Mwenye uelewa anisaidie tofauti ya raia na Mwananchi

Raia anatokana na mwananchi/wananchi, mfano wanachi mkoani Mbeya wamejiandikisha katika daftari la wapiga kura kujiandaa na uchaguzi wa mwaka huu. Lkn katika zoezi hill kumetokea na dosari kadhaa ikiwa ni pamoja na kuandikishwa kwa wananchi wasio na sifa za uraia. Mfano wa pili ni wakimaeneo kuna makazi ya kijeshi kama vile polisi, magereza,jwtz nk, haya tunaita makazi ya majeshi, lkn maeneo kama vile Manzese, mwanjelwa, magomeni, soweto, haya tunayaita makaazi ya raia lkn wote ni wananchi wa sehemu hizo
 
Mara nyingi maneno haya mawili yanataja watu walewale lakini inawezekana kuna tofauti. Mtazamo ni tofauti.

"Raia" inaangalia upande wa kisheria: je mtu fulani anatosheleza masharti ya kuitwa "raia" wa nchi fulani, pamoja na haki (kama kura, haki ya kusikilizwa na kulalamika, kutetewa na ubalozi wake akiwa ugenini) na wajibu (kwa mfano kwenda jeshini katika nchi nyingi, kushiriki katika wajibu fulani) za uraia.

"Mwananachi" inatazama zaidi tabia ya kuishi (kwa muda usio mfupi) katika nchi au sehemu fulani, kuwa mwenyeji wa huko.
Kwa kawaida hakuna utaratibu wa kisheria au masharti kamili ni nani anayeweza kuitwa "mwananchi", tofauti na "raia".

Unaweza kuishi katika nchi nyingine hadi umekuwa mwenyeji na kila mtu anakutazama kuwa mwananchi lakini bado hujafanya hatua ya kuomba uraia.

Mara nyingi tofauti hii si tatizo lakini kutegemeana na siasa ya nchi fulani tatizo linaweza kutokea.
Kwa mfano huko Marekani Bwana Trump anajaribu kuwaondoa watu waliokuwa wenyeji kwa muda mrefu hata kizazi cha pili kwa sababu zamani waliingia kutoka Meksiko, si raia.
Nakumbuka majadiliano sawa kuhusu Banamulenge nchini Kongo waliokuwa wenyeji na wananchi kwa vizazi lakini walinyimwa uraia na kutangazwa kuwa Warwanda kwa sababu za ukabila na siasa.
Naongezea juu ya maelezo ya wenzangu. Mwananchi ni mtu anayeishi katika nchi; ni mwenyeji wa nchi kijamii na kimakazi. RAIA ni mwenyeji wa nchi kisheria na kisiasa. Ana haki ya kushiriki maamuzi na matendo rasmi ya kisheria na kisiasa. Zingatia kwamba, mwananchi anaitwa hivyo sababu anaishi nchini, Ila RAIA in RAIA kwa belonging hata kama haishi nchini
 
Ni lazima kutafsiri? Basi ukipenda labda hivi:
Utaifa - nationality
raia - citizen (lakini pamoja na maneno mengine pia "mtu wa kawaida", yaani "wakristo raia - mapadre" au "watu raia" - "wanajeshi")
wakazi - inhabitants
wananchi - people of an area

Kama ni maneno yasiyotumiwa kisheria mara nyingi maana zinaingiliana.
Hayo in matumizi ya lugha ya kimtaani au matumizi mengine ya neno RAIA. Lakini, kwa maana yenyewe, hats mwanajeshi in RAIA was nchi
 
Mimi nadha ni kiswahili ni shida..

Uraia inabeba dhana ya utaifa wa mtu
Mwana+nchi inabeba dhana ya mzawa wa eneo husika maana yake raia ambaye ni mzawa wa nchi husika au sehem husika.....

Sasa linapokuka Suala la askar amengia uraiani
Wanachi wapgana na askari
Wanajeshi wapigana na raia
Hapo sasa ufafanuz wake ndo utata...
 
yote yana maana sawa ila yanatumika katika muktadha tofauti...hiyo ni kawaida katika lugha kuwa na visawe ktk lugha,
kwa mfano maneno angalia, tazama, ona yanamaana sawa but huwezi sema nilikuwa naona mpira bali utasema nilikuwa natazama mpira
 
Mkuu wapo wengi na wengine wametlelkezwa kwenye kambi huko ALASKA !!
Unachosema ni kweli kulingana na Historical Theories. Lakini kiuhalisia dunia hakuna binadamu mwenye asili hiyo. Historical Theories nyingi zimewapoteza watu wengi wenye elimu ndogo ya Historia. Mfano ni ile Dawning Theory inayosema binadamu wa kwanza wa Afrika alikuwa sokwe/nyani. Kwa mtu mwenye elimu Histori ya form four na six ataendelea kuelewa hivyo.
 
naomba nichangie kidogo,neno raia katika asili yake ya kiarabu lina maana ya watu wanaoongozwa,kwao wana neno rai ni kiongozi na raia waongozwa.
mwananchi ni muhusika wa nchi fulani bila ya kujali kama ni kiongozi au kiongozwa.
rai kikwete alizoea kusema"NDUGU WANANCHI WENZANGU" NA sio raia wenzangu
 
Kwa kuanza niseme lugha ya kiswahili ina namna zaidi ya kumi za uundaji wa maneno. Neno mwananchi liliundwa katika muundo ambatano yaani. Mwana lina maana mzawa au mtoto na neno Nchi linamaana eneo la kimpaka la taifa fulani, maneno haya ukiyachunguza yalitokana na shughuli za kisiasa.

Neno RAIA ni neno lenye maana ya ukaazi mtu wa nchi fulani kisheria
Jamani huwa nashndwa kujua au kutofautisha kti ya neno RAIA na MWANANCHI.Hebu nipeni ufafanunuzi.
 
yote yana maana sawa ila yanatumika katika muktadha tofauti...hiyo ni kawaida katika lugha kuwa na visawe ktk lugha,
kwa mfano maneno angalia, tazama, ona yanamaana sawa but huwezi sema nilikuwa naona mpira bali utasema nilikuwa natazama mpira
Naangalia
 
Back
Top Bottom