KWELI Msongo wa Mawazo (Stress) husababisha mtu kula sana na hatimaye kuongezeka uzito

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Je, ni kweli kuwa watu wenye stress hula sana na matokeo yake huwasababishia uzito kupita kiasi?

1710399266225.png
 
Tunachokijua
Msongo wa mawazo ni hali ya mtu kuzongwa na mawazo hasi ambayo mara nyingi hupelekea matokeo mabaya Kwa muhusika hasa pale asiposaidiwa au asipojisaidia kutoka kwenye changamoto hiyo.

Kula sana ni kitendo cha kula chakula kupita kiasi cha kawaida ambacho mwili wako unahitaji kiasi cha kukufanya ujisikie vibaya.

Kumekuwa na madai kwamba mtu anapokuwa katika msongo wa mawazo huweza kuchochea kuzalisha tabia ya kula sana isivyo na kuweza kupelekea kuongezeka uzito.

Upi ukweli kuhusu madai haya?
JamiiCheck imepita vyanzo mbalimbali ili kubaini ukweli wa madai haya. Chuo cha Afya cha Havard na Tovuti ya Medical news Today wanakubaliana na madai haya kwa kufafanua namna namna ambavyo Msongo wa mawazo huweza kuchochea kuzalisha tabia ya Kula sana na hatimaye kupelekea kuongezeka kwa uzito.

Kwa upande wao Chuo cha Afya cha Havard wanaelezea homoni ambayo huzaliwa mtu anapokuwa katika Msongo wa mawazo na kusababisha kuzaliwa kwa tabia ya kula isivyo kawaida. Wakifafanua jambo hilo katika makala yao wanasema:

Mtu anapokuwa na msongo wa mawazo, tezi za adrenalini huzalisha homoni iitwayo cortisol ambayo kazi yake kubwa ni kuuchochea mwili kufanya mambo mbalimbali. Miongoni mwa vichocheo vinavyoweza kuibuka wakati huu ni pamoja na kichocheo cha hamu ya Kula sana.
Aidha, kuhusu kuongezeka uzito Chuo cha Afya cha Havard wanaeleza kuwa Watafiti wamehusisha msongo wa mawazo na ongezeko la uzito. Utafiti wa Chama cha Kisaikolojia cha Marekani uibaini kuwa kati ya watu 10 wenye msongo wa mawazo watu 8 waliongezeka uzito.
Kwa upande wao Medical news Today wanafafanua kuwa kula kwa msongo wa mawazo ni kitendo cha mtu kula sana chakula kama njia moja wapo ya kuondokana hali aliyonayo. Wanasema:

Watu wengi hukumbana na kula kihisia kwa namna moja au nyingine. Tabia hii huweza kuonekana pale mtu anapochoka au anapofanya kazi ngumu na kuamua kujinunulia au kula chakula kizuri kwa lengo la kujipoza au kuwa sawa.
Hata hivyo, hali hii ikitokea mara kwa mara huweza kuathiri afya ya muhusika hata kupelekea mtu kupata uzito uliopitiliza.
Zaidi ya hayo, JamiiCheck imewasiliana na George B Chacha - Mwanasaikolojia wa Afya na Jamii ambaye naye amekubaliana na madai ya kwamba msongo wa mawazo huweza kupelekea kuzaliwa kwa tabia ya mtu Kula sana na hatimaye kuonezeka mwili na uzito. Akifafanua zaidi jambo hili Mwanasaikolojia Chacha

Suala hilo ni la kweli japokuwa inategemea na changamoto husika ya msongo wa Mawazo, jambo hilo lina uhusiano mkubwa na changamoto ya Afya ya Akili na Afya ya Mwili, ni vitu tofauti japokuwa vinaendana.
kuhusu Msongo wa Mawazo kusababisha mtu kula sana, ipi hivi kuna Homoni inayotengeneza njaa inaitwa Ghrelin Hormone au Hunger hormone, hii ndio inadhibiti kiwango cha ulaji, hivyo Homoni hiyo ikizidiwa inakuwa si rahisi kwa mhusika kuweza kudhibiti chakula anachotakiwa kula kwa kuwa Homoni inakuwa imeshavurugika na inaweza kumfanya mhusika kuwa na tabia ya kulakula.
Pia Msongo wa Mawazo unaweza kumfanya mtu awe anakula mara kwa mara sio kwa sababu anataka kuridhisha mahitaji ya tumbo, bali anaweza kufanya hivyo kama sehemu ya kujifariji, hiyo inaitwa Stress Eating.
Stress Eating inamfanya mtu anakula zaidi kwa hisia na sio kwa ajili ya kushiba bali ili tu awe bize, mara nyingi inawatokea wanaokuwa wapweke, wakiwa na hasira au ambao hawana cha kufanya.

Hivyo ni kweli kuwa Stress Eating inaweza kumfanya mtu akanenepa zaidi kwa kuwa anakula chakula kingi kuliko uhalisia, pia inaweza kumfanya mtu akonde kwa kuwa atakula chakula kingi ambacho si sahihi, sio muda sahihi na pi sio katika muda sahihi matokeo yake afya yake haitakuwa sawa na kumfanya akonde.
Hivyo, kutokana na ufafanuzi kutoka kwenye vyanzo hivyo hapo juu, JamiiCheck inaona kuwa hoja inayodai kuwa Msongo wa Mawazo hupelekea kuongezeka kwa hamu ya kula na hatimaye kuongezeka uzito ni ya kweli
Kama ni hivyo basi Matukunyema watakuwa wanaongoza kwa Stress.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
 
Weka:
Angalizo:
Hii ni kwa Ulaya na Marekani tu,
Huku kwetu sisi tunaopitisha siku kwa stress ya kutoona hata mlo mmoja haituhusu
 
Stress zipi unazozizungumzia hapo? Emu categorise vizuri ili tujue unazungumzia stress zipi? Maana bila ARV wale wenye Ngwengwe kilichokua kinawapeleka puta sio virus Ila ni stress mtu anagoma kunywa uji mara hataki kula Ugali
 
Je, ni kweli kuwa watu wenye stress hula sana na matokeo yake huwasababishia uzito kupita kiasi?

It's both ways kwa sbb ni psychological, kuna watu wanakula sn na wengine hawali kabisa kuelekea distribution line! Human beings reacts differently to stress based on personal stress threshold that's strongly related to makuzi na stress levels at younger age
 
Inategemea kati ya mtu na mtu.

Kuna ambao wakiwa na stress hawali, kuna ambao wanakula kupitiliza. Iwe kwa kula chakula kingi kwa muda mfupi ama kidogo kidogo throughout the day.

Hii ni kwasababu baadhi ya watu hutumia emotional eating kama njia ya kupunguza, kutuliza au kuzuia negative emotions.
 
Kabisa,

Mi nikiwa na stress naweza Kula sahani nzima ya ubwabwa na kushushia pepsi baridiii!! Nikimaliza ndio naanza kujilaumu.

Na Njaa inakuja chaap!
 
Wanazungumzia stress gani hawa jamaa? Unaijua stress au unaisikia? Unaletewa msosi unauona kama mawe! It depends na mtu labda
 

Similar Discussions

6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom