Nyama ngumu kama manati haipendezi, jitahidi mpishi ukipika nyama yoyote ile iwe laini

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,881
46,631
Wapishi wa nyama katika migahawa, Bar, hotel, sherehe na hata majumbani hakikisheni nyama zinaiva vizuri na kuwa laini kabisa. Iwe nyama ya kuchemsha, kuchoma au kukaanga nyama inatakiwa iwe laini kabisa uweze kuichambua au kuitoa kwenye mfupa au kuitenganisha kwa kijiko, uma au mkono mmoja tu.

Iwe nyama ya ng'ombe, mbuzi, kuku wa kienyeji au kitimoto nyama inatakiwa kuivishwa na kuwa laini kabisa. Iwe utumbo, mbavu, paja, mguu au sehemu yoyote ile inatakiwa iive iwe laini.

Haipendezi na Inakera sana kula nyama huku unavuta kwa mikoni miwili kama manati au unatafuna kama bigijii, Inakera kula nyama huku zinabaki kung'ang'ania katikati ya meno na kukuhitaji kumaliza toothpick kikopo kizima kusafisha mabaki ya nyama kwenye meno.
 
Roho huwa inaniuma nakunywa supu nashindwa kuvuta nyama za kwenye mifupa kisa ngumu, nikicheki watu wananiangalia.
Wengi hawajui kupika supu, nyama inatakiwa ichemshwe kwa kuongeza maji kidogo kidogo sana mpaka iive kabisa ndio uongeze maji hata kama ni pipa zima kama unavyotaka. Tofauti na hapo ukiijaza maji tokea mwanzo itakubidi utumie muda mrefu sana na moto mwingi sana kuichemsha mpaka iive kabisa.
 
Wengi hawajui kupika supu, nyama inatakiwa ichemshwe kwa kuongeza maji kidogo kidogo sana mpaka iive kabisa ndio uongeze maji hata kama ni pipa zima kama unavyotaka. Tofauti na hapo ukiijaza maji tokea mwanzo itakubidi utumie muda mrefu sana na moto mwingi sana kuichemsha mpaka iive kabisa.
Mimi ni mmojawapo ninayeongeza maji mengi
Nimechukua ujuzi hapa, Asante...!
 
Kwenye mwili wa mnyama kama ng'ombe, mbuzi n.k kuna maeneo tofauti tofauti yenye kutoa nyama zenye texture tofauti tofauti...

Kuna maeneo yanayotoa nyama laini sana, laini kiasi na ngumu kulingana na aina ya misuli iliyotengeneza nyama hiyo...

Utofauti huu wa hizi nyama, unapaswa kuambatana na matumizi ya hizi nyama pia...

Kuna nyama inayofaa kuchemshwa, kukaangwa, kuokwa na hata hizi aina tofauti za mapishi nazo pia hutofautiana...

Mathalani kwenye kuoka, kuna nyama inaokwa kwa jotoridi la taratibu na inaweza ikakaa motoni kwa masaa hadi 10 (mara nyingi hizi huwa ni zile nyama zenye misuli migumu na nyuzi nyuzi)...

Hivyo: Wapishi wengi huwa hawazingatii aina ya nyama na namna ya kuioanisha na aina ya mapishi...
 
Back
Top Bottom