Hii Serikali haiko Serious na Maafa, inawatelekeza sana Raia wenye maafa

BLACK MOVEMENT

JF-Expert Member
Mar 11, 2020
2,737
6,553
Nchi nyingi sana Duniani huwa zina take Care sana ya Raia wao, wakati wa shida hasa inapo tokea majanga kama mafuriko au moto au tetemeko, hata kama janga limekumba raia mmoja tu, haijalishi.

Na chi iko radhi iingie vitani kisa raia wake mmoja tu kafanyiwa vibaya au kauliwa.

Kwa Africa ni nchi chache zenye huo ustarabu. Tanzania ikiwa haimo kwenye huo ustarabu.

Swaka la mafuriko, ilianzia kule Hanang ambako ilichukua siku ya tatu Serikali kuanza kutuma wanajeshi wa kutafuta watu tena ni waliokufa, ila siku ya kwanza kazi ilifanywa na wananchi wa pale na askari police wa eneo husika. Wanajeshi wameletwa baadae sana siku ya tatu. Labda timu ya uokoaji ingekuwepo usiku ule ule labda watu wengi wangeokolewa. Ila haikuwa hivyo.

Sasa ni kule rufiji hakuna respond ya haraka ya Serikali kushughurikia maafa yale na kuokoa na kuwahudumia walio patwa na maafa. Kule sidhani kama kuna Mahemema kwa ajili ya waathiriwa zaidi ya kusikia wamepelekewa chakula. Sioni vikosi vya uokoaji kule wakiwa wanaokoa raia na mali zaom Raia wamepoteza maisha, mali zimeharibika na hakuna wa kuwasaidia.

Niliambiwa na mtu kule kwamba Raia wana jiokoa wenyewe hakuna cha Serikali wala nini.

Mafuriko ya Arusha jana, pamoja na kwamba sio mafuriko makubwa sana ila watu mali zai zimeharibika, watu wamepata hasara nyumba zimebomolewa, hakuna hata nukuta ya msaada kutoka Serikalini zaidi ya viongozi kwenda kupiga picha eneo la mafuriko.Wale watu kuna wanao hitaji misaada ya Chakula, mahema na kadhalika ila hakuna hata anaye hangaika. watawala wanaenda na V8 kupiga picha.

Kule Hanang nako V8 zilikuwa nyingi kuliko
vifaa vya uokoaji.

Sasa je Serikali Policy yao ya maafa ni ipi? Inasemaje? kuna sehemymu imechapishwa tuipate tusome? Kwa sababu ni kama raia wanadharaulika na utawala.

Vifaa vya uokoaji ni pesa ngapi?Wana mahema? Kuna Helicopta standby za kufanya uokoaji? Ni wanatakiwa watu wafe kaisi gani ndio Serikali irespond? Ni mali kiasi gani zinapaswa kuharibika ndio kuwe na respond?

Vipi siku ya kitokea maafa kwa wakati mmmoja sehemu tofauti tofauti hali itakuwaje? Vipi watu walioko mikoa kama Kigoma wakapata maafa itakuwaje? sipati picha kabisa kwa sababu walioko tu jirani na Ikulu wanapuwa vipi huko mbali?
 
Back
Top Bottom