Ng'wanapagi
JF-Expert Member
- Sep 18, 2013
- 9,125
- 8,631
Mwananchi ni kama wewe, raia wanatofautiana kuna raia vilaza na raia mtu
"Ulazima" wa nini?Ulazima hauna hiyari,tambua hilo
Naongezea juu ya maelezo ya wenzangu. Mwananchi ni mtu anayeishi katika nchi; ni mwenyeji wa nchi kijamii na kimakazi. RAIA ni mwenyeji wa nchi kisheria na kisiasa. Ana haki ya kushiriki maamuzi na matendo rasmi ya kisheria na kisiasa. Zingatia kwamba, mwananchi anaitwa hivyo sababu anaishi nchini, Ila RAIA in RAIA kwa belonging hata kama haishi nchiniMara nyingi maneno haya mawili yanataja watu walewale lakini inawezekana kuna tofauti. Mtazamo ni tofauti.
"Raia" inaangalia upande wa kisheria: je mtu fulani anatosheleza masharti ya kuitwa "raia" wa nchi fulani, pamoja na haki (kama kura, haki ya kusikilizwa na kulalamika, kutetewa na ubalozi wake akiwa ugenini) na wajibu (kwa mfano kwenda jeshini katika nchi nyingi, kushiriki katika wajibu fulani) za uraia.
"Mwananachi" inatazama zaidi tabia ya kuishi (kwa muda usio mfupi) katika nchi au sehemu fulani, kuwa mwenyeji wa huko.
Kwa kawaida hakuna utaratibu wa kisheria au masharti kamili ni nani anayeweza kuitwa "mwananchi", tofauti na "raia".
Unaweza kuishi katika nchi nyingine hadi umekuwa mwenyeji na kila mtu anakutazama kuwa mwananchi lakini bado hujafanya hatua ya kuomba uraia.
Mara nyingi tofauti hii si tatizo lakini kutegemeana na siasa ya nchi fulani tatizo linaweza kutokea.
Kwa mfano huko Marekani Bwana Trump anajaribu kuwaondoa watu waliokuwa wenyeji kwa muda mrefu hata kizazi cha pili kwa sababu zamani waliingia kutoka Meksiko, si raia.
Nakumbuka majadiliano sawa kuhusu Banamulenge nchini Kongo waliokuwa wenyeji na wananchi kwa vizazi lakini walinyimwa uraia na kutangazwa kuwa Warwanda kwa sababu za ukabila na siasa.
Hayo in matumizi ya lugha ya kimtaani au matumizi mengine ya neno RAIA. Lakini, kwa maana yenyewe, hats mwanajeshi in RAIA was nchiNi lazima kutafsiri? Basi ukipenda labda hivi:
Utaifa - nationality
raia - citizen (lakini pamoja na maneno mengine pia "mtu wa kawaida", yaani "wakristo raia - mapadre" au "watu raia" - "wanajeshi")
wakazi - inhabitants
wananchi - people of an area
Kama ni maneno yasiyotumiwa kisheria mara nyingi maana zinaingiliana.
Huwa hakuna muhindi mwekundu!RAIA ni mhamiaji aliye batizwa..
MWANANCHI ni mzawa asili...... (kama vile wagogo hapa TZ, wahindi wekundu huko US)
Mkuu wapo wengi na wengine wametlelkezwa kwenye kambi huko ALASKA !!Huwa hakuna muhindi mwekundu!
Unachosema ni kweli kulingana na Historical Theories. Lakini kiuhalisia dunia hakuna binadamu mwenye asili hiyo. Historical Theories nyingi zimewapoteza watu wengi wenye elimu ndogo ya Historia. Mfano ni ile Dawning Theory inayosema binadamu wa kwanza wa Afrika alikuwa sokwe/nyani. Kwa mtu mwenye elimu Histori ya form four na six ataendelea kuelewa hivyo.Mkuu wapo wengi na wengine wametlelkezwa kwenye kambi huko ALASKA !!
Jamani huwa nashndwa kujua au kutofautisha kti ya neno RAIA na MWANANCHI.Hebu nipeni ufafanunuzi.
Ni sawa tu kama vile nyumbu na wildebeest
Naangaliayote yana maana sawa ila yanatumika katika muktadha tofauti...hiyo ni kawaida katika lugha kuwa na visawe ktk lugha,
kwa mfano maneno angalia, tazama, ona yanamaana sawa but huwezi sema nilikuwa naona mpira bali utasema nilikuwa natazama mpira