ya miongo 2 iliyopita. Ya kwamba tulipo tunavuna tuliyopanda.
(v) Akamaliza Shivji bila shaka akitupa jiwe gizani.

b) Prof. Mkenda: akisimama ikiwamo kumkaribisha mgeni rasmi alianza na kuligusia suala "chungu kumeza hili."
Akaanza:
(i) "Akilizungumzia tatizo la kuhusu midahalo mashuleni, nilimwona mwalimu wangu Prof. Shivji akiwa ananikazia macho mimi tu, humu ndani!" Kauli iliyoibua kicheko kikubwa kwa kila mtu ukumbuni, hadi kwa kina sisi tuliokuwa kwenye runinga: TBC, huko!
(ii) Akiendelea Mkenda akasema, "hata hivyo nimhakikishie mwalimu wangu kuwa, sisi kama serikali pia tumeliona na mimi kama waziri mwenye dhamana tumeshaanza kulifanyia kazi na tunakwenda kulifanyia kazi kwa ari zaidi!"

c) Dk. Biteko: kabla ya utangulizi wake rasmi, naye akaanza:
(i) Prof. Mkenda amesema wakati Prof. Shivji akilisemea hili, alikuwa akimwona akimkazia macho yeye tu. 'Kwa hakika nami niseme ukweli wangu, kwa maana msema ukweli ni mpenzi wa Mungu.

(ii) Akaendelea Mh. Biteko:
"Mimi mbona ndiyo nilikuwa nimeona mkaziwa macho zaidi nilikuwa mimi...."!

Kauli iliyoibua kicheko kikubwa zaidi ya kile cha mwanzo!

6. Kwa hakika wenye akili zao tukawa tumewaelewa vyema hawa ndugu; na hasa ikizingatiwa:

"The guilty are always afraid "

7. Wale tulio soma Cuba tukawa tumawalewa vyema zaidi. Kwamba itakuwa kule kuibuka Kwa zile ajira zetu za laana, almaarufu kwa jina: machawa wa vyama na watu!

NB: Kwa hakika Mkenda ni Profesa. Kumbe hata kutokea jalalani na wengine wengi wapo!

"Excellent sense of humor."

Angalia Part 1 hapa:

Shivji: Chimbuko la wasiokuwa na Hoja au uthubutu wa Kuhoji, linalo ligharimu Taifa (Part 1)
 
SUA, imezungukwa na mashamba makubwa ambayo inayamiliki, lakini hakuna hata shamba moja kando ya barabara linalolinwa na kumvutia mwananchi aingie kwa kilimo. Yote mapori tu, wana Morogoro wanalima mashamba kwa elimu za mababu zao, hakuna ujirani mwema kati ya SUA na wananchi jirani.

Kongamano kubwa limefanyika kwao, nadhani nadhani ndio la kwanza tangu niifahamu SUA, tulizoea pale Nkurumah Hall kila jumamosi kuna jambo, walau kila mwezi.

Hatuoni critical diacussion kutoka SUA kwa nini kilimo na mifugo bado ni tatizo.
 
Lisu ni dalali wa mabeberu na sasa wamembebesha ajenda ya Muungano!

1. Nimecheka kama mazuri vile.

2. Inaweza kuonekana hivyo kwangu pia "labda tu kwa kushindwa kuwalaani hadharani Marekani na Israel kuhusiana na kukandamiza haki Palestina na za waandamanaji Marekani huko:

a) CHADEMA kukosa neno, utawala wa Sheria Migomo Marekani; ni Pigo kwa Chama, na pia kwa Ukombozi!

b) Ule Moto wa nyika wa migomo Marekani, wapindukia Canada!

2. Ni hapa tu, hata yule chawa Kindaki ndaki wa mabeberu MK254 atathibitisha mtizamo wangu huo kwenye ukimya wake Tundu Antipasti Lissu; hapa kwa hakika tunasubiri kusikia maelezo ya kina na mapema iwezekanavyo.

3. Uwezekano ni kuwa alizuiliwa kusema nje ya ridhaa yake kwa amri ya Ayatollah.

Proved, JokaKuu, Retired, imhotep, Allen Kilewella, Economist, @denoo JG, , Zawadini au wengine tokea ufipa jikoni kule, kuna mwenye taarifa kamili?

4. Kwenye list:

Tusilaumiane: Wako wapi kina Nyerere, Maalim Seif, Mtikila, Julius Malema au kina Tutu

Washupavu hao kwa hakika wasinge kaa kimya!
 
SUA, imezungukwa na mashamba makubwa ambayo inayamiliki, lakini hakuna hata shamba moja kando ya barabara linalolinwa na kumvutia mwananchi aingie kwa kilimo. Yote mapori tu, wana Morogoro wanalima mashamba kwa elimu za mababu zao, hakuna ujirani mwema kati ya SUA na wananchi jirani.

Kongamano kubwa limefanyika kwao, nadhani nadhani ndio la kwanza tangu niifahamu SUA, tulizoea pale Nkurumah Hall kila jumamosi kuna jambo, walau kila mwezi.

Hatuoni critical diacussion kutoka SUA kwa nini kilimo na mifugo bado ni tatizo.
Waalimu (Professors) wa SUA wanamiliki mabaa na ma guest houses hapo Morogoro.

Hata wenyewe hawaamini walicho kifundisha kwa wanafunzi wao, wanajua hakilipi.
 
Sanjari na alivyokuwa akisisitza Nyerere (RIP):

"Tunataka kuona katika Taifa hili, vijana jeuri na wenye kujiamini, si vijana waoga, akina "ndiyo bwana mkubwa", vijana wanaohoji na kupiga vita mifumo ya jamii isiyoshabihiana na matakwa na matarajio ya jamii ya kitanzania. Tunataka vijana waasi dhidi ya mifumo kandamizi, ubwana na ufisadi katika Taifa" Mwl J.K. Nyerere

8 Apr 2024 kuelekea kumbukizi ya kifo cha hayati Sokoine miaka 40, SUA Morogoro; bila kutarajiwa, Prof Shivji aliuvunja ukimya kuhusu ombwe la vijana hawa jeuri nchini, chanzo cha matatizo:

Angalia Part 1 hapa:

Shivji: Chimbuko la wasiokuwa na Hoja au uthubutu wa Kuhoji, linalo ligharimu Taifa (Part 1)
Thanks for this
P
 
SUA, imezungukwa na mashamba makubwa ambayo inayamiliki, lakini hakuna hata shamba moja kando ya barabara linalolinwa na kumvutia mwananchi aingie kwa kilimo. Yote mapori tu, wana Morogoro wanalima mashamba kwa elimu za mababu zao, hakuna ujirani mwema kati ya SUA na wananchi jirani.

Kongamano kubwa limefanyika kwao, nadhani nadhani ndio la kwanza tangu niifahamu SUA, tulizoea pale Nkurumah Hall kila jumamosi kuna jambo, walau kila mwezi.

Hatuoni critical diacussion kutoka SUA kwa nini kilimo na mifugo bado ni tatizo.

1. Mkuu mada hii haihusu makongamano, SUA wala lolote nje ya alichoongea chimbuko la uchawa Tanzania.

2. Ndiyo maana pamoja na uwapo wa wazungumzaji wengi na hata Shivji kusema Mengi mengine walioliongelea likiwemo la uchawa na kwa kiasi cha nukuu zao ni Prof. Mkenda na Dk. Biteko.

3. Ombwe la vijana jeuri liliongelewa na wachokoza mada watatu; likianzishwa na kuchomekewa kwa ufupi, uchungu na uangalifu; na profesa nguli, Issa Shivji.

4. Kwenye kongamano la kifo cha Sokoine miaka 40.

5. Ndiyo maana waliyoongea hawa:



MHE. ANNA MAKINDA[1]_page-0001_0.jpg


MHE. JAJI WARIOBA_page-0001_0.jpg

Hayakuwapo hapa kwani hawakuuongelea uchawa!

6. Tukijikita kwenye mada inapendeza zaidi.
 
Waalimu (Professors) wa SUA wanamiliki mabaa na ma guest houses hapo Morogoro.

Hata wenyewe hawaamini walicho kifundisha kwa wanafunzi wao, wanajua hakilipi.

1. Mkuu wote hao hakuongea lolote kuhusu chawa na chimbuko lake isipokuwa Shivji, Mkenda na Biteko.

2. Zingatia:

a) Ombwe la vijana jeuri liliongelewa na wachokoza mada watatu; likianzishwa na kuchomekewa kwa ufupi, uchungu na uangalifu; na profesa nguli, Issa Shivji:

b) Shivji: ndani ya wasilisho lake alisema alijisikia ilikuwa ni muhimu sana kulisemea. Kwamba, hata hivyo angependa aepuke sana kumnyooshea mtu kidole.

3. Pia watu hao chote walichosema kipo kwenye mada; si pungufu si zaidi.

4. Sasa kulikoni ndugu kuongelea masomo au hata biashara zao nje ya mada? Kwani kuna mahali mada imekugusa popote?

5. Bila kusahau si Mkenda, Shivji wala Biteko wote hao si wa SUA!

6. A gentleman reminder: "kujikita kwenye mada, inapendeza zaidi." Hasa ikizingatiwa nje ya mada hata kimbuga hidaya kimo!
 
Thanks for this
P

1. Inasikitisha watu kutokujua hata humu JF mashindano na kushawishiana kwa Hoja.

2. Huwezi kuja na issue ya Palestina na Israel ulichonacho ni ushabiki kama wa Yanga na Simba.

3. Kwa hakika ni aibu sana kwa machawa masomi ambayo kila mtu anayaona.

4. Kuwaitisha kunako magoma kina Allen Kilewella , Retired , JokaKuu, Economist, denoo JG na wa namna Hiyo japo Hawa CV inayojulikana badala ya kupotea:

"Vicky mtoto wa mama!
Vicky mbona umaeadimika?
Vicky mbona huonekani?

Hata kwenye magoma hutaki kufika?" 🎼🎵🎶. -- Jabali la muziki

Ni kwa lengo la kuwaalika kutoa shamba darasa tu na si vinginevyo. Kwamba kushawishiana na kushindana ni kwa hoja si ushabiki.

5. Kwamba kwenye mambo ya Simba na Yanga huwa tunanyamaza ni Kwa sababu huko hushindanishwa upumbavu si hoja!

6. Au vinginevyo tulikwenda shule kutembea? Au nini tofauti yetu na Lucas?
 
1.Inasikitisha watu kutokujua hata humu JF mashindano na kushawishiana kwa Hoja.

2. Huwezi kuja na issue ya Palestina na Israel ulichonacho ni ushabiki kama wa Yanga na Simba.

3. Kwa hakika ni aibu sana kwa machawa masomi ambayo kila mtu anayaona.

4. Kuwaitisha kunako magoma kina Allen Kilewella , Retired , JokaKuu, Economist, denoo JG na wa namna Hiyo japo Hawa CV inayojulikana badala ya kupotea:

"Vicky mtoto wa mama!
Vicky mbona umaeadimika?
Vicky mbona huonekani?

Hata kwenye magoma hutaki kufika?" 🎼🎵🎶. -- Jabali la muziki

Ni kwa lengo la kuwaalika kutoa shamba darasa tu na si vinginevyo. Kwamba kushawishiana na kushindana ni kwa hoja si ushabiki.

5. Kwamba kwenye mambo ya Simba na Yanga huwa tunanyamaza ni Kwa sababu huko hushindanishwa upumbavu si hoja!

6. Au vinginevyo tulikwenda shule kutembea? Au nini tofauti yetu na Lucas?

..Tatizo ni kubwa kuliko alivyolizungumzia Prof.Shivji. Na lina historia ndefu.

..Tangu tupate UHURU Watanganyika / Watanzania tumekuwa tunafundishwa UCHAWA.

..mambo ya msingi yanayolisibu taifa letu yamekuwa yakijadiliwa kama mjadala wa Simba vs Yanga.

..kwa muda mrefu watawala wamekuwa na magenge yao ya kuchafua na kudhalilisha wote waliokuwa na mawazo mbadala.

..Katika Tanganyika na Tanzania yetu hakuna ambaye alitofautiana na watawala akaachwa bila kutukanwa, kudhalilishwa, na hata kuumizwa.

..Namshangaa Prof.Shivji anashangazwa na hapa tulipofika kama jamii na taifa.
 
brazaj wanafalsafa hunikera sana na ubaridi wao kwenye kuwasilisha mada. Huacha Kila mtu atafsiri kivyake na kila tafsiri kwao watasema ni sahihi.

Napenda sana uwasilishaji mada wa watu wa mtaani. Wao husema " hapa kuna dalili ya fedha kuibwa" Lakini CAG atasema " fedha zilitumiwa bila ya uthibitisho wa risiti"
 
Hii midahalo yenu haileti maendeleo zaidi ya porojo ....Mpaka mpate mtu mweny idea ya kujenga nchi hapo mnapigana kelele tu kama debate za wanafunzi.

1. Umefahamu kuwa huu ulikuwa mdahalo kuhusu kumbukizi ya maisha ya Sokoine? Au hukutaka Sokoine akumbukwe ndugu?

PROF. ISSA[1]_page-0001_1.jpg


2. Kwamba hilo halina cha kufanya na ukombozi wa nchi!

3. Kwenye ukombozi tuko vizuri. Huko tulishatoka. Tuko Huku:

a) Lwaitama: Kwenye maslahi ya nchi, adui yetu ni CCM

b) Ukombozi dhidi ya CCM utapatikana na wanaharakati sio na wanasiasa

c) Tutambuane: Wenye ujasiri au sababu za kuikabili CCM

4. Zingatia inataka kujua tatizo ni nini, na namna sahihi ya kulitanzua.

5. Huku hatuna haja na chawa, wala mabwana zao!

a) Lissu ndilo tegemeo tulilo nalo kwenye kuikomboa nchi hii sasa

b) CHADEMA wakaneni hadharani chawa hawa wa mitandaoni

c)
Lissu: Tukubali kukosolewa, tuukatae u CCM
 
1. Umefahamu kuwa huu ulikuwa mdahalo kuhusu kumbukizi ya maisha ya Sokoine? Au hukutaka Sokoine akumbukwe ndugu?

View attachment 2980761

2. Kwamba hilo halina cha kufanya na ukombozi wa nchi!

3. Kwenye ukombozi tuko vizuri. Huko tulishatoka. Tuko Huku:

a) Lwaitama: Kwenye maslahi ya nchi, adui yetu ni CCM

b) Ukombozi dhidi ya CCM utapatikana na wanaharakati sio na wanasiasa

c) Tutambuane: Wenye ujasiri au sababu za kuikabili CCM

4. Zingatia inataka kujua tatizo ni nini, na namna sahihi ya kulitanzua.

5. Huku hatuna haja na chawa, wala mabwana zao!

a) Lissu ndilo tegemeo tulilo nalo kwenye kuikomboa nchi hii sasa

b) CHADEMA wakaneni hadharani chawa hawa wa mitandaoni

c)
Lissu: Tukubali kukosolewa, tuukatae u CCM

..sidhani kama Sokoine alikuwa sahihi, na alitenda haki, ktk kampeni ya kukamata "wahujumu" uchumi.

..naamini uchumi wetu ulihujumiwa na sera mbaya za Ccm.
 
Sanjari na alivyokuwa akisisitza Nyerere (RIP):

"Tunataka kuona katika Taifa hili, vijana jeuri na wenye kujiamini, si vijana waoga, akina "ndiyo bwana mkubwa", vijana wanaohoji na kupiga vita mifumo ya jamii isiyoshabihiana na matakwa na matarajio ya jamii ya kitanzania. Tunataka vijana waasi dhidi ya mifumo kandamizi, ubwana na ufisadi katika Taifa"

8 Apr 2024 kuelekea kumbukizi ya kifo cha hayati Sokoine miaka 40, SUA Morogoro; bila kutarajiwa, Prof Shivji aliuvunja ukimya kuhusu ombwe la vijana hawa jeuri nchini, chanzo cha matatizo:

1. Yalisemwa mengi mema kabisa ya kumtofautisha hayati Sokoine kuelekea kumbukizi hiyo huko Morogoro:

View attachment 2980396

2. Katika wazungumzaji wakuu, Joseph Warioba, Anna Makinda, Prof. Shivji, Prof. Mkenda, Dk. Biteko kuwataja wachache; walikuwa na mawasilisho bora kabisa yenye kuakisi uthubutu na ya kujifunza; yenye kumtofautisha waziri mkuu huyu, aliyefariki akiwa na umri wa miaka 44; na wengi wengine.

3. Ikumbukwe Sokoine aliteuliwa kuwa wazIri mkuu kwa mara ya kwanza akiwa na umri wa miaka 39.

4. Akichaguliwa kuwa mbunge akiwa na umri wa miaka 27, akateuliwa kuwa naibu waziri akiwa na miaka 29 na waziri kamili (ulinzi) akiwa na miaka 34!

5. Kwa hakika Sokoine hakuwa aina za vijana wale wa "hovyo" wa zama za kwetu.

6. Ombwe la vijana jeuri liliongelewa na wachokoza mada watatu; likianzishwa na kuchomekewa kwa ufupi, uchungu na uangalifu; na profesa nguli, Issa Shivji:

a) Shivji: ndani ya wasilisho lake alisema alijisikia ilikuwa ni muhimu sana kulisemea. Kwamba, hata hivyo angependa aepuke sana kumnyooshea mtu kidole.

kwamba:
(i) hili lilikuwa ni matokeo mabaya kabisa ya matumizi ya nguvu kubwa iliyopitiliza ya kuuuwa uhuru wa kujieleza na hasa kuuwa hamasa ya midahalo, kwenye taasisi za elimu na zaidi sana kwenye elimu ya juu.
(ii) Kukapotezwa dhana ya nguvu ya hoja na kuwa ni muhimu sana hoja kushindanishwa kupata iliyo bora.
(iii) Ubora wa hoja ukabinafshwa kuwa kwa matabaka. Ikawa wenye hoja bora ni wale au yule tu; bila kujali kasema nini; au wengine nao wanasema je.
(iv)Haya yakitokea, zaidi sana yakipewa msukumo mkubwa na serikali za ndani ya miongo 2 iliyopita. Ya kwamba tulipo tunavuna tuliyopanda.
(v) Akamaliza Shivji bila shaka akitupa jiwe gizani.

b) Prof. Mkenda: akisimama ikiwamo kumkaribisha mgeni rasmi alianza na kuligusia suala "chungu kumeza hili."
Akaanza:
(i) "Akilizungumzia tatizo la kuhusu midahalo mashuleni, nilimwona mwalimu wangu Prof. Shivji akiwa ananikazia macho mimi tu, humu ndani!" Kauli iliyoibua kicheko kikubwa kwa kila mtu ukumbuni, hadi kwa kina sisi tuliokuwa kwenye runinga: TBC, huko!
(ii) Akiendelea Mkenda akasema, "hata hivyo nimhakikishie mwalimu wangu kuwa, sisi kama serikali pia tumeliona na mimi kama waziri mwenye dhamana tumeshaanza kulifanyia kazi na tunakwenda kulifanyia kazi kwa ari zaidi!"

c) Dk. Biteko: kabla ya utangulizi wake rasmi, naye akaanza:
(i) Prof. Mkenda amesema wakati Prof. Shivji akilisemea hili, alikuwa akimwona akimkazia macho yeye tu. 'Kwa hakika nami niseme ukweli wangu, kwa maana msema ukweli ni mpenzi wa Mungu.

(ii) Akaendelea Mh. Biteko:
"Mimi mbona ndiyo nilikuwa nimeona mkaziwa macho zaidi nilikuwa mimi...."!

Kauli iliyoibua kicheko kikubwa zaidi ya kile cha mwanzo!

6. Kwa hakika wenye akili zao tukawa tumewaelewa vyema hawa ndugu; na hasa ikizingatiwa:

"The guilty are always afraid "

7. Wale tulio soma Cuba tukawa tumawalewa vyema zaidi. Kwamba itakuwa kule kuibuka Kwa zile ajira zetu za laana, almaarufu kwa jina: machawa wa vyama na watu!

NB: Kwa hakika Mkenda ni Profesa. Kumbe hata kutokea jalalani na wengine wengi wapo!

"Excellent sense of humor."

Angalia Part 1 hapa:

Shivji: Chimbuko la wasiokuwa na Hoja au uthubutu wa Kuhoji, linalo ligharimu Taifa (Part 1)

Hakika ni zaidi ya tatizo.

Hadi mahala pa kazi akitokea mtu wa kuhoji na kujenga hoja anaonekana ni treat.
Anaanza kuchukiwa na kuandamwa!
Kwanini hamtaki fikra mbadala?

Kwani aliegundua umeme ndie aligundua gari ?

Fikra tofauti tofauti ndio huleta ufanisi wa mambo mengi mazuri.
 
Back
Top Bottom