Cute Wife

Senior Member
Nov 17, 2023
124
306
ummy.jpeg

Kufuatia mapitio ya orodha ya Taifa ya Dawa Muhimu (National Essential Medicine List -NEMLIT) yaliyofanywa na Wizara ya Afya Aprili 30, 2024 kwa kujumuisha muunganiko,muundo na nguvu kwa dawa 178 pamoja na kujumuisha dawa nne zilizokuwepo kwenye Mwongozo wa Taifa wa Matibabu lakini hazikuwemo kwenye NEMLIT na hatimaye kusaini nyongeza (addendum), Mfuko wa Bima ya Afya wa Taifa umejumuisha dawa hizo katika Kitita chake cha Mafao cha Mwaka 2023.

Hatua hii inaongeza wigo wa upatikanaji wa dawa kwa wanachama kwa kuzingatia miongozo ya tiba nchini. Kutokana na maboresho hayo, fuko wa Taifa Bima ya Afya unawahakikishia wanachama wake kuwa huduma za matibabu zitaendelea kupatikana katika vituo vyote vilivyosajiliwa nchi nzima.

Endapo kutakuwa na changamoto za kiutekelezaji Mfuko unashauri vituo vya kutoa huduma viasiliane na ofisi za Mfuko kuepuka usumbufu usio wa lazima kwa wateja wao.

Kwa nyongeza, iwapo mwanachama atakutana na changamoto yoyote katika upatikanaji wa huduma tafadhali asisite kuwasiliana na Mfuko kupitia Kituo cha Huduma kwa Wateja kwa kupiga simu bila malipo namba 199.

1715243098257.png

Pia soma: 'Dawa 178 na Vifaa Tiba 15 vilivyoondolewa kwenye Kitita kipya cha NHIF'
 
Kwanini walizitoa,
Kwanini wamerudisha?

Waliothirika na wao kuziondoa watawalipa nini?
 
Baada ya Malalamiko Yaliyodumu kwa Miezi kadhaa na Kufikia Hatua baadhi ya Hospitali Binafsi kususia ama kuzuia Matumizi ya Bima hiyo hatimaye Leo Dawa 178 Zimerudishwa Tena kwenye Kitita Hicho kama ilivyokuwa zamani..

Nawashukuru Wananchi wote wanaoendelea Kupiga Kelele wanapoona Jambo halijaenda sawa Na nashukuru Pia Wote walioguswa na Uboreshwaji wa Bima hii kwa Namna Nzuri Mbaya...
Nawapongeza sawa JF Kuwa Ni miongoni mwa wanaochochea maendeleo..

Naamini Wizara ya Afya Tanzania Itaendelea kuboresha Miundo mbinu ili iwe Rafiki kwa Wadau na watumiaji Shukrani...
Screenshot_20240509_114637_X.jpg


20240509_114707.jpg


20240509_114640.jpg

20240509_114643.jpg

20240509_114646.jpg
20240509_114646.jpg

20240509_114648.jpg
 
Baada ya Malalamiko Yaliyodumu kwa Miezi kadhaa na Kufikia Hatua baadhi ya Hospitali Binafsi kususia ama kuzuia Matumizi ya Bima hiyo hatimaye Leo Dawa 178 Zimerudishwa Tena kwenye Kitita Hicho kama ilivyokuwa zamani..

Nawashukuru Wananchi wote wanaoendelea Kupiga Kelele wanapoona Jambo halijaenda sawa Na nashukuru Pia Wote walioguswa na Uboreshwaji wa Bima hii kwa Namna Nzuri Mbaya...
Nawapongeza sawa JF Kuwa Ni miongoni mwa wanaochochea maendeleo..

Naamini Wizara ya Afya Tanzania Itaendelea kuboresha Miundo mbinu ili iwe Rafiki kwa Wadau na watumiaji Shukrani...
View attachment 2985481

View attachment 2985487

View attachment 2985480
View attachment 2985482
View attachment 2985483View attachment 2985483
View attachment 2985484
Issue ni kwamba zimerudishwa kwenye makaratasi je hospilini zipo? Kwa sababu Hospital zote za serikali ngazi ya msingi mpaka taifa kila kitu unaambiwa kanunue dukani.
 
Mbinu ya CCM ni ileile.

Tengeneza tatizo na taharuki kwenye jamii, kisha litatue uonekane unaupiga mwingi.Jirekebisheni

Ombi langu kwa serikali sikivu ya CCM. Ruhusini na toeni vibali kwenye njia ya mjini mpaka kimara hadi mbezi daladala zirudi zianze kupiga kazi. Mwendo kasi imefeli pakubwa inahitaji ushindani ili iboreshe huduma. Wananchi wanateseka.

Naomba sana hili ili nipate kura za udiwani 2025 la sivyo wananchi hawatanielewa.
 
Back
Top Bottom