X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,817
Pilau Ya Kuku
Vipimo
- Mchele wa basmati........................ 3 Vikombe
- Kuku.............................................½
- Viazi.............................................. 4
- Vitunguu........................................ 2
- Thomu iliyosagwa........................... 2 Vijiko vya supu
- Binzari ya pilau nzima...................... 1 Kijiko cha chakula
- Binzari ya pilau.................................½ kijiko cha chai
- Pilipili manga nzima......................... ½ kijiko cha chai
- Karafuu nzima................................. 8
- Iliki nzima......................................... 6
- Mdalasini nzima................................. 5 Vijiti
- Pilipili mbichi iliyosagwa...................... 2
- Chumvi............................................. Kiasi
- Mafuta ya kupikia...............................¼ Kikombe
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika:
- Osha mchele na roweka kwa muda kutegemea na aina ya mchele.
- Kata kuku vipande upendavyo, safisha kisha mchemshe kwa chumvi, pilipili iliyosagwa, thomu na tangawizi.
- Akiwiva kuku, mtoe weka kando, bakisha supu katika sufuria.
- Katika sufuria, kaanga vitunguu hadi vigeuke rangu ya hudhurungi.
- Tia thomu na tangawizi na binzari zote kaanga kidogo
- Kisha tia viazi kanga kidogo kisha tia kisha tia vipande vyako vya kuku na supu acha ichemke kidogo kisha tia maji ukisie kutokana na mchele unaotumia.
- Mwisho tia mchele koroga uchanganye na vitu vyote acha ichemke kiasi kisha funika na punguza moto mpaka uive (huku ukiugeuzageuza)
- Ukishakuwa tayari pakua kwenye sahani tayari kwa kula na salad na pilipili.