Nashauri mikopo ya elimu ya juu ifutwe, mbona wenzao wa diploma wanasoma bila mkopo iweje wao?

Sina mood

JF-Expert Member
Nov 15, 2018
229
1,388
Nashauri hii mikopo ya elimu ya juu ifutwe, mbona wanachuo wenzao wa diploma wanasoma bila mkopo na hatusikii kelele zozote?

Tofauti yao na wenzao wa diploma ipo wapi?

Nimeona Serikali inataka kuwapa mikopo na hawa diploma, hili nalo litakuwa kosa kubwa sana, yaani kujibebesha mzigo juu ya mzigo, cha muhimu hapo Serikali wapige kimya tu na huko kwa ngazi ya degree wawafutie kabisa kama ikibidi labda wawape ada tu, pesa ya kula wajitegemee.
 
Nashauri hii mikopo ya elimu ya juu ifutwe,mbona wanachuo wenzao wa diploma wanasoma bila mkopo na hatusikii kelele zozote?

Tofauti yao na wenzao wa diploma ipo wapi?

Nimeamka serikali unataka kuwapa mikopo na hawa diploma,, hili nalo litakuwa kosa kubwa sana, yani kujibebesha mzigo juu ya mzigo ,,, cha muhimu hapo serikali wapige kimya tu na huko kwa ngazi ya degree wawafutie kabisa kama ikibidi labda wawape ada tu ,pesa ya kula wajitegemee.
NB.
Tanzania sio dar es salamaa pekee Kuna Kaya maskini huko mikoani kiasi hawawezi kugharamia masomo hata kula yao ya siku
 
Ungejua msoto wanaopitia vijana wa diploma na certificate wanaotoka familia duni hata usingesema.
Wapo wanaoacha wengi kwa kukosa ada au wengine nauli.

Tena angalau vyo vya kati vinavyokua na mabweni kisha wanafunzi wanapewa chakula
hakuna kitu kama hicho
 
HIyo serikali isipopoteza hela kuwakopesha wasoma diploma pesa hizo zitapotelea tu kwenye mifuko ya watu binafsi.
Ikiwezekana wanafunzi wakopeshe tangu primary schools pesa ipo
wawakopeshe wanafunzi pesa wakati hata dawa hospitalini hakuna, vifaa tiba hakuna, barabara mbovu
 
Back
Top Bottom