SOFTWARE Nauza mfumo utakaokusaidia kutunza kumbukumbu za mauzo na manunuzi hata kama upo mbali na biashara yako

MASTERCHIEF 255

JF-Expert Member
Sep 26, 2014
468
917
FedhaBook: Mfumo wa kusimamia hesabu za biashara yako hata kama upo mbali na biashara yako
2dashboard.png

Okoa muda na kujichosha kupiga mahesabu kwa kichwa na kalamu na daftari na uutumie muda huo kufanya mambo mengine binafsi na ya kimaendelea au ya kifamilia

Ni mambo gani unaweza kuyafanya ukiwa na mfumo wa fedhabook hata kama ni mjasiriamali mdogo.
3POS.png

1.Utatunza kumbukumbu zote za manunuzi ya bidhaa zako

2. Msimamizi wako uliyemuweka atatunza taarifa zote za mauzo aliyofanya siku husika
4stockreport.png

3.Kama unafanya biashara kwa bei za jumla na rejareja pia mfumo utakuruhusu kufanya hivyo

4.Utatunza gharama zingine zote za kimatumizi ndani ya biashara yako kama vile umeme, pango, kodi, usafiri n.k
6profitandloss.png

5.Utaweza ku control matumizi ya mfumo kulingana na majukumu unayomkabidhi mtu.
kama ni mtu wa mauzo basi kwenye system ataona sehemu ya mauzo tu na sio mambo mengine

6.Utaweza kuprint risiti ikiwa utahitaji mfumo ufanye hivyo

7.System yenyewe sasa itakusaidia kuchakata taarifa zako na kukuonesha faida uliyoingiza kwa siku, wiki, mwezi n.k

8.System utakuonesha bidhaa zilizobaki, bidhaa zinazoelekea ku expire, na bidhaa zilizoisha kabisa.

9.System itakuonesha bidhaa ipi inakuletea faida zaidi ya bidhaa nyingine.

10.System itakuwezesha kusimamia biashara zaidi ya moja na hata kama utahitaji kuhamisha biadhaa kutoka ofisi moja kwenda nyingine itawezekana ndani ya system.

11.Kwakuwa system ni ya online huhitaji kutembelea ofisi zako kwa ajili ya mahesabu.Utaweza kujua kila kinachoendelea katika biashara yako popote utakapokuwa katika dunia hii.

Mfumo huu utaweza kuupata kwa gharama ya Tsh 150,000 tu.
 
Good initiative mkuu, hongera kwa kazi nzuri.

Haya jamani tuje kumuunga mkono mdau amefanya jitihada za kuja na mfumo rahisi kwa ajili ya kumanage business.

Mara kadhaa humu tumekuwa tukiwananga wasomi wetu kuwa hawawezi kutatua changamoto kwa kutumia elimu zao, bila shaka hii ni moja ya namna ya kuitikia zile critics
 
Good initiative mkuu, hongera kwa kazi nzuri.

Haya jamani tuje kumuunga mkono mdau amefanya jitihada za kuja na mfumo rahisi kwa ajili ya kumanage business.

Mara kadhaa humu tumekuwa tukiwananga wasomi wetu kuwa hawawezi kutatua changamoto kwa kutumia elimu zao, bila shaka hii ni moja ya namna ya kuitikia zile critics
shukran sana
 
Iwapo nina bidhaa nyingi mfumo utaniwezesha kuziongeza (add) na vipi kuhusu review ya mfumo itafanyikaje (nitakutana physically na wewe au itakuwaje). Natanguliza Shukrani.
kama upo dar es salaam tunaweza onana...

ila kuna demo site ipo active online
kama upo interested tunawaasiliana nakupa hiyo link ya demo site unaingia mwenyewe na kujionea inavyofanya kazi
 
kama upo dar es salaam tunaweza onana...

ila kuna demo site ipo active online
kama upo interested tunawaasiliana nakupa hiyo link ya demo site unaingia mwenyewe na kujionea inavyofanya kazi
Mimi sipo Dar, nipo mikoani (nimekuelewa). Vipi kuhusu review inakuwaje?
 
Ongera sana ila kwanini ungetuma mfumo hata kwa laki kisha kuwe na kulipia mfumo kwa mwaka ada iwe hata elfu hamsini kuliko kila mwaka kulipa 150,000?
 
kama upo dar es salaam tunaweza onana...

ila kuna demo site ipo active online
kama upo interested tunawaasiliana nakupa hiyo link ya demo site unaingia mwenyewe na kujionea inavyofanya kazi
Kwa kuwa mimi ni mfanyabiashara Mfumo huo nimeupenda ila nataka kujiridhisha na baadhi ya features ninazotamani ziwepo au nije niziongeze baadaye. Kwa kuanzia utatusaidia wengi.
 
Ongera sana ila kwanini ungetuma mfumo hata kwa laki kisha kuwe na kulipia mfumo kwa mwaka ada iwe hata elfu hamsini kuliko kila mwaka kulipa 150,000?
Kutokana na faida anazozipata mmiliki wa biashara kuanzia kutunza muda, usahihi wa hesabu na utunzaji wa kumbukumbu za biashara ...

Bei ya 150,000 ni nzuri tu kwa system kama hii ya biashara
 
Back
Top Bottom