Nishati safi ya Kupikia – Gharama Nafuu (Kuanizia 0 Tshs)

Logikos

JF-Expert Member
Feb 26, 2014
12,777
19,939
Huu ni muendelezo wa Uzi wa Kuhoji Nishati gani kwa Tanzania ni Safi na Ina Uwezekano mkubwa kufanikiwa.

Kwenye huu Uzi taelezea ni jinsi Gani Nishati hii Safi na Bora kuliko Gesi inaweza kuwa na Gharama mpaka ya 0 Kwa mtumiaji, Na hapo bila / kabla ya Serikali Kushuka Bei ya Units. Kwahio kwenye huu uzi tutajikita kwenye maelezo ni Vipi watu wanaweza kutumia Umeme huu bila kulipia gharama ya Kifedha, Ukizingatia wengi wanaotumia Kuni vijijini hawahitaji kutoa pesa kutumia kuni hizo zaidi ya nguvu zao

Utangulizi:
Ili kufahamu gharama ambayo itatumika au inatakiwa kutumika ni vema kwanza tukafahamu mahitaji (wastani wa kila kaya inatumia nishati kiasi gani katika mapishi), baada ya hapo tutahitaji kuangalia na kufahamu ni vyombo vya aina gani vyenye ufanisi vitakavyomsaidia mtumiaji. Na mwisho kabisa tutaangalia njia za kuweza kufanya kwa mtumiaji huyu kuweza kupika kwa gharama ndogo au bila gharama yoyote. Na hapa ni kwa kutazama (worse case scenario) iwapo Serikali na Taasisi husika hazitashusha bei za umeme.

Mahitaji ya Nishati katika Mapishi katika Kaya ya Mwafrika.
Hapa sababu sina takwimu zangu binafsi nimeangalia kwenye mtandao na nimeona hii

The World Energy Council (1999) found that daily cooking energy consumption per capita varied from 11.5 to 49 MJ, based on field measurements. Despite a wide range of locations and conditions, the range of consumption is quite small. In households where modern cooking energy sources and equipment are used, and the preparation of partially cooked food is common, specific fuel consumption is found to be in the region of 2 to 3 MJ/capita/day.” Balmer 2007

However, even here although he acknowledges that modern energy requires a lot less than biomass, he does not dig into the details of the amount of energy required with modern cooking. Indeed I am not sure where he gets his 2 to 3MJ/capita/day which is 2.2 to 3.3KWh per day per household of 4 person
.

Ingawa hio report ilikuwa ya 2015 na sasa hivi vyombo vina ufanisi zaidi lakini tukichukulia hio kama guide tutaona kwamba familia ya watu wanne inaweza ikatumia 2.2 mpaka 3.3 Units kwa siku, ingawa katika vyanzo mbalimbali namba hio ni kubwa na uhalisia unaweza kuwa 1.2 Units.

Vyombo vyenye Ufanisi
Kwa sasa tuna vyombo vyenye ufanisi sana na kila aina ya pishi ukitumia chombo mahususi gharama itapungua, maji ukichemsha kwa jug kettle, chips ukipikia flyer, chakula ukipasha kwa microwave, wali ukipikia rice cooker, vitu vinavyotumia muda kuiva ukitumia pressure cooker n.k. Lakini sasa hivi kuna majiko kama Induction cooker ambayo ufanisi wake wa kutokupoteza nishati ni mpaka asilimia 90.

Kwahio kwa karne hii kuna kila aina ya vifaa vya kupikia mpaka kuna Slow Cooker ambapo matumizi yake huenda yakawa ni kama taa za zamani. Ingawa kifaa hiki kinatumia muda mrefu ila kwa Maisha ya sasa mtu anaweza akaset jiko lake asubuhi na kuondoka na kuacha ameweka chakula chake akirudi baada ya masaa nane anakuta ndio kimeiva… na kimekula chini ya unit moja.

Jinsi ya Kufanya Familia zitumie gharama ndogo au bila Gharama za Kifedha
Ili kufanisha hili itabidi uwepo ushirikiano na Kampuni ya Ufuaji na Usambazaji wa Umeme (TANESCO) ili iweze kuzifanya Kaya sio tu ziwe Watumiaji wa Nishati bali Wazalishaji wa Nishati hio. Kwa ufupi nyumba hizi zikiwekewa Solar Panels (ambazo kwa sasa duniani gharama imeshuka sana na Serikali nyingi zinatoa Ruzuku) na bila hata kuwa na mfumo wa Storage (Battery) ambazo mpaka sasa ndio gharama zaidi katika mfumo wa Solar, Kaya hizi zinaweza zikawa zinalisha umeme kutoka kwenye Mapaa yao na badala ya kutunza umeme huo unaunganishwa moja kwa moja kwenye Grid na kwa kutumia Smart Meter (Direct to Grid Meters) Tanesco watampa Credit huyu mzalishaji hivyo kama matumizi yake ni madogo kuliko anavyozalisha atajikuta anapata credit (umeme unaongezeka kwenye Luku na sio Kupungua). Hivyo matumizi yake / Mapishi hayatamgharimu pesa yoyote.

Na kwa vile huko vijijini wazee wetu huenda hawana pesa (cash) lakini nina uhakika wana paa la nyumba hivyo kwa kutumia hilo paa lao kuzalisha umeme wanaweza kujikuta uzalishaji wao huo unawafanya waweze kupika bure bila kutoa hata senti moja….

Na tukiangalia hapo juu kama familia ya watu wanne inatumia kama units 3.3 kwa siku, tukichukulia na losses katika ubadilishaji wa umeme kutoka DC mpaka AC na tukasema labda tuzalishe units 5 hapo mtu atahitaji panels kama 12 za 415w na eneo linalotakiwa kwa panels hizo za 1.8 x 1.1m ni 28m2 (mita za mraba 28) tu.

Kwahio mtu huyu atawekewa hizo panels kwenye paa lake (hata kwa mkopo au credit) na kila anavyozalisha atakuwa anapunguza pesa ambazo angenunulia umeme.


Mahitaji ya kufanikisha hilo hapo Juu.

Ili kufanikisha hilo inabidi Tanesco anunue na kufunga smart meters kwa watumiaji wote na kila umeme utakavyokuwa unazalishwa unapelekwa moja kwa moja kwenye grid na mzalishaji anapata credit na akitumia anatumia credit zake, akitumia zaidi analipa.

Na sababu umeme wa solar unazalishwa mchana na hivyo hii huenda ikapelekea uzalishaji mkubwa wa nishati mchana kuliko wakati mwingine Tanesco wanaweza kuweka bei katika Tariffs kwamba mtu akitumia mchana bei inakuwa ndogo kuliko akitumia usiku. Vilevile kwa kutumia Bwawa la Nyerere na Mabwawa mengine yote ya umeme kama Battery / Storage (mchana umeme ukizalishawa utakwenda kwenye grid na kutumia umeme huo kurudisha maji kwa pump kutoka Bwawa la chini mpaka juu ili usiku maji yale yakishuka tena yazalishe umeme) hii itasaidia kuweka uwiano katika uzalishaji na utumiaji.

Hitimisho
Uwezo tunao, na mahitaji tunayo..., Ili tufanikishe hili kilichobaki ni kuwa na Nia Pekee…, kwa kufanikisha hili tutaweza kuondokana na matumizi ya Nishati chafu na Tanzania kuwa moja ya nchi inayotumia nishati safi kabisa katika kupikia (Jua na Maji) hivyo tutakuwa tumefanikiwa kwa upande wetu kutunza mazingira ya dunia.

Na kwa yule ambaye leo yupo Kijijini anapikia Bure itakuwa rahisi kukuelewa ukimwambia ahamie huku ambapo atakuwa anapikia bure au kwa gharama ndogo kulingana na matumizi yake, Na vilevile kama wananchi tutakuwa tumeongeza chanzo cha uzalishaji mwingine katika Energy Mix ya Tanesco / Umeme, na kwa kufanya hivyo tutakuwa tumejizatiti zaidi kama taifa.
 
Kila la heri, ni wazo zuri.
Mkuu kila la heri kwenye nini tena ? Hili wazo likifanikiwa litatutoa kimaso-maso wote wahitaji wa kupika na chakula sababu gharama za maisha zitapungua (na binafsi nadhani halitafanikiwa sababu gesi inapigiwa promo zaidi) kwahio nimeweka hapa bandiko Habari na Hoja Mchanganyiko ili tufahamishane huenda nimekosea sehemu na umeme ni gharama na haufai (binafsi kila nikiangalia sioni kwanini tupigie chapio LPG - Ambayo ni Propane Gas na Hatuizalishi nchini)
 
  • Thanks
Reactions: K11
Huu ni muendelezo wa Uzi wa Kuhoji Nishati gani kwa Tanzania ni Safi na Ina Uwezekano mkubwa kufanikiwa.

Kwenye huu Uzi taelezea ni jinsi Gani Nishati hii Safi na Bora kuliko Gesi inaweza kuwa na Gharama mpaka ya 0 Kwa mtumiaji, Na hapo bila / kabla ya Serikali Kushuka Bei ya Units. Kwahio kwenye huu uzi tutajikita kwenye maelezo ni Vipi watu wanaweza kutumia Umeme huu bila kulipia gharama ya Kifedha, Ukizingatia wengi wanaotumia Kuni vijijini hawahitaji kutoa pesa kutumia kuni hizo zaidi ya nguvu zao

Utangulizi:
Ili kufahamu gharama ambayo itatumika au inatakiwa kutumika ni vema kwanza tukafahamu mahitaji (wastani wa kila kaya inatumia nishati kiasi gani katika mapishi), baada ya hapo tutahitaji kuangalia na kufahamu ni vyombo vya aina gani vyenye ufanisi vitakavyomsaidia mtumiaji. Na mwisho kabisa tutaangalia njia za kuweza kufanya kwa mtumiaji huyu kuweza kupika kwa gharama ndogo au bila gharama yoyote. Na hapa ni kwa kutazama (worse case scenario) iwapo Serikali na Taasisi husika hazitashusha bei za umeme.

Mahitaji ya Nishati katika Mapishi katika Kaya ya Mwafrika.
Hapa sababu sina takwimu zangu binafsi nimeangalia kwenye mtandao na nimeona hii



Ingawa hio report ilikuwa ya 2015 na sasa hivi vyombo vina ufanisi zaidi lakini tukichukulia hio kama guide tutaona kwamba familia ya watu wanne inaweza ikatumia 2.2 mpaka 3.3 Units kwa siku, ingawa katika vyanzo mbalimbali namba hio ni kubwa na uhalisia unaweza kuwa 1.2 Units.

Vyombo vyenye Ufanisi
Kwa sasa tuna vyombo vyenye ufanisi sana na kila aina ya pishi ukitumia chombo mahususi gharama itapungua, maji ukichemsha kwa jug kettle, chips ukipikia flyer, chakula ukipasha kwa microwave, wali ukipikia rice cooker, vitu vinavyotumia muda kuiva ukitumia pressure cooker n.k. Lakini sasa hivi kuna majiko kama Induction cooker ambayo ufanisi wake wa kutokupoteza nishati ni mpaka asilimia 90.

Kwahio kwa karne hii kuna kila aina ya vifaa vya kupikia mpaka kuna Slow Cooker ambapo matumizi yake huenda yakawa ni kama taa za zamani. Ingawa kifaa hiki kinatumia muda mrefu ila kwa Maisha ya sasa mtu anaweza akaset jiko lake asubuhi na kuondoka na kuacha ameweka chakula chake akirudi baada ya masaa nane anakuta ndio kimeiva… na kimekula chini ya unit moja.

Jinsi ya Kufanya Familia zitumie gharama ndogo au bila Gharama za Kifedha
Ili kufanisha hili itabidi uwepo ushirikiano na Kampuni ya Ufuaji na Usambazaji wa Umeme (TANESCO) ili iweze kuzifanya Kaya sio tu ziwe Watumiaji wa Nishati bali Wazalishaji wa Nishati hio. Kwa ufupi nyumba hizi zikiwekewa Solar Panels (ambazo kwa sasa duniani gharama imeshuka sana na Serikali nyingi zinatoa Ruzuku) na bila hata kuwa na mfumo wa Storage (Battery) ambazo mpaka sasa ndio gharama zaidi katika mfumo wa Solar, Kaya hizi zinaweza zikawa zinalisha umeme kutoka kwenye Mapaa yao na badala ya kutunza umeme huo unaunganishwa moja kwa moja kwenye Grid na kwa kutumia Smart Meter (Direct to Grid Meters) Tanesco watampa Credit huyu mzalishaji hivyo kama matumizi yake ni madogo kuliko anavyozalisha atajikuta anapata credit (umeme unaongezeka kwenye Luku na sio Kupungua). Hivyo matumizi yake / Mapishi hayatamgharimu pesa yoyote.

Na kwa vile huko vijijini wazee wetu huenda hawana pesa (cash) lakini nina uhakika wana paa la nyumba hivyo kwa kutumia hilo paa lao kuzalisha umeme wanaweza kujikuta uzalishaji wao huo unawafanya waweze kupika bure bila kutoa hata senti moja….

Na tukiangalia hapo juu kama familia ya watu wanne inatumia kama units 3.3 kwa siku, tukichukulia na losses katika ubadilishaji wa umeme kutoka DC mpaka AC na tukasema labda tuzalishe units 5 hapo mtu atahitaji panels kama 12 za 415w na eneo linalotakiwa kwa panels hizo za 1.8 x 1.1m ni 28m2 (mita za mraba 28) tu.

Kwahio mtu huyu atawekewa hizo panels kwenye paa lake (hata kwa mkopo au credit) na kila anavyozalisha atakuwa anapunguza pesa ambazo angenunulia umeme.


Mahitaji ya kufanikisha hilo hapo Juu.

Ili kufanikisha hilo inabidi Tanesco anunue na kufunga smart meters kwa watumiaji wote na kila umeme utakavyokuwa unazalishwa unapelekwa moja kwa moja kwenye grid na mzalishaji anapata credit na akitumia anatumia credit zake, akitumia zaidi analipa.

Na sababu umeme wa solar unazalishwa mchana na hivyo hii huenda ikapelekea uzalishaji mkubwa wa nishati mchana kuliko wakati mwingine Tanesco wanaweza kuweka bei katika Tariffs kwamba mtu akitumia mchana bei inakuwa ndogo kuliko akitumia usiku. Vilevile kwa kutumia Bwawa la Nyerere na Mabwawa mengine yote ya umeme kama Battery / Storage (mchana umeme ukizalishawa utakwenda kwenye grid na kutumia umeme huo kurudisha maji kwa pump kutoka Bwawa la chini mpaka juu ili usiku maji yale yakishuka tena yazalishe umeme) hii itasaidia kuweka uwiano katika uzalishaji na utumiaji.

Hitimisho
Uwezo tunao, na mahitaji tunayo..., Ili tufanikishe hili kilichobaki ni kuwa na Nia Pekee…, kwa kufanikisha hili tutaweza kuondokana na matumizi ya Nishati chafu na Tanzania kuwa moja ya nchi inayotumia nishati safi kabisa katika kupikia (Jua na Maji) hivyo tutakuwa tumefanikiwa kwa upande wetu kutunza mazingira ya dunia.

Na kwa yule ambaye leo yupo Kijijini anapikia Bure itakuwa rahisi kukuelewa ukimwambia ahamie huku ambapo atakuwa anapikia bure au kwa gharama ndogo kulingana na matumizi yake, Na vilevile kama wananchi tutakuwa tumeongeza chanzo cha uzalishaji mwingine katika Energy Mix ya Tanesco / Umeme, na kwa kufanya hivyo tutakuwa tumejizatiti zaidi kama taifa.
Bado sijajua manufaa ya huu uzi, wiki iliyopita niliandika kuwapa wafugaji na wakulima mitungi ya gesi ni serikali kujikita kibiashara zaidi kuliko kumsaidia mwananchi kupata nishati safi. Mkulima na mfugaji anao uwezo mkubwa sana wa kujitegemea kuzalisha gesi kutokana na mabaki ya mazao na samadi ya mifugo yake, hivyo ununuzi wa gesi na majiko ya umeme hayamuhusu.
Huu utengenezaji wa gesi unaweza pia kufanywa na wakazi wa mijini ambao kila siku wanamabaki mengi sana ya vyakula na takataka nyingine zinazooza kirahisi, hawa wote gharama ya nishati ya kupikia na taa ni sifuri.
 
  • Thanks
Reactions: K11
Bado sijajua manufaa ya huu uzi,
Manufaa ya huu uzi ni ku-pose swali la nishati gani ni safi na nafuu ya kupikia kwa mazingira ya Tanzania na mimi nimekuja hapo na jibu la umeme tena likiunganishwa na uzalishaji kwa kutumia solar litakuwa na ufanisi na practicability bila shida yoyote
wiki iliyopita niliandika kuwapa wafugaji na wakulima mitungi ya gesi ni serikali kujikita kibiashara zaidi kuliko kumsaidia mwananchi kupata nishati safi.
Hilo wala halina ubishi na sio Serikali kujikita kwenye biashara tu bali kuwa madalali wa wafanyabiashara ambao sio necessarily wanatoka nchini sababu hii Propane (LPG) tunaagiza
Mkulima na mfugaji anao uwezo mkubwa sana wa kujitegemea kuzalisha gesi kutokana na mabaki ya mazao na samadi ya mifugo yake, hivyo ununuzi wa gesi na majiko ya umeme hayamuhusu.
Naam Biogas is the way to go ila kwanini hawafanyi ? Biogas inahitaji manpower pia ya kukoroga hio kitu na sehemu kama Mageraza hata wanaweza kutumia kinyesi chao ila ndio hivyo kuna manpower ya kufanya hii kitu na maintenance ya mara kwa mara ili kuhakikisha hii kitu inafanya kazi at peak performance
Huu utengenezaji wa gesi unaweza pia kufanywa na wakazi wa mijini ambao kila siku wanamabaki mengi sana ya vyakula na takataka nyingine zinazooza kirahisi, hawa wote gharama ya nishati ya kupikia na taa ni sifuri.
Ukiongelea taa utataka kuwafanya watu warudi kwenye Karabai (Ukisema ubadilishe hii methane ili uwashe taa za kawaida unapunguza efficiency) na sidhani kama utaniambia hata wewe mwenyewe hapo kazi ya ku-maintain hizi bio-digester kwa mtu ambaye sio mkulima wala mfugaji ni jambo rahisi... In comparison kwenye proposal yangu yoyote mwenye paa lake la nyumba akishaweka hivyo vitu haviguzi yeye ni kuwasha tu switch ya umeme na kupika....
 
  • Thanks
Reactions: K11
Huu ni muendelezo wa Uzi wa Kuhoji Nishati gani kwa Tanzania ni Safi na Ina Uwezekano mkubwa kufanikiwa.

Kwenye huu Uzi taelezea ni jinsi Gani Nishati hii Safi na Bora kuliko Gesi inaweza kuwa na Gharama mpaka ya 0 Kwa mtumiaji, Na hapo bila / kabla ya Serikali Kushuka Bei ya Units. Kwahio kwenye huu uzi tutajikita kwenye maelezo ni Vipi watu wanaweza kutumia Umeme huu bila kulipia gharama ya Kifedha, Ukizingatia wengi wanaotumia Kuni vijijini hawahitaji kutoa pesa kutumia kuni hizo zaidi ya nguvu zao

Utangulizi:
Ili kufahamu gharama ambayo itatumika au inatakiwa kutumika ni vema kwanza tukafahamu mahitaji (wastani wa kila kaya inatumia nishati kiasi gani katika mapishi), baada ya hapo tutahitaji kuangalia na kufahamu ni vyombo vya aina gani vyenye ufanisi vitakavyomsaidia mtumiaji. Na mwisho kabisa tutaangalia njia za kuweza kufanya kwa mtumiaji huyu kuweza kupika kwa gharama ndogo au bila gharama yoyote. Na hapa ni kwa kutazama (worse case scenario) iwapo Serikali na Taasisi husika hazitashusha bei za umeme.

Mahitaji ya Nishati katika Mapishi katika Kaya ya Mwafrika.
Hapa sababu sina takwimu zangu binafsi nimeangalia kwenye mtandao na nimeona hii



Ingawa hio report ilikuwa ya 2015 na sasa hivi vyombo vina ufanisi zaidi lakini tukichukulia hio kama guide tutaona kwamba familia ya watu wanne inaweza ikatumia 2.2 mpaka 3.3 Units kwa siku, ingawa katika vyanzo mbalimbali namba hio ni kubwa na uhalisia unaweza kuwa 1.2 Units.

Vyombo vyenye Ufanisi
Kwa sasa tuna vyombo vyenye ufanisi sana na kila aina ya pishi ukitumia chombo mahususi gharama itapungua, maji ukichemsha kwa jug kettle, chips ukipikia flyer, chakula ukipasha kwa microwave, wali ukipikia rice cooker, vitu vinavyotumia muda kuiva ukitumia pressure cooker n.k. Lakini sasa hivi kuna majiko kama Induction cooker ambayo ufanisi wake wa kutokupoteza nishati ni mpaka asilimia 90.

Kwahio kwa karne hii kuna kila aina ya vifaa vya kupikia mpaka kuna Slow Cooker ambapo matumizi yake huenda yakawa ni kama taa za zamani. Ingawa kifaa hiki kinatumia muda mrefu ila kwa Maisha ya sasa mtu anaweza akaset jiko lake asubuhi na kuondoka na kuacha ameweka chakula chake akirudi baada ya masaa nane anakuta ndio kimeiva… na kimekula chini ya unit moja.

Jinsi ya Kufanya Familia zitumie gharama ndogo au bila Gharama za Kifedha
Ili kufanisha hili itabidi uwepo ushirikiano na Kampuni ya Ufuaji na Usambazaji wa Umeme (TANESCO) ili iweze kuzifanya Kaya sio tu ziwe Watumiaji wa Nishati bali Wazalishaji wa Nishati hio. Kwa ufupi nyumba hizi zikiwekewa Solar Panels (ambazo kwa sasa duniani gharama imeshuka sana na Serikali nyingi zinatoa Ruzuku) na bila hata kuwa na mfumo wa Storage (Battery) ambazo mpaka sasa ndio gharama zaidi katika mfumo wa Solar, Kaya hizi zinaweza zikawa zinalisha umeme kutoka kwenye Mapaa yao na badala ya kutunza umeme huo unaunganishwa moja kwa moja kwenye Grid na kwa kutumia Smart Meter (Direct to Grid Meters) Tanesco watampa Credit huyu mzalishaji hivyo kama matumizi yake ni madogo kuliko anavyozalisha atajikuta anapata credit (umeme unaongezeka kwenye Luku na sio Kupungua). Hivyo matumizi yake / Mapishi hayatamgharimu pesa yoyote.

Na kwa vile huko vijijini wazee wetu huenda hawana pesa (cash) lakini nina uhakika wana paa la nyumba hivyo kwa kutumia hilo paa lao kuzalisha umeme wanaweza kujikuta uzalishaji wao huo unawafanya waweze kupika bure bila kutoa hata senti moja….

Na tukiangalia hapo juu kama familia ya watu wanne inatumia kama units 3.3 kwa siku, tukichukulia na losses katika ubadilishaji wa umeme kutoka DC mpaka AC na tukasema labda tuzalishe units 5 hapo mtu atahitaji panels kama 12 za 415w na eneo linalotakiwa kwa panels hizo za 1.8 x 1.1m ni 28m2 (mita za mraba 28) tu.

Kwahio mtu huyu atawekewa hizo panels kwenye paa lake (hata kwa mkopo au credit) na kila anavyozalisha atakuwa anapunguza pesa ambazo angenunulia umeme.


Mahitaji ya kufanikisha hilo hapo Juu.

Ili kufanikisha hilo inabidi Tanesco anunue na kufunga smart meters kwa watumiaji wote na kila umeme utakavyokuwa unazalishwa unapelekwa moja kwa moja kwenye grid na mzalishaji anapata credit na akitumia anatumia credit zake, akitumia zaidi analipa.

Na sababu umeme wa solar unazalishwa mchana na hivyo hii huenda ikapelekea uzalishaji mkubwa wa nishati mchana kuliko wakati mwingine Tanesco wanaweza kuweka bei katika Tariffs kwamba mtu akitumia mchana bei inakuwa ndogo kuliko akitumia usiku. Vilevile kwa kutumia Bwawa la Nyerere na Mabwawa mengine yote ya umeme kama Battery / Storage (mchana umeme ukizalishawa utakwenda kwenye grid na kutumia umeme huo kurudisha maji kwa pump kutoka Bwawa la chini mpaka juu ili usiku maji yale yakishuka tena yazalishe umeme) hii itasaidia kuweka uwiano katika uzalishaji na utumiaji.

Hitimisho
Uwezo tunao, na mahitaji tunayo..., Ili tufanikishe hili kilichobaki ni kuwa na Nia Pekee…, kwa kufanikisha hili tutaweza kuondokana na matumizi ya Nishati chafu na Tanzania kuwa moja ya nchi inayotumia nishati safi kabisa katika kupikia (Jua na Maji) hivyo tutakuwa tumefanikiwa kwa upande wetu kutunza mazingira ya dunia.

Na kwa yule ambaye leo yupo Kijijini anapikia Bure itakuwa rahisi kukuelewa ukimwambia ahamie huku ambapo atakuwa anapikia bure au kwa gharama ndogo kulingana na matumizi yake, Na vilevile kama wananchi tutakuwa tumeongeza chanzo cha uzalishaji mwingine katika Energy Mix ya Tanesco / Umeme, na kwa kufanya hivyo tutakuwa tumejizatiti zaidi kama taifa.
We mwandishi unaishi nchi gani? Yaani umejaa kirahisi hivyo na kupoteza muda wako kutushauri ujinga.

Serikali tunapowambia wananchi juu ya nishati safi, nishati rahisi na blaa blaani kibao ni kuawazuga tu.

Wewe si unajua mwaka huu kuna uchaguzi wa serikali za mitaa na mwaka kesho serikali kuu?
Sasa sisi hatuna nia ya kuwapatia nishati safi wala nini.
Nia yetu ni ili mjae mtupe mi-kura hiyo ili tuendelee kufisadi, kutanua na ma-VX V8 na kuzuzura duniani na lile airbus 220.

Sasa nyie acheni kutumia mkaa na kuni mkisubiria nishati hewa safi. Mtasubiri sana.
 
We mwandishi unaishi nchi gani? Yaani umejaa kirahisi hivyo na kupoteza muda wako kutushauri ujinga.
Mkuu wewe unaongelea what is, mimi nakwambia what can / might be (ni nini kinawezekana., sababu kilichopo au kitakachokuja huenda sio kizuri)..., Kuna Pesa nyingi sana sasa hivi duniani inatoka kuchangia katika Green Earth..., Solar Panels duniani zimewekewa Ruzuku za kutosha na Hapa nchini umeanzishwa mfuko wa Nishati Safi..., Ni kwamba hizo Pesa zipo..., Sasa kitakachotokea huenda hizo Pesa zikanufaisha watu na Biashara zao au kuwekezwa kwenye Nishati ya gharama ambayo haitamsaidia mwananchi...

Kwahio hapa wewe unachoita ni kukulisha ujinga (mimi naita ni kushauri na kuanzisha Debate) Je ni kweli Nishati ya Gesi / Mitungi ambayo kuna uwezekano mkubwa ndio itapigiwa chapio ya kuwa Nishati ndio the best katika alternative zilizopo...., Kwahio badala ya kukushauri Ujinga nakupa upande wa pili wa shilingi ili hata ukiambiwa chukua hizi gesi au gesi imeshuka bei na kuwa nusu (fahamu kwamba huenda hio nusu nyingine unailipia kivingine kwa kodi zako)
Serikali tunapowambia wananchi juu ya nishati safi, nishati rahisi na blaa blaani kibao ni kuawazuga tu.
Hapo kuna Pesa na mfuko umeanzishwa kwahio kuna lobbyists na wadau wameshaona fursa ya kupiga pesa..., ni kama sasa hivi hatujaanza safari na kuna njia mbili huenda njia tutakayokwenda itakuwa na miiba na mabonde kwahio kuliko kwenda huko ni vema tukaangalia njia tofauti ambayo ni bora..., Kwahio nadhani kwa uhai wa mjadala sio nini Serikali inafanya au itafanya bali ni njia ipi ni bora kwetu...,
Wewe si unajua mwaka huu kuna uchaguzi wa serikali za mitaa na mwaka kesho serikali kuu?
Sasa sisi hatuna nia ya kuwapatia nishati safi wala nini.
Nia yetu ni ili mjae mtupe mi-kura hiyo ili tuendelee kufisadi, kutanua na ma-VX V8 na kuzuzura duniani na lile airbus 220.

Sasa nyie acheni kutumia mkaa na kuni mkisubiria nishati hewa safi. Mtasubiri sana.
Tena kwanza watakachofanya hapa sio nguvu ya kupata kura (huenda hapo kuna propaganda za kwamba tumefanya hiki au kile) baada tu ya uchaguzi zitakuja sheria za kupiga marufuku mkaa na kuni ambapo Nishati hizo zitakuwa magendo na kupanda bei maradufu (kama utazipata)..., Kwahio narudia tena huu uzi sio Serikali inafanya nini au itafanya nini bali ni kipi kinachoweza kufanyika ambacho ni bora..., Sababu tukienda kwa mfumo wa LPG (Propane) Mitungi ya nyumbani ili kushuka bei itakuwa ni Ruzuku..., Tukisema tuote ndoto za Alinacha kusambaza gesi ya Mtwara kama maji kwenye kila Kaya (Hizo gharama za Infrastructure itakuwa balaa)..., Tukisema tutumie miundombinu iliyopo kwenye kaya karibia zote (UMEME) hio ni practical, rahisi na itakuwa convenient kwa kila mwana-kaya

Kwahio Mdau tuache kupiga Siasa na tuangalie kwanza Kipi ni Bora kwa Tanzania na kipi Kinawezekana, Katika hili tufanye Opportunity Cost ambayo tukichagua vibaya Kodi zetu zitaumia na bado maisha yataendelea kuwa magumu (gharama ya upishi)
 
Manufaa ya huu uzi ni ku-pose swali la nishati gani ni safi na nafuu ya kupikia kwa mazingira ya Tanzania na mimi nimekuja hapo na jibu la umeme tena likiunganishwa na uzalishaji kwa kutumia solar litakuwa na ufanisi na practicability bila shida yoyote

Hilo wala halina ubishi na sio Serikali kujikita kwenye biashara tu bali kuwa madalali wa wafanyabiashara ambao sio necessarily wanatoka nchini sababu hii Propane (LPG) tunaagiza

Naam Biogas is the way to go ila kwanini hawafanyi ? Biogas inahitaji manpower pia ya kukoroga hio kitu na sehemu kama Mageraza hata wanaweza kutumia kinyesi chao ila ndio hivyo kuna manpower ya kufanya hii kitu na maintenance ya mara kwa mara ili kuhakikisha hii kitu inafanya kazi at peak performance

Ukiongelea taa utataka kuwafanya watu warudi kwenye Karabai (Ukisema ubadilishe hii methane ili uwashe taa za kawaida unapunguza efficiency) na sidhani kama utaniambia hata wewe mwenyewe hapo kazi ya ku-maintain hizi bio-digester kwa mtu ambaye sio mkulima wala mfugaji ni jambo rahisi... In comparison kwenye proposal yangu yoyote mwenye paa lake la nyumba akishaweka hivyo vitu haviguzi yeye ni kuwasha tu switch ya umeme na kupika....
Ndoo moja ya maji ukichanganya na ndoo moja ya samadi inakutosha kwa siku kadhaa na hautashindwa kukoroga, baada ya kuanza kinachofuatia ni kuongeza au kuzimua.
 
Ndoo moja ya maji ukichanganya na ndoo moja ya samadi inakutosha kwa siku kadhaa na hautashindwa kukoroga, baada ya kuanza kinachofuatia ni kuongeza au kuzimua.
Na hii kwako wewe unaona ni efficient kuliko mtu kuwa na panels kwenye Paa lake na bila kufanya lolote ?, Na undhani hii inaweza ikawa replicated kwa kila kaya ?

Watu ni wavivu na hawataki kufanya lolote ndio maana watu kama magereza na mashule ambao wanazalisha kilo za kutosha za kinyesi hawajaamia kwenye hizi Biogas..., Na kwa ushauri wangu kama tungekuwa hatuna vyanzo vingine rahisi ningeshauri kuwepo na bio-digester za kuchukua uchafu wa miji na kutengeneza methane ili kuchemshia maji / boiler na na kupata umeme kuunganisha kwenye Grid...., In Tanzania hatuwezi ku-beat umeme kutokana na advantage kwamba infrastructure yake imesambaa kuliko nishati nyingine yoyote....
 
Na hii kwako wewe unaona ni efficient kuliko mtu kuwa na panels kwenye Paa lake na bila kufanya lolote ?, Na undhani hii inaweza ikawa replicated kwa kila kaya ?

Watu ni wavivu na hawataki kufanya lolote ndio maana watu kama magereza na mashule ambao wanazalisha kilo za kutosha za kinyesi hawajaamia kwenye hizi Biogas..., Na kwa ushauri wangu kama tungekuwa hatuna vyanzo vingine rahisi ningeshauri kuwepo na bio-digester za kuchukua uchafu wa miji na kutengeneza methane ili kuchemshia maji / boiler na na kupata umeme kuunganisha kwenye Grid...., In Tanzania hatuwezi ku-beat umeme kutokana na advantage kwamba infrastructure yake imesambaa kuliko nishati nyingine yoyote....
Mimi ninazo panel ni kwa ajili ya taa tu, nikihitaji na kupikia itanigharimu sana, hata hivyo uchanganyaji haufanyiki kila siku, inawezekana mara moja kwa wiki..
 
Mimi ninazo panel ni kwa ajili ya taa tu, nikihitaji na kupikia itanigharimu sana, hata hivyo uchanganyaji haufanyiki kila siku, inawezekana mara moja kwa wiki..
Kutumia panel DC kwa ajili ya kupikia ni kujidangaya haiwezekani ufanye hivyo directly vifaa vingi ni AC na Wattage ni kubwa na kutoa kwenye panels, kupeleka kwenye battery alafu kubadilisha tena kuwa AC alafu upikie utakuwa wendawazimu...., Kwahio process ipo vipi angalia.....

Tanesco na umeme wake ndio unapelekwa kwa wadau ili waweze kupikia unless unasema kwamba umeme kwa Tanzania hauwezi ukawa Nishati safi na salama na practical na hapo tunaweza tuka-argue katika uzi huu kwa kujiuliza ni Nishati gani Safi na Nafuu....

Sasa kama tutakubaliana kwamba umeme ni Nishati Safi kwa kupikia point ya huu uzi ni kuongeza uzalishaji wa umeme...., wewe na hizo panel zako kwenye paa lako ukizalisha umeme hauhitaji hizo battery zako (bei ya battery na maintenance unaweza kuongezea panels nyingine nyingi zaidi) sasa kama kwako unatumia units 1.2 - 3.3 kwa siku kwa kupikia paa lako kama linazalisha units kama hizo au zaidi badala ya kuzitunza au kuzitumia smart meter inazipeleka moja kwa moja kwenye grid wewe unaendelea kutumia iwapo utakuwa unazalisha units 3.3 lakini unatumia 1.2 utajikuta kwamba haulipii umeme sababu luku yako itakuwa inajaa credit au ukizidi matumizi utakuwa unalipia nafuu sababu realistically jua kwenye paa lako litakuwa linakusanywa kwa kukusaidia wewe katika mapishi yako....
 
Kutumia panel DC kwa ajili ya kupikia ni kujidangaya haiwezekani ufanye hivyo directly vifaa vingi ni AC na Wattage ni kubwa na kutoa kwenye panels, kupeleka kwenye battery alafu kubadilisha tena kuwa AC alafu upikie utakuwa wendawazimu...., Kwahio process ipo vipi angalia.....

Tanesco na umeme wake ndio unapelekwa kwa wadau ili waweze kupikia unless unasema kwamba umeme kwa Tanzania hauwezi ukawa Nishati safi na salama na practical na hapo tunaweza tuka-argue katika uzi huu kwa kujiuliza ni Nishati gani Safi na Nafuu....

Sasa kama tutakubaliana kwamba umeme ni Nishati Safi kwa kupikia point ya huu uzi ni kuongeza uzalishaji wa umeme...., wewe na hizo panel zako kwenye paa lako ukizalisha umeme hauhitaji hizo battery zako (bei ya battery na maintenance unaweza kuongezea panels nyingine nyingi zaidi) sasa kama kwako unatumia units 1.2 - 3.3 kwa siku kwa kupikia paa lako kama linazalisha units kama hizo au zaidi badala ya kuzitunza au kuzitumia smart meter inazipeleka moja kwa moja kwenye grid wewe unaendelea kutumia iwapo utakuwa unazalisha units 3.3 lakini unatumia 1.2 utajikuta kwamba haulipii umeme sababu luku yako itakuwa inajaa credit au ukizidi matumizi utakuwa unalipia nafuu sababu realistically jua kwenye paa lako litakuwa linakusanywa kwa kukusaidia wewe katika mapishi yako....
Sina la kusema.
Kutumia panel DC kwa ajili ya kupikia ni kujidangaya haiwezekani ufanye hivyo directly vifaa vingi ni AC na Wattage ni kubwa na kutoa kwenye panels, kupeleka kwenye battery alafu kubadilisha tena kuwa AC alafu upikie utakuwa wendawazimu...., Kwahio process ipo vipi angalia.....

Tanesco na umeme wake ndio unapelekwa kwa wadau ili waweze kupikia unless unasema kwamba umeme kwa Tanzania hauwezi ukawa Nishati safi na salama na practical na hapo tunaweza tuka-argue katika uzi huu kwa kujiuliza ni Nishati gani Safi na Nafuu....

Sasa kama tutakubaliana kwamba umeme ni Nishati Safi kwa kupikia point ya huu uzi ni kuongeza uzalishaji wa umeme...., wewe na hizo panel zako kwenye paa lako ukizalisha umeme hauhitaji hizo battery zako (bei ya battery na maintenance unaweza kuongezea panels nyingine nyingi zaidi) sasa kama kwako unatumia units 1.2 - 3.3 kwa siku kwa kupikia paa lako kama linazalisha units kama hizo au zaidi badala ya kuzitunza au kuzitumia smart meter inazipeleka moja kwa moja kwenye grid wewe unaendelea kutumia iwapo utakuwa unazalisha units 3.3 lakini unatumia 1.2 utajikuta kwamba haulipii umeme sababu luku yako itakuwa inajaa credit au ukizidi matumizi utakuwa unalipia nafuu sababu realistically jua kwenye paa lako litakuwa linakusanywa kwa kukusaidia wewe katika mapishi yako....
"Kutumia panel DC kwa ajili ya kupikia ni kujidangaya haiwezekani ufanye hivyo", No comment.
Kutumia panel DC kwa ajili ya kupikia ni kujidangaya haiwezekani ufanye hivyo directly vifaa vingi ni AC na Wattage ni kubwa na kutoa kwenye panels, kupeleka kwenye battery alafu kubadilisha tena kuwa AC alafu upikie utakuwa wendawazimu...., Kwahio process ipo vipi angalia.....

Tanesco na umeme wake ndio unapelekwa kwa wadau ili waweze kupikia unless unasema kwamba umeme kwa Tanzania hauwezi ukawa Nishati safi na salama na practical na hapo tunaweza tuka-argue katika uzi huu kwa kujiuliza ni Nishati gani Safi na Nafuu....

Sasa kama tutakubaliana kwamba umeme ni Nishati Safi kwa kupikia point ya huu uzi ni kuongeza uzalishaji wa umeme...., wewe na hizo panel zako kwenye paa lako ukizalisha umeme hauhitaji hizo battery zako (bei ya battery na maintenance unaweza kuongezea panels nyingine nyingi zaidi) sasa kama kwako unatumia units 1.2 - 3.3 kwa siku kwa kupikia paa lako kama linazalisha units kama hizo au zaidi badala ya kuzitunza au kuzitumia smart meter inazipeleka moja kwa moja kwenye grid wewe unaendelea kutumia iwapo utakuwa unazalisha units 3.3 lakini unatumia 1.2 utajikuta kwamba haulipii umeme sababu luku yako itakuwa inajaa credit au ukizidi matumizi utakuwa unalipia nafuu sababu realistically jua kwenye paa lako litakuwa linakusanywa kwa kukusaidia wewe katika mapishi yako....
Mbona zipo 12vdc rice cooker za solar na gari, kwahiyo watengenezaji hawajui walichokitengeneza!
 
Sina la kusema.

"Kutumia panel DC kwa ajili ya kupikia ni kujidangaya haiwezekani ufanye hivyo", No comment.

Mbona zipo 12vdc rice cooker za solar na gari, kwahiyo watengenezaji hawajui walichokitengeneza!
Ofcourse hata pasi za DC au kila kifaa kinaweza kuwa converted na kufanya kazi directly from DC ila kuna vyombo vingapi watu wanavyo vya DC na je watakuwa na DC kuanzia Induction, mpaka Microwave, electronics nyingi ni DC na ni efficient kutumia DC hata kwenye AC ni kwamba huwa zinakuwa converted back to DC.... (Simu, TV n.k.) ndio maana zinakuwa na adaptor...

Kwahio kwa ufanisi wa kutumia panels ni kwanza iende directly to Grid alafu mtu aweze kutumia majiko yake ambayo ndio mengi AC
 
Ofcourse hata pasi za DC au kila kifaa kinaweza kuwa converted na kufanya kazi directly from DC ila kuna vyombo vingapi watu wanavyo vya DC na je watakuwa na DC kuanzia Induction, mpaka Microwave, electronics nyingi ni DC na ni efficient kutumia DC hata kwenye AC ni kwamba huwa zinakuwa converted back to DC....

Kwahio kwa ufanisi wa kutumia panels ni kwanza iende directly to Grid alafu mtu aweze kutumia majiko yake ambayo ndio mengi AC
Caravan au garinyumba zinavifaa vya kupikia vya voti 12dc na vinafanyakazi kwa ufanisi na hiyo ya sola nayo ni voti 12 japo paneli ni zaidi ya Voti 12 ili iweze kuchaji betri na hauwezi kuunganisha chombo bila kupitia betri.
 
Na hii kwako wewe unaona ni efficient kuliko mtu kuwa na panels kwenye Paa lake na bila kufanya lolote ?, Na undhani hii inaweza ikawa replicated kwa kila kaya ?

Watu ni wavivu na hawataki kufanya lolote ndio maana watu kama magereza na mashule ambao wanazalisha kilo za kutosha za kinyesi hawajaamia kwenye hizi Biogas..., Na kwa ushauri wangu kama tungekuwa hatuna vyanzo vingine rahisi ningeshauri kuwepo na bio-digester za kuchukua uchafu wa miji na kutengeneza methane ili kuchemshia maji / boiler na na kupata umeme kuunganisha kwenye Grid...., In Tanzania hatuwezi ku-beat umeme kutokana na advantage kwamba infrastructure yake imesambaa kuliko nishati nyingine yoyote....
Umeme is the best alternative, lakini Asilimia kubwa ya Kaya vijijini hamna umeme, wanasiasa wanadanya kuwa karibia vijiji vyote vina umeme lakini ni uongo mtu. Tanzania bado hatuna ujanja wa kukwepa kuni kama chanzo cha nishati namba moja, ikifuatiwa na mkaa.
 
Umeme is the best alternative, lakini Asilimia kubwa ya Kaya vijijini hamna umeme, wanasiasa wanadanya kuwa karibia vijiji vyote vina umeme lakini ni uongo mtu. Tanzania bado hatuna ujanja wa kukwepa kuni kama chanzo cha nishati namba moja, ikifuatiwa na mkaa.
Naam badala ya kutumia pesa zetu kujaribu kupelekea watu mitungi ya gesi au kufanya maigizo ya kuwapa mitungi hio ni vema nguvu hizo zikatumika kuwauganisha na umeme hawa ndugu zetu wa vijijini....
 
Caravan au garinyumba zinavifaa vya kupikia vya voti 12dc na vinafanyakazi kwa ufanisi na hiyo ya sola nayo ni voti 12 japo paneli ni zaidi ya Voti 12 ili iweze kuchaji betri na hauwezi kuunganisha chombo bila kupitia betri.
Chombo chochote unaweza kupata za DC ila sababu majority wameungwa kwenye grid vyombo vingi vya umeme ni AC..., na kwenye gari pia kuna advatange ukiwa kwenye mwendo ile nishati ya uendeshaji inachaji battery pia...., mimi hapa kwenye suggestion yangu tuachane kabisa na issue za battery yaani ondoa battery kwenye equation (money saved) na kila umeme unaozalisha peleka kwenye grid wewe tumia umeme wa from grid wakati wowote, ule uliozalisha ni kama umewekeza benki
 
Nimesikia Serikali na Wizara ya Nishati inajiweka sawa ili kuongeza miundombinu ya kuweza kupokea gesi nyingi zaidi (yaani kuagiza) kweli nimesikitika sana..., Hii ni kuonyesha kwamba tumeamua kwenda njia ya Propane gesi (gesi ya kuagiza)
 
Back
Top Bottom