Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,485
- 31,576
- Thread starter
- #21
MGAO WA FEDHA ZA KODI ZITOKANAZO NA WAFANYAKAZI WA MUUNGANO
Wazanzibar wakieleza malalamiko husemwa ni 'kero za Muungano' Watanganyika inasemwa ni chuki.
Watanganyika wanapoeleza ya moyoni hupuuzwa. Prof Magamba alisema ' wakiyatoa Muungano upo matatizoni'
Kati ya kero za Wazanzibar zilizotatuliwa na awamu ya sita ni fedha za Bajeti 4.5% iliyokuwepo hadi 9% ya Rais SSH kama alivyobainisha mwenezi wa CCM bwana Mbeto.
Pili, kuwa na 21% ya Watumishi wa Muungano- iliyowekwa na Waziri Mchengerwa wakati huo
Haikuwekwa wazi 21% ya nafasi za Muungano zinahusu maeneo gani.
Inafahamika kila lenye jinaTanzania ni la Muungano hivyo ajira 21% zinahusu yasiyo ya Muungano pia
Kutoa 21% kwa Wazanzibar ni 'kuficha ukweli' kwamba ajira zinatolewa Wizara zisizo za Muungano kama TAMISEMI, Afya, Madini, Kilimo, Maji, miundo mbinu, Elimu, Maliasili, Ujenzi , Mawasiliano n.k. na Taasisi kama Tanzania Bureua Standards, Bandari n.k. si sehemu ya 21%.
Utaratibu huo unawanyima Watanganyika fursa kwa kuwapa Wazanzibar 21% na pia 79% za Tanganyika
Kwa utaratibu huu, Wazanzibar wana fursa hizi za ajira
1. Kutoka SMZ ambapo Watanganyika hawaruhusiwi
2. 21% zilizotengwa mahususi kwao na si kwa mkoa mwingine wowote
3. Uwezo wa kuomba kutoka 79% ya Tanganyika wakitumia jina ' Tanzania''
Watumishi wa Muungano wanalipa kodi. Zanzibar ililalamika haipewi kodi za Watumishi hao kama kutoka JMT ambayo ni Tanganyika. Utaratibu umewekwa, kodi za Watumishi wa Muungano sehemu ipewe Zanzibar.
Kisichoelezwa ni Watumishi kutoka wapi.
Kwa maneno mengine kodi za Watumishi wa TAMISEMI, Elimu, Kilimo, Madini, Ufugaji , Ujenzi, Maliasili na Taasisi zisizo za Muungano zinapelekwa Zanzibar kama mgao wa kodi za Watumishi JMT.
21% ya Watumishi wa Muungano kutoka Zanzibar inalipwa na fedha za Tanzania ambazo ni za Tanganyika.
Yaani Zanzibar wanapewa nafasi 21% halafu Tanganyika wanabeba mzigo wa mishahara na mafao yao.
Haijaelezwa mchango wa Zanzibar katika Muungano kutoka Bajeti ya Muungano, au ya Zanzibar
Gavana wa Bank Kuu marehemu Ndulu alisema Zanzibar haijachangia Muungan takribani miaka 40+
Ni Wazanzibar hawa wanaolalamika mambo ya Muungano kuingizwa kinyemea.
Wanapoajiriwa katika taasisi na Wizara zisizo za Muungano , wanakaa kimya. UNAFIKI.
Hitimisho: Wazanzibar wanapata yafuatayo kwa gharama za Tanganyika
1. Hawachangii Muungano na hakuna takwimu zinazoonesha hivyo
2. Wanapata 21% ya ajira za Muungano ambazo pia zinahusu maeneo yasiyo ya Muungano
3. Hawalipi mishahara ya 21% ya watumishi inayopewa kwa jina la Watumishi wa Muungano
4. Wanalipwa kodi zinazotokana na 21% ya watumishi wasiowalipa wao na wanaopatikana maeneo yasiyo ya Muungano.
Wazanzibar wakieleza malalamiko husemwa ni 'kero za Muungano' Watanganyika inasemwa ni chuki.
Watanganyika wanapoeleza ya moyoni hupuuzwa. Prof Magamba alisema ' wakiyatoa Muungano upo matatizoni'
Kati ya kero za Wazanzibar zilizotatuliwa na awamu ya sita ni fedha za Bajeti 4.5% iliyokuwepo hadi 9% ya Rais SSH kama alivyobainisha mwenezi wa CCM bwana Mbeto.
Pili, kuwa na 21% ya Watumishi wa Muungano- iliyowekwa na Waziri Mchengerwa wakati huo
Haikuwekwa wazi 21% ya nafasi za Muungano zinahusu maeneo gani.
Inafahamika kila lenye jinaTanzania ni la Muungano hivyo ajira 21% zinahusu yasiyo ya Muungano pia
Kutoa 21% kwa Wazanzibar ni 'kuficha ukweli' kwamba ajira zinatolewa Wizara zisizo za Muungano kama TAMISEMI, Afya, Madini, Kilimo, Maji, miundo mbinu, Elimu, Maliasili, Ujenzi , Mawasiliano n.k. na Taasisi kama Tanzania Bureua Standards, Bandari n.k. si sehemu ya 21%.
Utaratibu huo unawanyima Watanganyika fursa kwa kuwapa Wazanzibar 21% na pia 79% za Tanganyika
Kwa utaratibu huu, Wazanzibar wana fursa hizi za ajira
1. Kutoka SMZ ambapo Watanganyika hawaruhusiwi
2. 21% zilizotengwa mahususi kwao na si kwa mkoa mwingine wowote
3. Uwezo wa kuomba kutoka 79% ya Tanganyika wakitumia jina ' Tanzania''
Watumishi wa Muungano wanalipa kodi. Zanzibar ililalamika haipewi kodi za Watumishi hao kama kutoka JMT ambayo ni Tanganyika. Utaratibu umewekwa, kodi za Watumishi wa Muungano sehemu ipewe Zanzibar.
Kisichoelezwa ni Watumishi kutoka wapi.
Kwa maneno mengine kodi za Watumishi wa TAMISEMI, Elimu, Kilimo, Madini, Ufugaji , Ujenzi, Maliasili na Taasisi zisizo za Muungano zinapelekwa Zanzibar kama mgao wa kodi za Watumishi JMT.
21% ya Watumishi wa Muungano kutoka Zanzibar inalipwa na fedha za Tanzania ambazo ni za Tanganyika.
Yaani Zanzibar wanapewa nafasi 21% halafu Tanganyika wanabeba mzigo wa mishahara na mafao yao.
Haijaelezwa mchango wa Zanzibar katika Muungano kutoka Bajeti ya Muungano, au ya Zanzibar
Gavana wa Bank Kuu marehemu Ndulu alisema Zanzibar haijachangia Muungan takribani miaka 40+
Ni Wazanzibar hawa wanaolalamika mambo ya Muungano kuingizwa kinyemea.
Wanapoajiriwa katika taasisi na Wizara zisizo za Muungano , wanakaa kimya. UNAFIKI.
Hitimisho: Wazanzibar wanapata yafuatayo kwa gharama za Tanganyika
1. Hawachangii Muungano na hakuna takwimu zinazoonesha hivyo
2. Wanapata 21% ya ajira za Muungano ambazo pia zinahusu maeneo yasiyo ya Muungano
3. Hawalipi mishahara ya 21% ya watumishi inayopewa kwa jina la Watumishi wa Muungano
4. Wanalipwa kodi zinazotokana na 21% ya watumishi wasiowalipa wao na wanaopatikana maeneo yasiyo ya Muungano.