Nape Nnauye: Nashangaa Watanzania wanaokwenda kusikiliza upuuzi wa Lissu. Tumkemee, tumtenge na tumlaani

Heparin

Senior Member
Sep 24, 2021
152
571
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Tanzania, Nape Nnauye amelaani vikali kauli iliyotolewa na Makamu mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu kuhusu madai ya Rais Samia kuwaondoa Wamasai wa Ngorongoro kisa yeye ni Mzanzibari.

Waziri Nape amesema kauli hii inapaswa kupingwa na kila mwenye akili timamu kwani ni hoja za watu waliofilisika kisiasa.

"Watanzania tusikubali upuuzi huu, na mimi nitawashangaa watanzania waliozaliwa wakati wa Muungano hata wanaokwenda kumsikiliza mpuuzi huyu, tumkemee, tumtenge, tumlaani" amesema Nape.

Amebainisha ikiwa watanzania wataendelea kuangalia vitendo hivi vya ukosoaji kwa Rais kwa kutumia jinsia, kabila au sehemu anakotoka watakuwa hawaitendei haki nchi.


Ameongeza, "Ni Rais huyu ndiye amesema andamaneni, polisi kawalindeni, na leo walikuwa wanaandamana hapa. Wamelindwa na Polisi, wamesindikizwa walipoenda, wamesababisha foleni dodoma hapa, magari yamesimamishwa ili wao waandamane, kwa uungwana wa huyu mama anayemtukana"
Pia soma:
 
Kwa hakika Lissu anapaswa kutengwa na kulaaniwa sana na kukemewa kwa nguvu zote na watanzania wote wenye mapenzi mema na Taifa letu, kwa kuendekeza tabia yake ya kutoa maneno yenye kuchochea ubaguzi.

Mdomo wa Lissu haunaga adabu wala staha wala hekima.anazungumzaga vitu visivyoendana na umri wake ni mtu wa kuropoka ropoka tu utafikiri mgonjwa.

Anashindwa kujenga hoja akaeleweka badala yake anakimbilia kujenga chuki na ubaguzi tu wa kijinga jinga .akifikiri ndio njia ya kupata kura za wananchi.
 
Kwani Lissu kasema jambo gani ambalo Nape halijui??!!?? Kwa taarifa kwa Nape Lissu katoa ufafanuzi leo Dodoma kwa yale aliyoyasema kule Babati na ambayo yamemkera Nape.

Ukweli tunaujua Nape anaweweseka tu.

Nape amezoea kusema uongo ndiyo tabia yake. Wale walioiba uchaguzi wote wa mwaka 2020 mbona hatukuwatenga?

Tanganyika ipo tu hata Nape akiweweseka.
 
Samia kawa Rais kwa mujibu wa katiba na katiba hiyo hiyo ndio inawapa CHADEMA haki ya kuandamana na kulindwa na Polisi tunaowalipa mishahara kwa kodi zetu.

Nape asifikiri kwakuwa cheo alichonacho ni kwa hisani ya Rais, basi na haki za kikatiba tulizonazo nazo ni kwa hisani ya Rais.
 
Kwa hakika Lissu anapaswa kutengwa na kulaaniwa sana na kukemewa kwa nguvu zote na watanzania wote wenye mapenzi mema na Taifa letu...
Mimi ni kati ya watu ambao hawapendi mada za Lissu hasa pale anapoongea na kutumia matusi hata ya nguoni.

Kuachana na matusi yake, hata huyo Nnauye naye siyo msafi maana huutumia mdomo wake mchafu kutukana.

Ila pia lazima tukubali kuwa Wamasai wasilazimishwe kuhama Ngorongoro.

Ukweli ni kuwa utafika wakati watahama. Sasa hivi Tanzania kuna makabila mawili ambayo yametapakaa Tanzania nzima wakichunga ng'ombe, nayo ni Wamasai na Wasukuma.

Siku hizi Wasukuma na Wamasai wako mikoa yote ya Tanzania wakichunga ng'ombe. Hata Zanzibar na Pemba wamasai wamejaa. Hawa wa visiwani ni walinzi na wauza madawa ya kienyeji!
 
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia wa Habari wa Tanzania, Nape Nnauye amelaani vikali kauli iliyotolewa na Makamu mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu kuhusu madai ya Rais Samia kuwaondoa Wamasai wa Ngorongoro kisa yeye ni Mzanzibari.

Waziri Nape amesema kauli hii inapaswa kupingwa na kila mwenye akili timamu kwani ni hoja za watu waliofilisika kisiasa.

"Watanzania tusikubali upuuzi huu, na mimi nitawashangaa watanzania waliozaliwa wakati wa Muungano hata wanaokwenda kumsikiliza mpuuzi huyu, tumkemee, tumtenge, tumlaani" amesema Nape.

Amebainisha ikiwa watanzania wataendelea kuangalia vitendo hivi kwa ukosoaji kwa Rais kwa kutumia jinsia, kabila au sehemu anakotoka watakuwa hawaitendei haki nchi.

Ameongeza, "Ni Rais huyu ndiye amesema andamaneni, polisi kawalindeni, na leo walikuwa wanaandamana hapa. Wamelindwa na Polisi, wamesindikizwa walipoenda, wamesababisha foleni dodoma hapa, magari yamesimamishwa ili wao waandamane, kwa uungwana wa huyu mama anayemtukana"


View: https://www.youtube.com/live/2FZwDIHGIYE?si=sJH-YKoIJDyvB8rQ

KUMBE wanamfatilia mwamba LISSU wewe nyapu LISSU sio size Yako wewe bishana na kina makonda na kina zuchu
 
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia wa Habari wa Tanzania, Nape Nnauye amelaani vikali kauli iliyotolewa na Makamu mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu kuhusu madai ya Rais Samia kuwaondoa Wamasai wa Ngorongoro kisa yeye ni Mzanzibari.

Waziri Nape amesema kauli hii inapaswa kupingwa na kila mwenye akili timamu kwani ni hoja za watu waliofilisika kisiasa.

"Watanzania tusikubali upuuzi huu, na mimi nitawashangaa watanzania waliozaliwa wakati wa Muungano hata wanaokwenda kumsikiliza mpuuzi huyu, tumkemee, tumtenge, tumlaani" amesema Nape.

Amebainisha ikiwa watanzania wataendelea kuangalia vitendo hivi kwa ukosoaji kwa Rais kwa kutumia jinsia, kabila au sehemu anakotoka watakuwa hawaitendei haki nchi.

Ameongeza, "Ni Rais huyu ndiye amesema andamaneni, polisi kawalindeni, na leo walikuwa wanaandamana hapa. Wamelindwa na Polisi, wamesindikizwa walipoenda, wamesababisha foleni dodoma hapa, magari yamesimamishwa ili wao waandamane, kwa uungwana wa huyu mama anayemtukana"


View: https://www.youtube.com/live/2FZwDIHGIYE?si=sJH-YKoIJDyvB8rQ

Lissu anazungumza ukweli, sio matusi.
 
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia wa Habari wa Tanzania, Nape Nnauye amelaani vikali kauli iliyotolewa na Makamu mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu kuhusu madai ya Rais Samia kuwaondoa Wamasai wa Ngorongoro kisa yeye ni Mzanzibari.

Waziri Nape amesema kauli hii inapaswa kupingwa na kila mwenye akili timamu kwani ni hoja za watu waliofilisika kisiasa.

"Watanzania tusikubali upuuzi huu, na mimi nitawashangaa watanzania waliozaliwa wakati wa Muungano hata wanaokwenda kumsikiliza mpuuzi huyu, tumkemee, tumtenge, tumlaani" amesema Nape.

Amebainisha ikiwa watanzania wataendelea kuangalia vitendo hivi kwa ukosoaji kwa Rais kwa kutumia jinsia, kabila au sehemu anakotoka watakuwa hawaitendei haki nchi.

Ameongeza, "Ni Rais huyu ndiye amesema andamaneni, polisi kawalindeni, na leo walikuwa wanaandamana hapa. Wamelindwa na Polisi, wamesindikizwa walipoenda, wamesababisha foleni dodoma hapa, magari yamesimamishwa ili wao waandamane, kwa uungwana wa huyu mama anayemtukana"


View: https://www.youtube.com/live/2FZwDIHGIYE?si=sJH-YKoIJDyvB8rQ

Samahani! Hivi Tundulisu na Nape ni Nani ana akili?
 
Back
Top Bottom