Serikali ajirini Walimu wa masomo yote, walimu wa Arts wanaelemewa

White party

JF-Expert Member
May 5, 2015
1,021
1,151
Nawasalimu kwa kina la Jamhuri ya Muungano,

Kumekuwa na utaratibu wa serikali tangu mwaka 2017 kuajiri walimu wa sayansi na hesabu tu,ikitokea arts imeguswa basi ni Kiingereza pekee hali hii imefanya idadi ya walimu wa masomo mengine ya arts kuzidi kupungua mashuleni na hata kama hawapungui wanafunzi wanazidi kuongezeka kila kukicha kwa sababu ya elimu bure.

Mwaka 2016 hadi 2018 tumepitia uhakiki na walimu kibao wametumbuliwa,serikali haikuajiri kuziba pengo hilo badala yake walimu wa sekondari wakashushwa Shule za Msingi na bado hao wa Sekondari pengo halikuzibwa.

Mhe. Rais, Waziri wa TAMISEMI, elimu na utumishi tunaamini mnalijua hilo naomba msilifumbie macho, hali sio nzuri mashuleni, Shule ina walimu wawili au mmoja wa kiswahili au Historia sekondari! Ni mzigo mkubwa hasa Shule za Vijijini.

Tafadhali tunaomba muajiri walimu wa masomo yote angalau kupunguza pengo mliloacha wakati wa uhakiki, pengo linaloachwa na wastaafu, kufariki, kuacha kazi nk

Nawasilisha.
 
Serikali inaajiri walimu wa sayansi tu hawa wengine hawana tija kwa nchi. Wewe unasomea historia, siasa, sijui kiswahili nani hajui kuongea kiswahili?

Sijui geografia nani hajui milima, mito nk yaani blabla tupu! kwani ukimfundisha mtoto masomo haya itamsaidia nini kwenye maisha yake? Hebu waafrika tujitambue wenzetu wanawekeza kwenye sayansi nyie manataka ujinga.

Halafu nyie mliosomea arts (kwa kiswahili wanaita USANII) hata akili ya kujiajiri hamna serikali itaajiri nchi nzima maana muko wengi kama mchwa! Nawambia ukweli muache kulialia kila siku enyi wasanii!

Mnajua mnaniudhi sana nyie ndiyo mliosababisha vijana wavute majani ulaya mitaani! sasa mtu kasoma historia atakuwa na ubunifu gani wa kumsaidia!
 
stock ya walimu wa art serikalini ni kubwa mno!
kuna kipindi walikuwa wanahamishwa toka secondary to primary

we kajiajiri tu
Sio kweli hata kidogo kusema serikali ina stock ya walimu wa art, kuna mashule mengi sana hata walimu wa history na kiswahili bado ni tatizo ukiachana na walimu wa english ambao wao tatizo lao inajulikana kwamba ni adimu lakini mtaani wamejaa, hapa niligundua kitu kimoja kinacho fanyika wakuu wa shule na ma afisa elimu wanapo peleka takwimu ya idadi ya walimu waliopo mashuleni hawapeleki idadi halisi.

Kuna shule x yenye wanafunzi wapatao elfu mbili na mia tatu na shule nzima ina walimu watatu wa maths lakini ukiangalia kwenye mfumo inaonekana ni shule ambayo walimu wa maths wamejaa katika shule hiyo
 
Serikali inaajiri walimu wa sayansi tu hawa wengine hawana tija kwa nchi. Wewe unasomea historia, siasa, sijui kiswahili nani hajui kuongea kiswahili?

Sijui geografia nani hajui milima, mito nk yaani blabla tupu! kwani ukimfundisha mtoto masomo haya itamsaidia nini kwenye maisha yake? Hebu waafrika tujitambue wenzetu wanawekeza kwenye sayansi nyie manataka ujinga.

Halafu nyie mliosomea arts (kwa kiswahili wanaita USANII) hata akili ya kujiajiri hamna serikali itaajiri nchi nzima maana muko wengi kama mchwa! Nawambia ukweli muache kulialia kila siku enyi wasanii!

Mnajua mnaniudhi sana nyie ndiyo mliosababisha vijana wavute majani ulaya mitaani! sasa mtu kasoma historia atakuwa na ubunifu gani wa kumsaidia!
Kwani sisi ndo tuliotunga mtaala mkuu?!...kama havina tija nyie watunga mitaala mvifute basi sio kutupa adhabu ya wanafunzi elfu mbili kwa walimu wawili wa "usanii"
 
Sio kweli hata kidogo kusema serikali ina stock ya walimu wa art, kuna mashule mengi sana hata walimu wa history na kiswahili bado ni tatizo ukiachana na walimu wa english ambao wao tatizo lao inajulikana kwamba ni adimu lakini mtaani wamejaa, hapa niligundua kitu kimoja kinacho fanyika wakuu wa shule na ma afisa elimu wanapo peleka takwimu ya idadi ya walimu waliopo mashuleni hawapeleki idadi halisi.

Kuna shule x yenye wanafunzi wapatao elfu mbili na mia tatu na shule nzima ina walimu watatu wa maths lakini ukiangalia kwenye mfumo inaonekana ni shule ambayo walimu wa maths wamejaa katika shule hiyo
Hilo ni kweli kabisa mkuu mzigo tulionao kwa sasa ni mzito mno na watu wanabaki na idea za enzi hizo walimu walipokua wanaajiriwa kila mwaka.

Tangu 2017 walimu wa art hawajaajirwa je walimu hawafi?hawastaafu?hawaachi kazi?
 
Serikali inaajiri walimu wa sayansi tu hawa wengine hawana tija kwa nchi. Wewe unasomea historia, siasa, sijui kiswahili nani hajui kuongea kiswahili?

Sijui geografia nani hajui milima, mito nk yaani blabla tupu! kwani ukimfundisha mtoto masomo haya itamsaidia nini kwenye maisha yake? Hebu waafrika tujitambue wenzetu wanawekeza kwenye sayansi nyie manataka ujinga.

Halafu nyie mliosomea arts (kwa kiswahili wanaita USANII) hata akili ya kujiajiri hamna serikali itaajiri nchi nzima maana muko wengi kama mchwa! Nawambia ukweli muache kulialia kila siku enyi wasanii!

Mnajua mnaniudhi sana nyie ndiyo mliosababisha vijana wavute majani ulaya mitaani! sasa mtu kasoma historia atakuwa na ubunifu gani wa kumsaidia!
Umetoa mawazo yako kijinga kweli.Jina la utotoni unaitwa nani mkuu?
 
Mimi nimeajiriwa kitambo hivyo naongea uhalisia wa hali ilivyo huku
Weee acha uongo. Walimu wa masomo ya sanaa wanakula Bata.
Yaani mwalimu wa sayansi anafundisha at least one class. Ila walimu wa sanaa wabagawana stream. Huko kuzidiwa kunatokea aje. Au walimu wa sanaa wameacha kazi kwa wingi?
 
Hilo ni kweli kabisa mkuu mzigo tulionao kwa sasa ni mzito mno na watu wanabaki na idea za enzi hizo walimu walipokua wanaajiriwa kila mwaka.

Tangu 2017 walimu wa art hawajaajirwa je walimu hawafi?hawastaafu?hawaachi kazi?
Wacha bwana wee. Mbona kuna walimu wa sanaa walikuwako mwaka jana majina yalivyotoka.
 
Weee acha uongo. Walimu wa masomo ya sanaa wanakula Bata.
Yaani mwalimu wa sayansi anafundisha at least one class. Ila walimu wa sanaa wabagawana stream. Huko kuzidiwa kunatokea aje. Au walimu wa sanaa wameacha kazi kwa wingi?
Walipelekwa primary baada ya uhakiki mwaka 2017na tangu hapo hawajaajirwa tena,sasa piga hesabu ndogo tu tangu 2017 hadi leo waliobaki wapo tu? Au hata kama wapo si kila siku mnasikia wanafunzi wanaongezeka kutokana na elimu bure? Wewe unaweza kusahisha daftari 600 peke yako kila siku? Au tujuzane hilo bata wenzetu mnakula mkiwa wapi?

@Moisemufajiografii nisamehe mkuu jina lako limejibandika kwny kiandikio changu na limegoma kutoka
 
Back
Top Bottom