SAUT yafuta degree za Madaktari wa Afya 162 waliohitimu Chuo cha Mt. Francis

Utendaji wao upo kwenye mashaka au basi tu ni ukaidi wao ndio unapelekea kukomoana ?

Kama ni ukaidi pekee naona waendelee kufanya shughuli ndogo ndogo kama kutumbua majipu kama ni weledi / utendaji pia upo kwenye mashaka basi popote pale walipo wanyanganywe hata hio stethography na hizo scrubs haraka sana
 
Ndugu Hakuna injunction kwenye rulling and judgment. Injunction ni kuomba kuweka zuio kwa Jambo lililoamuriwa na chombo ambacho sio Cha mahakama, ili mahakama isikilize shauri Hilo. Refer kesi ya akina mdee.
Injunction inafanyika pale ambapo jambo linaendelea na bado halijatolewa maamuzi, means linatakiwa lizuiwe ili lisije kuathiri haki ya mtu hapo baadae baada ya maamuzi/judgement...linaweza fanywa au kuombwa ktk mahakama yoyote kutokana tu na Jambo lako linahusu nini, au hata ktk tribunal/mabaraza.

Concern yako Sasa: Vyombo ambavyo si mahakama Kama taasisi let say vyuo, vyama vya siasa, makanisa na agencies mbalimbali huwa zinafanya maamuzi kupitia kwa board au committee zao walizojiwekea,...Sasa ikitokea wamefanya maamuzi ambayo yameathiri haki ya mtu, mtu huyo ataenda mahakama kuu kwa ajili ya JUDICIAL REVIEW, kwenye judicial review hiyo ambayo inafanyika high court mtu anaweza akaomba order ya Mandamus, certiorari, injunction, prohibition n.k
 
Mimi nilisomea huo Udokta? Usiniboe!
Uspanic Mkuu Thread Iko wazi ni St Francis ni kampasi nafikiri hii itakuwa ya Ifakara kama Niko sawa.Ila Sauti Wana vyuo vingi Vya Udaktari kikiwemo Bugando.Niko tayari kurekebishwa.
 
Administrative law hiyo! Hiyo seneti iliwaita wote hao 162 kwa notisi kwa ajili ya defence? Pamoja au mmoja mmoja,... principle za natural justice zimefuatwa? Kama vile Rule against bias, Audi alteram paterm, Nemo judex in causa sua? Au wameamka tu wakawafuatia huko huko...yasije yakatokea Kama ya SHABIBU MRUMA dhidi ya chuo cha Mzumbe, au Simon Manyaki dhidi ya IFM kesi zote hapa maamuzi ya board au committee yalipigwa chini... Evidence ya wito au notisi kwamba rudisha transcript iliwasilishwaje kwa wahusika na je kila mtu aliipata kwa wanafunzi 2015-2019. Any let us wait
 

Chuo kikuu cha St. Augustine kimebatilisha shahada ilizotoa kwa madaktari 162 waliohitimu chuo cha udaktari cha St. Franscis kuanzia mwaka 2015-2019.

St. Augustine imechapisha tangazo kwenye gazeti la Daily news ikitoa notisi kubatilisha shahada za wanafunzi hao 162 ambao inadai wamegoma kurejesha nyaraka ya matokeo(Transcripts) ambazo walipewa bila baraza la senete la chuo kuwa na taarifa na kuziidhinisha.

Taarifa hiyo iliyosainiwa na mwenyekiti wa seneti ya chuo hicho, balozi Prof Costa Mahalu imesema maamuzi hayo yamefikiwa baada ya mkutano wa senet ilioketi mwezi wa pili.

===

Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Tanzania (SAUT) kimewafutia shahada Madaktari 162 waliohitimu Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha St Francis (SFUCHAS) kuanzia mwaka 2015-2019.

Notisi kwa Umma iliyochapishwa katika Gazeti la Daily mnamo Jumatatu (27 Machi, 2023), ilisema wahitimu 162 walikataa kimakusudi kurudisha nakala za masomo, 'Transcript' walizopewa bila ufahamu na uidhinishaji wa seneti ya chuo kikuu licha ya kukumbushwa kwa muda mrefu.

Taarifa hiyo iliyotiwa saini na Mwenyekiti wa seneti ya SAUT Balozi Prof. Costa Mahalu inaeleza uamuzi wa kuondoa shahada hiyo umekuja baada ya kikao cha Seneti cha Chuo Kikuu kilichofanyika Februari mwaka huu.

"SAUT kupitia Seneti ya Chuo Kikuu katika Seneti yake ya 54 isiyo ya kawaida, mkutano uliofanyika tarehe 25 Februari 2023 katika chuo kikuu cha SAUT na kwa mujibu wa Kifungu cha 47(1) & (2) cha Sheria ya Vyuo Vikuu, Sheria Na. 7 ya 2005 ikisomwa pamoja na Vifungu. 6(3)(ii), 7,8 na Kanuni ya 29 (1) ya Mkataba wa SAUT GN. HAPANA. 580 ya 2020 ilifuta shahada walizopewa wahitimu 162 wa Madaktari wa Udaktari wa SFUCHAS kuanzia 2015 -2019,” inasomeka taarifa hiyo.

Source: Daily News
Kuna kitu kimetokea kati ya 2015 -2019.

SAUT wawe wazi tu lakini si kuzungurusha maisha ya watu.
 

Chuo kikuu cha St. Augustine kimebatilisha shahada ilizotoa kwa madaktari 162 waliohitimu chuo cha udaktari cha St. Franscis kuanzia mwaka 2015-2019.

St. Augustine imechapisha tangazo kwenye gazeti la Daily news ikitoa notisi kubatilisha shahada za wanafunzi hao 162 ambao inadai wamegoma kurejesha nyaraka ya matokeo(Transcripts) ambazo walipewa bila baraza la senete la chuo kuwa na taarifa na kuziidhinisha.

Taarifa hiyo iliyosainiwa na mwenyekiti wa seneti ya chuo hicho, balozi Prof Costa Mahalu imesema maamuzi hayo yamefikiwa baada ya mkutano wa senet ilioketi mwezi wa pili.

===

Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Tanzania (SAUT) kimewafutia shahada Madaktari 162 waliohitimu Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha St Francis (SFUCHAS) kuanzia mwaka 2015-2019.

Notisi kwa Umma iliyochapishwa katika Gazeti la Daily mnamo Jumatatu (27 Machi, 2023), ilisema wahitimu 162 walikataa kimakusudi kurudisha nakala za masomo, 'Transcript' walizopewa bila ufahamu na uidhinishaji wa seneti ya chuo kikuu licha ya kukumbushwa kwa muda mrefu.

Taarifa hiyo iliyotiwa saini na Mwenyekiti wa seneti ya SAUT Balozi Prof. Costa Mahalu inaeleza uamuzi wa kuondoa shahada hiyo umekuja baada ya kikao cha Seneti cha Chuo Kikuu kilichofanyika Februari mwaka huu.

"SAUT kupitia Seneti ya Chuo Kikuu katika Seneti yake ya 54 isiyo ya kawaida, mkutano uliofanyika tarehe 25 Februari 2023 katika chuo kikuu cha SAUT na kwa mujibu wa Kifungu cha 47(1) & (2) cha Sheria ya Vyuo Vikuu, Sheria Na. 7 ya 2005 ikisomwa pamoja na Vifungu. 6(3)(ii), 7,8 na Kanuni ya 29 (1) ya Mkataba wa SAUT GN. HAPANA. 580 ya 2020 ilifuta shahada walizopewa wahitimu 162 wa Madaktari wa Udaktari wa SFUCHAS kuanzia 2015 -2019,” inasomeka taarifa hiyo.

Source: Daily News
Sasa unafutaje ujuzi wao,kama mtu amekuwa anapractise udokta kwa muda wote huo,ukifuta degree yake,ujuzi wake unapotea?
Hizi ni siasa tu,ni njia ya kulazimisha malipo,ni Sawa na kuzuia cheti mpaka mtu amalizie ada
 
Nadhani Kuna kitu SAUT wanaficha. Inawezekana IT wao alisaidia baadhi ya watu kwa Siri bila kujulikana.
Ndio ilikuwa kawaida ya IT wa pale ingawa waliokuwa wanafanya hivyo walifutwa kazi. Mdogo wangu katoka Dip hapo mwaka 2021, probably walikuwa wanafanya hivyo 2020 kurudi nyuma na ukitazama hiki chuo kimewafutia hao wa 2019. Seneti nzima sio wapumbavu wakae vikao miezi na miezi watoe maamuzi ya kiwendawazimu.

Pande zote mbili zina makosa
 
Tatizo la kutoa cheti kwa makosa/kimakosa linarekebishika (ni curable) Utaratibu wa kuzingatia katika kufanya Marekebisho ni pamoja na kuretrieve hizo Transcripts. Na hilo SAUT wamelifanya kwa muda mrefu sana lakini bila mafanikio - Madokta wakekaza shingo. Hatua ya mwisho ndo hiyo ya kuzifuta juu kwa juu ww unabaki na karatasi lisilo na thamani i.e. halitambuliwi kisheria. Endapo Hawatafikia Muafaka, bado ni hatari kubwa zaidi kwani Waajiri (Serikali au Private Sector) watafuatiliwa kuhusu Ajira kwa Mujibu wa Qualifications. Wewe Utakuwa ni mmojawapo wa waathirka - Huna qualifications za Udaktari. Hapo utakuwa mgeni wa nani???
Lakini kwa nini kote huko?? Si urudishe karatasi la watu halafu mengine mtayajenga? Hakuna lisilowezekana chini ya hili jua. Nyie ni watu wazima -fanyeni mambo yenu ki-Utu uzima. Umeshafanya kazi kwa zaidi ya 6yrs na nina amini unao uzoefu wa kutosha kazini. Hili la karatasi linakushindaje?
Unaogopa nini?
Hao wasiotaka kurudisha transcript hawajagoma tu bila sababu. Na hao seneti hawajafuta vyeti vyao bila sababu, maprof wazima hawawezi kaa vikao nenda rudi wakafuta vyeti. Wakati huo daktari anayejiamini hawezi kaa miaka mitatu anaombwa arudishe transcript akagoma wakati mtu yeyote aliyechukua cheti cha chuo anatakiwa ajue hiyo ni mali ya chuo.

Lazima kuna kitu hakitajwi hapa kwenye taarifa. Hicho kitu ni cha kuchafua jina la chuo na sifa za hao madaktari. Na pande zote wanajua
 
Back
Top Bottom