Nyumba zazungukwa na maji Karatu. Wananchi wakosa makazi

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,865
4,693
Mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta athari katika wilaya ya Karatu mkoani Arusha, baada ya baadhi ya nyumba kufunikwa na kuzingirwa na maji, hivyo baadhi ya wananchi kukosa makazi.

Kutokana na changamoto hiyo, wengine wamelazimika kwenda kutafuta nyumba za kupanga, wengine wakienda shule na baadhi kuhamia kwa ndugu na jamaa zao.

Akipotafutwa na Mwananchi Digital kuzungumzia athari za mvua hizo, Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Dadi Kolimba amesema yuko msibani na kwamba atatoa taarifa baadaye.

Mvua hizo zilizonyesha tangu wiki iliyopita zinatajwa kuathiri maeneo mbalimbali wilayani humo, ikiwemo Kata ya Qurus na Karatu.

Wakizungumza na Mwananchi Digital leo Jumanne Aprili 16, 2024, baadhi ya wananchi wameiomba Serikali kuangalia namna ya kuwasaidia kwa haraka kabla madhara hayajawa makubwa.

Jeneth Mfanya, mkazi wa Mtaa wa Bwawani amesema amelazimika kwenda kuupanga kutokana na nyumba yake kujaa maji.

Amesema mvua hiyo iliyoanza kunyesha tangu wiki iliyopita imeleta athari kubwa kwao, kwani mbali na nyumba yake kujaa maji, pia saluni aliyokuwa anaitegemea kama kitega uchumi nayo imejaa maji na amefanikiwa kuokoa vifaa vichache.
 
Mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta athari katika wilaya ya Karatu mkoani Arusha

Maji haya yanaelekea Dodoma na Morogoro 16 April 2024, je serikali za mikoa ya Dodoma, Morogoro zimejipanga vipi na maji haya ya mafuriko yanayotafuta njia ya asili kuelekea mikoa hiyo kwa maji kufika huko ndani ya siku kadhaa zijazo ?

Toka maktaba:
03 December 2023



Ukubwa wa mto Bubu na uelekeo wake kusini hadi katikati ya Tanzania


View: https://m.youtube.com/watch?v=3JRYJYVLMb0

Topolojia mto Bubu unakusanya maji kutoka mito na vijito vinavyoanzia katika miinuko ya plateau ya kusini mashariki ya wilaya ya Hanang na kuelekea hadi bonde la Bahi mkoani Dodoma

Jiografia :
Bonde la Bahi ni sehemu ya Bonde la Kati nchini Tanzania
Bonde hili linajumuishwa na Mito na Vijito vinavyoingiza maji yake katika Ziwa Ambali linapatikana katika Kanda ya Kati ya Kaskazini. Vijito vidogovidogo vinavyotoka Ziwa Natron mpakani mwa Kenya kuelekea Tanzania kwenye bonde la Bahi. Eneo la bonde kwa upande wa Tanzania ni kilometa za mraba 153800.

Maziwa makuu inayomwaga maji katika bonde hili ni Ziwa Eyasi linalopokea maji kutoka katika Mto Wembere na Manonga iliyopo Kaskazini mwa Tabora na Mashariki mwa Shinyanga. Ziwa Manyara hupokea maji yake kutoka kwenye ardhi chepechepe ya Bubu. Maziwa mengine madogo yaliyopo katika bonde hili ambayo hayamwagi maji yake nje ni ziwa Basuto na Natron. Bonde hili liko katika maeneo kame ya Tanzania, ambapo wastani wa mvua kwa mwaka ni kati ya 500 Milimita katika maeneo ya Bahi na 900 Milimita katika vilima vya Mbulu.
source : https://www.maji.go.tz/pages/basin-water-boards

Wilayani Bahi tarehe 15 Desemba 2020.

Mto Bubu na fursa wilaya ya Bahi


Awali akitoa taarifa ya majaribio ya kilimo cha zao hilo, Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda amesema utafiti huo umeonyesha mafanikio makubwa katika eneo hilo na tayari wilaya imeshaandaa hekta 412 za kuanzia ili baada ya wakulima kuvuna mpunga waweze kupanda ngano, zao ambalo linahitajika kwa wingi hapa nchini.

Kwa upande wake Afisa Mtafiti Mkuu wa Kilimo Taasisi ya Utafiti wa Mazao – TARI, Dkt. Rose Mongi amesema utafiti pamoja na majaribio ya shamba darasa katika Wilaya ya Bahi vimefanyika kwa mafanikio makubwa hivyo, eneo la Bonde la Bahi linafaa kabisa kwa kilimo cha ngano.

“Mheshimiwa Naibu Waziri, majaribio yalilenga kuanzisha kilimo cha ngano katika Wilaya ya Bahi na ngano ilipandwa baada ya kuvuna mpunga, wakulima wameshuhudia mavuno yaliyotokana na zao hilo. Hivyo zao hili litawawezesha kulima mara mbili kwa mwaka na kujiongezea kipato mara mbili.” Amesema Dkt. Mongi.


Naye, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Donald Mejiti amewasihi wananchi kulipokea jambo hilo kama fursa kwao ili waweze kusonga mbele kimaendeleo.

Wilaya ya Bahi ni miongoni mwa maeneo yanayozalisha kwa wingi zao la mpunga hivyo, kuanzishwa kwa kilimo hiki cha ngano itakuwa fursa nyingine kwa wakulima kujiongezea kipato.


0L7A5339.jpg


0L7A5353.jpg


0L7A5363.jpg


0L7A5369.jpg


0L7A5374.jpg


Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe (aliyevaa suti ya kijivu) akizungumza mara baada ya kutembelea Mto Bubu ambao ndiyo chanzo kikuu cha kilimo cha umwagiliaji katika skimu mbalimbali za Bahi. (Picha zote na Benton Nollo)
 
Mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta athari katika wilaya ya Karatu mkoani Arusha, baada ya baadhi ya nyumba kufunikwa na kuzingirwa na maji, hivyo baadhi ya wananchi kukosa makazi.

Kutokana na changamoto hiyo, wengine wamelazimika kwenda kutafuta nyumba za kupanga, wengine wakienda shule na baadhi kuhamia kwa ndugu na jamaa zao.

Akipotafutwa na Mwananchi Digital kuzungumzia athari za mvua hizo, Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Dadi Kolimba amesema yuko msibani na kwamba atatoa taarifa baadaye.

Mvua hizo zilizonyesha tangu wiki iliyopita zinatajwa kuathiri maeneo mbalimbali wilayani humo, ikiwemo Kata ya Qurus na Karatu.

Wakizungumza na Mwananchi Digital leo Jumanne Aprili 16, 2024, baadhi ya wananchi wameiomba Serikali kuangalia namna ya kuwasaidia kwa haraka kabla madhara hayajawa makubwa.

Jeneth Mfanya, mkazi wa Mtaa wa Bwawani amesema amelazimika kwenda kuupanga kutokana na nyumba yake kujaa maji.

Amesema mvua hiyo iliyoanza kunyesha tangu wiki iliyopita imeleta athari kubwa kwao, kwani mbali na nyumba yake kujaa maji, pia saluni aliyokuwa anaitegemea kama kitega uchumi nayo imejaa maji na amefanikiwa kuokoa vifaa vichache.
Na hii litasingiziwa Bwawa la Mwl. Nyerere
 
Mafuriko Mto Wa Mbu na Karatu. Hali ni mbaya. Kwa Mto Wa Mbu inaonekana Mitaro iliziba na haikuzibuliwa mapema japo pia Ziwa Manyara linajaa.
IMG_20240413_140028_999.jpg
IMG_20240413_140025_653.jpg
IMG_20240413_140017_121.jpg
 
Mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta athari katika wilaya ya Karatu mkoani Arusha, baada ya baadhi ya nyumba kufunikwa na kuzingirwa na maji, hivyo baadhi ya wananchi kukosa makazi.

Kutokana na changamoto hiyo, wengine wamelazimika kwenda kutafuta nyumba za kupanga, wengine wakienda shule na baadhi kuhamia kwa ndugu na jamaa zao.

Akipotafutwa na Mwananchi Digital kuzungumzia athari za mvua hizo, Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Dadi Kolimba amesema yuko msibani na kwamba atatoa taarifa baadaye.

Mvua hizo zilizonyesha tangu wiki iliyopita zinatajwa kuathiri maeneo mbalimbali wilayani humo, ikiwemo Kata ya Qurus na Karatu.

Wakizungumza na Mwananchi Digital leo Jumanne Aprili 16, 2024, baadhi ya wananchi wameiomba Serikali kuangalia namna ya kuwasaidia kwa haraka kabla madhara hayajawa makubwa.

Jeneth Mfanya, mkazi wa Mtaa wa Bwawani amesema amelazimika kwenda kuupanga kutokana na nyumba yake kujaa maji.

Amesema mvua hiyo iliyoanza kunyesha tangu wiki iliyopita imeleta athari kubwa kwao, kwani mbali na nyumba yake kujaa maji, pia saluni aliyokuwa anaitegemea kama kitega uchumi nayo imejaa maji na amefanikiwa kuokoa vifaa vichache.
Unaweza kuta Tanzania nzima ipo katika mkondo wa maji, maana sasa hivi kila sehemu ni mafuriko, kila mkoa ni mafuriko dah!!
 
Back
Top Bottom