Muundo wa Muungano au Mambo ya Muungano?

SMU

JF-Expert Member
Feb 14, 2008
9,616
7,864
Mimi ni mmoja wa watu wanaoamini kuwa mchakato huu wa kuandika katiba mpya (kubadilisha katiba) ungetakiwa uanze kwa mjadala wa kitaifa na kisha kura ya maoni - referendum- (badala ya tume kukusanya maoni) juu ya uwepo wa muungano wenyewe na mambo ambayo tunataka kuungana/kushirikiana.

Lakini mchakato ndio hivyo tena umeshaanza kama ulivyoanza na sasa bunge maalumu la katiba linapitia na kujadili sura ya kwanza na ya sita za rasimu ya katiba. Kuna uwezekano mkubwa tu, bunge hili likashindwa kuvuka kizingiti hiki cha kwanza. Sura ya sita inafanya rejea kwatika mambo ya muungano ambayo yameorodheshwa kwenye "Nyongeza" (ya Kwanza?) ya rasimu ya katiba.

Bila ya shaka jambo kubwa na mijadala mingi juu ya katiba hii imejikita zaidi kwenye muundo wa muungano (serikali mbili ama tatu) . Tatizo ninaloliona katika mijadala mingi ni kuwa tumesahahu kabisa kujadili kwa uzito wake mambo ambayo tunataka kuungana ("Mambo ya Muungano"). Kwa maoni yangu mjadala ungeelekezwa kwanza kwenye mambo ya muungano kwa sababu ndio mambo ya msingi ambayo tunataka kushirikiana. Baada ya kukubaliana, kuridhiana na kuafikiana juu ya mambo yote tunayotaka kuungana/kushirikiano ndipo sasa tunaweza kuona ama kujadili vizuri zaidi muundo wa muungano ambao utakidhi kwa mambo ya muungano tulioafikiana.

Hii ni nukuu ya sehemu mojawapo ya hotuba ya Jaji Warioba kwa bunge maalumu la katiba:

Wakati Tume ilipokuwa inakusanya maoni, wananchi wengi wa Zanzibar kutoka makundi yote mawili, yaani wale waliotaka Muungano wa Serikali Mbili na wale waliotaka Muungano wa Mkataba, wote walipendekeza mambo mengi yaondolewe kwenye Orodha ya Muungano. Wale waliotaka Muungano wa Mkataba walitaka mambo yote yaondolewe kwenye Orodha ya Mambo ya Muungano isipokuwa suala la ulinzi. Wale waliotaka Muundo wa Serikali mbili walitaka mambo yote ya uchumi yaondolewe kwenye Orodha ya Mambo ya Muungano.

Kwa sasa rasimu inataja mambo ya muungano yafuatayo:
1. Katiba na mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
2. Ulinzi na Usalama wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
3. Uraia na Uhamiaji;
4. Sarafu na Benki Kuu;
5. Mambo ya Nje;
6. Usajili wa Vyama vya Siasa; na
7. Ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo ya kodi yatokanayo na mambo ya Muungano.

Je, mambo haya yanayopendekezwa kwenye rasimu yanatosha? Nini kiongezwe? Nini kiondolewe? Kwa nini?


CC: Chabruma Skype Buchanan Ngekewa Nguruvi3 Pasco ...na wadau wengine!
 
Mkuu, hakika umeanzisha mada ambayo ni kiini cha haya malumbano yanayoendelea. Kama tuna nia ya dhati ya kuwa na muungano, ni vema tukaangalia ni mambo yepi yanalifanya taifa liwe Imara. Hapa jambo kuwa ni uchumi, ulinzi na usalama, watu nk. Hivyo kama tunataka serikali ya muungano iwe imara zaidi kuliko serikali shirikishi, ni vema tukaipa uwezo wa kucontrol hayo yote. Ila kama tunataka kuiweka serikali ya muungano iwe dhaifu, mambo hayo na mengine ambayo wadau watachangia tunaweza kuyapeleka kwenye serikali za nchi washirika
 
Mimi ni mmoja wa watu wanaoamini kuwa mchakato huu wa kuandika katiba mpya (kubadilisha katiba) ungetakiwa uanze kwa mjadala wa kitaifa na kisha kura ya maoni - referendum- (badala ya tume kukusanya maoni) juu ya uwepo wa muungano wenyewe na mambo ambayo tunataka kuungana/kushirikiana.

Lakini mchakato ndio hivyo tena umeshaanza kama ulivyoanza na sasa bunge maalumu la katiba linapitia na kujadili sura ya kwanza na ya sita za rasimu ya katiba. Kuna uwezekano mkubwa tu, bunge hili likashindwa kuvuka kizingiti hiki cha kwanza. Sura ya sita inafanya rejea kwatika mambo ya muungano ambayo yameorodheshwa kwenye "Nyongeza" (ya Kwanza?) ya rasimu ya katiba.

Bila ya shaka jambo kubwa na mijadala mingi juu ya katiba hii imejikita zaidi kwenye muundo wa muungano (serikali mbili ama tatu) . Tatizo ninaloliona katika mijadala mingi ni kuwa tumesahahu kabisa kujadili kwa uzito wake mambo ambayo tunataka kuungana ("Mambo ya Muungano"). Kwa maoni yangu mjadala ungeelekezwa kwanza kwenye mambo ya muungano kwa sababu ndio mambo ya msingi ambayo tunataka kushirikiana. Baada ya kukubaliana, kuridhiana na kuafikiana juu ya mambo yote tunayotaka kuungana/kushirikiano ndipo sasa tunaweza kuona ama kujadili vizuri zaidi muundo wa muungano ambao utakidhi kwa mambo ya muungano tulioafikiana.

Hii ni nukuu ya sehemu mojawapo ya hotuba ya Jaji Warioba kwa bunge maalumu la katiba:



Kwa sasa rasimu inataja mambo ya muungano yafuatayo:


Je, mambo haya yanayopendekezwa kwenye rasimu yanatosha? Nini kiongezwe? Nini kiondolewe? Kwa nini?


CC: Chabruma Skype Buchanan Ngekewa Nguruvi3 Pasco ...na wadau wengine!

CCM wanaelewa kabisa kuwa muungano unahitaji utaratibu wa muda mrefu katika kuutengeneza huu muungano. Tatizo kubwa ni wahafidhina wa CCM wa Zanzibar. Hawa ndio waliotowa shinikizo kwa sababu mbili kubwa;
1.Kwa kuundwa muundo wa kila upande kujitegemea utasababisha masilahi yanayopatikana kupitia Chama yatapotea kwani kiuchumi CCM Zanzibar haina njia ya kukusanya pesa. Viongozi wa CCM Zanzibar ukiwafuatilia utaona hawana njia nyengine ya kupata riziki zaidi ya siasa. Ndiyo maana viongozi wengi wa CCM Zanzibar ni watu wasio na elimu ambayo wangeitumia kupata mahitaji yao kama si uwepo wa siasa. Kazi zao ni kuwatisha wafanyabiashara kwa jina la Chama.
2. Ni kuwa kwa kila upande kujitegemea kutakuwa na maana kuwa nguvu ya CCM itazidi kuporomoka Zanzibar. Vyombo vya dola havitoweza tena kuiokoa CCM Zanzibar.

CCM Tanganyika wanalazimika kukubali matakwa ya wahafidhina wa CCM wa Zanzibar kwa kuogopa kunyimwa kura za pamoja kutoka CCM Zanzibar. Wanaogopa matokeo yaliyowakuta JK na Salim A Salim. CCM Tanganyika wengi wao hawajiamini na ndio maana wanapotishwa wanabaki kutii amri.
 
  • Thanks
Reactions: SMU
CCM wanaelewa kabisa kuwa muungano unahitaji utaratibu wa muda mrefu katika kuutengeneza huu muungano. Tatizo kubwa ni wahafidhina wa CCM wa Zanzibar. Hawa ndio waliotowa shinikizo kwa sababu mbili kubwa;
1.Kwa kuundwa muundo wa kila upande kujitegemea utasababisha masilahi yanayopatikana kupitia Chama yatapotea kwani kiuchumi CCM Zanzibar haina njia ya kukusanya pesa. Viongozi wa CCM Zanzibar ukiwafuatilia utaona hawana njia nyengine ya kupata riziki zaidi ya siasa. Ndiyo maana viongozi wengi wa CCM Zanzibar ni watu wasio na elimu ambayo wangeitumia kupata mahitaji yao kama si uwepo wa siasa. Kazi zao ni kuwatisha wafanyabiashara kwa jina la Chama.
2. Ni kuwa kwa kila upande kujitegemea kutakuwa na maana kuwa nguvu ya CCM itazidi kuporomoka Zanzibar. Vyombo vya dola havitoweza tena kuiokoa CCM Zanzibar.

CCM Tanganyika wanalazimika kukubali matakwa ya wahafidhina wa CCM wa Zanzibar kwa kuogopa kunyimwa kura za pamoja kutoka CCM Zanzibar. Wanaogopa matokeo yaliyowakuta JK na Salim A Salim. CCM Tanganyika wengi wao hawajiamini na ndio maana wanapotishwa wanabaki kutii amri.


Mkuu, ingawa upo nje ya mada, yaelekea ukawa sahihi lakini pia ukapotoka kwa upande mwingine. Usahihi wake ni kwamba muungano huu unafanya chama kitegemeane kwa kila upande. Ni watu walioishi kwa muda mrefu na kutwgemeana kwa kila upande.

Ila ujue kuwa CCM inakubalika kila upande na ndo maana imeshinda uchaguzi kwa pande zote. Hii ni tofauti namvyama vingine ambavyo hukubalika na upande mmoja tu wa Jamhuri ya Muungano. Mathalan, CUF ina wabunge 3 tu Tanzania Bara ambapo wawili ni wa kuchaguliwa na mmoja ni wa viti maalum. Kule Zanzibar, CUF ina wabunge zaidi ya 50 kama sikosei na asilimia kubwa ya wabunge wake wanatoka kisiwa cha Pemba. Hivyo CUF hata Zanzibar haikubaliki. CHADEMA nao kwa upande wao wanakubalika Tanzania Bara tu tena si maeneo yote. Wanakubarika kwenye makao makuu ya mikoa to na ndiko kwenye wabunge wao. CHADEMA hawana mbunge hata mmoja kule Zanzibar. Hii ni kusema kuwa CHADEMA hakikubaliki visiwani Zanzibar. Hivyo ukiangalia takwimu hizo, hapo CCM inakuwa rahisi kutetea aina ya muungano uliopo. CHADEMA na CUF wanatetea aina ya muungano ambayo hawana hakika yake. Ila ni haki yao kuwa na msimamo kama huo.
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Mkuu, ingawa upo nje ya mada, yaelekea ukawa sahihi lakini pia ukapotoka kwa upande mwingine. Usahihi wake ni kwamba muungano huu unafanya chama kitegemeane kwa kila upande. Ni watu walioishi kwa muda mrefu na kutwgemeana kwa kila upande.

Ila ujue kuwa CCM inakubalika kila upande na ndo maana imeshinda uchaguzi kwa pande zote. Hii ni tofauti namvyama vingine ambavyo hukubalika na upande mmoja tu wa Jamhuri ya Muungano. Mathalan, CUF ina wabunge 3 tu Tanzania Bara ambapo wawili ni wa kuchaguliwa na mmoja ni wa viti maalum. Kule Zanzibar, CUF ina wabunge zaidi ya 50 kama sikosei na asilimia kubwa ya wabunge wake wanatoka kisiwa cha Pemba. Hivyo CUF hata Zanzibar haikubaliki. CHADEMA nao kwa upande wao wanakubalika Tanzania Bara tu tena si maeneo yote. Wanakubarika kwenye makao makuu ya mikoa to na ndiko kwenye wabunge wao. CHADEMA hawana mbunge hata mmoja kule Zanzibar. Hii ni kusema kuwa CHADEMA hakikubaliki visiwani Zanzibar. Hivyo ukiangalia takwimu hizo, hapo CCM inakuwa rahisi kutetea aina ya muungano uliopo. CHADEMA na CUF wanatetea aina ya muungano ambayo hawana hakika yake. Ila ni haki yao kuwa na msimamo kama huo.

Ndugu yangu takwimu zako ulizozitumia ni takwimu za maandiko na wala si za kweli.
Kabla ya kwenda huko naomba nikueleze kuwa suala la Katiba si saw3a na chaguzi kwani Katiba inakuwa na maslaha makubwa zaidi kuliko chaguzi. Tatizo la muungano ni zile zinazoitwa kero za muungano na wananchi wa pande zote bila kujali itikadi zao za chama zinawakera na wanataka kuziondowa.

Kuhusu takwimu zako ulizotowa ningeomba ufahamu kuwa kwa upande wa Zanzibar CCM haina ukubaliko namna unavyofahamu wewe. Iwapo uchaguzi ndio kigezo basi elewa kuwa kila chaguzi kunakuwa na ulalamishi na nakueleza nikiwa natoka huko hivyo naelewa vituko vyote.

Kuhusu suala la kutegemeana ni kweli CCM wanategemeana lakini utegemezi wenyewe sio katika kutatua mambo ya muungano lakini ni utegemezi wa masilahi binafsi. Kama nilivyosema ni kuwa CCM Zanzibar inategemea CCM Tanganyika kwa masilahi ya kuwepo kwao kimatumizi na kiutawala. Aidha kwa upande wa Tanganyika CCM wanategemea CCM Zanzibar kwa kura za pamoja za CCM Zanzibar.
 
Ndugu yangu takwimu zako ulizozitumia ni takwimu za maandiko na wala si za kweli.
Kabla ya kwenda huko naomba nikueleze kuwa suala la Katiba si saw3a na chaguzi kwani Katiba inakuwa na maslaha makubwa zaidi kuliko chaguzi. Tatizo la muungano ni zile zinazoitwa kero za muungano na wananchi wa pande zote bila kujali itikadi zao za chama zinawakera na wanataka kuziondowa.

Kuhusu takwimu zako ulizotowa ningeomba ufahamu kuwa kwa upande wa Zanzibar CCM haina ukubaliko namna unavyofahamu wewe. Iwapo uchaguzi ndio kigezo basi elewa kuwa kila chaguzi kunakuwa na ulalamishi na nakueleza nikiwa natoka huko hivyo naelewa vituko vyote.

Kuhusu suala la kutegemeana ni kweli CCM wanategemeana lakini utegemezi wenyewe sio katika kutatua mambo ya muungano lakini ni utegemezi wa masilahi binafsi. Kama nilivyosema ni kuwa CCM Zanzibar inategemea CCM Tanganyika kwa masilahi ya kuwepo kwao kimatumizi na kiutawala. Aidha kwa upande wa Tanganyika CCM wanategemea CCM Zanzibar kwa kura za pamoja za CCM Zanzibar.
Kabla sijachangia mada ya SMU nimeshtushwa na kauli zako.
Leo unasema kero si kuvunja muungano!!1 Leo unasema kero si znz huru! leo unasema kero si serikali 3.
Umebadilika, nini kimetokea ndugu yangu?
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: SMU
Kabla sijachangia mada ya SMU nimeshtushwa na kauli zako.
Leo unasema kero si kuvunja muungano!!1 Leo unasema kero si znz huru! leo unasema kero si serikali 3.
Umebadilika, nini kimetokea ndugu yangu?

Mbona Sheikh Nguruvi3 unanilisha maneno?
Sijawahi kusema kuvunja muungano lakini msimamo wangu ni kuwa kama hauna utatuzi basi na uvunjike kuliko kuoeneana !
Hivyo Zanzibar huru ni kero kwa nani? Kwa Zanzibar hilo ndio tunalolitaka na huru hiyo iwe ndani ya muungano au nje ya muungano

Serikali tatu si kero kwa Wazanzibari kwani wao ndio walioanza kampeni za kutaka serikali tatu. Tatizo kwa seerrikali 3 liko kwa rafiki zako CCM (tena ni viongozi wachache wahafidhina).
 
Mimi ni mmoja wa watu wanaoamini kuwa mchakato huu wa kuandika katiba mpya (kubadilisha katiba) ungetakiwa uanze kwa mjadala wa kitaifa na kisha kura ya maoni - referendum- (badala ya tume kukusanya maoni) juu ya uwepo wa muungano wenyewe na mambo ambayo tunataka kuungana/kushirikiana.

Lakini mchakato ndio hivyo tena umeshaanza kama ulivyoanza na sasa bunge maalumu la katiba linapitia na kujadili sura ya kwanza na ya sita za rasimu ya katiba. Kuna uwezekano mkubwa tu, bunge hili likashindwa kuvuka kizingiti hiki cha kwanza. Sura ya sita inafanya rejea kwatika mambo ya muungano ambayo yameorodheshwa kwenye "Nyongeza" (ya Kwanza?) ya rasimu ya katiba.

Bila ya shaka jambo kubwa na mijadala mingi juu ya katiba hii imejikita zaidi kwenye muundo wa muungano (serikali mbili ama tatu) . Tatizo ninaloliona katika mijadala mingi ni kuwa tumesahahu kabisa kujadili kwa uzito wake mambo ambayo tunataka kuungana ("Mambo ya Muungano"). Kwa maoni yangu mjadala ungeelekezwa kwanza kwenye mambo ya muungano kwa sababu ndio mambo ya msingi ambayo tunataka kushirikiana. Baada ya kukubaliana, kuridhiana na kuafikiana juu ya mambo yote tunayotaka kuungana/kushirikiano ndipo sasa tunaweza kuona ama kujadili vizuri zaidi muundo wa muungano ambao utakidhi kwa mambo ya muungano tulioafikiana.

Hii ni nukuu ya sehemu mojawapo ya hotuba ya Jaji Warioba kwa bunge maalumu la katiba:



Kwa sasa rasimu inataja mambo ya muungano yafuatayo:

Je, mambo haya yanayopendekezwa kwenye rasimu yanatosha? Nini kiongezwe? Nini kiondolewe? Kwa nini?

CC: Chabruma Skype Buchanan Ngekewa Nguruvi3 Pasco ...na wadau wengine!
Leo Tarehe 26 April, 2020 ni sikukuu ya Muungano, sikukuu hii ndio sikukuu muhimu kuliko hata uhuru kwasababu hii ni siku JMT ilipozaliwa. Lakini kutokana na janga hili la Corona, siku hii inaadhimishwa kimya kimya.
Naawatakia Muungano mwema huku nikisisitiza
Nautakia huu muungano wetu adhimu udumu milele na hivyo kukitokea yoyote anayetaka kuuchokoa muungano, namshauri chokochoko amchokoe pweza, muungano hutauweza kwasababu tutaulinda kwa gharama yoyote.
Nawatakia muungano mwema.
P
 
Leo Tarehe 26 April, 2020 ni sikukuu ya Muungano, sikukuu hii ndio sikukuu muhimu kuliko hata uhuru kwasababu hii ni siku JMT ilipozaliwa. Lakini kutokana na janga hili la Corona, siku hii inaadhimishwa kimya kimya.
Naawatakia Muungano mwema huku nikisisitiza
Nautakia huu muungano wetu adhimu udumu milele na hivyo kukitokea yoyote anayetaka kuuchokoa muungano, namshauri chokochoko amchokoe pweza, muungano hutauweza kwasababu tutaulinda kwa gharama yoyote.
Nawatakia muungano mwema.
P
Ha ha ha! Sawa mkuu, mimi nakuelewa("ga") vizuri sana.
 
Leo Tarehe 26 April, 2020 ni sikukuu ya Muungano, sikukuu hii ndio sikukuu muhimu kuliko hata uhuru kwasababu hii ni siku JMT ilipozaliwa. Lakini kutokana na janga hili la Corona, siku hii inaadhimishwa kimya kimya.
Naawatakia Muungano mwema huku nikisisitiza
Nautakia huu muungano wetu adhimu udumu milele na hivyo kukitokea yoyote anayetaka kuuchokoa muungano, namshauri chokochoko amchokoe pweza, muungano hutauweza kwasababu tutaulinda kwa gharama yoyote.
Nawatakia muungano mwema.
P


CORONA ITALETA HERI ; KWENYE TUMBO LA SHARI ; HERI HUTOKEA HUMO
 
Leo Tarehe 26 April, 2020 ni sikukuu ya Muungano, sikukuu hii ndio sikukuu muhimu kuliko hata uhuru kwasababu hii ni siku JMT ilipozaliwa. Lakini kutokana na janga hili la Corona, siku hii inaadhimishwa kimya kimya.
Naawatakia Muungano mwema huku nikisisitiza
Nautakia huu muungano wetu adhimu udumu milele na hivyo kukitokea yoyote anayetaka kuuchokoa muungano, namshauri chokochoko amchokoe pweza, muungano hutauweza kwasababu tutaulinda kwa gharama yoyote.
Nawatakia muungano mwema.
P
Leo tunapo adhimisha miaka 60 ya huu muungano wetu adhimu, nafanya tafakuri, niliwahi kuandika nini humu kuhusu muungano wetu.
Nawatakia maadhimisho mema ya miaka 60 ya muungano wetu adhimu.
Ujumbe wangu ni muungano wetu adhimu udumu milele, na sasa ni muda muafaka tuachane na huu muungano wa kimaghumashi, wa union na federation, sasa twende kwenye muungano wa kweli wa union wa nchi moja, serikali moja, na rais mmoja!.
Mungu Ibariki Tanzania
Mungu Tusaidie
P
 
Back
Top Bottom