Southern Highland
JF-Expert Member
- Mar 22, 2017
- 13,434
- 21,988
Me sree zem one
Me sree zem one
Katika hivyo vipengele, Jeshi la polisi ni suala la muungano babu,Muungano una vipengele babu,1964 vilikua 11,Leo vimefika 20+, muungano si kwenye kila kitu
Kule Kuna valantia,kmkm,sheha ana watu wake,jiridhishe kwanza kipi ni kipiKatika hivyo vipengele, Jeshi la polisi ni suala la muungano babu,
Wanawajibika kwenye sheria za muungano...
Jeshi la polisi ndilo lililo kamata watu,Kule Kuna valantia,kmkm,sheha ana watu wake,jiridhishe kwanza kipi ni kipi
Katiba inazuwia Hilo la Zanzibar kukamata watu wanokula mchana wa Ramadan hadharani?..maana hili Jambo la zamaniJeshi la polisi ndilo lililo kamata watu,
Fuatilia kwenye vyombo vya habari, check Ayo TV
Kwanza ni kujua aina ya wanaolalamika na uwezo wao kiuchumi. Hii itakuwa rahisi kuwapa location kadili ya ukubwa wa mfuko wao.Wape location maana waliopo bara ndio wana wasiwasi wakati wenzao wanaishi huko miaka kibao ..wanafanya shughuli zao kidini daily
Nilishakaa Zanzibar mda wa miezi mi3,ikiwemo na Ramadhani...Cha ajabu watalii hawaguswi, siyo kwa mavazi ama kula...Katiba inazuwia Hilo la Zanzibar kukamata watu wanokula mchana wa Ramadan hadharani?..maana hili Jambo la zamani
KAtiba ya Jamhuri ya Muungano ila zanzibar Ina Katiba yake pia Mkuu..Huyu naye mweupe kichwani hajui mambo ya muungano
Polisi Zanzibar wamevunja katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Polisi ni jeshi la muungano wa Tanzania na linaongozwa na kusimamiwa ba katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwenye kazi zao.Katiba ya muungamo inatamka wazi. Kuwa mambo ya dini yatakuwa nje ya mambo ya serikali. Hao waliokamatwa wakila hadharani mwezi wa Ramadhani hawajavunja katiba yeyote kipengele chochote cha katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania
Polisi Zanzibar ambao ni jeshi linalosimamiwa na katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ndio wamevunja katiba na PGO ya polisi.
Wanatakiwa hao Polisi waburuzwe mahakamani kwa kuvunja katiba ya Jamhuri ya muungano ya Tanzania ambayo ndio wanatakiwa kuisimamia na ambayo ndimo jeshi hilo liko chini yake ya wizara ya mambo ya ndani ya muungano
Wamevunja katiba ya Jamhuri ya muungano hao Polisi.Wamewakamata hao watu kinyume cha katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania wawaachie
Polisi hawakuwa na mamlaka ya kuwakamata wala kuwashikilia wala kueafungulia mashtaka ya kula urojo hadharani au kutafuna big ji hadharani
Hawana nguvu hiyo kwa katiba ya Jamhuri ya muungano iliyowapa huo upolisi
Nahisi wageni ndio wanapata tabu ila mliokaa huko fresh tu, jamaa yangu ni mlevi kafanya kazi hotelini miaka 2 .Kwanza ni kujua aina ya wanaolalamika na uwezo wao kiuchumi. Hii itakuwa rahisi kuwapa location kadili ya ukubwa wa mfuko wao.
Aidha kwa haraka haraka, kama ulikuwa unakula kwa Mama Lishe kabla ya mfungo, ni Mama huyo huyo ambaye hutoa location kwa wateja wake ni wapi atapatika wakati wa mfungo.
Kwa wanywaji, Baa zinazokuwa wazi zinajulikana na zaidi unaweza kupata msosi kama kawaida. Hivyo hili sio tatizo kwao.
Kwa wageni, unapofika bandarini au airport ulizia kwa bodaboda, taxi driver na Bajaj... Hapa hapana guarantee ya kupelekwa sehemu salama.
Zaidi kambi zote za Jeshi zenye Officers Mess wanakuwa wazi, baadhi ya Baa zilizo chini ya CCM, Hotel za kitalii n.k
Kubwa zaidi ni ukubwa wa mfuko wako na Cha muhimu kabisa ni kiheshimu waliofunga.
Namuunga mkono kwenye upande wa kutembea na mke wa mtu lakini sikubaliani naye kwenye hoja ya kosa la kula hadharani, hapo amekosea kwa sababu masuala ya dini na urndeshaji wake hayapaswi kuingiliwa na Serikali kwa mujibu wa Katiba ya muungano, kitendo cha serikali kutunga sheria ndogo za kuzuia watu wasile hadharani wakati wa Ramadan ni kwamba serikali imejiingiza kwenye dini
Uislam haukatazi mtu kula mchana wa Ramadan, Qur'an inatambua Kuna wenye udhuru wa kufunga(wasafiri na wagonjwa),lakini pia QUR'AN imeweka wazi kuwa funga ni Kwa 'walioamini'..mi muislam Ila huwa sielewi huo msimamo wa ZanzibarNilishakaa Zanzibar mda wa miezi mi3,ikiwemo na Ramadhani...Cha ajabu watalii hawaguswi, siyo kwa mavazi ama kula...
Nilijihisi mfungwa, yani shida kunywa maji,chakula mpaka mtu ukale kwenye mgahawa ya kujificha....
Hata kama havikuwepo katiba ni kitu kinachobadilika kuendana na wakati lakini kikiridhiwa na pande zote za muungano na baraza la wawakilishi na bunge shida iko wapi kama viliridhiwa na baraza la wawakilishi kwenye mabadiliko ya katiba?Wizara ya mambo ya ndani ilikuwepo kwenye vile vipengele 11 vya muungano alivyosaini karume,au mliingiza kwa Hila baadae?
Viridhiwe wapi!!..Hata kama havikuwepo katiba ni kitu kinachobadilika kuendana na wakati lakini kikiridhiwa na pande zote za muungano na baraza la wawakilishi na bunge shida iko wapi kama viliridhiwa na baraza la wawakilishi kwenye mabadiliko ya katiba?
Yawe ya katiba ya muungano au ya Zanzibar hakuna shida
So kula pilau tujifungie ndani?Katazo la kusherehekea Pasaka halijawah kuwepo Zanzibar
Wana katiba ya Zanzibar pia na PGO ya zanzibar piaHuyu mama anaota hasomi katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wala kujua kazi za polisi kwa mktadha wa katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ambalo ni chombo cha muungano wa jamhuri ya muungano wa Tanzania na PGO yao ya Polisi kama chombo cha muungano na kazi zao kitendo cha polisi kukamata hao wala mchana hakiko sahihi kikatiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania
Kuna Katiba ya zanzibar piaNamuunga mkono kwenye upande wa kutembea na mke wa mtu lakini sikubaliani naye kwenye hoja ya kosa la kula hadharani, hapo amekosea kwa sababu masuala ya dini na urndeshaji wake hayapaswi kuingiliwa na Serikali kwa mujibu wa Katiba ya muungano, kitendo cha serikali kutunga sheria ndogo za kuzuia watu wasile hadharani wakati wa Ramadan ni kwamba serikali imejiingiza kwenye dini