Nadharia: Jinsi law of magnetics itakavyozuia ajali barabarani

Wakuu habari!

Leo nikiwa barabarani niliona magari mawili yaliyotaka kugongana uso kwa uso ghafla likanijia wazo ambalo limenisukuma kuandika uzi huu namna ya kuzuia ajali kama hizi.

View attachment 2958107
Picha nmetoa mtandaoni

Kikawaida ncha mbili za sumaku zikikutana hukwepana, mfano angalia hapa chini kwenye pichaView attachment 2958106
Sasa ikiwa magari yote yatatengenezwa kwa sumaku kwa mbele ktk mtindo wa ncha mbili zinazofanana yakikutana uso kwa uso yatakwepana (yatasukumana bila kugongana) yaani kama ule mchezo wa kusukumana lakini hapa itakua bila kugusana,

Chukulia mfano semi trailer inakutana uso kwa uso na V8, ili zisigongane zikwepane itahitajika sumaku kubwa sana iwekwe mbele ya gari mfano sumaku yenye ukubwa wa shina la mbuyu kwa kila gari yaani semi na V8, kitu ambacho kitaathiri uzito wa kila gari na balance haitakuwdpo,

Kwa vile chuma laini kikizungushiwa nyaya kwa mtindo wa coil kisha kuunganishwa na umeme huwa kinakua sumaku hii njia itafaa zaidi kutengeneza sumaku yenye nguvu kubwaView attachment 2958127
Zingatia pia ujio wa magari ya umeme.

Chini ntatoa ufafanuzi wa kimahesabu , Nakaribisha maoni kinzani.
Wazo ni zuri na limelenga kuepusha contact zisikutane.

Ok, zitapishana kwa force ambayo ni kali na pia kumbuka itakuwa haijahusisha concsiousness ya drivers, sasa hapo sio kwamba itasababisha madhara makubwa zaidi na ukizingatia nature ya lane za barabara zinawatumiaji wengi zaidi ya hizo machine mbili zitakazopishana?

Na vipi zikiwa katika mstari wa kufuatana je hazitovutana maana hapo gari ya nyuma itakuwa na magnetic na ya mbele itakuwa haina, hivyo chuma itakuwa attracted kwa magnetic.

Na vipi ikikutana na material mengine ya chuma, si ndio itavuta kila chuma kitachokuwa kwa range ya hiyo magnetic field ama hata yenyewe inaweza ikavutwa hapo itategemea na uzito wa chuma?

Hapo solition ni nini mkuu
 
hata JF ni mtandao unaotumia intarnet mkuu, wewe umekariri research mpaka utembee na makaratasi? hata hapa tunafanya research na wewe umechangia bila kujua AHSANTE
Unaweza kuwa sahihi kwa kiasi fulani mkuu, lakini mimi nilitaka uchukuwe initiative zaidi kwa ku-present mada yenye logic zaidi. Yaani unge-fine tune zaidi na kuna na kitu chenye logic baada ya kufanya research isiyohusisha hadhara. Ni kweli, udadisi siyo jambo baya na hata kiswahili tunaambiwa kuuliza siyo ujinga bali ni kutaka kujua, lakini kuna maswali mengine au udadisi unaoweza kufanya watu wakakuelewa kivingine. Pengine huwezi kuamini lakini hata mimi hili jambo nimewahi kuliwaza sana nilipokuwa bado mdogo lakini baada ya kwenda shule nikajikuta naliondoa kwenye mawazo yangu kwa kuwa haliednani na uhalisia.
 
Hii inasound vizuri kichwani lakini kiuhalisia ni impossible na highly impractical. Hata kama hii idea ingekuwa practical, gari inayotembea 80 km/h ikikutana na giant magnet, kutokana na umbali hiyo magnet inaanza kuwa active, kitakachotokea ni way worse than kugongana uso kwa uso.

Solution ya kuzuia ajali za magali barabarani ni kujenga one way roads za kutosha na kuweka kizuizi imara zisikutane kivyovyote. Au kujenga subway stations na treni za kutosha mijini na nje ya miji. Hivyo ndivyo wanavyofanya wenzetu nje.
 
Mkuu umewaza kuhusu zikikaribiana kwa nyuma ile sumaku si itavuta na kusababisha ajali iwe rahisi kutokea?
 
Picha hapa chini inaonyesha semi trailer na V8 zikikutana uso kwa usoView attachment 2958136
Semi trailer kikawaida ina maximum speed ya 80 km/h na ina uzito wa 42345kg.
VX V8 ina maxmum speed ya 300Km/hr na ina uzito wa 3350kg

kitu chochote chenye uzito na speed kina FORCE kwa muujibu wa newton fitst law of motion

F = M × {(V2 - V1)/t}
F -FORCE
M-MASS
V2 -FINAL VELOCITY
V1-INITIAL VELOCITY

Gari namba moja lina force 1
Pia lina magnetic fotce 1
Gari la pili lina force 2
Pia lina magnetic force 2
Effect ya inertia itakuwaje kwa watu waliomo kwenye hayo magari? Kwa sababu hakuna collisison hata airbags hazitafumuka hawakawii pita madirishani maana gari baada ya magari ku repel each other against motion.
sema mkuu nadhani teknolojia imekua sana. Niliona video moja ya gari la tesla lilikuwa road halafu jamaa aliyekuwa mbele ya hilo gari alikuwa anaendesha hovyo akahama lane yani ile ingesababisha kulivamie, ile gari wanasema pasipo dereva kuchukua haisee ile gari ilihama yenyewe faster kwenye lane nyingine in a mater of milliseconds. Halikuwa tangazo ilikuwa uhalisia.
 
Magari kupiishana ndiyo uchawi wenyewe hakuna issue ya magnet wala baba yake nane, zijengwe barabara ambazo magari hayapishani, yaani ni one way, yaani magari yanayoenda mfano Morogoro hayapishani na magari yanayotoka morogoro
Tatizo urasimu katika ujenzi wa miundombinu. Jiulize inawezekanaje pesa zinapoteq tu bure badala ya kufanya mambo ya maana
 
Picha hapa chini inaonyesha semi trailer na V8 zikikutana uso kwa usoView attachment 2958136
Semi trailer kikawaida ina maximum speed ya 80 km/h na ina uzito wa 42345kg.
VX V8 ina maxmum speed ya 300Km/hr na ina uzito wa 3350kg

kitu chochote chenye uzito na speed kina FORCE kwa muujibu wa newton fitst law of motion

F = M × {(V2 - V1)/t}
F -FORCE
M-MASS
V2 -FINAL VELOCITY
V1-INITIAL VELOCITY

Gari namba moja lina force 1
Pia lina magnetic fotce 1
Gari la pili lina force 2
Pia lina magnetic force
Suala la kuzuia ajali balabalani ni ngumu sana.. kwani nyingi husababishwa na uzembe wa baadhi ya madereva kutokuwa makini kwenye vyombo vya Moto. Baadhi ya ajali husababishw na nguvu na Giza pale mashetani,wachawi,majini wanapoitaji kutoa kafara zao si dhani kama hizo magnetic zitaweza kuwazuia...

Hapo ni ngumu Sana Taifa kama marekani limeshindwa kuzuia ajali balabalani kwa asilimia 100% sembuse nchi kama hii Tanzania viongozi wanajari maslahi yao binafsi
 
mbele yangekwepana lakin nyuma yangevutana sana... lakin pia ukiweka magnet crank shaft na engine kwa ujumla ingepata wapi mzunguko(initial velocity), gear zingevutana sana na mpangilio usingekuepo pia. Laws zitagoma hapo kaka. wacha mifumo ya breaks(PSI) ifanye kazi ila madereva wafate sheria pia tukiboresha miundombinu ajali zitapungua sana
 
Sio wameshindwa nadhani ni sisi ndio tumeshindwa kufikiria ipasavyo kwasababu ni swala la kitaalamu zaidi.

Hivi kwa kufikiri tu unadhani utahitaji sumaku ngapi katika gari ili uweze kuwa secured na ajali?

Vipi kwenye swala la parking na kuendesha chombo kwenye barabara yenye foleni?

Maana yake itahitajika kuwepo na gape kubwa kutoka kwenye gari moja hadi lingine.

So ili kuepuka collisions itabidi kutoka Vingunguti stendi mpaka Mfugale iwe ni distance ya kutosha magari matano tu.

Tungetoboa mpaka hapo?

Lakini fikiria tu power ya hiyo sumaku jinsi ambavyo ingekuwa.

Kwasababu kama Sumaku imefumwa kwa nguvu ya kuweza kufanya gari lenye uzito wa tani kuweza kusukumwa maana yake hiyo ni nguvu kubwa mno.

Hivyo maana yake kama ni gari inatoka Mbeya kuja Dar basi kila kipande cha chuma kilichokuwa njiani lazima kivutwe na sumaku.

Hapo unaweza kujikuta umetengeneza ajali nyingine kwasababu hiyo force ya hivyo vyuma jinsi vitavyovutwa itakuwa ni kubwa mno kiasi iweze ku damage gari lenyewe.

We nae vipi kwamba iwepo distance ya nn sasa? Kwan huo mfumo si unaweza kuwa wa kuwasha na kuzima. Ukiwa kwenye mwendo wa kawaida unazima ukiwa highwayunawadha
 
teh! Mkuu umemaanisha yataacha njia?
1. "Unlike poles repelling each other" hii ni nadharia mojawapo ya sumaku sasa kama usumaku ni mkubwa kwenye gari A ukakutana na mwengine ambao ni mkubwa pia kwenye gari B tena yakiwa kwenye mwendo mkubwa unadhani nini kitatokea kama si magari yatasukumiwa pembeni na kusababisha maafa zaidi.

2. Gharama , coil ambazo zitatumika kwenye hizo gari zitakuwa ni nyingi si kitoto ili tu kuweza kuzalisha usumaku unaotakiwa kingine pia itabidi kila gari either iwe na mfumo wa umeme wa AC (alternating current) ili usumaku uweze kuzalishwa kwenye hizo coil , tuseme tutatumia battery ya gari ambayo utakuwa inachajishwa na alternator ya kwenye gari husika ambapo tutaongeza tu inverter ambayo itabadilisha umeme wa DC kwenda AC kiuhalisia halitafanya kazi maana battery moja ndogo ya gari haitatosheleza kuzalisha umeme mkubwa wa kuweza kuzalisha usumaku unaotakiwa .

Njia ambayo itakuwa rahisi ni kupitisha line za umeme na kufunga kwenye kila gari kichukuzi cha umeme wa AC moja kwa moja kwenye hizo line kama treni za umeme zilivyo, sasa hii itakuwa haimpi mtu uhuru wa kuendesha gari lake maana itabidi lipite sehemu husika tu na sehemu ambayo hakuna hizo line basi gari haitopita.

3. Kingine jua kwamba usumaku huwa una pande mbili za kufikirika ( immaginary poles) yaani north pole na southpole sasa kama tutakubaliana kwamba tufanye upande wa mbele uwe noth pole hii inamaanisha lazima utafute upande ambao utakuwa southpole kikawaida labda tuuweke nyuma hii itasababisha gari igeuke kuwa sumaku moja kubwa inayotembea barabarani , hii itapelekea kutokee mambo mawili

1. Magari ambayo pande zake mbili zinazotofautiana pindi yakikutana yataanza kuvutana (attraction)

2. Magari ambayo pande zake mbili zinafanana yakikutana basi yatasukumana (repulsion)

Hii itasabisha maafa zaidi badala ya faida.

4. Kingine usumaku unapotua kwenye chuma huwa unazalisha umeme mdogo unaozunguka (rotating current) kwenye uso wa chuma hicho ambao umeme huo utazalisha usumaku mdogo ambao utaingiliana na usumaku mkubwa hii itasababisha uzalishwaji wa joto (eddy current losses) kwenye chuma hicho na kitaendelea kupata joto na inaweza kufikia kiwango kikubwa cha kusababisha madhara baadae maana chuma cha kawaida kina sifa ya kuhifadhi usumaku hata baada ya visababishi kuondolewa, pia umeme utakuwa unalika mwingi.

Ili kuepuka hilo itabidi sasa either frame za magari zitengenezwe kwa materials tofauti na chuma ambazo huwa ni gharama zaidi au dhaifu kuliko chuma hivyo kupelekea magari
Kuwa ghali zaidi mfano tunaweza kutumia carbon fibres ambazo ni ghali sana au soft irons ambazo hazina nguvu kama chuma .

Conclusion
Nadhani njia nzuri ni barabara kuboreshwa na pia ziwekwe sheria kali sana za barabarani ambazo zitawabana watu kutokuzembea pindi wanapokuwa kwenye vyombo vya moto .
 
We nae vipi kwamba iwepo distance ya nn sasa? Kwan huo mfumo si unaweza kuwa wa kuwasha na kuzima. Ukiwa kwenye mwendo wa kawaida unazima ukiwa highwayunawadha
Jama yupo sahihi kimahesabu ipo hivyo sasa kama unasema uwekwe mfumo wa kuwasha na kuzima basi huo mfumo hauna maana kwa sababu ajali huwa haisubiri mpaka ufike highway mkuu inatokea popote pale na pi kimahesabu ni gharama zaidi kuweka usumaku kuliko kuweka sheria ngumu na pia elimu iongezwe kwa waendeshaji magari.
 
Ni hivi nchi za wenzetu kuna kua na barabara inayoenda tu mfano Morogoro, na inayotoka morogoro inakua iko upande mwingine, yaani hakuna magari yanayopishana
Yes mkuu mfano mzuri ni N1 kutoka Joberg hadi polokwane ni zaidi ya 300km,kwetu barabara zetu zinajengwa chini ya kiwango na finyu mno,T1 inatakiwa ijengwe upya na sip kuitia viraka,yellow line ziwepo on both sides of the road,zile 50km ndani ya mikumi national park,ipanuliwe zaidi na itumike kama airstrip (Botswana wamelifanya hili)
 
We nae vipi kwamba iwepo distance ya nn sasa? Kwan huo mfumo si unaweza kuwa wa kuwasha na kuzima. Ukiwa kwenye mwendo wa kawaida unazima ukiwa highwayunawadha
Kwanza unapojadili hii dhana uwe una relate na miundombinu ya barabara zetu jinsi zinavyo operates.

Mfano kama barabara zetu za one way ambazo ndio zipo nyingi.

1713081076866.png

Ukizima sumaku ili kupunguza gape la kuokoa foleni, yule wa nyuma atajuaje kuwa wewe umezima sumaku?

Maana yake kama gari yake sumaku yake bado ipo active basi akikusogelea tu lazima uvutwe.

Na kwasababu barabara ni single way, vipi kuhusu vyombo vinavyopita upande wa pili wenu katika uelekeo tofauti na nyie?

Vipi kama hivyo vyombo sumaku zao zipo active?
 
Wakuu habari!

Leo nikiwa barabarani niliona magari mawili yaliyotaka kugongana uso kwa uso ghafla likanijia wazo ambalo limenisukuma kuandika uzi huu namna ya kuzuia ajali kama hizi.

View attachment 2958107
Picha nmetoa mtandaoni

Kikawaida ncha mbili za sumaku zikikutana hukwepana, mfano angalia hapa chini kwenye pichaView attachment 2958106
Sasa ikiwa magari yote yatatengenezwa kwa sumaku kwa mbele ktk mtindo wa ncha mbili zinazofanana yakikutana uso kwa uso yatakwepana (yatasukumana bila kugongana) yaani kama ule mchezo wa kusukumana lakini hapa itakua bila kugusana,

Chukulia mfano semi trailer inakutana uso kwa uso na V8, ili zisigongane zikwepane itahitajika sumaku kubwa sana iwekwe mbele ya gari mfano sumaku yenye ukubwa wa shina la mbuyu kwa kila gari yaani semi na V8, kitu ambacho kitaathiri uzito wa kila gari na balance haitakuwdpo,

Kwa vile chuma laini kikizungushiwa nyaya kwa mtindo wa coil kisha kuunganishwa na umeme huwa kinakua sumaku hii njia itafaa zaidi kutengeneza sumaku yenye nguvu kubwaView attachment 2958127
Zingatia pia ujio wa magari ya umeme.

Chini ntatoa ufafanuzi wa kimahesabu , Nakaribisha maoni kinzani.
vipi kuhusu size ya hiyo sumaku itakuwa na ukubwa gani??....lakini pia sumaku inaweza hata kung'ang'ania piston za engine,,,,,labda kama itakuwa electro magnet ambayo itafanya kazi wakati wa ajali tu ambayo ni sekunde 2 au 1 kumbuka ajali ni kitu kinachotokea kwa sekunde 1 au 2 muda wa kuandaa sumaku ni mchache!!!!!! kama itafanya kazi muda wote basi engine haitaweza kutembea na hata magari yatashindwa kupisha lazima yatasukumana yanapopishana which is dangerous
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom