Logikos
JF-Expert Member
- Feb 26, 2014
- 12,777
- 19,939
Huu ni muendelezo wa Uzi wa Kuhoji Nishati gani kwa Tanzania ni Safi na Ina Uwezekano mkubwa kufanikiwa.
Kwenye huu Uzi taelezea ni jinsi Gani Nishati hii Safi na Bora kuliko Gesi inaweza kuwa na Gharama mpaka ya 0 Kwa mtumiaji, Na hapo bila / kabla ya Serikali Kushuka Bei ya Units. Kwahio kwenye huu uzi tutajikita kwenye maelezo ni Vipi watu wanaweza kutumia Umeme huu bila kulipia gharama ya Kifedha, Ukizingatia wengi wanaotumia Kuni vijijini hawahitaji kutoa pesa kutumia kuni hizo zaidi ya nguvu zao
Utangulizi:
Ili kufahamu gharama ambayo itatumika au inatakiwa kutumika ni vema kwanza tukafahamu mahitaji (wastani wa kila kaya inatumia nishati kiasi gani katika mapishi), baada ya hapo tutahitaji kuangalia na kufahamu ni vyombo vya aina gani vyenye ufanisi vitakavyomsaidia mtumiaji. Na mwisho kabisa tutaangalia njia za kuweza kufanya kwa mtumiaji huyu kuweza kupika kwa gharama ndogo au bila gharama yoyote. Na hapa ni kwa kutazama (worse case scenario) iwapo Serikali na Taasisi husika hazitashusha bei za umeme.
Mahitaji ya Nishati katika Mapishi katika Kaya ya Mwafrika.
Hapa sababu sina takwimu zangu binafsi nimeangalia kwenye mtandao na nimeona hii
Ingawa hio report ilikuwa ya 2015 na sasa hivi vyombo vina ufanisi zaidi lakini tukichukulia hio kama guide tutaona kwamba familia ya watu wanne inaweza ikatumia 2.2 mpaka 3.3 Units kwa siku, ingawa katika vyanzo mbalimbali namba hio ni kubwa na uhalisia unaweza kuwa 1.2 Units.
Vyombo vyenye Ufanisi
Kwa sasa tuna vyombo vyenye ufanisi sana na kila aina ya pishi ukitumia chombo mahususi gharama itapungua, maji ukichemsha kwa jug kettle, chips ukipikia flyer, chakula ukipasha kwa microwave, wali ukipikia rice cooker, vitu vinavyotumia muda kuiva ukitumia pressure cooker n.k. Lakini sasa hivi kuna majiko kama Induction cooker ambayo ufanisi wake wa kutokupoteza nishati ni mpaka asilimia 90.
Kwahio kwa karne hii kuna kila aina ya vifaa vya kupikia mpaka kuna Slow Cooker ambapo matumizi yake huenda yakawa ni kama taa za zamani. Ingawa kifaa hiki kinatumia muda mrefu ila kwa Maisha ya sasa mtu anaweza akaset jiko lake asubuhi na kuondoka na kuacha ameweka chakula chake akirudi baada ya masaa nane anakuta ndio kimeiva… na kimekula chini ya unit moja.
Jinsi ya Kufanya Familia zitumie gharama ndogo au bila Gharama za Kifedha
Ili kufanisha hili itabidi uwepo ushirikiano na Kampuni ya Ufuaji na Usambazaji wa Umeme (TANESCO) ili iweze kuzifanya Kaya sio tu ziwe Watumiaji wa Nishati bali Wazalishaji wa Nishati hio. Kwa ufupi nyumba hizi zikiwekewa Solar Panels (ambazo kwa sasa duniani gharama imeshuka sana na Serikali nyingi zinatoa Ruzuku) na bila hata kuwa na mfumo wa Storage (Battery) ambazo mpaka sasa ndio gharama zaidi katika mfumo wa Solar, Kaya hizi zinaweza zikawa zinalisha umeme kutoka kwenye Mapaa yao na badala ya kutunza umeme huo unaunganishwa moja kwa moja kwenye Grid na kwa kutumia Smart Meter (Direct to Grid Meters) Tanesco watampa Credit huyu mzalishaji hivyo kama matumizi yake ni madogo kuliko anavyozalisha atajikuta anapata credit (umeme unaongezeka kwenye Luku na sio Kupungua). Hivyo matumizi yake / Mapishi hayatamgharimu pesa yoyote.
Na kwa vile huko vijijini wazee wetu huenda hawana pesa (cash) lakini nina uhakika wana paa la nyumba hivyo kwa kutumia hilo paa lao kuzalisha umeme wanaweza kujikuta uzalishaji wao huo unawafanya waweze kupika bure bila kutoa hata senti moja….
Na tukiangalia hapo juu kama familia ya watu wanne inatumia kama units 3.3 kwa siku, tukichukulia na losses katika ubadilishaji wa umeme kutoka DC mpaka AC na tukasema labda tuzalishe units 5 hapo mtu atahitaji panels kama 12 za 415w na eneo linalotakiwa kwa panels hizo za 1.8 x 1.1m ni 28m2 (mita za mraba 28) tu.
Kwahio mtu huyu atawekewa hizo panels kwenye paa lake (hata kwa mkopo au credit) na kila anavyozalisha atakuwa anapunguza pesa ambazo angenunulia umeme.
Mahitaji ya kufanikisha hilo hapo Juu.
Ili kufanikisha hilo inabidi Tanesco anunue na kufunga smart meters kwa watumiaji wote na kila umeme utakavyokuwa unazalishwa unapelekwa moja kwa moja kwenye grid na mzalishaji anapata credit na akitumia anatumia credit zake, akitumia zaidi analipa.
Na sababu umeme wa solar unazalishwa mchana na hivyo hii huenda ikapelekea uzalishaji mkubwa wa nishati mchana kuliko wakati mwingine Tanesco wanaweza kuweka bei katika Tariffs kwamba mtu akitumia mchana bei inakuwa ndogo kuliko akitumia usiku. Vilevile kwa kutumia Bwawa la Nyerere na Mabwawa mengine yote ya umeme kama Battery / Storage (mchana umeme ukizalishawa utakwenda kwenye grid na kutumia umeme huo kurudisha maji kwa pump kutoka Bwawa la chini mpaka juu ili usiku maji yale yakishuka tena yazalishe umeme) hii itasaidia kuweka uwiano katika uzalishaji na utumiaji.
Hitimisho
Uwezo tunao, na mahitaji tunayo..., Ili tufanikishe hili kilichobaki ni kuwa na Nia Pekee…, kwa kufanikisha hili tutaweza kuondokana na matumizi ya Nishati chafu na Tanzania kuwa moja ya nchi inayotumia nishati safi kabisa katika kupikia (Jua na Maji) hivyo tutakuwa tumefanikiwa kwa upande wetu kutunza mazingira ya dunia.
Na kwa yule ambaye leo yupo Kijijini anapikia Bure itakuwa rahisi kukuelewa ukimwambia ahamie huku ambapo atakuwa anapikia bure au kwa gharama ndogo kulingana na matumizi yake, Na vilevile kama wananchi tutakuwa tumeongeza chanzo cha uzalishaji mwingine katika Energy Mix ya Tanesco / Umeme, na kwa kufanya hivyo tutakuwa tumejizatiti zaidi kama taifa.
Kwenye huu Uzi taelezea ni jinsi Gani Nishati hii Safi na Bora kuliko Gesi inaweza kuwa na Gharama mpaka ya 0 Kwa mtumiaji, Na hapo bila / kabla ya Serikali Kushuka Bei ya Units. Kwahio kwenye huu uzi tutajikita kwenye maelezo ni Vipi watu wanaweza kutumia Umeme huu bila kulipia gharama ya Kifedha, Ukizingatia wengi wanaotumia Kuni vijijini hawahitaji kutoa pesa kutumia kuni hizo zaidi ya nguvu zao
Utangulizi:
Ili kufahamu gharama ambayo itatumika au inatakiwa kutumika ni vema kwanza tukafahamu mahitaji (wastani wa kila kaya inatumia nishati kiasi gani katika mapishi), baada ya hapo tutahitaji kuangalia na kufahamu ni vyombo vya aina gani vyenye ufanisi vitakavyomsaidia mtumiaji. Na mwisho kabisa tutaangalia njia za kuweza kufanya kwa mtumiaji huyu kuweza kupika kwa gharama ndogo au bila gharama yoyote. Na hapa ni kwa kutazama (worse case scenario) iwapo Serikali na Taasisi husika hazitashusha bei za umeme.
Mahitaji ya Nishati katika Mapishi katika Kaya ya Mwafrika.
Hapa sababu sina takwimu zangu binafsi nimeangalia kwenye mtandao na nimeona hii
“The World Energy Council (1999) found that daily cooking energy consumption per capita varied from 11.5 to 49 MJ, based on field measurements. Despite a wide range of locations and conditions, the range of consumption is quite small. In households where modern cooking energy sources and equipment are used, and the preparation of partially cooked food is common, specific fuel consumption is found to be in the region of 2 to 3 MJ/capita/day.” Balmer 2007
However, even here although he acknowledges that modern energy requires a lot less than biomass, he does not dig into the details of the amount of energy required with modern cooking. Indeed I am not sure where he gets his 2 to 3MJ/capita/day which is 2.2 to 3.3KWh per day per household of 4 person.
Ingawa hio report ilikuwa ya 2015 na sasa hivi vyombo vina ufanisi zaidi lakini tukichukulia hio kama guide tutaona kwamba familia ya watu wanne inaweza ikatumia 2.2 mpaka 3.3 Units kwa siku, ingawa katika vyanzo mbalimbali namba hio ni kubwa na uhalisia unaweza kuwa 1.2 Units.
Vyombo vyenye Ufanisi
Kwa sasa tuna vyombo vyenye ufanisi sana na kila aina ya pishi ukitumia chombo mahususi gharama itapungua, maji ukichemsha kwa jug kettle, chips ukipikia flyer, chakula ukipasha kwa microwave, wali ukipikia rice cooker, vitu vinavyotumia muda kuiva ukitumia pressure cooker n.k. Lakini sasa hivi kuna majiko kama Induction cooker ambayo ufanisi wake wa kutokupoteza nishati ni mpaka asilimia 90.
Kwahio kwa karne hii kuna kila aina ya vifaa vya kupikia mpaka kuna Slow Cooker ambapo matumizi yake huenda yakawa ni kama taa za zamani. Ingawa kifaa hiki kinatumia muda mrefu ila kwa Maisha ya sasa mtu anaweza akaset jiko lake asubuhi na kuondoka na kuacha ameweka chakula chake akirudi baada ya masaa nane anakuta ndio kimeiva… na kimekula chini ya unit moja.
Jinsi ya Kufanya Familia zitumie gharama ndogo au bila Gharama za Kifedha
Ili kufanisha hili itabidi uwepo ushirikiano na Kampuni ya Ufuaji na Usambazaji wa Umeme (TANESCO) ili iweze kuzifanya Kaya sio tu ziwe Watumiaji wa Nishati bali Wazalishaji wa Nishati hio. Kwa ufupi nyumba hizi zikiwekewa Solar Panels (ambazo kwa sasa duniani gharama imeshuka sana na Serikali nyingi zinatoa Ruzuku) na bila hata kuwa na mfumo wa Storage (Battery) ambazo mpaka sasa ndio gharama zaidi katika mfumo wa Solar, Kaya hizi zinaweza zikawa zinalisha umeme kutoka kwenye Mapaa yao na badala ya kutunza umeme huo unaunganishwa moja kwa moja kwenye Grid na kwa kutumia Smart Meter (Direct to Grid Meters) Tanesco watampa Credit huyu mzalishaji hivyo kama matumizi yake ni madogo kuliko anavyozalisha atajikuta anapata credit (umeme unaongezeka kwenye Luku na sio Kupungua). Hivyo matumizi yake / Mapishi hayatamgharimu pesa yoyote.
Na kwa vile huko vijijini wazee wetu huenda hawana pesa (cash) lakini nina uhakika wana paa la nyumba hivyo kwa kutumia hilo paa lao kuzalisha umeme wanaweza kujikuta uzalishaji wao huo unawafanya waweze kupika bure bila kutoa hata senti moja….
Na tukiangalia hapo juu kama familia ya watu wanne inatumia kama units 3.3 kwa siku, tukichukulia na losses katika ubadilishaji wa umeme kutoka DC mpaka AC na tukasema labda tuzalishe units 5 hapo mtu atahitaji panels kama 12 za 415w na eneo linalotakiwa kwa panels hizo za 1.8 x 1.1m ni 28m2 (mita za mraba 28) tu.
Kwahio mtu huyu atawekewa hizo panels kwenye paa lake (hata kwa mkopo au credit) na kila anavyozalisha atakuwa anapunguza pesa ambazo angenunulia umeme.
Mahitaji ya kufanikisha hilo hapo Juu.
Ili kufanikisha hilo inabidi Tanesco anunue na kufunga smart meters kwa watumiaji wote na kila umeme utakavyokuwa unazalishwa unapelekwa moja kwa moja kwenye grid na mzalishaji anapata credit na akitumia anatumia credit zake, akitumia zaidi analipa.
Na sababu umeme wa solar unazalishwa mchana na hivyo hii huenda ikapelekea uzalishaji mkubwa wa nishati mchana kuliko wakati mwingine Tanesco wanaweza kuweka bei katika Tariffs kwamba mtu akitumia mchana bei inakuwa ndogo kuliko akitumia usiku. Vilevile kwa kutumia Bwawa la Nyerere na Mabwawa mengine yote ya umeme kama Battery / Storage (mchana umeme ukizalishawa utakwenda kwenye grid na kutumia umeme huo kurudisha maji kwa pump kutoka Bwawa la chini mpaka juu ili usiku maji yale yakishuka tena yazalishe umeme) hii itasaidia kuweka uwiano katika uzalishaji na utumiaji.
Hitimisho
Uwezo tunao, na mahitaji tunayo..., Ili tufanikishe hili kilichobaki ni kuwa na Nia Pekee…, kwa kufanikisha hili tutaweza kuondokana na matumizi ya Nishati chafu na Tanzania kuwa moja ya nchi inayotumia nishati safi kabisa katika kupikia (Jua na Maji) hivyo tutakuwa tumefanikiwa kwa upande wetu kutunza mazingira ya dunia.
Na kwa yule ambaye leo yupo Kijijini anapikia Bure itakuwa rahisi kukuelewa ukimwambia ahamie huku ambapo atakuwa anapikia bure au kwa gharama ndogo kulingana na matumizi yake, Na vilevile kama wananchi tutakuwa tumeongeza chanzo cha uzalishaji mwingine katika Energy Mix ya Tanesco / Umeme, na kwa kufanya hivyo tutakuwa tumejizatiti zaidi kama taifa.