Naomba Ushauri: Rafiki yangu alinidharau na kuniambia nanuka sasa ananiomba msamaha na anamtaka mume wangu

Mimi ni mama wa watoto 3 na nimeolewa; ndoa yangu ina miaka 7 sasa. Mimi na mume wangu tulikuwa vizuri, lakini mwaka jana, kuna rafiki yangu mmoja alifiwa mume wake nilimsaidia kwa kumchukua tukaanza kuishi naye. Kila kitu kilikuwa vizuri ila katikati ya mwaka jana nikaona kama mambo yanabadilika; akawa bize sana na mume wangu na akaanza kunionyeshea dharau.

Wakati huo, mimi nilikuwa nahangaika kumtafutia kazi maana alikuwa akiishi kwangu kwani ni yule ambaye alimaliza chuo tukiwa tumeolewa na mambo ya kazi yalikuwa bado. Nilibahatika nikamuunganisha kwenye benki moja akafanyiwa usahili na kweli aliipata hiyo kazi.

Baada ya kupata kazi mwaka jana mwisho, nikamuambia sasa anaweza kwenda kupangisha kwake. Mwanzo aligoma, lakini dada yangu ambaye ndiye alinielekeza kwao, akaniambia "ukimsaidia mtu msaidie kwa mbali; umemchukua kwako huu ni mwaka na kazi umemtafutia, hataki kuondoka? Hapana, kuna kitu!"

Nikaanza kama kumshuku, nikaja kugundua kuwa ana mahusiano na mume wangu. Nilimuuliza, akanitukana sana akiniambia mambo yangu ya ndani. Mume wangu alikuwa anamwambia rafiki yangu siri zangu, kama vile nanuka, nina vitu gani. Ni kweli mimi nina shida flani, ya kutoa jasho kali sehemu za siri; si kunuka, lakini natoka jasho jingi hivyo kuna wakati naloana kama nimejikojolea.

Ni siri ambayo ni mume wangu tu anajua, lakini alimwambia rafiki yangu naye akanitajia ili kuniumiza. Kweli niliumia, nikataka kuondoka na mwanaume akaniambia "ondoka". Lakini mama mkwe wangu aliposikia hicho kitu, akaja na kumtoa huyo dada na kumuambia mume wangu "kama umemchoka huyu mwanamke ondoka, muache akae na wajukuu zangu".

Mume wangu aliondoka na rafiki yangu, hiyo ilikuwa ni mwezi wa kwanza mwaka huu. Dada yangu akanileta kwako, nikaanza kukusoma; sijaongea nawe lakini nilipata amani kidogo. Mwezi wa 3, mume wangu alirudi na kuniomba msamaha na kuandaa kikao cha kuomba msamaha, akisema alikosea na ni shetani, hata yeye hajui nini kilitokea. Kweli nilikubali, tukarudiana na sasa hivi tuna amani.

Sababu ya kuja kwako ni hivi, jana rafiki yangu alinipigia simu, analia na kuniomba msamaha. Ananiambia tangu kukua kwake hajawahi kukutana na mwanaume aliyemfanya vizuri mpaka kuridhika kama mume wangu. Inaonekana kakubali kuwa mume wangu ananipenda lakini anaomba nimpe ruhusa mume wangu awe analala naye tu hata kwa wiki mara moja kwani anajua hawezi kupata mwanaume mwingine kama yeye.

Bila aibu ananiambia kuwa ataheshimu ndoa yangu, hatanisumbua lakini anaomba nimruhusu tu mume wangu kwani tangu kuondoka kwake hajamtafuta. Hapokei simu zake na alishaenda kumfuata mpaka kazini akaondolewa na mlinzi. Hivyo anahisi kuchanganyikiwa, kweli nimeona kama ni chizi. Hata mume wangu sijaongea naye kuhusu madai yake. Anadai nisipomruhusu kitakachotokea kake ni juu yangu akam akijidhuri nijue mimi ndiyo sababu, nisaidieni jamani namfanyaje huyu mtu aniache na amani!
Toka lini george aloyce akawa Mama wa watoto wa3.
Tuanzie hapo kwanza..
 
Back
Top Bottom